Maoni yangu binafsi juu ya masuala mbalimbali yanayoendelea duniani

Maoni yangu binafsi juu ya masuala mbalimbali yanayoendelea duniani

1700541369314.png
ninaamini
 
Marekebisho ya sheria za uchaguzi na muundo wa Tume ya uchaguzi zinalenga kuwadhulumu wapigakura haki yao ya kikatiba ya kujichagulia viongozi wao wanaowaamini
 
Hivi mhimili wa mahakama unatoka wapi kuteua tume ya uchaguzi kama lengo siyo kuwapitisha makada wa CCM watufanyie finishing?
 
Hawa majaji na hulka yao ya kupendelea serikali sasa mguu mmoja uko mahakamani na mwingine uko kwenye tume ya uchaguzi tutapona kweli?
 
Jaji mkuu ndiye mwenyekiti wa kamati ya uteuzi wa makamishina wa Tume ya uchaguzi sasa ikija kesi ya kupinga zoezi zima la uteuzi wa hao makamishina atatoa wapi uhalali wa kuunda jopo la majaji wamchunguze yeye mwenyewe kama hakuhongwa wakati alipokuwa akiyatelekeza majukumu yake.

Atajifunga kengele mwenyewe au atateua jopo analojua litamsafisha.

Swali la msingi kuliko yote ni sahihi kwa majaji kuwa mahakimu kwenye kesi yao yenyewe?

Pia, je ni sahihi kwa wateule wa Rais kuwa wajumbe wa Tume ya uchaguzi kama lengo siyo kuijaza Tume ya uchaguzi na makada wa CCM ili watangaze matokeo ya uchaguzi bila kuhesabu kura?

Ieleweke tuliyoyashuhudia kwa macho yetu wenyewe uchaguzi wa 2020 ndiyo yanatusukuma tuoni kama tunavyooni.

Hatuna imani na wateule wote wa Rais kujihusisha na Tume ya Uchaguzi kwa sababu wanayo masilahi binafsi ya kuhakikisha CCM inaendelea kutawala hata kama wapigakura wameikataa kwenye masanduku ya kura

Si sahihi kwa Mwenyekiti wa Tume ya uchaguzi kuwa jaji kwani kuhesabu kura tuna kesi ya kuamua? Jaji na kuhesabu kura wapi na wapi?

Sifa ya ujaji ni unafiki mtupu wa kuipa Tume ya uchaguzi sifa ya haki wakati haina bali ni kijiwe na kichinjio dhidi wa wagombea wa vyama vya siasa vya upinzani

Halafu bado tunajigamba tuna Mwanasheria Mkuu mbavu zangu hoi
 
Halafu wahariri wa hii sheria wanajaribu kutuhadaa eti ni Tume Huru ya uchaguzi.

Ingelikuwa huru sheria isingesema ni huru. Ukiona mtu au sheria inajihami ujue ni kinyume chake.
 
Uhuru wa Tume ya uchaguzi unatokana na kujigamba yenyewe ni huru au jinsi ilivyopatikana na inavyofanya kazi?

Majigambo siyo uhalisia
 
Kimuundo na jinsi itakavyofanya kazi hii tume ya uchaguzi ni kitengo cha kuiba kura ndani ya CCM haina hata harufu ya uhuru
 
Matatizo yote ambayo tumepitia kuanzia mwaka 1995 hadi 2020 hakuna hata moja limetatuliwa na mapendekezo ya marekebisho ya sheria za chaguzi
 
Tunatamka rasmi uwepo wa majaji kwenye kamati ya uteuzi au mteule yeyote wa Rais kwaajili ya majukumu mengine kama Mwanasheria mkuu kuna haramisha tume ya uchaguzi na inapoteza uhuru wake na kuiita jina tume huru huku Rais mwenye chama cha siasa chenye masilahi mapana ya kuiba kura ndiye anaiunda kupitia wateule wake sisi hatukubali kudanganyika na tambo za kuibatiza tume ya uchaguzi kilemba cha ukoka ya kujigamba ni tume huru wakati ni tume ya mgombea Urais wa CCM
 
Tatizo kubwa kuliko yote tulilonalo ni ukapa wa uongozi bora na haya marekebisho ya sheria za uchaguzi kamwe hayatatua haya matatizo bali zitayakoleza.

Uwakilishi haramu ndilo chimbuko la umasikini hapa nchini hasa ukiona hata Bashite anaonekana ni jembe la wezi wa kura ujue tumefikia pabaya mno
 
Kabla ya kutunga au kurekebisha sheria za uchaguzi malengo yake yajulikane hapa ni wazi malengo ni kuhakikisha kura hazitahesabiwa
 
Malengo ni kuwahadaa watanzania na wapigakura kuna uchaguzi hufanyika lakini kinachoendelea ni kuwachagulia wananchi viongozi wasiwataka na kwa haya marekebisho yasiyo na dhamira ya kuwawezesha wapigakura kuwachagua viongozi wanawaamini tutarajie uwakilishi haramu kutawala na kuwa kichocheo cha wizi, ubadhirifu na rushwa kukithiri
 
Uhuru wa tume ni kuhakikisha kamati ya uteuzi wa makamishina wa Tume ya uchaguzi hakuna hata mmoja ni mteule wa Rais yaani hana kofia mbili mbili.

Lazima wajumbe ya kamati ya uteuzi watoke kwenye vyama vya siasa vilivyosajiliwa na taasisi za kidini zilizosajiliwa kama wawakilishi wa wapigakura
 
Kamati ya uteuzi tajwa inapaswa iwe na wajumbe walioteuliwa na mikutano mikuu ya vyama vya siasa kwa kazi hiyo tu na wasiwe na nyadhifa zozote serikalini au kwenye vyama vya siasa.

Yaani wawe watu wa kawaida siyo viongozi kwenye ngazi yoyote ile na wasiwe watumishi wa umma
 
La maana tuliloliona kamati ya uteuzi haina sura ya utaifa ila wale wale wanaotuongezea umasikini ndiyo wanakaza buti kutuchagulia viongozi yaani kuhakikisha business as usual wakati mustakabali wa nchi uko njia panda
 
Lingine wahariri wa hii sheria wako usingizini wameuchapa hawawezi hata kutafakari matatizo ya nchi hii ni yapi ma yanasababishwa na nini?
 
Hii jitihada ya marekebisho ya sheria inalenga kulinda mfumo wa kiutawala tuliorithi kutoka kwa mkoloni zaidi ya miaka 60 iliyopita sasa utuambie nchi hii tuna wasomi.

Tunao wenye makabrasha lakini wabunifu hatunao huu ndiyo ukweli wetu
 
Chombo huru hujiuza chenyewe kwa matendo yake ukiona kinajitembeza kuwa ni huru jua fika kinafungamana na aliyewateua
 
Tunahitimisha kwa kusema marekebisho ya sheria za chaguzi yamegubikwa na hila, unafiki na tunasisitiza yeyote anayeshabikia huu upotolo ajue mbinguni ataziona lakini hatakwenda huko atabaki hapahapa Jahanamu na Lucifer mungu wake maana hii ndiyo mbingu yake na hana nyingine ya kuwapa
 
Back
Top Bottom