Mapaja yangu yanatoa unga, tatizo ni nini?

Kijana kijana

JF-Expert Member
Joined
Mar 11, 2018
Posts
2,546
Reaction score
2,621
Wakuu moja kwa moja kwenye mada,.
nimekuwa na tatizo yani kati kati ya mapaja ambapo zile mbegu mbili zaegemea(zinapumzikia)naona kuna alama fulani imejichora na kisha huwa nikiwasha hutoka unga unga wakuu na jana nimetizama naona kama kuna vijipele ambavyo kwa mbali kama mabaka .

tatizo ni nini wakuu naombeni ushauri wenu wa awali
 
fangai hao we nenda, na umbuka kuji kausha vizuri ukitoka kuoga na uwe una paka angalau mafuta
 
Hiyo ni fungus tumia gentrisone cream asubuhi ukioga unapaka na jioni ukioga unapaka kwa muda wa wiki 6 mpaka 8 utapona, ukitumia hiyo cream ndani ya wiki moja utaacha kuwashwa ila usiache kutumia mpaka baada ya muda huo
 
Pole mkuu, fangas hao nenda hospitali. Huwa nawakubali sana wachina na utamaduni wao wa kusalimiana bila kushake hands, hapa nimewaza huyu jamaa katoka kujikuna afu anakupa hi kwa mkono na huo unga unga. Anyway Mungu anatulinda sana basi tu.
 
Hongera Sana mkuu, Mungu ameona hii Ni serikali ya viwanga hivyo kaamua kukupa kiwanda Cha sembe. Mwite mh Rais aje azindue uanze supply.....(joke)

Pole mkuu, nenda hospitali kamuone dermatologist
 
Hongera Sana mkuu, Mungu ameona hii Ni serikali ya viwanga hivyo kaamua kukupa kiwanda Cha sembe. Mwite mh Rais aje azindue uanze supply.....(joke)

Pole mkuu, nenda hospitali kamuone dermatologist
 
Hongera Sana mkuu, Mungu ameona hii Ni serikali ya viwanga hivyo kaamua kukupa kiwanda Cha sembe. Mwite mh Rais aje azindue uanze supply.....(joke)

Pole mkuu, nenda hospitali kamuone dermatologist
tehehdheh, dah japo umeandika pumba lakini umenichekesha,Asante kwa ushauri wako .

nawe ukamuone mwana saikolojia hospital
 
Pole Mkuu, ukimaliza kuoga jikaushe vizuri kwenye maeneo yanayozunguka korodani (mbegu kama ulivyoandika kwenye uzi wako na mbegu zenyewe sijui zitakuwa za mmea gani) na uvae nguo za ndani zilizokauka/pasiwa. Tahadhari: EPUKA KUVAA NGUO AMBAZO ZINA UNYEVUUNYEVU. Hii itakusaidia kupunguza kutoa unga pamoja na kwamba hujabainisha ni unga wa aina gani. Over
 
Hiyo ni fungus tumia gentrisone cream asubuhi ukioga unapaka na jioni ukioga unapaka kwa muda wa wiki 6 mpaka 8 utapona, ukitumia hiyo cream ndani ya wiki moja utaacha kuwashwa ila usiache kutumia mpaka baada ya muda huo
Solution...
 
Pole mkuu, fangas hao nenda hospitali. Huwa nawakubali sana wachina na utamaduni wao wa kusalimiana bila kushake hands, hapa nimewaza huyu jamaa katoka kujikuna afu anakupa hi kwa mkono na huo unga unga. Anyway Mungu anatulinda sana basi tu.
Aiseeee...
Ndio maana ukipewa mkono wewe jikaushe au jifanye mikono yako michafu, au gonga ngumi...
Ila mkuu kuna mambo mengi sana tu, handles za milango, milango, mabomba kwenye daladala, chenji, milango ya magari, kuokota okota vitu hovyo barabarani, hela tunazopokea na kutoa, matunda kula bila kuosha, PC kwenye internet cafes, lock za milango ya choo, ukiomba pen ya mtu, upandapo kwenye boda lazima utashika mabomba au chochote, ...the list is endless...
Unaweza hata kuwa kichaa kipi ushike kipi usishike, ndio maana kuna watu kunawa mikono kwao ni jadi na kawaida, kila wakati na kila muda...
End of the day mie naona ni kudra za mwenyezi mungu kutuokoa na magonjwa...
Hii thread imenikumbusha tena umuhimu wa kunawa mikono kila wakati, na kuepuka kushika shika watu au vitu..
 
Usafi unatakiwa

Dont use gentrisone in broken skin

Hosp is so important
 
NI FUNGAL INFECTION, TUMIA DAWA HIZI KUPAKA

BETAMETHASONE na CLOTRIMAZOLE

ZOTE NI ZA KUPAKA KUTWA MARA MBILI BAADA YA KUSAFISHA HIYO SEHEMU NA KUKAUSHA KWA KITAMBAA SAF

HAKIKISHA UNABADILISHA BOXA SAFI MARA KWA MARA NA UWE MKAVU MUDA WOTE.

N. B:TAFADHALI HALI IKIZIDI MUONE DAKTARI
 
Twende zetu tukamuone wazilri wa viwanda Charles mwijage. Uchumi unao unaukalia.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…