#COVID19 Mapambano dhidi ya COVID-19: Rais Samia anayo dhamira ya kweli? Kinachoendelea India kinatisha

Kwa style ya uongozi wa JPM (ukali wa pilipili, hataki kukosolewa, mbanaji pesa, fukuza fukuza, very undeplomatic, n.k) usingeweza kuamini kwamba mtu kama huyu angeweza kupendwa na watu. La kushangaza JPM ni kiongozi pekee aliyeweza kukonga mioyo ya watu wengi nchini na hata nje ya nchi. Why mtu mgumu kama yule aweze kugusa mioyo ya watu?

Hii kitu mi naamini iwape funzo wanasiasa wote nchini na duniani kote. Kumbe ubora wa kiongozi si kuto speech nzuri nzuri au kuonekana mtu "cool". Sifa ya kwanza ya kiongozi bora na kuishi kile anachokihubiri. Kwa vurugu za JPM asingekuwa anaonyesha kwa mfano wake mwenyewe kwamba "Hapa Kazi Tu" nadhani angekuwa kiongozi mbovu kabisa kuwahi kutokea kwa aina ya personality yake. Lakini kumbe people wanajali mambo deep zaidi nayo ni kuishi kile unachikihubiri -- na hapo ndipo JPM alifanikiwa.

Legacy ya kwanza kabisa ya JPM ni ya kiongozi aliyefia akiwa mstari wa mbele vitani kabisa. Iwe ni kwa Corona, iwe ni kwa adui mtu, the man feared no evil, aliipambani nchi yake hadi pumzi yake ya mwisho.

Rest in Peace JPM, your services to this country will always be hardcoded onto the souls of the nation.
 
Sidhani nchi yoyote waliamini Covid imekwisha wakatiw a kulegeza lockdown, walidhani wameshusha kiwango cha maambukizi kwa kutosha.
Isipokuwa Tanzania kulikuwa na ujinga wa wanasiasa kutangaza "Tumeshinda!"

Naamini Magufuli alifanya vizuri kutoingia lockdown. Uwezekano mkubwa aliokoa uhai kwa njia hiyo. Naamini alifanya kipumbavu kupuuza tahadhari, kukemea watu waliovaa barakoa na kadhalika. Wengi walimwaini. Uwezekano mkubwa aliharibu uhai kwa njia hiyo.

Menginevyo dalili zinaongezeka kiwango cha hatari hapa ikweta iko duni kiasi - angalia

Lakini bado inaua, na tunaweza kusubiri tu mabadiliko ya virusi. Bila hofu lakini kwa tahadhari.
 
Mkuu Nyani, nakusalim kwa jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Naomba nikutoe wasiwasi kuwa, kwa Sasa hali ya COVID-19 cases kwa Tz ni ndogo Sana. shughuli zinaendelea, Kkoo kunafurika Kama siku zote, bar na viwanja vya michezo vinafurika lakini cases zimeshuka Sana. Kwa Sasa Kelele za Ambulance na misiba ya ghafla tuliyoshuhudia January - February hazipo tena. So, usihofu kuwa hali ya India Kama inaweza kutukuta. Huu Ugonjwa uko seasonal Kama umeona vizuri epidemiology yake. Kwetu cases huwa zinapeak January-february.
 
Hakukemea kuvaa barako ila alitahadharisha kuhusu barakoa zinazongizwa nchini kuwa hazina "guarantee" kama siko salama.

Na alisisitiza kushona barakoa zetu wenyewe ikiwezekana.

Na wananchi wengi waliitikia wito huo wameshona barakoa kwa kutumia vitambaa vya hapahapa Tanzania.
 
1) kuhusu consistency ya Magu, unachosema ni kwamba unampongeza kwa kukomalia jambo hata kama hayuko sahihi. Well, good for you. Kwangu mimi consistence inatokana na principle ipi inamguide mhusika. Siyo ishu ya kukomaa tu. Unakomalia nini?
Concern yako kwamba India wanateketea, inashangaza. Hata wakati wa Magu kukomaa, kuna nchi walikuwa wanateketea, Brazil for one.

2) kuachwa Solemba. Umesema hukubaliana na kauli ya Magu pale St. Peter, kuwakosoa masista kwa kuvaa Barakoa. Magu alikuwa consistent na sera zake na misimamo yake, ambayo unaipongeza. Yet unamkosoa. Solemba.
3) CHADEMA
Hawa walitangaza kwamba kufuatia vifo vilivyotokea bungeni, wanajikarantini kwa siku 14. Kama wewe ulielewa kwamba wanaacha ubunge, hiyo ni tafsiri yako ambayo siyo sahihi. Suala la kujikarantini unapohisi umecontact infected person, Ni la kawaida. Baadae unaendelea huku ukichukua tahadhari. Not rocket science, is it?
BTW, naelewa you are sick with hatred for CHADEMA. lakini kumbuka wamesurvive mashambulizi makali ya kuua chama na viongozi. Yet Tume mbovu ya uchaguzi imewapa 13 percent kura za urais. Incredible!

4) Samia
Vitendo na kauli za wanasiasa huwa zinalenga makundi fulani, sometimes. Samia amechagua kubadili uelekeo wa Magufuli, kwa tahadhari. Anapoaddress wanaccm ambao wangependa kuona Umagufuli unadumu, pengine ni tofauti na anapoliaddress taifa kwa ujumla. Hebu tusubiri angalau 100 days. Tutapata picha nzuri zaidi.
 
Boya kama boya.

Za siku?
 
COVID 19 is a nightmare , siyo jambo la kukwepeka kirahisi hivyo.
Mwendazake alijaribu kwenye hili lakini ni jambo tata sana huwezi kusema alkosea au alifanikiwa ....
Hakuna nchi ambayo imefanikiwa pamoja na chanjo (vaccine) zote.
 
3rd wave ishaanza ya uviko hapa TZ ,itakuwa India Variant ,nimepata taarifa ya misiba mitano sasa kwa watu naowajua achilia mbali taarifa za kwenye facebook na twitter.

Tuchukue Tahadhari.
 
Sema wewe: Je barakoa zinaweza kuwa na hatari gani???
Ninakumbuka eti ilidokezwa barakoa kutoka nje zinaweza kuleta virusi (!!!) - ambayo ni dhana ya kitoto. Je kuna mfano mmoja uliotazamwa na kurekodiwa (wapi, lini, na nani?)
Naona hamna.
Yeyote anayejielimisha kidogo tu atajua: Barakoa za kushona, ni sawa na zile za karatasi za bei ya chini (mara nyingi buluu-nyeupe). Zinapunguza kiasi cha matone ya mate tunayotoa wakati wa kuongea, hivyo kupunguza hatari kutoka yule anayeivaa, ilhali wanamkinga mvaaji kiasi (si sana) dhidi ya kuvuta ndani matone ya pumzi ya mtu mwingine mwenye virusi. Hazina kinga cha juu sana, lakini kama wote wanazivaa, maambukizi yanapungua kiasi kikubwa.

Barakoa za hali ya juu zaidi kama FFP-2 (jina la Ulaya) au N95 zinapendekezwa kwa watu wanaohudumia wagonjwa, ni hali ya juu, hazitengenezwi nchini, zote zinaingizwa kutoka nje.
 
Zipo barakoa za kawaida kabissa ambazo kila mwananchi aweza kuzivaa.

Hizi ndizo alizopendekeza hayati Magufuli.

Hizo barakoa za mahospitalini haziwezi kuzuiwa maana zina ngazi tofauti za kukinga maambukizi huko mahospitalini.

Pia zipo barakoa za viwandani na zile za kuzuia vumbi.

Nadhani yeye alikuwa azungumzia barakoa za kawaida kabisa yaani basic ambazo ndizo twaweza zishona wenyewe.

Nikukumbushe tu ndugu kuwa si kila bidhaa ijayo Afrika ni sawa na bidhaa itumikayo Ulaya na Marekani.

Na ndo maana hata hizi chanjo za COVID-19 zipo zile za kutumika hukohuko duniani na zipo za kupelekwa katika nchi kama Tanzania.

Ndo maana hata India ilipokumbwa na maswahiba ya COVID-19 kushika kasi, basi nchi zilizojiwekea akiba ya chanjo hizi huko duniani waliweza kugawa dawa hizo hata kama zilikuwa na siku chache kabla ya kuisha muda wake.
 
Asante kwa jibu lakini uliepukana na swali langu: Kuna hatari gani katika barakoa yoyote?? - isipokuwa kuna aina zenye kinga kidogo, kama hizo za kushona (alizotaja marehemu). Menginevyo hizi barakoa sahili za karatasi (rangi buluu-nyeupe) hutengenzewa kwa mabilioni hasa China na kuuzwa kote duniani.

Onyo la marehemu dhidi ya "barakoa kutoka nje" lilikuwa mchezo wa kisiasa tu. Kwa bahati mbaya alipata watu wa kutosha waliopumzisha akili zao na kupokea habari hiyo kama uwezekano na hata ukweli. Masikini!
 
Hii mada izingatiwe na kama wapo watu wanaoweza kumshauri Rais katika hili wafanye hivyo

Idadi ya misiba hapa Kilimanjaro kwasasa ni kubwa kwakweli, kuna uwezekano mkubwa COVID 19 Ipo kwa sehemu kubwa na inaua haswa.

Let us be serious katika hili.
 
I doubted Samia’s seriousness in fighting C-19 long time ago.

Now look what’s happening.

Just some half-hearted efforts to look like they are doing something.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…