Mapenzi: Jinsi ya kumtongoza mwanamke unayemtaka na ukampata kwa urahisi

Mapenzi: Jinsi ya kumtongoza mwanamke unayemtaka na ukampata kwa urahisi

Naona kimya kimetawala
Mkuu kwa mimi ratiba zangu ndo shida ila napenda sana kuchangia mawazo na washkaji.Nimeona post moja hapo juu nilisema nitatoa mbinu ya kumtongoza demu kwenye party. Nitaiweka muda si mrefu
 
ndalichako unawapa frustration vijana kwakeli yaan thread nyingne
 
Wakuu habari zenu, kuna baadhi ya wanaume huwawia vigumu sana suala la kutongoza.Wakati kwa wengine tunaona kama hakuna kazi rahisi kama hiyo.Sasa katika uzi huu kama kuna demu umempenda na unawaza namna ya kumteka unashindwa msaada unaweza kuupata hapa.

Labda tu utueleze na mazingira gani alipo bar, party, ofisini njiani n.k. msaada utaupata hapa wakali wa hii burudani tupo.Utani hautakiwi. Utakula watoto hadi utajikataa.

Karibuni.
Nipe mbinu ya kumpata Dada yako
 
Wasalaam Gentlemen & Ladies,

Kutongoza mwanamke wakati mwingine inaweza kuwa na tatizo. Hizi hapa ni mbinu na ujanja 15 za jinsi ya kutongoza wanawake na wafall na wewe.

Tumeshapitia hapo. Kuna yule mwanamke mrembo ambaye umekufia naye na una hamu ya kutaka kumjua. Lakini kuna lile tatizo linajitokeza ambalo linakufanya ushindwe kuongea na yeye uso kwa uso. Unatamani kuwa na uwezo wa kumu-approach ili umsome akili yake na umwambie yale yote yaliyo moyoni mwako.

Hapo hapo, ijapokuwa kutongoza mwanamke huwa inakuja automatic kwa baadhi ya watu, kwa wengine inawafanya wajihisi wako katika hali ngumu. Yale mawazo tu ya kumu-approach mwanamke yakiwajia wanaanza kutokwa na kijasho kwa mikono, midomo inakauka, na unaanza kuongea kama kigugumizi unapotamka maneno – yaani inakuwa mbaya kujieleza na si vizuri itokee kwa mwanaume yeyote. Watu wa aina hii tumezoea kuwaita 'Domo Zege'

Habari njema ni kuwa unaweza kujifunza njia za kutongoza, na ufanye mazoezi ya kutongoza hadi ujihisi kuwa umejiamini na tayari kuandama msichana unayempenda.

Na kwa hilo, nimekuja na mbinu 15 ambazo unaweza kuzitumia kutongozea wanawake.

#1 Tabasamu

Kutabasamu ni hatua ya kwanza bora ya kuanzia, haswa wakati ambapo umeingiwa na kibaridi. Hakikisha ya kuwa anayaangalia macho yako na unamaintain mtizamo wa macho yenu. Tabasamu huku unajiamini na usiwe wa kwanza wa kuangalia kando.

Kama atakurushia tabasamu, basi angalia kando kwa dakika chache halafu mwangalie tena huku ukitabasamu. Njia hii itampa ishara ya kumwambia kuwa uko interested na yeye. Lakini usifanye kosa la kurudia rudia kumtabasamia kwa sababu atakuona kama fala. So unachohitajika ni kujiandaa kumuapproach ili uanze mazungumzo.

#2 Tumia miondoko ya mwili inayofaa.

Hakikisha unamakinika na miondoko ya mwili wako wakati unapozungumza na yeye. Kama umeingiwa na wasiwasi, usitie shaka muaproach mwanamke huyu kana kwamba hauko interested na yeye. Kuikunja mikono yako, kuangalia miguu, na kuangalia kando hupaswi kufanya kamwe.

Kuwa wazi na utumie macho yako kuwasiliana naye – mwangalie bila kuona aibu! Tumia mwili wako kumtongoza. Mwonyeshe kuwa umevutiwa na yeye.

#3 Mguse

Njia rahisi ya kumtongoza mwanamke ni kumgusa. Unaweza kumsugua na mkono wako, ama kama umekaa kando yake unaweza kuuachilia mguu wako umguse. Iwapo amependezwa na wewe hatauondoa.

Kama unamjua zaidi, kumgusagusa hua inafanya kazi vizuri sana. Mkumbatie, weka mkono wako kiunoni mwake wakati unaongea na yeye na hali kadhalika. Fanya haya yote iwapo tu hakatai. Na ukiona kama anarudia kile ambacho unamfanyia basi ujue umefaulu.

#4 Mfanye acheke

Ucheshi ni kitu cha kwanza ambacho wanawake huangalia kwa mwanaume, hivyo basi ni lazima ujifunze tabia ya kuwa mcheshi kama unataka kufaulu katika sanaa ya kutongoza. Kama unaweza kumchekesha basi utamfanya ajifeel amerelax na wewe mara moja hivyo kumvutia.

Si lazima uwe mcheshi kama Kingwendu ama Churchill ili umfanye acheke, la. Kinachohitajika ni uwe mhalisi. Kila mtu katika huu ulimwengu ana kipawa chake cha ucheshi. Hivyo unaweza kukumbuka jambo lolote ambalo ushawahi kuchekesha mtu. Mwanamke akikupenda anaweza kuchekeshwa na kila neno ambalo utasema.

#5 Mwache aombe nguo zako

Anapenda kuvalia lile vazi lako kubwa, so mpatie avae kama kuna baridi. Hakikisha pia linanukia marashi yako, na kama anakupenda, atatamani akae nalo ili alikumbatie kwa kitanda na akuote katika ndoto zake.

#6 Msifu

Kumsifu mwanamke huwa ni mbinu nzuri ya kutumia wakati unapotongoza mwanamke, so mwonyeshe kuwa anavutia. Kama hutaki kwenda haraka unaweza kuanza na maneno kama ‘leo unapendeza’ ama ‘nimependezwa na kiatu chako’. Hii ni njia ya rahisi kumwambia mwanamke kuwa anavutia bila kusema neno ambalo litamuudhi.

#7 Kuwa mzuri mbele ya marafiki zake

Hakikisha kuwa unajipa time na marafiki zake. Kama ataona kuwa unajaribu kuwasiliana na marafiki zake, itampa ishara kwake kuwa umependezwa naye na uko tayari kuspend muda naye. Kama bado hajaamua basi atatafuta ushauri kutoka kwa marafiki zake na itakuwa rahisi kwao kukuidhinisha kwake.

#8 Muulize maswali

Kama unataka kujua kutongoza wanawake basi lazima uonyeshe interest kwa kumuuliza maswali mengi.

Atashukuru ule muda wote ambao umekaa na yeye ukimuuliza maswali kutaka kumjua zaidi. Hakikisha unamakinika na majibu yote ambayo atakwambia ili wakati mwingine mtakapokutana usisahau chochote kile wakati ambapo atakuuliza swali.

#9 Ijue familia yake

Kuijua familia yake ni njia nyingine ya kuonyesha kuwa umevutiwa na yeye na uko tayari kujipa muda kujua zaidi kumhusu.

#10 Mfanyie favour/fadhila

Kutongoza mwanamke huwa kunakuja na njia tofauti tofauti. Kumwonyesha ukarimu mwanamke kwa kumfanyia jambo asilotarajia ni njia murua ya kuhakikisha kuwa utawini penzi lake.

#11 Mnunulie kinywaji

Wakati mwingine vile vitu rahisi huwa ndivyo bora. Kama unataka maongezi yenu yawe rahisi na yaliyotulia basi huna budi kumnunulia kinywaji halafu mazungumzo yaanze na hapo.

#12 Mnunulie zawadi

Zawadi nzuri na yakuvutia ni njia nzuri ya kumtandaza mwanamke katika hali ya kumtongoza. Unaweza kumzawadia zawadi cheshi na yakufurahisha haswa kutokana na mambo ambayo ameyataja kutokana na mazungumzo yenu ya awali. Hii itamvutia. Hakikisha haumnunulii zawadi ambayo ni ya gharama ama iliyo serious coz unaweza kumuogopesha.

#13 Kuwa interested na mambo anayopenda

Pata kujua kile kitu anachopenda na kufanya wakati yuko free, vitu anavyopenda na kila kitu. Hii itakupa nafasi ya kuwa na mambo mengi ya kuongea kuhusu. Ataona kana kwamba mnafanana kimtizamo flani.

#14 Mtumie SMS

Mazungumzo ya SMS ni njia nzuri kwa kutongoza. Kwa mtu mwenye kuona aibu inakuwa rahisi kwake kabla ya kuanza mazungumzo ya moja kwa moja. Mtumie jumbe za kutongoza, cheshi, na kama atajibu inavyostahili unaweza kumtumia jumbe zaidi.

#15 Mtese

Kumtesa kwa upole ni njia nzuri ya kuanza kutongoza mwanamke. Kila mtu anajua kuwa wale wavulana wadogo hupenda kuvuta nywele za wasichana wadogo ambao wamependezwa nao. Hivyo hivyo kumtatiza mwanamke kwa upole, unampa ishara kumwambia kuwa umevutiwa naye. Hii mbinu ina utata lakini ni kweli.

Mbinu ndizo hizi tushakupa. Usingojee tena. Jiamini uanze kumuapproach yule dada saa hizi!


NB: Kuna watakaokuja na hoja ya "siku hizi hamna haja ya kutongoza ni Pesa yako tu" Sijakataa, ila acha wengine wajifunze, najua pesa ina nafasi yake kwenye mahusiano kwani ikipungua na mapenzi vilevile hupungua.

Vilevile, kama kuna mbinu nyingine unayo karibu maana najua kuna wale magwiji waliotukuka katika sanaa hii. [emoji123]
00ff820152ff3306f2d01c218616d6f2.jpg


C,E&P

CREDITS GOES TO: Nesimapenzi dotcom

Sent from my Apple iPhone 5s using JamiiForums Auto-reply Mobile app
 
Back
Top Bottom