Mapenzi ya jinsia mmoja tunawahukumu kwa lipi hasa!

Nadhani tunaongelea
Homasexual hapa
Na mimi point yangu inalenga kwaO

Ikija topic ya kufanya sex na
Watoto walio under age nita react nakujibu
Ipasavyo..

nimetoa mfano huo, kwa sababu mantiki ni ile ile ya watu kuachwa wafanye wanavyotaka kwa sababu tu wameridhia au wanaona ni halali kwao.
Naheshimu uhuru wa kila mtu kufanya apendacho, lakini kuna mipaka,.Kama Lizzy alivyosema hapo juu, kama ingekuwa homosexual ni dili, basi angeumba watu wanawake tu au wanaume tu..

sorry kama nimeku-offend, lakini nilikuwa naangalia your thinking
 
Tofauti hapa ni namna tunavyo hukumu watenda shambi hii kama vile ndio dhambi kubwa kuliko zote! mbona wanasayansi wamethibitisha kuwa baadhi ya matendo haya ni sababu za kimaumbile hapo napo unasemaje!Mungu ganai aliyewaumba hawa au ndio ...kazi ya shetani!
 
ndio maana samtaimu najipakazia wewe ni galfriend wangu, yaani umemwaga mapointi kuliko rais wa bukina faso.
 
ndio maana samtaimu najipakazia wewe ni galfriend wangu, yaani umemwaga mapointi kuliko rais wa bukina faso.

duh...mkuu ile TOPIC ya BROKEN HEART na LD ma-mod wameipeleka wapi?? duh..hawa jamaa utafikiri magaidi...offtopic
 
Tofauti hapa ni namna tunavyo hukumu watenda shambi hii kama vile ndio dhambi kubwa kuliko zote!
Elewa neno mazoea!Wizi umezoeleka..japo haukubaliki.Mapenzi ya jinsia moja bado sisi hatujayazoea na watu wanajaribu kustopisha kabla nayo haijazoeleka ndo maana unaona kama inakandiwa sana.Hata kwenye biblia tumewekewa amri za nini tusifanye ila ya mahusiano ya jinsia moja hamna maana hata Mungu hakutegemea kwamba tutaharibika kiasi hicho!
 
duh...mkuu ile TOPIC ya BROKEN HEART na LD ma-mod wameipeleka wapi?? duh..hawa jamaa utafikiri magaidi...offtopic
dah! haipo tena?, itakuwa Biharusi katekwa nyara. inamaa halusi imehairishwa. dah! sorry mleta mada bana kwa hii ofutopik hakyanani haturudii tena.
:focus:
 
dah! haipo tena?, itakuwa Biharusi katekwa nyara. inamaa halusi imehairishwa. dah! sorry mleta mada bana kwa hii ofutopik hakyanani haturudii tena.
:focus:

dah..kuna jamaa na yeye ana jina la kidonge..ndo kaitekeza, sijui alikuwa na hisa...duh..usijali sana mleta mada kwa hizi offtopic.

back to the topic: mapenzi ya jinsia moja hayakubaliki..
 
Binafsi kichwa kinaniuma sana kuhusu hawa jamaa,hivi hawaujui utamu wa Mbunye?Eti dume zima linapenda kuhemewa mgongoni na jike nalo linapenda kunyonywa naniliyu yake baada ya kuruhusu shaft iingie. tunawachukia kwasababu kama wazazi we2 wangekuwa kama wao cc 2cngezaliwa na cc 2kiwa kama wao hatuwezi kuzaa
 

Mie hat hukuni offend
thank you..

Kwa jinsi mi ninavyofikirini hivi
Mtu kama hafanyi kitu kinacHoumiza watu wengine
kuna shida gani?
I mean kuumiza watu physical au mentality..
hao sijui wauwaji, wabakaji hao wasiruhusiwe kwenye
community.. lakini homosexual wenyewe ni wao na
familia zao ndo wanapitia.. kwa ninaowafahamu
ni watu waliokubalika kwenye jamii yao..

Sanasana tinachoogopa
ni watoto wetu kufanya mambo kama hayo
kwa sababu jamii zingine hazikubali lakini ukimfundisha
mwanao hatayafuata hata aishi nao..

Ok tukija kwenye point
ya Mungu ..
Mungu kamuumba kila binadamu kwa madhumuni yake
Hata j
haowauwaji na wabakaji wametoka kwake
ila choice ya vitu tunavyofanya hapa duniani ndo kitu
muhimu kwake .. tunaweza kusema Homosexual niwatu wa baya
lakini kwa mimi sioni mtu mmbaya ila vitu wanavyofanya ndo vibaya..
na hicho kitu kama hakimuumizi mtu yeyote sioni
ubaya wake....

I'M NO ONE TO JUDGE ANY ONE..

Hopeful nimekujibu..
 

Uko sawa kutokana na unacho amini..
Hapo kwenye RED, bado suala ni lile lile, kwa sababu tu majambazi hawajavamia kwako, basi ni sawa tu; Kama inaweza kumuathiri binadamu mwingine, basi kuna siku na wewe utaathirika kwa namna moja ama nyingine!
'kwa sababu hili jambo linahusiana na kupata raha' haimaanishi kwamba sio kosa
Najua uuaji au ujambazi unaweza kusababisha umwagaji wa damu, ndo maana unaweza kuonekana una madhara ya moja kwa moja..
Kwa kweli licha ya dini tu kukataza, pia jamii zetu nyingi hazikulia katika mazingira kama haya; kwa sababu ni kinyume na asili (nature).
 
mkuu halaf hata vitoto vya shule si vinarizia wenyewe kupewa dozi na mapedeshee, sasa kwanini tusiviachie vikaenjoy tu?, hii freedom ina limit bana. nimekugongea like, acha niludi kugonga na senks.

Klorokwini na mwenzako hapa argument yenu inakosa mashiko..... suala la under age liko hivi. Kitaalamu kuna umri ambao mtu anweza kufanya maamuzi hivyo hakuna mtoto anayeamua kwa hiyari yake yake kufanya mapenzi na pedeshee, huo ni ubakaji kwasababu huyo,pedeshee anatumia udhaifu wa huyu mtoto kufanya maamuzi sahihi. kama vile kufanya mapenzi na mtu baada ya kumlewesha pombe,kufanya mapenzi na mtu mwenye mtiindio wa ubongo n.k

nadhani mleta hoja ameleta a good topic for dicsussion tuwe objective kila mmoja atoa pointi zake akieleza anaegemea wapi kupinga au kukubali. Ipo mitazamo mingi (katika kupinga na kukubali); dini, baolojia, Sheria za nchi n.k tuache kutoa matusi na kuita watu majina kama bwabwa, choko nk...hii ni stigma (unyanyapaa). Nitarudi baadae na mimi nitoa hoja zangu kupinga u kukubali....
 

katika process ya ku-argue kama kuna mifano inayofanana kwanini isitumike. Ukisoma vizuri, hoja ya mleta mada imejengwa katika wazo la kuwa 'kwa sababu ni wao' wameamua na hawamuumizi yoyote kwa nini wasiachwe tu wale raha zao. Kwa mtazamo huo, na mimi kama mchangia mada ninajaribu kutoa hoja kulingana na topic..
Nadhani mchango wako utathaminika tu
 

Nakubaliana nawe
Lakini point yangu bado iko pale
pale hata hao majambazi I mean mtu
yeyote sio mmbay a ila kitu anachofanya mtu ndio
Kitu kibaya .. na watu dunia hii tunaishi na ku judge watu kwa vitu
Wanavyofanya .. which ni sawa sababu sisi ni binadamu..

Tukija kwenye point yako ya jamii
pia nakubaliana nawe ni jamii nyingi
Sana hawakubaliani na hili lakini kumbuka na yule
ni mtoto wa mtu kama familia yake inamsaport kwa yeye
kuwa homosexual shida iko wapi... wanaweza wasipende analofanya
lakini wako naye na wanamsaidia ..
Kuna wengine wanaogopa kusema ajili ya reaction ya jamii zao
Na watu kuwasuta na hao wanaishia kufanya kwa siri
Na wengine kutoa maisha yao....

Sasa kama familia yao inakubali
Haisaidii mimi kumkataza nitampa saport yangu na kuomba
Mungu isitokee kwangu na familia yangu ..lakini tunazaa
lakini hatujui tunacho zaa hatujui watakuja kuwa nini..

Nahakika hata hao majambazi, wauwaji,wabakaji n. K
wamama zao wangefurahi zaidi kama wangukuwa madocto r mapilot
mj. .. lakini haikutokea hivyo ...
 
Mimi ninachokiona hapa, kuna misimamo mitatu:
Msimamo wa kwanza wa kidini, kama alivyosema mtoa mada, tunachagua madhambi, dhambi gani nzuri na dhambi gani mbaya. Watu wa dini zote, turejee tena kwenye AMRI KUMI (na pengine zaidi) za Mungu. Ni ngapi tunazisigina hivi hivi bila kujali. Mfano, dini zote zimekataza zinaa, mbona tunazini? Hivi Mungu atamsamehe anayezini kwa mbele na kumwadhibu anayezini kwa nyuma, au wanaozini wanaume kwa wanawake na kuwaadhibu wanaozini wanaume kwa wanaume/wanawake kwa wanawake?
Msimamo wa pili wa kimaadili, tukubali kuwa mambo ya "gays & lesbians" yalikuwepo tangu enzi za mitume na hakuna hata jamii moja iliyoyakubali. Tafauti ya zamani na sasa ni kuwa mwanzo walifanya siri na sasa wanafanya dhahiri na kujitangaza. Jamii zenye wavumilivu, wanavumiliwa, jamii zisizo wavumilivu, wanakataliwa. Binafsi ninao marafiki wngi wanaume na wanawake na ninawaheshimu. Sio mimi wa kuwahukumu. Silifurahii lakini silipingi.
Msimamo wa tatu wa kiliberali, unafana na ule wa mwanzo na wa pili ambapo kila mtu anachagua kuvumilia au kuchukia aina ya dhambi au tendo. Kwa wengine bia halali lakini gongo haramu; ukahaba dhambi lakini nyumba ndogo haramu; kwa wengine ukahaba halali, lakini ushoga na usagaji haramu; sigara halali lakini bangi haramu. Baadhi ya wakuu wetu wa kijamii, kidini na kisiasa, utawasikia wako mbele kukemea "matendo maovu, ya shetani" hadharani lakini pembeni wanaiba, wanaua, wanazini hata kinyuume ya maumbile, wanasema uongo n.k. Mimi ninachosema, kwa kufuata kauli ya Yesu, "Ikiwa yupo msafi asiye na dhambi awe wa mwanzo kumlengea jiwe mwenye dhambi".
 

nimekuelewa...kwamba tuwapende. yah, kama sehemu ya jamii na wao ni binadamu wanastahili kupendwa. hakuna anayependa mtoto au ndugu yake awe jambazi.
Nimefurahi tu kujua tu kwamba haukubaliani na kitendo chenyewe!
Tatizo langu mimi ninajaribu kufikiri kwa njia ya tofauti,kwamba si vizuri ku-justfy homosexuality kwa sababu tu dhambi nyingine hazikemwei sana. Nadhani dhambi ni dhambi tu haijalishi nani kafanya, au imefanywa wapi.
Labda swala la hapa ni kwanini tunataka kuhalalisha homosexuality??
 
Dahhhh afadhali
tumeelewana soma hapo juu
MAMMAMIA kafafanunua kwa undani
zaidi..
Asantee .
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…