Mapinduzi baridi ndani ya chama kongwe, iliyokuwa CCM Mpya ya mwendazake yafukiwa rasmi

Mapinduzi baridi ndani ya chama kongwe, iliyokuwa CCM Mpya ya mwendazake yafukiwa rasmi

01 April 2022
Dodoma, Tanzania

Abdulrahman kinana - asisitiza Sasa ni mwendo wa haki kwa wote




Makamu Mwenyekiti wa CCM (bara) akazia kuwa Chama kirudishe demokrasia ndani ya chama ili kurudisha ushawishi wa kisiasa.

Hakuna mwenye haki miliki ndani ya CCM, wanachama wakimchagua mtu hakuna kukata majina labda iwepo sababu nzito amesisitiza kanali mstaafu Abdulrahman Kinana .

Abdulrahman Kinana anaendelea haki hiyo siyo tu iishie ndani ya CCM bali iende kwa waTanzania wote hata wale walio nje ya CCM na ndiyo haki na demokrasia halisi asisitiza kada mkongwe wa chama ambacho kilikuwa kimebatizwa chama dola kutokana na kukosa ushawishi wa kisiasa mbele ya waTanzania.
 
01 April 2022
Dodoma, Tanzania

Abdulrahman kinana - asisitiza Sasa ni mwendo wa haki kwa wote




Chama kirudishe demokrasia ndani ya chama ili kurudisha ushawishi wa kisiasa.

Hakuna mwenye haki miliki ndani ya CCM, wanachama wajimchagua mtu hakuna kukata majina labda iwepo sababu nzito amesisitiza kanali mstaafu Abdulrahman Kinana .

Abdulrahman Kinana anaendelea haki hiyo siyo tu iishie ndani ya CCM bali iende kwa waTanzania wote hata wale walio nje ya CCM na ndiyo haki na demokrasia halisi asisitiza kada mkongwe wa chama ambacho kilikuwa kimebatizwa chama dola kutokana na kukosa ushawishi wa kisiasa mbele ya waTanzania.


Haiki ipi ya kununua wapiga kura? Ya kuchakuchua? Wakina nani wanaiba kura? Kwa mujibu wa tuhuma tunazo sikia wakati wa michakato ya uchaguzi hapa nchini. Je ni chama au serikali?
 
Tumeanza kuonja asari huyu Mzee anazeeka vibaya labda yeye na wanae huko ndo wanaonja hiyo asari huku kajamba nani maisha magumu kila kitu kimepanda..
 
Tumeanza kuonja asari huyu Mzee anazeeka vibaya labda yeye na wanae huko ndo wanaonja hiyo asari huku kajamba nani maisha magumu kila kitu kimepanda..
Nawaza kama hotuba hii ingetolewa pale barabara ya sita tTanga hali ingekuwaje!
 
Mwenyekiti aangalie tu asije akawekwa kwenye siti ya mbele katika mapambano vitani kama Mzee Makamva alivyo tuhadithia ya huko Kagera, akashangalia akifikiri ni kuheshimiwa kumbe kafanywa "an easy target and a shield from a sniper's short.

Kwa kauli hii ya "serikali inatumwa na CCM" Nina pata mashaka inaweza kufanya Rais wa nchi akawa ni Makamu Mkt wa CCM bara ama anaye mtuma. Sijui ushawishi wa hawa...Mh Rais SSH, Makamu Mkt CCM upande wa Visiwani, KM, Mh Rais Mwinyi jR., kama kati yao yuko anaye mshinda/mzidi Mzee Kinana umaarufu na ushawishi ndani na nje ya CCM.

Wahusika mliangalie hilo kwa umakini na mchukue hatua madhubuti. Bila kufanya hivyo Tanzania itakuwa na Rais ambaye si Rais ie Rais wa Makaratasi na kupiga mwikwaju na Rais asiye oneka akawa ndiye anaiongoza nchi. Kwa mabadiliko haya ya CCM ya nafasi ya Makamu mwenyekiti bara Tanzania tunaweza kukutana na kile kule Vatican kiitwacho Black Pope.

Na ndivyo ilivyo ndiyo unaona leo? Hii Nchi inaongozwa Na majeshi
 
TOKA MAKTABA :

TAARIFA YA HALI YA KISIASA YA CCM MPYA 2021


16 Juni 2021

CCM Asilia ikitaka kurejesha utengamano nchini, inabidi itambue CCM Mpya ilivyokengeuka na ijisahihishe. Ili kurejesha imani kwa waTanzania inapata kuelewa haya yafuatayo :



Katika vyama vyote vya siasa vilivyosajiliwa Tanzania kwa muda huu 2021, CCM ni chama dhaifu kupita vyote hata cha CHAUMA chini ya mwenyekiti mzee Hashim Rungwe ni chama thabiti kuliko CCM.



Sababu ni kuwa mwendazake baada ya kuua mihimili ya dola, mahakama na bunge akamalizia kukimaliza chama kilichomweka madarakani. Muda huu CCM haina Mwenyekiti wa Taifa wala Katibu Mkuu wa chama.



Hali hii imefikiwa kwa vile CCM ilishindwa kumdhibiti mwendazake kufanya mambo yake ya kuwaondoa vigogo tishio ndani ya CCM na kuleta "wageni" na kuwazawadia vyeo kwa sharti wamuimbie mapambio anayopenda kusikia.



Kina Bashiru Ally Kakurwa, Humphrey Polepole ni aina ya viongozi ambao viongozi walikuwa hawawezi kumuambia chochote Mwenyekiti ambacho wao wanaamini kinyume na kama kina Nape Nnauye , January Makamba na hata wazee kama Yusuf Makamba, Abdulrahman Kinana.



Tukija katika dola, mwendazake aliiyumbisha na kuivuruga kabisa mfumo wa utumishi serikalini yaani civil service. Aliwachukua watu wasio na ujuzi wa utumishi serikalini na kuwapachika vyeo vya u DED, Makatibu Wakuu na kujaribu kuhitimisha pigo kuu la kuua utumishi serikalini kwa kumuapisha Dr. Bashiru Ally Kakurwa kama Katibu Mkuu Kiongozi ambaye ktk historia ndiye Katibu Mkuu aliyekuwa hana uzoefu kabisa ktk utumishi wa serikali kuu.



Tukija katika mhimili wa Mahakama tuliona alivyouburuza na kuwapa vyeo vya ujaji kwa vigezo dhaifu mfano kuandika hukumu kwa kiSwahili huku kesi hiyo ikiwa ni nyepesi mno.



Bunge pia lilipelekeshwa kwa Spika kuelekezwa kuwashughulikia wabunge wake kwa kuwatoa nje ili waje kushughulikiwa na mwendazake nje ya Bunge. Wabunge wa CCM pia hawakuepuka kipigo cha kisiasa toka kwa mwendazake, ktk kuelekea uchaguzi wa 2020 walishughulikiwa na 'wajumbe' na kama waliweza kupenya walikutana na rungu la Mwenyekiti wa CCM.



Vyeo katika ngazi za uwaziri tumeona waliojiunga mwishoni ktk CCM toka vyama mbadala walitunikiwa vyeo huku wale waliokulia ktk UVCCM na Jumuiya za CCM toka utotoni wakiambulia kuwa backbenchers. Yote hii ilikuwa kuonesha CCM imekufa na sasa mtu mmoja ndiyo kila kitu hivyo wasifurukute au kuwashwa kuhoji au kutoa mawazo mbadala.



Tanzania ilikuwa inaelekea kubaya, lakini kama uzi huu ulivyotabiri wa mwana JF Mvuv, inaonekana ndani ya CCM ndiyo kulikuwa na fukuto kubwa la kutokubaliana na kinachoendelea na sasa tunasikia baada ya mwendazake kuondoka, wabunge wa CCM na SPIKA mwanaCCM wanaanza kutoa maoni ambayo yanaonekana na waimba pambio wa mwendazake kuwa ni unafiki.



Ili kuirejesha Tanzania katika mstari wa haki ikiwemo na CCM yenyewe Asilia kuweza kuaminika kusimamia haki na katiba ya nchi, Tume ya Kijaji lazima iundwe.



Tume ya KiJaji ipewe hadidu rejea Kuchunguza ukiukwaji mkubwa wa katiba, haki za binadamu na ukatili uliotendeka ktk utawala wa CCM iliyojiita CCM Mpya


Updates 21 March 2022

CCM KATIKA HARAKATI ZA MWENDELEZO WA JITIHADA ZA KUJIVUA GAMBA LA CHAMA-DOLA

Kikosi kazi chasema Tume sio huru​


JUMATATU , 21ST MAR , 2022
NA MWANDISHI WETU
Mwenyekiti wa Kikosi kazi cha kuratibu maoni ya wadau wa demokrasia ya vyama vingi nchini Profesa Mukandala, amesema kuwa tume zote mbili za uchaguzi siyo huru na kwamba wapo baadhi ya watendaji katika tume hizo ambao wanavunja sheria za uchaguzi.



MUKANDALA.jpg

Profesa Rwekaza Mukandala, Mwenyekiti wa Kikosi kazi cha kuratibu maoni ya wadau wa demokrasia ya vyama vingi nchini.
Profesa Mukandala ameyasema hayo hii leo Machi 21, 2022 wakati kikosi kazi kuratibu maoni ya wadau wa demokrasia ya vyama vingi ilipokutana na Rais Samia Suluhu Hassan ili kumkabidhi taarifa ya kikosi kazi hicho.

Profesa Mukandala amemshukuru Mhe Rais kwa kukubali kukutana nao ili wamkabidhi ripoti hiyo.
Aidha, Profesa Mukandala ameongeza kwamba wamebaini kuwa uchaguzi wa serikali za mitaa unakuwa mgumu kwasababu unasimamiwa na Ofisi ya Rais TAMISEMI jambo linalowapelekea baadhi ya wananchi walioandikishwa kupiga kura kutoshiriki kikamilifu na hata kutokupiga kura kabisa, na kwamba kuna haja ya kufanyia marekebisho sheria ya uchaguzi na vyama vya siasa.

Kikosi kazi hicho pia kimepenmdekeza kwamba kuna ulazima wa Tume Ya Uchaguzi kufanyiwa tathimini, lakini pia ufanyike ubainifu kisha mapendekezo ya namna bora ya kuwa na Tume Huru Ya Uchaguzi katika nchi yetu.

Profesa Mukandala amesema kuwa kikosi kazi hicho kimebaini kuwa mchakato wa katiba mpya uliacha baadhi ya mambo ya msingi katika Katiba pendekezwa.

Lakini pia kikosi kazi kimependekeza kuwa hakuna haja ya kuwa na katiba mpa kwani katiba iliyopo inaweza kufanyiwa marekebisho


 
https://www.dw.com › ccm-kutathm...
CCM kutathmini marekebisho ya enzi za Hayati Magufuli - DW

16 hours ago — Mkutano mkuu maalum wa chama kinachotawala nchini Tanzania, CCM, unafanyika jijini Dodoma. ... Tarehe 01.04.2022; Mwandishi...Pamoja na mambo mengine ajenda kuu itakayotawala mkutano huo ni pamoja na marekebisho yaliyofanywa wakati wa uongozi wa Hayati John Magufuli aliyewaondoa makatibu wakuu wa mikoa kuingia katika vikao vya Halmashauri kuu kwa kile kilichoelezwa kupunguza gharama....



01 Aprili 2022
Dodoma, Tanzania

Rais Samia ataka chama cha CCM kuendana na mabadiliko​


1648863652804.png


MWENYEKITI wa Chama cha Mapinduzi CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa mabadiliko yaliofanyika katika Katiba ya Chama yanalenga kwenda sambamba na kufuata mifumo ya kisiasa katika dunia.

Rais Samia ametoa kauli hiyo leo April 1, 2022 wakati akitoa hotuba yake kwa wajumbe wa mkutano mkuu maalum wa Chama cha Mapinduzi uliofanyika Jijini Dodoma.

Rais Samia amesema kuwa wamelazimika kubadili katiba hiyo ya mwaka 1977 kwa dhamira ya kukifanya Chama chenye nguvu nchini Tanzania na chenye kufuata siasa za kimataifa badala ya kungangania kubakia katika mfumo wa sasa ambao umepitwa na mazingira ya kisasa ya siasa.

‘Mwaka huu 2022 ni mwaka wa uchaguzi ndani ya CCM na hawawezi kubakia walipo sasa na ni vyema kamati za siasa zianze kujipanga kuona uchaguzi unakuwa wa uhuru na haki na sio kuwekeana visasi.’

”Mabadiliko hayo yanakusudia kuongeza ufanisi wa kazi za chama na sio kubakia walipo sasa, kwani wamerudisha mfuko wa kuwashirikisha Makatibu Wakuu kwenye Vikao vya Halmashauri kuu ili waweze kufuata maelekezo ya Chama yanapotolewa na sio wasubiri washushiwe.”amesema Rais Samia

Pia amesema kuwa malengo mengine ni kwa ajili ya kutafuta njia za kusimamia vyema mfumo wa serikali za mitaa kwani kumeonesha kuna kasoro katika kusimamia miradi ya chama katika ilani yake.
 
Ijumaa April 1, 2022
Dodoma, Tanzania


ABDULRAHMAN KINANA ATAKA KUIMARISHWA HAKI NDANI YA CCM ILI HAKI PIA ITENDEKE NJE YA CCM


IMG-20220401-WA0049.jpg
Abdulrahman Kinana akihutubia mkutano maalum wa CCM leo mjini Dodoma .

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Samia Suluhu Hassan ameongoza kikao Cha Mkutano Mkuu maalum ambacho kimemchagua wa asilimia 100 kanali mstaafu Abdulrahaman Kinana kuwa Makamu Mwenyekiti wa Chama hicho Bara.

Mkutano huo ambao uliwakusanya wajumbe na viongozi mbalimbali wastaafu wa Chama na Serikali umepitisha mapendekezo ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa kuhusu marekebisho ya katiba ya chama hicho ya mwaka 1977 toleo la 2020

Akiongea kwenye Mkutano huo uliofanyika jana Jijini Dodoma Rais Samia Suluhu Hassan amesema ataendelea kutenda haki kwa kila mwanachama ili kuinua zaidi haki na maendeleo .

Akiongea mara baada ya kuchaguliwa leo, Makamu Mwenyekiti was CCM Abdulrahman Kinana alimshukuru Mwenyekiti wa CCM taifa Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kumpa imani kubwa ya kumtaka kufanya tena shughuli za chama .

“Juzi uliniita nikawa najiulia nimeitiwa nini, nikajua ni katika kusalimiana. Rais akaniambia nataka uwe Makamu Mwenyekiti, nikamwambia sina hiari, sina budi kukubali, napenda kukuhakikishia Mwenyekiti nitajitahidi kadri ya uwezo wangu kufikia matarajio yako,niseme sitokuangusha”

Kinana pia amemshukuru Kamati Kuu kwa kupitisha jina lake, pamoja na wajumbe wa Halmashauri kuu kwa kupitisha na kuidhinisha jina lake na kusema wamempa imani kubwa na kwamba amejifunza mengi kutoka kwao.

“Kama mzee Philip Mangula asingeamua kustaafu, basi leo nisingekuwa Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi”

Makamu Mwenyekiti anayechukua hatamu toka kwa Philip Mangula amewashukuru Wenyekiti wote kuanzia Baba wa Taifa mpaka sasa Rais Samia Suluhu Hassan .

Kadhalika ametumia nafasi hiyo kuahidi kwenda kusimamia Chama kuwa imara kidemokrasia na kusimamia haki ya kuchaguliwa bila upendeleo na haki.

"Tukiweza kuimarisha haki ndani ya CCM, tutaweza kuimarisha haki nje ya CCM na kwa waTanzania wote "amesema Kinana .

Makamu mwenyekiti (bara) mpya ameeleza kuwa Tanzania ni nchi inayosimamia na kutetea haki hivyo lazima kusimamia haki na kuikataa dhuluma

"Lazima tutambue kuwa CCM sio mali ya Serikali japo serikali hizi mbili ya muungano na ile ya Zanzibar zinatokana na CCM, lakini pia hatupokei maelekezo kutoka Serikalini ila serikali inaelekezwa na sisi,"amefafanua na kuongeza kuwa "Serikali isithubutu kutunyanganya hiyo haki kila mwana CCM ana wajibu wa kuitetea serikali lakini inapovunja sheria tuna haki ya kuongea, tusiseme kwa kukejeli wala kufoka tuna vikao vya Chama, tutawaelekeza yale yaliyosemwa na ilani , si sawa mwanachama kwenda hadharani kuisema Serikali yake vibaya" amesema Kinana

Licha ya hayo amewataka viongozi wa CCM kuujenga utamaduni wa kuwatembelea wananchi na kuwasikiliza matatazio yao ili waendelee kuwachagua kwa sababu watatambua kuwa wanawajali na kujali shida zao kwa kuzifanyia kazi kwa njia ya kuzitatua changamoto.



"Nina hakika nitapata nafasi ya kutembelea kila mkoa kuzungumza na wanachama kwa niaba ya mwenyekiti wetu kama Katika inavyosema, nakuahidi utumishi uliotukuka sio utukufu wa kujikweza"amesema.

Licha ya hayo amezungumzia masuala yanayokwamisha maendeleo ya nchi na kueleza kuwa kichaka cha ukabila, kichaka cha udini na kichaka cha ubara na visiwani haviendani sawa na chama hicho.

Tunaweza kutofautiana kwa mengine lakini sisi ni wamoja “Lazima wanachama wawe huru kutoa mawazo, hakuna mwenye hakimiliki ya mawazo, lazima tumsikilize kila mwananchi, na wanachama wakimchagua mtu kwani sisi ni nani wa kupinga” anasema

Amesisitiza kusimamia Demokrasia na kusema ni lazima kusimamia haki.

“Nimekuwa nikimsikia Rais akisisitiza mara zote katika kusimamia haki, nilimsikia akisema vyeti peke yake siyo sifa, vyeti viendane na uadilifu, kukubalika. Nchi hii inajulikana kwa haki ndani na nje ya Nchi”anasema

Awali akimuelezea Kinana kabla ya zoezi la kupiga kura mmoja wa makada wa chama hicho na aliyewahi kushika nafasi za juu katika awamu mbalimbali kwenye serikali ya chama cha CCM, Steven Wasira amesema kuwa Kinana anazo sifa za kuwa makamu mwenyekiti wa CCM kutokana na mambo makubwa aliyoyafanya ndani ya serikali na chama kwa ujumla hususani wakati chama hicho kilipopoteza mvuto na kukabiliwa na upinzani mkali kutoka vyama vya siasa mnamo mwaka 2012.

AJENDA ZA MKUTANO

Moja ya ajenda Kuu za mkutano mkuu maalum wa chama Cha Mapinduzi (CCM) ni pamoja na marekebisho yaliyofanywa wakati wa uongozi wa Hayati John Pombe Joseph Magufuli aliyewaondoa makatibu wakuu wa mikoa kuingia katika vikao vya Halmashauri kuu kwa kile kilichoelezwa kupunguza gharama.

Aidha ajenda kuu ya mkutano huo maalumu ilikuwa ni kuiidhinisha jina la kada wa chama hicho Abdulraham Kinana lililopitishwa na Kamati kuu ya CCM na hatimaye kupigiwa kura ya ndio na wajumbe wa mkutano mkuu huo maalumu, ambao mbali na ajenda hiyo pia mkutano huo ulifanya marekebisho ya vifungu na kanuni katika katiba yake ikiwa ni pamoja na sehemu ya nane ya marekebisho kwenye ibara ya 91 kifungu kidogo cha kwanza mpaka cha tisa kama anavyoelezea Katibu mkuu wa CCM Daniel Chongolo.
 
Back
Top Bottom