Mapinduzi Cup 2025 kushirikisha timu za taifa sio vilabu tena, bingwa kuondoka na Tsh. Milioni 100

Mapinduzi Cup 2025 kushirikisha timu za taifa sio vilabu tena, bingwa kuondoka na Tsh. Milioni 100

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Wakuu

ZFF wamekuja na mfumo mpya wa Mapinduzi Cup!

Michuano ya Kombe la Mapinduzi kwa 2025 itashirikisha timu za Taifa na sio vilabu kama ilivyozoeleka ambapo michuano hiyo itachezwa kwa mtindo wa makundi, nusu fainali na fainali itakayopigwa Januari 13, 2025 na mechi zote zitapigwa katika uwanja wa Gombani Pemba huku Bingwa akitarajiwa kutia kibindoni kitita cha Tsh. Milioni 100.
IMG_1429.jpeg
Hayo yameelezwa na Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Zanzibar (ZFF) na Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Mapinduzi Cup 2025, Dkt. Suleiman Mahmoud Jabil na kubainisha kuwa timu zitakazoshiriki ni wenyeji Zanzibar Heroes na Kilimanjaro Stars, Kenya (Harambee Stars), Uganda (The Cranes), Burundi na Burkina Faso.
IMG_1430.jpeg
 
Wakuu

ZFF wamekuja na mfumo mpya wa Mapinduzi Cup!

Michuano ya Kombe la Mapinduzi kwa 2025 itashirikisha timu za Taifa na sio vilabu kama ilivyozoeleka ambapo michuano hiyo itachezwa kwa mtindo wa makundi, nusu fainali na fainali itakayopigwa Januari 13, 2025 na mechi zote zitapigwa katika uwanja wa Gombani Pemba huku Bingwa akitarajiwa kutia kibindoni kitita cha Tsh. Milioni 100.
Hayo yameelezwa na Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Zanzibar (ZFF) na Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Mapinduzi Cup 2025, Dkt. Suleiman Mahmoud Jabil na kubainisha kuwa timu zitakazoshiriki ni wenyeji Zanzibar Heroes na Kilimanjaro Stars, Kenya (Harambee Stars), Uganda (The Cranes), Burundi na Burkina Faso.
Ni vyema mashindano yanakosa maana kuna wahuni wanapeleka vikosi vya watoto bora wangerudisha ligi ya muungano tu!
 
Ni mashindano yasiyo na umuhimu wowote, sidhani Kama cecafa watakubali maana itakuwa hamna tofauti na mashindano ya cecafa.

ZanZibar watafute namna nyingine ya kuendeleza soka lao au waombe kuandaa umiseta.
Au waandae mashindano ya visiwa. Hapo wataipata Comoros, Madagascar, Mauritius, Syshelles, Cuba kama wanacheza mpira na Cape Verde.
 
Hakuna kitu hapo. Hayo ni mashindano tu ya bonanza.
 
Yaani Muda, Bacca na Shekhan washiriki MASHINDANO hayo.? Wamchukue fei toto na wengine.
 
Ni mashindano yasiyo na umuhimu wowote, sidhani Kama cecafa watakubali maana itakuwa hamna tofauti na mashindano ya cecafa.

ZanZibar watafute namna nyingine ya kuendeleza soka lao au waombe kuandaa umiseta.
Mkuu wa Cecafa si Karia we unadhani atawawekea ngumu?
 
Back
Top Bottom