Mapinduzi ya sheria na mifumo ya kodi kwa maendeleo

Mapinduzi ya sheria na mifumo ya kodi kwa maendeleo

mwanamichakato

JF-Expert Member
Joined
Mar 20, 2015
Posts
1,188
Reaction score
1,090
Mamlaka ya Mapato wamekuwa wakijitahidi sana kukusanya mapato (kodi) kwa kutumia mbinu mbalimbali ili kufikia malengo ya mwezi na mwaka. Mpanuko wa mahitaji ya fedha katika nchi umekuwa ukiongezeka kila leo na kila mwaka, hivyo mahitaji ya fedha yamekuwa makubwa hata kupelekea nchi kukopa zaidi. Dawa ya deni ni kulipa. Sasa nchi inalipaje? Kwa kukusanya mapato (kodi) na tozo.

Kwa mujibu wa idadi ya watu katika nchi, takwimu zinaonyesha kwamba wanaolipa kodi ni kundi dogo sana la wafanyabiashara wasiofika milioni 4 kati ya wananchi milioni 60. Hii ni janga na msingi wa umaskini mkubwa wa nchi. Lazima TRA iongeze wigo wa walipa kodi katika nchi. Bado wafanyabiashara wengi wenye vipato hawalipi kabisa kodi. Na ili hili lifanyike, kuna haja kubwa ya kufanyia mfumo na sheria za kodi marekebisho hapa nchini.

Kukamua wafanyabiashara wachache ni kuua uchumi. Wafanyabiashara wadogo na wa kati ndio nguzo ya uchumi wa mataifa yaliyoendelea na yanayoendelea. Zipo taarifa za ukwepaji mkubwa wa kodi za forodha unaofanywa na wafanyabiashara wakubwa wenye kukingwa na vivuli vya viongozi wakubwa. Hii ni kansa kubwa. Tunapoteza mabilioni ya fedha sababu ya upendeleo au uswahiba usio na uzalendo.

Misamaha ya kodi pia inapaswa kufanyiwa marekebisho. Kunapaswa kufanyika ukaguzi maalum kwa maslahi mapana ya Taifa kuhusu misamaha ya kodi. Nchi yetu ni maskini sana kuendelea kutoa misamaha ya kodi isiyo na tija katika kuondoa umaskini ama kuongeza mapato. Na katika hili, mamlaka ya Waziri wa Fedha au viongozi wa kisiasa yapaswa kupunguzwa ili kuondoa ukakasi wa dhamira, nia, na matamanio yenye kuakisi matumizi mabaya ya mamlaka, fursa, na rushwa. Tutazidi kusonga mbele.
 
Viwango vya kodi vishushwe, Ili Kila mtu alipe. Japo hata hivyo hakuna mtu asiyelipa kodi labda kama unaongelea direct tax. Matumizi mabaya ya fedha za umma kupitia viongozi wa serekali, ni sehemu inayofanya kodi inayolipwa kutokukidhi mahitaji halisi ya nchi.
 
Mamlaka ya Mapato wamekuwa wakijitahidi sana kukusanya mapato (Kodi)kwa kutumia mbinu mbalimbali ili kufikia malengo ya mwezi na mwaka..

Mpanuko wa mahitaji ya fedha ktk nchi yamekuwa yakiongezeka kila leo,kila mwaka hivyo mahitaji ya fedha kuwa makubwa hata kupelekea nchi kukopa haswaa..Dawa ya deni ni kulipa..Sasa nchi inalipaje?..Kwa kukusanya mapato (Kodi)..Tozo..

Kwa mujibu wa idadi ya watu ktk nchi takwimu zinaonyesha wanaolipa kodi ni kundi dogo sana la wafanyabiashara wasiofika Milioni 4 nje ya wananchi milioni 60..Hii ni disaster na base ya umaskini mkubwa wa nchi.

Lazima TRA waongeze wigo wa walipa kodi ktk nchi..Bado wafanyabiashara wengi wenye vipato hawalipi kabisa kodi..Na ili lifanyike kuna haja kubwa ya kufumua mfumo na sheria za kodi hapa nchini..

Kukamua wafanyabiashara wachache ni kuua uchumi..Wafanyabiashara wadogo na wa kati ndio nguzo ya uchumi wa mataifa yalioendelea na yanayoendelea..

Zipo taarifa za ukwepaji mkubwa wa kodi za forodha unaofanywa na wafanyabiashara wakubwa wenye kukingwa na vivuli vya viongozi wakubwa..Hii ni kansa kubwa..Tunapoteza mabilioni ya fedha sababu ya upendeleo au uswahiba usio na uzalendo..

Misamaha ya kodi,hili nalo lapaswa kufumuliwa..kunapaswa kufanyika special audit kwa maslahi mapana ya Taifa juu ya misamaha ya kodi..Nchi yetu ni maskini mnoo kuendelea kutoa misamaha ya kodi isiyo na tija ktk kuondoa umaskini ama kuongeza mapato..Na ktk hili Mamlaka ya Waziri wa Fedha au viongozi wa kisiasa yapunguzwe kuondoa ukakasi wa dhamira,nia na matamanio yenye kuakisi matumizi mabaya ya mamlaka,Fulsa na Rushwa.

Tutaendelea
Mkuu kwanza nikupongeze kwa andiko lako hili. Umejaribu kuchambua vizuri na nafikiri kama waziri na TRA watapita humu kuna kitu watakiona. Kodi ndiyo msingi wa maendeleo na ndiyo chanzo na mfuko wa serikali. Hata mikopo inayokopwa mwisho wa siku inalipwa kwa kupitia kodi tunazolipa. Kukopa ni kwa sababu kodi inalipwa kidogokidogo na mahitaji hayasubiri mpaka mwisho wa mwaka.Tukirudi kwenye andiko lako ni kweli malalamiko ya kodi yapo ila nachokiona ni watu wachache kulipa kodi na wengi kuona kama ni ujanja kukwepa kulipa. Na inapokuja wenye mamlaka ya kukusanya kulalamikiwa kuwa wanalazimika kufanya audit kuangalia madeni ya waliokwepa kipindi flani. Nimemsikia waziri husika akifafanua juzi kuhusu madeni ya nyuma nampongeza kwa kujitokeza na kulisemea. Kiukweli watanzania wenzangu ukweli unauma ila tunawajibika kulipa kodi kwa ajili ya maendeleo yetu wenyewe. Kwa wanaokumbuka wakati ule ukifika Dodoma kwenda mwanza kulikuwa hakuna lami lakini leo hii nchi hii kwa kiwango kikubwa kimeungwanishwa na lami.Hii maana yake kodi zetu.Sasa fikiria kama wote tukipila kodi kwa wakati na tinayostahili naamini hata viwango vya kodi vitapungua kwa kuwa base itaongezeka.
 
Mkuu kwanza nikupongeze kwa andiko lako hili. Umejaribu kuchambua vizuri na nafikiri kama waziri na TRA watapita humu kuna kitu watakiona. Kodi ndiyo msingi wa maendeleo na ndiyo chanzo na mfuko wa serikali. Hata mikopo inayokopwa mwisho wa siku inalipwa kwa kupitia kodi tunazolipa. Kukopa ni kwa sababu kodi inalipwa kidogokidogo na mahitaji hayasubiri mpaka mwisho wa mwaka.Tukirudi kwenye andiko lako ni kweli malalamiko ya kodi yapo ila nachokiona ni watu wachache kulipa kodi na wengi kuona kama ni ujanja kukwepa kulipa. Na inapokuja wenye mamlaka ya kukusanya kulalamikiwa kuwa wanalazimika kufanya audit kuangalia madeni ya waliokwepa kipindi flani. Nimemsikia waziri husika akifafanua juzi kuhusu madeni ya nyuma nampongeza kwa kujitokeza na kulisemea. Kiukweli watanzania wenzangu ukweli unauma ila tunawajibika kulipa kodi kwa ajili ya maendeleo yetu wenyewe. Kwa wanaokumbuka wakati ule ukifika Dodoma kwenda mwanza kulikuwa hakuna lami lakini leo hii nchi hii kwa kiwango kikubwa kimeungwanishwa na lami.Hii maana yake kodi zetu.Sasa fikiria kama wote tukipila kodi kwa wakati na tinayostahili naamini hata viwango vya kodi vitapungua kwa kuwa base itaongezeka.

Asante kwa mchango wako

Tufike sehemu kodi ziwe rafiki

Kodi ziendane na uhalisia

Kodi zisiwe chachu ya kuua biashara

Kodi zisiwe mateso..

Kodi zisiwe mkuki kwa wanaothubutu kujiajiri

Kodi zisiwe kero

Kodi zisidaiwe kwa mtutu
 
Viwango vya kodi vishushwe, Ili Kila mtu alipe. Japo hata hivyo hakuna mtu asiyelipa kodi labda kama unaongelea direct tax. Matumizi mabaya ya fedha za umma kupitia viongozi wa serekali, ni sehemu inayofanya kodi inayolipwa kutokukidhi mahitaji halisi ya nchi.

Umenena vema

🦋Tupunguze miradi mikubwa na hili liende sambamba na mpango wa maendeleo wa miaka 30;50;100..nchi iendeshwe kwa mipango thabiti ya maendeleo na sio ilani..

🦋Miradi ya maendeleo iendane na uhalisia wa uchumi wa nchi.. Kuna miradi inafanya nchi i safocate..

🦋Tupunguze ukubwa wa Uongozi wa kisiasa..Ukubwa wa Baraza la Mawaziri,Tupunguze ukubwa wa Bunge,Tupunguze Vyeo visivyo na tija..Tupunguze Zaidi Taasisi na mashirika yenye kushabihiana kimajukumu/Dhima..

🦋Tudhibiti wizi,Tufirisi wezi wa mali za umma..

🦋Utendaji wa viongozi wa kisiasa usijikite kwenye kushinda uchaguzi bali kuleta maendeleo yenye tija kwa nchi na taifa..
 
Receive Cordial Greetings from CTI.

As you might be aware TRA has issued several Agency Notices to businesses associated with the freezing of respective bank accounts.

While CTI stands for full compliance of the country’s regulations including tax / fiscal regulations, it does advocate for measures that are business-friendly and facilitate ease of doing business in the country.

CTI in collaboration with other Private Sector Organisations intends to engage TRA and other authorities with a view of coming up with a solution to the prevailing situation. In that regard, we kindly request your cooperation (those of you who have been served with Agency Notices and had their operations disrupted), in sharing with us the necessary information relating to the matter, including the frozen accounts, the tax assessment issued, etc., to enable us to engage positively with the authorities.
 
Receive Cordial Greetings from CTI.

As you might be aware TRA has issued several Agency Notices to businesses associated with the freezing of respective bank accounts.

While CTI stands for full compliance of the country’s regulations including tax / fiscal regulations, it does advocate for measures that are business-friendly and facilitate ease of doing business in the country.

CTI in collaboration with other Private Sector Organisations intends to engage TRA and other authorities with a view of coming up with a solution to the prevailing situation. In that regard, we kindly request your cooperation (those of you who have been served with Agency Notices and had their operations disrupted), in sharing with us the necessary information relating to the matter, including the frozen accounts, the tax assessment issued, etc., to enable us to engage positively with the authorities.

Confederation of Tanzania Industries memo to its members
 
Wafanyabiashara na wenye viwanda wanapaswa kulipa kodi stahili kwa uhai wa Taifa letu.

Kodi zinazolipwa zinapaswa kutumika vema,Kulindwa na kusimamiwa vema na si kufujwa.

Mchakato wa kukusanya kodi stahili unapaswa kufanyika kwa kuzingatia uhalisia wa kibiashara na kulinda mazingira bora ya uendelezaji wa biashara.

Wigo wa walipa kodi bado ni mdogo mnoo ukizingatia idadi ya raia wa nchi ama wanufaika wa matunda husika.

Tunakopa kufadhiri miradi lukuki..Tutalipa,Lazima tulipe..Kwa miaka mingi ijayo..Lazima tukuze shughuri mbalimbali za kiuchumi sasa na baadae..

Hatupaswi kuua biashara kwa msingi wa kukusanya mapato ili kuvunja rekodi..Hatupaswi kunyanyasa wafabiashara na wenye viwanda kwa kivuli cha kufurahisha wanasiasa..Hatupaswi kuziba masikio lundo la biashara likifa kwa sababu ya ukatiri wa maafisa kodi..

Dunia inapita ktk changamoto nyingi za kibiashara kimataifa..Tujifunze na kuchukua hatua stahiki kuchukua hatua stahiki kulinda sekta binafsi na wenye viwanda..

TUACHE:-
UBABE
KIBURI
DHARAU
UKATIRI
 
Back
Top Bottom