Mapinduzi ya Zanzibar na Nyerere

Mapinduzi ya Zanzibar na Nyerere

Hiyo sio main theme ya kitabu.

Anapozungumzia mapinduzi ya Zanzibar amelaumu Tanganyika kwa kutaja hasa Waislam na Wakristo na kulaumu Mirengo ya kisiasa kuchochea mapinduzi

Na kuwalaumu wazungu





Ukisoma hizo page chache ulizoweka ni kwamba kuna lawama dhidi ya Wakristo, kwa kudai eti historia ya mapambano ya uhuru ya Waislamu ilifichwa, hivi kuna haja kila mtu akifanya jambo jema atajwe na dini yake?
 
Wapi nimesema ninaamini yaliyoandikwa kwenye hicho kitabu?

Btw hivi unaamini kweli kuna mtu angeweza kumuuliza Nyerere au Karume kuhusika kwao na mapinduzi?

Na kwa mfano kama Nyerere alihusika unatarajia angeulizwa angekiri?

Soma maelezo yangu nime stick kwa Kambona kwa sababu kitabu ndicho kilichojaribu kuproove kuhusika kwake kwa kutumia watu mbalimbali na documents za kibalozi.

Nyerere amehusishwa by association tu kuwa lazima alijua aliyofanya Kambona (kwa nilivyoelewa)


M
Ndio maana nikasema wangeulizwa akina Nyerere, Okello, Karume na wote waliohusika directly, sio kuacha watangulie mbele ya haki then tunaanza kuambiwa afterthoughts! Well, unaamini inawezekana Okello anadanganya lakini unaamini yaliyoandikwa na ndugu zako, strange indeed!
 
Waislamu huwa hawana jema toka kwa Mkristo hata siku moja, hata kama ukiwalamba nyuma watakudharau tu! Huwezi ukawasikia wanamlalamikia Dikteta Iddi Amin Dada wa Uganda pamoja na maovu yake yote simply kwa sababu alikuwa mwislamu! Similrly kwa magaidi kama akina Osama bin Laden, pamoja na unyama wote wanaofanya, kwao ni mashujaa! Hata hivyo si ajabu kwa sababu asili ya chuki waliyo nayo iko moja kwa moja ndani ya Quran (death manual)!
Mmh! Kweli kabisaa
 
Hiyo sio main theme ya kitabu.

Anapozungumzia mapinduzi ya Zanzibar amelaumu Tanganyika kwa kutaja hasa Waislam na Wakristo na kulaumu Mirengo ya kisiasa kuchochea mapinduzi

Na kuwalaumu wazungu

Kila kilichoandikwa kwenye kitabu kina maana yake ndugu, otherwise yasingeandikwa! Kama sio main theme basi ni sub-theme na ina maana yake, pia inatoa clue kwa mwandishi kwamba ni mtu wa aina gani!
 
Wapi nimesema ninaamini yaliyoandikwa kwenye hicho kitabu?

Btw hivi unaamini kweli kuna mtu angeweza kumuuliza Nyerere au Karume kuhusika kwao na mapinduzi?

Na kwa mfano kama Nyerere alihusika unatarajia angeulizwa angekiri?

Soma maelezo yangu nime stick kwa Kambona kwa sababu kitabu ndicho kilichojaribu kuproove kuhusika kwake kwa kutumia watu mbalimbali na documents za kibalozi.

Nyerere amehusishwa by association tu kuwa lazima alijua aliyofanya Kambona (kwa nilivyoelewa)


M

Alaaaah, ni hisia kama nilivyosema!
 
Kitu kimoja ambacho ni kizuri kwa kitabu hicho ni kuwa kina maneno yake mwenyewe muandishi machache mno. ( chapters za introduction na conclusion tu)

Karibu ya theluthi mbili ya kitabu ni direct quotes na documents.

Kwa hiyo ni rahisi kupuuza opinion ya muandishi lakini ukajisomea references ambazo ni za kibalozi na direct quotes za wahusika.

Hata kama wazee wa Zanzibar hawaaminiki nafikiri kuna mazungumzo ya mwandishi na rais Wa Algeria na msaidizi wake pia.



Kila kilichoandikwa kwenye kitabu kina maana yake ndugu, otherwise yasingeandikwa! Kama sio main theme basi ni sub-theme na ina maana yake, pia inatoa clue kwa mwandishi kwamba ni mtu wa aina gani!
 
kitabu kinaendelea ...... sura ya kwanza siri nzito


takriban viongozi wote wa chama cha Shirikisho la Wafanyakazi wa Tanganyika (Tanganyika Federation of Labour). Wote walipelekwa kwenye vituo vya polisi kwa kuhojiwa na baadhi yao baadaye waliwachiwa huru. Rais [Nyerere] kwenye hotuba yake ya redio ya jana usiku aliligusiya suala hili na aliongeza kwa kusema kuwa Mkuu wa Wilaya mmoja pia amekamatwa.
Nyerere alitamka kwenye hotuba hiyo ya redio kuwa watu hawa, wa vyama vya wafanyakazi, walikuwa wamekula njama na viongozi wa uasi wa kijeshi "kusababisha mtafuruku zaidi." Kulikuwa na uvumi mwingi wiki iliyopita kuwa vyama vya wafanyakazi vilikuwa vinapanga mgomo wa jumla au angalau mgomo wa wafanyakazi wa gatini na wa reli. Pia inaaminiwa kuwa viongozi kadhaa wa vyama vya wafanyakazi walikuwa wakipitisha wakati wao mwingi kwenye kambi ya kijeshi ya Colito.14
Msomaji anaombwa baadaye aunganishe mchango wa vyama vya wafanyakazi katika mapinduzi ya Zanzibar ya tarehe 12 Januari 1964 na uasi wa jeshi la Tanganyika wa tarehe 20 Januari 1964.
Waingereza hawakuwacha kuuhusisha uasi wa jeshi la Tanganyika na mchango wa Oscar Kambona ambaye wakati huo alikuwa ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ulinzi. Walimuandikiya makala kwenye ukurasa wa nyuma wa gazeti la Daily Telegraph la tarehe 22 Januari 1964 ambayo ilimuudhi sana Kambona. Balozi wa Kiiengereza aliyekuwepo Dar es Salaam alielezeya kwenye barua yake aliyompelekea Bwana W.G. Lamarque wa Commonwealth Relations Office, Downing Street, London, kuwa "Stephen Miles alipokutana na Rais [Nyerere] wiki iliyopita waligusiya kuwa Kambona alikuwa kiongozi wa uasi wa kijeshi, na Rais, kama unavyojuwa, alimwambiya Oscar kuwa ‘Masikini Oscar, maisha yeye ndiye mwenye kulaumiwa.' Kwa kusema kweli, Oscar alikasirishwa sana alipozisikiya habari hizo na akaanguwa kilio na ikabidi apewe siku moja nzima ya mapumziko."15
Waingereza walimtiliya shaka sana Kambona kuwa alikuwa amehusika na uasi wa jeshi la Tanganyika kwa kuzingatiya kuwa katika siku mbili za kwanza za uasi, Kambona alikuwa akitangaza kwenye redio kila baada ya nusu saa na kuwa alikuwa tayari achukuwe khatamu za serikali na ajitangaze kuwa ni Rais lakini aliogopa dakika za mwisho. Pia walilalama kwa kusema "Lazima iulizwe kwanini ulinzi wa ndani wa Tanganyika dhidi ya tukio kama la uasi wa jeshi ukawa dhaifu namna hii. Hapana shaka kukosekana kwa taarifa kutoka vyombo vya usalama kuipa serikali kumetokana na Kambona na [Job] Lusinde kulibomowa Tawi la Usalama na badala yake kuwaweka watu wa T.A.N.U. aliowachaguwa Kambona."16 Licha ya kuwa hawakuwa na taarifa za kiusalama watawala wa Kiingereza waliamuwa kupeleka jeshi la Makamandoo kurudisha amani na utulivu Tanganyika na kumrudisha kitini Mwalimu Nyerere.
Na Zanzibar ikapinduliwa, mauwaji ya halaiki yakafanywa, na Bwana Adrian Forsyth-Thompson aliyekuwa Permanent Secretary katika ofisi ya Waziri Mkuu
Siri Nzito 7
Bwana Mohammed Shamte akaondoka Zanzibar tarehe 8 Februari 1964, na alitarajiwa kuondoka Nairobi kuelekeya Cape Town, Afrika Kusini, tarehe 11 Februari 1964. Baba yake Adrian alikuwa ni ofisa katika serikali ya kikoloni ya Kiingereza na alistaafu Cape Town. Adrian aliondoka Cape Town tarehe 18 Machi kwenda kwenye kazi yake mpya katika visiwa vya Seychelles.
Forsyth-Thompson alikuwa ni ofisa wa usalama kwenye ofisi ya Balozi wa Kiingereza Zanzibar na punde tu kabla ya mapinduzi alikabidhiwa kazi na Katibu Mkuu wa Kiingereza, Bwana Mervyn Vice Smithyman, katika ofisi ya Waziri Mkuu Bwana Mohammed Shamte kuleta mabadiliko katika vyombo vya usalama vya Zanzibar. Alipokuwapo Nairobi na tayari kuondoka kwenda Cape Town, Forsyth-Thompson alitowa ripoti muhimu ambayo ilipelekwa Commonwealth Relations Office, London kwa njia ya telegram na kopi zikapelekwa ubalozi wa Kiingereza Dar es Salaam, Aden, Kampala, Washington na Cape Town. Ujumbe huo ulikuwa ni mfupi ukiufananisha na ripoti yake yenye kurasa nane aliyoiandika alipokuwa Nairobi tarehe 10 Februari 1964.
Kwenye ripoti fupi aliyoitowa Nairobi na iliyopelekwa London na Washington, Forsyth-Thompson aliziwasilisha nukta tano lakini hapa tutainukuu nukta ya kwanza na nukta ya nne:
1) Hakuna (rudia hakuna) ushahidi wa mkono kutoka nje katika mapinduzi ambayo yalikuwa ni mapinduzi ya Afro-Shirazi Youth League dhidi ya siasa ya Kiarabu ya Serikali iliyokuwepo, na mapinduzi yalifanywa katika kipindi ambacho viongozi wa ASYL na washabiki wao wakiamini patatokeya ukamataji wa viongozi wakati wowote. Babu alichupiya, na Karume (? Alichaguliwa) na wanamapinduzi kuwa ndiye kiongozi anayejulikana na Okello alichomoza tu.
4) Kwa mtizamo wa mbali mustakbal wa Zanzibar umo katika uhusiano wa karibu na maeneo ya bara ikiwa ndani ya Shirikisho au kuunganishwa na Tanganyika. Hili litafanyika kwa urahisi ikiwa Tanganyika au Kenya watakuwa tayari kupeleka vikosi vya polisi (kwa mfano kikosi cha huduma) kutokana na ombi la Karume ambaye atakubali kutokana na hali ya mambo ilivyo ikiwa Watanganyika na Wakenya watampa ishara kuwa wako tayari.17
Kwenye ripoti yake ya kurasa nane, Forsyth-Thompson anaelezeya kuwa:
Umma Party na viongozi wa ASP wenye mitizamo isiyo mikali hawakujuwa chochote [kuhusu mapinduzi]. Saleh Saadalla labda akijuwa…Alkhamisi tarehe 9 [ASYL] walisikiya kuwa mzigo wa meli wa silaha kutoka Algeria ulikuwa utaletwa na Serikali…Hadithi za silaha kutoka Algeria zilikuwa zimezagaa kwenye wiki baada ya mapinduzi: na kwa hakika ulikuwa ni upuuzi mtupu.18
Kuhusu mapinduzi yenyewe, anaelezeya Forsyth-Thompson, "yalipangwa na kutekelezwa ndani ya muda mfupi na hii ni dalili ya kukosekana kabisa taarifa
8 Mlango wa Kwanza
zozote kutoka kitengo cha usalama (Special Branch) kuwa kulikuwa na mpango. Kwa muda mrefu kulikuwa na mazungumzo ya kufanya fujo, lakini hakukuwa na pendekezo la mpango wa kuipinduwa Serikali kwa kutumiya nguvu."19
Kamati ya Ukombozi wa Afrika
Mkutano wa nchi huru za Kiafrika uliofanyika Addis Ababa mwezi wa Mei 1963 uliunda Kamati ya Ukombozi wa nchi tisa yenye makao makuu Dar es Salaam. Nchi zilizounda kamati hiyo zilikuwa Tanganyika, Nigeria, Uganda, Algeria, Umoja wa Jamhuri ya Kiarabu (U.A.R.), Guinea, Senegal, Ethiopia na Kongo. Ghana haikuwemo.
Nyerere hakupendeleya makao makuu ya Kamati ya Ukombozi ichukuliwe na Ghana, U.A.R. au Algeria. "Alikhofiya kuwa kati ya nchi hizo Kamati ingelitumiliwa na Rais wa Dola kujijengeya sifa, na mtizamo wa kamati ungelikuwa juu ya utumiaji nguvu badala ya shinikizo la amani."20
Baada ya uchaguzi wa mwisho wa Zanzibar wa kabla ya mapinduzi wa tarehe 8 Julai 1963, Mwalimu Nyerere alifanya ziara ya Marekani na alionana na Rais John F. Kennedy, na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa U Thant. Pia aliitembeleya nchi ya Canada kwa muda mfupi na alikuwa na mazungumzo na Waziri Mkuu wa nchi hiyo, Bwana Lester Pearson. Tarehe 21–25 Julai alikuwa mgeni wa Serikali ya Uingereza. Mwalimu na ujumbe wake uliondoka London siku ya Alkhamisi tarehe 25 Julai kuelekeya Algiers, mji mkuu wa Algeria.
Katika msafara wa Rais Nyerere walikuwemo:
Rais Nyerere
Bwana Oscar Kambona, Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje na Ulinzi
Bwana I. M. Bhoke Munanka (Waziri Mdogo, Ofisi ya Makamo wa Rais)
Bwana A. B. C. Danieli (Katibu Msaidizi, Mambo ya Nje)
Bwana G. Rockey (Katibu wa Habari)
Bwana F. Sangu (A.D.C.)
Bwana P. Mwinbo (Mkuu wa Maofisa Wafanyakazi)
Bwana J. M. Simba (Katibu Khasa wa Rais)
Bwana U. Nyondo (Ofisa Mfanyakazi wa Rais)
Bwana K. Kondo (Ofisa Mfanyakazi wa Bwana Kambona)
Ziara rasmi ya Rais Nyerere na msafara wake nchini Algeria ilikuwa kuanziya tarehe 25 mpaka tarehe 28 Julai. Inavyoonesha Ubalozi wa Kiingereza mjini Algiers hakuambuliya kitu chochote cha maana kati ya mazungumzo ya Rais Nyerere na Ahmed Ben Bella, Waziri Mkuu wa Algeria na baadaye Rais wa nchi hiyo.
Katika mwezi huohuo wa Julai 1963 Waingereza walikuwa wameshazipata
Siri Nzito 9
habari kutoka jeshi la Tanganyika kuwa kulikuwa na silaha zikitarajiwa kutoka Algeria. Baina ya mwezi wa Agosti na Septemba 1963 listi ya silaha ilionekana Wizara ya Ulinzi. Halafu kimya mpaka wiki ya kwanza ya Januari 1964.21
Tarehe 2 Januari 1964, meli iliyopewa jina la mwanafalsa maarufu duniani wa historia, MV Ibn Khaldun kutoka nchi ya Kiarabu ya Afrika ya Kaskazini ya Algeria, ilitia nanga Dar es Salaam huku ikibeba shehena ya silaha zilokusudiwa kupelekwa Msumbiji na kwa ajili ya mapinduzi ya Zanzibar. MV Ibn Khaldun haikuwa Sultana iliotiya nanga New York Alkhamisi, tarehe 30 Aprili mwaka 1840 na iliyobeba ujumbe wa amani na biashara kutoka Zanzibar kwa Sultan Sayyid Said bin Sultan.
Meli ya MV Ibn Khaldun ilikuwepo Dar es Salaam kwa siku nane, kuanziya tarehe 2 Januari 1964 na iliondoka tarehe 9 Januari 1964. Ilipowasili mara ya kwanza meli hiyo "ilikaa nje ya bandari ya Dar es Salaam kwa muda wa masaa arubaini na nane. Kutokana na kuhojiwa kwa maofisa wa Kiafrika waliohusika na upakuwaji wa mizigo ya meli ilikuwa dhahiri baadhi ya mizigo iliondolewa na inawezekana sana kuwa baadhi yake iliondolewa kabla ya meli kufunga gati."22 Rais Nyerere aliongozana na Bwana Djoudi aliyekuwa Charge d'Affaires katika Ubalozi wa Algeria Tanganyika katika kuikaguwa meli hiyo. Djoudi pia alikuwa mhusika wa mafunzo ya kijeshi wa Kamati ya Ukombozi wa nchi tisa za Kiafrika. Kijana mdogo mwenye umri wa miaka 24 aitwaye Racchid Ben-Yelles alikuwa Kepteni wa meli hiyo ya MV Ibn Khaldun.
Kepteni Ben-Yelles alitowa maelezo kuwa meli hiyo ambayo alichukuwa dhamana ya kuiyendesha miezi mitatu nyuma ilikuwa kwa kawaida yake ikifanya kazi kwenye Bahari ya Mediterranean. Mzigo wa kawaida wa meli hiyo ulikuwa ni ulevi wa zabibu na meli hiyo ambayo ikimilikiwa na Serikali ilikuwa na matenki yenye uwezo wa kubeba tani 2,000. Meli ilipoondoka, Rais Nyerere aliwapungiya mkono kepteni na wafanyakazi wake na kuwaombeya safari njema. Wakati inaondoka meli hiyo ilikuwa imebeba shehena ya tani 80 za kahawa na tani 100 za mbao kutoka Tanganyika na ilielekeya Tanga kuongeza mizigo zaidi.23
Kwa mujibu wa ripoti ambayo haiyoneshi imetoka kwa nani na inakwenda kwa nani, Serikali ya Tanganyika iliwalipa Waalgeria "thamani ya pauni za Kiingereza 260,000 za kahawa na bidhaa nyengine."24 Wapi pesa hizo zilitoka bado ni suala la michirizi yake kufuatiliwa. La muhimu ni kahawa na mbao yalikuwa ni malipo kwa ajili ya silaha zilizoletwa kutoka Algeria na meli ya Ibn Khaldun. Kwa amri ya Oscar Kambona, kazi ya upakuwaji wa mizigo ya silaha hizo alipewa Kepteni Nyerenda na aliamrishwa mzigo wote wa silaha auweke kunako ghala za P.W.D. (Public Works Department).25
Huo ulikuwa ni wakati wa uanzishaji wa harakati za ukombozi wa Msumbiji na baadaye kuanzishwa kambi za kuwapa mafunzo wapiganiya uhuru wa Msumbiji Tanganyika. Oscar Kambona aliwababaisha waandishi wa habari kwa kuwaambiya kuwa silaha kutoka Algeria zilikuwa kwa ajili ya Tanganyika
10 Mlango wa Kwanza
Rifles lakini Waingereza walipotaka taarifa zaidi kutoka kwake aliwajibu kuwa "…ni za Tanganyika Rifles isipokuwa maboxi yaliopigwa krosi nyeusi. Maboxi haya yanatakiwa yawekwe karibu na mlango wa ghala ili yaweze kuondolewa kwa haraka. Pia alisema kuwa maboxi hayo yasifunguliwe. Tuliyafunguwa baadhi yake…Zanzibar ilitokeya Jumapili iliyofuatiliya, tarehe 12 Januari na maboxi yale bado yalikuwepo kunako ghala. Baada ya hapo yakawa hayana umuhimu wowote."26
 
Kitu kimoja ambacho ni kizuri kwa kitabu hicho ni kuwa kina maneno yake mwenyewe muandishi machache mno. ( chapters za introduction na conclusion tu)

Karibu ya theluthi mbili ya kitabu ni direct quotes na documents.

Kwa hiyo ni rahisi kupuuza opinion ya muandishi lakini ukajisomea references ambazo ni za kibalozi na direct quotes za wahusika.

Hata kama wazee wa Zanzibar hawaaminiki nafikiri kuna mazungumzo ya mwandishi na rais Wa Algeria na msaidizi wake pia.

Well, na mimi nalenga kwenye opinion yake mwenyewe na pia hizo sources inategemea zimekuwa oriented namna gani ili kuhakikisha anachokiamini kinaeleweka kama anavyotaka yeye na sio kama kilivyo!
 
Okay sir

Well, na mimi nalenga kwenye opinion yake mwenyewe na pia hizo sources inategemea zimekuwa oriented namna gani ili kuhakikisha anachokiamini kinaeleweka kama anavyotaka yeye na sio kama kilivyo!
 
Mlango wa Pili
Mirengo ya Kizalendo na Mapinduzi
Mapinduzi yalikuwa, kwa kiasi fulani ni kisasi dhidi ya utumwa, yaliofanywa na watu na kufanyiwa watu ambao hawahusiki na utumwa. -Yasmin Alibhai-Brown
Fikra ya uzalendo ya Pan-Africanism ambayo ilikuwa ikiongozwa na hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ilikuwa kila asiye "Muafrika" ni mgeni Afrika na kwa hiyo asiyekuwa na asili yenye kutoka bara la Afrika basi ni mgeni Zanzibar hata kama alizaliwa na alikuwa na mizizi mirefu ndani ya nchi hiyo. Na aliyekuwa ana asili ya Kiafrika na hata kama hakuzaliwa na wala hana mizizi mirefu Zanzibar basi ana haki zaidi juu ya kuitawala Zanzibar kwa sababu ni "Muafrika."
Neno "Afrika" linatokana na neno Ifriqiya, ambayo kihistoria ilikuwa ni jimbo la Kaskazini ya Afrika katika nchi ambayo leo inajulikana kwa jina la Tunisia. Ibn Khaldun, mwanafalsafa wa historia maarufu duniani na baba wa sayansi ya jamii (sociology) aliyeishi miaka 676 nyuma, anamtaja katika kitabu chake Mfalme wa zamani wa Yemen Afriqus b. Qays b. Sayfi, ambaye "aliishi wakati wa [Nabii] Musa au labda kidogo kabla yake" na kuwa wanahistoria wanajisemea kuwa ndie alieivamia "Ifriqiyah".1 Ibn Khaldun hakuwa anashuku kuwepo kwa mfalme kutoka Yemen ambaye akijulikana kwa jina la "Afriqus" ambalo inawezekana sana likawa moja wapo wa asili ya jina la "Afrika." Wako wenye kusema neno "Afrika" linatokana na lugha ya kienyeji ya Afrika ya Kaskazini iitwayo "Berber."2 Lini bara la Afrika lilianza kujulikana kwa jina la "Afrika" ni jambo liloanzishwa na wakoloni wa kizungu na ni suala linahohitajia kuthibitishwa kwa ushahidi wa kiutafiti.
Fikra zilizozagaa ni kwamba Zanzibar ni ya Muafrika mweusi mwenye asili ya bara peke yake kuliko Muafrika mwingine yeyote hata kama amezalika huko Zanzibar kwa daraja nyingi. Fikra hii inatokana na fikra nyengine iliyokalishwa kwenye fikra za wengi yakuwa "Bara la Waafrika" ni Bara la watu weusi tu, na
Mlango wa Pili
12
labda tuseme la Mungu Mweusi. Na watu weusi wenyewe ni wanaotokana na asili ya Kibantu na Wabantu wenyewe wawe hawana asili au uhusiano wa karibu na Waarabu.
Na mizizi ya "Waafrika ni Wabantu peke yao" inalitenga kundi kubwa la Waafrika wa Afrika ya Kaskazani, Ethiopia, Somalia, Djibouti, Eritrea, Mauritius, wazungu wa Afrika Kusini, au Zimbabwe, Kenya, pamoja na Mayahudi na Wahindi wazalendo wa Afrika, na makabila yote ya kibinaadamu ambayo yana chimbuko lao Afrika.
Hapana shaka yoyote kuwa Afrika imedhulumiwa na Waafrika weusi bado hawajachukuwa dhamana ya kushiriki kwa machifu na makabila yaliyoshiriki kuwatia utumwani Waafrika wenzao. Haya yameelezwa kwa ufasaha ndani ya kitabu Zanzibar: Kinyang'ayiro na Utumwa na mwaka 2009 kimetoka kitabu muhimu chenye kichwa cha maneno It's Our Turn to Eat (Sasa ni Zamu Yetu Kula) ambacho kinaelezea kwa undani namna ufisadi ulivyokumbatiana na ukabila nchini Kenya.3
Historia yote na kharita (ramani) zenye kulionyesha bara la Afrika kabla halikupewa jina la "Afrika" huonekana kuwa haina maana. Kwa hiyo kharita za miaka ya 1860 na za nyuma sana kabla ya hapo, zenye kuonyesha eneo la Afrika Mashariki kuwa likijulikana kama ni "Ethiopia" au mwambao wa "Azania" au "Sudan" au "Zinjibar" huonekana ni dalili tosha za ushahidi wa ubeberu kabla ya "Waafrika" kujitawala baada ya Wazungu kulipa bara lote jina la "Afrika."
Tawi la uafrika ni mtu mweusi lina mzizi mrefu katika kuyakana makabila mengine ya Kiafrika ambayo yaliwasili mwambao wa Afrika hata kabla ya kuwasili Wabantu Pwani ya Afrika ya Mashariki. Anaelezea Profesa Ibrahim Noor Shariff:
Kuna baadhi ya watu wanafikiri kuwa "Waafrika" wote ni "Wabantu" na kuwa kila asiyekuwa Mbantu ni mgeni Afrika Mashariki. Ukweli ni kuwa "Wabantu" ndio katika waliofika Afrika Mashariki, khasa sehemu za Pwani karibuni kabisa. Kwa mfano, "Wabantu" Wagiriama wamewasili "Giriama" Kenya kama miaka mia tatu iliyopita. (Soma kitabu cha chifu wao R. G. Ngala kiitwacho "Nchi na Desturi za Wagiriama." E. A Literature Bureau. 1949. Ukurasa wa 2).4
`Mohamed Said ni msomi wa kwanza kabisa aliyeweza kuweka mkono wake juu ya mpigo wa moyo wa propaganda ya TANU kuhusu suala la Ubantu na wasio Wabantu, yaani, Waislamu. Kwa mujibu wa Mohamed Said:
Katika mwaka 1955, kikundi cha TANU Bantu kiliundwa makhsusi kukabiliana na tatizo la udini kutokana na hisia za baadhi ya Waislam ndani ya TANU. Tangu kuundwa kwa TANU, kulikuwa na hisia ya kupinga Ukristo ndani ya chama. Tatizo hili la udini lilikuwa likichemka pole pole na chini kwa chini ndani ya TANU.
Ilikuwa kazi ya kikundi cha TANU Bantu kuwafichua na kuwapiga vita wanachama wa TANU waliokuwa na hisia kama hizo. Bantu ilifanikiwa sana katika
Mirengo ya Kizalendo na Mapinduzi
13
hili hadi kudiriki kupiga marufuku mamkuzi ya Waislam ya "Asalaam Alaikum" (Amani iwe juu yako) baina ya Waislam kwa msingi kuwa ilikuwa inawabagua Wakristo na hivyo inawatenga…Mamkuzi yale ya Kiislam yalionekana kama yanakwenda kinyume na imani ya TANU na ilishauriwa kuwa "salaam aleikum" ipigwe marufuku isitumike. Ikiwa mathalan kwa kusahau Muislam mmoja atatoa salaam kwa Muislam mwenzake, kwa kawaida angejibiwa "Alaikum salaam" maana yake "Amani iwe juu yako pia." Badala ya majibu haya mazuri, majibu yaliyobuniwa na Bantu yalikuwa-"Ahlan tabu" maana yake-"ah tabu tu!"5
Lengo la Bantu Pan-Africanism si kuutumikiya uhakika wa historia au kuwapenda Waafrika na kuwachukiya Waarabu, bali ni kulipuuza suala zima la makabila, tamaduni, na staarabu na dini ya Kiisilamu zilizokuwepo Afrika ya Mashariki kabla ya kuwasili kwa Wabantu na khasa kwa Ukristo kutoka Ulaya. Mgeni mmoja kutoka Umoja wa Mataifa aliyekwenda kuitembeleya taasisi ya kihistoria ya kitaifa iliopo Dar es Salaam, alisikitishwa sana kuona historia ya Waarabu Tanzania imeshirikishwa na kitu kimoja tu: utumwa. Wanahistoria na wataalamu wa ilimu ya athari (archaeology) wanashindana na kuukiuka au kuuficha ukweli wowote ule wenye kuonyesha kuwa hakujakuwepo makabila yasiyo ya Kibantu Afrika ya Mashariki kabla ya kuwasili kwa Wabantu.
Ile historia ndefu ya Bahari ya Hindi yenye kuiunganisha Afrika ya Mashariki na ya Kati na Bara Arabu, Uajemi, Bara Hindi, Uchina, Misri, n.k, huwa inaonekana haina maana kwa sababu haikidhi haja na hoja za kisiasa. Au kama itatambulikana itakuwa kujengea hoja kuwa ilikuwa historia ya kibeberu iliyokuwa na kituo chake Zanzibar. Marejeo ya historia ya Afrika ya Mashariki yaliyoandikwa na akina Ibn Battuta, au Muruj al-Dhahab wa Ma'adin al Jawhar cha Al-Masudi, au Kilwa Chronicles iliopo jumba la makumbusho la Uingereza, hayapitiwi na wasomi wengi wa Tanganyika waliojazwa na kujaa chuki dhidi ya makabila mengine yasiyo ya Kibantu ya Afrika ya Mashariki.
Katika utangulizi wa kitabu chao Mapambano ya Ukombozi Zanzibar, B.F. Mrina na W.T. Matokke wa Chuo Kikuu cha Chama, Kivukoni, wanafafanuwa kuwa: "Madhumuni ya kuandika kitabu hiki ni kujaribu kukusanya pamoja data kwa ajili ya kuweza kufundishia. Jitihada zilizofanywa zilikuwa na lengo la kupata maandishi ambayo yanaweza kutumiwa na walimu na wanafunzi katika Vyuo vya Chama Cha Mapinduzi."6
Pia katika sifa iliyopewa kitabu na kampuni ya uchapaji, Tanzania Publishing House, ni hii propaganda bila ya kizoro ambayo nainukuu kwa urefu:
Historia ya Afrika ni hadithi ndefu ya mapambano ya wananchi wake dhidi ya ubeberu ili waishi katika ardhi yao kwa amani na ustawi. Visiwa vya Unguja na Pemba havikukwepa adha ya kuwa sehemu ya uwanja wa mapambano hayo na kwa vizazi vingi vimekuwamo katika harakati moja baada ya nyingine hadi Mapinduzi ya 1964 yaliyokatilia mbali minyonyoro ya ukoloni mkongwe na kuashiria maisha mapya.
14 Mlango wa Pili
Mapambano ya Ukombozi Zanzibar ni kitabu cha kwanza kuchapishwa kinachofuatilia kwa undani safari ndefu ya wananchi wa Zanzibar kuelekea ukombozi tangu majilio ya kwanza ya wageni kwenye pwani ya Afrika Mashariki yapata miaka 2000 sasa….Ndugu Mrina na Ndugu Matokke wamefanya utafiti wa hali ya juu uliowawezesha kutalii sehemu nyingi za historia ya Zanzibar ambazo hazijaguswa na mwandishi mwingine yeyote. Matokeo yake ni kitabu cha lazima kwa wanafunzi wa historia na siasa katika ngazi zote.7
Bila ya kutowa ushahidi wa marejeo yoyote yale, Mrina na Matokke wanakiri kuwa "Pwani ya Afrika Mashariki ilikuwa imefikiwa na wageni kutoka sehemu za mashariki ya mbali yapata miaka 500 kabla ya kuzaliwa Kristo."8 Katika safari yao ndefu ya "utafiti wa hali ya juu" Mrina na Matokke hawakutaka kujuwa nini kimeandikwa katika kitabu maarufu duniani The Periplus of the Erythrean Sea kilichoandikwa miaka 2000 iliyopita kuwepo kwenye pwani ya Afrika Mashariki kwa karne nyingi tawala za kifalme za Arabuni ya Kusini na kuwa Waarabu "walikuwa wameingiliana na kuowana na wenyeji na wakiifahamu pwani nzima na lugha zilizokuwa zikizungumzwa."9
Mrina na Matokke hawakujali kuyapitia matokeo ya utafiti makini wa wanahistoria na mabingwa wa ilimu ya athari (archaeology) au hata Biblia yenye kumtaja Kush na watu wa kutoka ustaarabu wa Kikushi ambao wanaiunganisha Afrika Mashariki na Somalia, Ethiopia na Bara Arabu. Lakini hilo halikuwa lengo lao na ndio maana safari yao haikuwapeleka huko. Lengo lao lilikuwa kupiga siasa na kuziharibu akili za walimu na wanafunzi kutoka Zanzibar na Tanganyika.
Misafara ya masomo ya dhiki na dhuluma
Hadithi dhidi ya Waswahili na Waarabu ambazo hazitegemei aina yoyote ile ya ushahidi zimekithiri kama uyoga kunako vichwa na nyoyo zenye kuipa jina baya Dola ya Zanzibar ili ipatikane sababu ya kuiangusha au kuizuwia isije juu. Yako mambo mtu akisema hapohapo hutakiwa ushahidi na hoja mpaka msikilizaji aridhike na kuna mambo hayahitajii hata chembe moja ya ushahidi midamu makapi ya hoja yanaonekana.
Kwa mfano, R. K. Mwanjisi kwenye kijitabu chake Abeid Amani Karume utakuta ameandika kuwa:
Kuna mambo mengi sana ambayo yalitendeka nchini Unguja na Pemba na ambayo hayana budi yathibitishwe kwa ushahidi kamili, na kuandikwa kwa makini.
Kuna nyumba Unguja iitwayo "Mambo Msiige" ambayo baada ya kumalizika kujengwa wale Waafrika walioijenga waliuwawa wote ili wasiige maarifa ya ujenzi wa nyumba kama ile.
Yasemekana pia kuwa wake za Waarabu siku hiyo wakifurahi huwaambia mabwana zao "mie sijapata kuona mtoto anavyokaa tumboni mwa mwanamke,
Mirengo ya Kizalendo na Mapinduzi 15
nataka kuona hivi leo." Basi bwana wa Kiarabu hutuma watumwa wake wamlete mama wa Kiafrika mja mzito na akapasuliwa tumbo kumwonyesha bibi mkubwa jinsi mtoto anavyokaa tumboni! Kisha maiti ya yule mjakazi wa Kiafrika ikatupwa shimoni!
Yasemekana kuwa wakati huo Mwarabu akitaka kuhakikisha ikiwa gobori lake lina nguvu humwambia mmoja wa watumishi wake apande mnazi. Akiisha fika juu yule "Bwana" alifyatua gobori lake, kisha "Mtumwa" akalia "Yallah" akaanguka chini na kufa. Kiisha yule Mwarabu akaja na kuipiga teke ile maiti na kusema "Ama, hivi kafa huyu!"
Inasemekana kuwa kuna Mwarabu mmoja alizaa mtoto na mtumwa wake Mwafrika. Jambo hili lilipojulikana yule Mwarabu akachukua kisu akamwua yule kijakazi wake na kumtumbukiza chooni!10
Hizo ni sumu kali ndani ya kijitabu ambacho lengo lake ni kuzielezeya habari za maisha ya Mzee Abeid Amani Karume kwa wasomaji ambao wanatakiwa wafahamu kuwa:
Unguja na Pemba imepita katika tanuri la moto wa utumwa, udanganyifu wa wafanya biashara na washika misahafu, utawala wa kigeni, ubaguzi wa rangi, utetezi, juhudi za uhuru, mapinduzi na ujamaa.11
Cha Mwanjisi ni kijitabu kidogo kilichotungwa kwa ajili ya wasomaji wa kawaida. Mambo yalizidi kuwa hatari wakati kasumba kama za Mwanjisi zilipoingizwa ndani ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania, Zanzibar. Na hayo yalifanywa na Wazanzibari Waafrika Waislamu ambao walitekwa akili na hadithi za utumwa zisizokuwa na hata chembe moja ya uthibitisho. Angalau Mwanjisi alitahadharisha kuwa hadithi zake kuhusu ushenzi na mambo maovu kabisa ya Waarabu waliyowafanyiya Waafrika "hayana budi yathibitishwe kwa ushahidi kamili, na kuandikwa kwa makini."
Akina Luteni Kanali Musa Maisara Kheri, mkuu wa uandishi na muandikaji wa utangulizi, Maalim Ubwa Mamboya Ismail, Mwenyekiti wa halmshauri ya uandishi wa kitabu cha Jeshi la Wananchi wa Tanzania, 1964–1974, Zanzibar na ndugu zao wengine wa Kiislamu walioshiriki kwenye uandishi wa kitabu hicho, hawakuiyona haja wala madhara ya kuitumiya sumu ya hadithi zisizo na uthi-bitisho wowote midam sumu hiyo iliwapa uhai wenye utukufu wa kidunia. Mafunzo ya dini ya Kiislamu na ule msemo wa Imam Ali usemao "Utukufu hupatikana kwa kumtumikia Muumba na mwenye kuutafuta kwa viumbe hatoupata" haukuwa na maana yoyote kwao.
Jambo la kupendeza lilikuwa kwamba mpaka mwaka 1974 kulikuwa na Jeshi la Wananchi wa Tanzania, Zanzibar. Zanzibar ikijilinda wenyewe. Mambo makubwa zaidi ni yale yenye kuwasononesha wale waliohusika katika kushiriki kuwauwa ndugu zao ambao leo wameshakuwa watu wazima na kesho kuna kukutana na Muumba wao. Kitabu hicho kiliandikwa chini ya uwenyekiti wa
 
Uzushi mtupu, wengi wa hao wazee hawafahamu lolote kuhusu hayo mapinduzi na sababu za kuwapo kwake. Kama wasivyofahamu kuhusu muungano.
 
Babkey

Si utufahamishe basi hizo sababu? Au ni siri?


Uzushi mtupu, wengi wa hao wazee hawafahamu lolote kuhusu hayo mapinduzi na sababu za kuwapo kwake. Kama wasivyofahamu kuhusu muungano.
 
Waislamu huwa hawana jema toka kwa Mkristo hata siku moja, hata kama ukiwalamba nyuma watakudharau tu! Huwezi ukawasikia wanamlalamikia Dikteta Iddi Amin Dada wa Uganda pamoja na maovu yake yote simply kwa sababu alikuwa mwislamu! Similrly kwa magaidi kama akina Osama bin Laden, pamoja na unyama wote wanaofanya, kwao ni mashujaa! Hata hivyo si ajabu kwa sababu asili ya chuki waliyo nayo iko moja kwa moja ndani ya Quran (death manual)!
Tatizo lako hufaamu hasa kiini cha vita ya uganda, wala septemba 11, kama lengo ni kumkamata Osama kwa nini raia wa afaghnistani wasio kuwa na kosa wauawe kwa ajili ya kumtafuta mtu mmoja kwani kuna wahalifu wangapi wakivita duniani hawatafutwi kwa kuuwa raia wa nchi husika kama rais wa yugoslavia ? hapa utaona kuwa ni wazi kabisa Rais Bush alivyo dhamiria kumwaga damu za waislamu kwa chuki zake za kidini, kwani ktk tamko lake la kwanza kulitoa baada ya sept 11 alisema " This is CRUSADE" (hivi ni vita vya msalaba) usiweke udini mbele badala ya kuchambua hoja kitaalamu
 
Tatizo lako hufaamu hasa kiini cha vita ya uganda, wala septemba 11, kama lengo ni kumkamata Osama kwa nini raia wa afaghnistani wasio kuwa na kosa wauawe kwa ajili ya kumtafuta mtu mmoja kwani kuna wahalifu wangapi wakivita duniani hawatafutwi kwa kuuwa raia wa nchi husika kama rais wa yugoslavia ? hapa utaona kuwa ni wazi kabisa Rais Bush alivyo dhamiria kumwaga damu za waislamu kwa chuki zake za kidini, kwani ktk tamko lake la kwanza kulitoa baada ya sept 11 alisema " This is CRUSADE" (hivi ni vita vya msalaba) usiweke udini mbele badala ya kuchambua hoja kitaalamu

Wewe ndiye usiyejua kwamba Marekani wana interest na mafuta tu na ndio maana wanatoa misaada sana kwa baadhi ya nchi za kiarabu ili kuleta influence. Hayo ya udini huwa yanatumiwa ili kupata support ndio maana hata wewe unataja kuwa "damu za waislamu" bila kujali kama kuna watu wengine wasio waislamu wanaouawa!
 
Mlango wa Pili
halmashauri ya uandishi wa kitabu chini ya uongozi wa Kanali Seif Bakari Omari, na Luteni Kanali Musa Maisara Kheri akiwa Mkuu wa Uandishi na muandikaji wa Utangulizi. Propaganda ya "misafara ya dhiki na dhuluma" inasema:
Vikosi vya jeshi la wananchi wa Tanzania Zanzibar katika kazi yake ya siasa hufanya misafara kila mwaka mara mbili kwa kuvizuru vituo vyote ambamo wakiteswa Waafrika katika zama za utawala wa kifalme na vibaraka vyao ili kuelewa wanakotoka kwa makusudi ya kunyanyua juu nguvu za kimapigano na kuwa na chuki kwa matendo hayo waloyofanyiwa wafanyakazi na wakulima. Halmashauri ya siasa baada ya kukaa na kuzingatia ilitoa mpango maalumu kwa vikosi vyote kupita sehemu zote ambazo masalio ya baadhi ya vitu ambavyo Waafrika wakiteswa…Vituo hivyo ni:-
1. Mkunazini – U.M.C.A.
2. Tumekuja
3. Maruhubi
4. Kijichi
5. Dunga jumba la mawe
BEIT – El AJAB [Beit alajaib – jumba la maajabu]
Hapo Forodhani Unguja lipo jumba kubwa la ghorofa tatu lililojengwa na mflame Baraghashi katika mwaka wa 1883 na mpaka hivi leo lipo bado.
Ujenzi wa jumba hili ulipoteza roho chungu nzima za Waafrika wasio na hatia. Ilikuwa ni desturi kwa mujibu wa itikadi za kiarabu-kuchinja kinyama kama mbuzi, au ngombe ili awe kinga kwa kila baya. Watawala wa kiarabu badala ya kuchinja vinyama wao waliwachinja Binadamu badala yake! Dhulma ilioje!!!
Katika sehemu zote hizo zilizokwisha elezwa ndio sehemu muhimu kwa historia ya Waafrika walimoteswa na ndizo sehemu muhimu. Kwa hivi sasa zinazo pitiwa na wanajeshi na kufahamishwa hali ya tawala za kisultani na vibaraka vyao walivyo watesa kikatili Waafrika katika nchi hii. Ili kuwafanya wanajeshi wa kimapinduzi wawe na chuki kubwa mioyoni mwao kwa wapinga maendeleo ya kimapinduzi.12
Kuwatia chuki wasomaji na wanajeshi kwa kutoa mifano ya unyama wa Waarabu dhidi ya Waafrika ambayo imetumiwa na Mwanjisi hata baada ya kutanabahisha kuwa "hayana budi yathibitishwe kwa ushahidi kamili, na kuandikwa kwa makini" ni kushiriki katika uovu wa kimsingi ambao unaonekana katika mifano yote ya mauwaji ya halaiki ya viwiliwili na ya saikolojiya baada ya kuwanyima watuhumiwa haki yao ya kuishi na kuishi bila ya khofu au huzuni.
Misafara ya dhiki na dhuluma ambayo tunayazungumziya hayana nguvu kwenye Zanzibar ya leo kama ilivyokuwa kwenye miaka iliyopita ingawa juhudi ya kuvipiga marufuku vitabu au vijitabu vyenye kuwatia sumu Waafrika dhidi ya Waarabu au Waarabu dhidi ya Waafrika bado haijafanyika kama inavyopasa kufanywa. Ipo haja kubwa ya kuandikwa vitabu na vijitabu vipya na vyombo vya habari kutoa ilimu yenye kusimama juu ya ushahidi wa hadithi za utumwa walioufanya Waarabu, Waafrika, Wazungu na Wahindi.
Mirengo ya Kizalendo na Mapinduzi 17
Hii leo, hamira za fitina za kubuni na zisokuwa na ushahidi wowote za utumwa wa Waarabu na ukombozi ulioletwa na Ukristo kuwaokoa Waafrika zinaendeleya kuwalisha na kuwakogesha watalii wanaolizuru Kanisa la Anglikan Mkunazini Zanzibar. Kwa shilingi elfu 3,500 (au dola 3 za Kimarekani) watembezaji watalii hao ambao wengi wao si Wazanzibari, hutowa darasa kwa kila mtalii anayefika hapo kuwa Waarabu wameleta vitu viwili vibaya Afrika: Uislamu na Utumwa. Kilele cha darasa hufikiwa pale mtalii anapoongozwa na kuonyeshwa alama ya duara dogo jeupe la jiwe la marmar liliopo ndani ya kanisa ambalo linamahanisha alama mbele ya meza panapotolewa dhabihu au kafara (altar) na panaposemekana kuwa ndipo palipokuwa pamesimama mti wa Mkunazi ambao Waarabu wakiwafunga watumwa wa biashara yao na kuwapiga viboko.
Kwa mujibu wa mwalimu wa watalii wa msafara wa dhiki na dhuluma, duara
hilo jeupe limezungukwa na jiwe refu jengine la marmar lenye rangi nyekundunyekundu ambayo ni alama ya damu ya Waafrika iliyokuwa ikichururuzika kutoka na mipasuko ya viboko vya Waarabu (Waisilamu). Kinachosafirishwa kwenye akili ya mtalii ni namna gani wafuasi wa Nabii Issa (sala na salamu za Mwenye Enzi Mungu zimfikie) wamekuja kusimama kunako alama iliyokuja kuwakombowa Waafrika kutokana na biashara ya utumwa wa Waarabu (Waislamu) na kuupa kasi ufalme wa Yesu Afrika.
Watu wenye akili za kibiashara wametambuwa kuwa fitina za utumwa zinaweza kufanyiwa biashara juu ya migongo ya Waarabu na Waislamu na pengine hata bila ya kutambuwa kuwa kunajenga mazingira mapya ya chuki dhidi ya Waislamu wa Zanzibar na wa Tanganyika. Mkutano wa kimataifa ambao umeandaliwa na taasisi ya African Diaspora Heritage Trail ya Marekani, ulitangaziwa kufanyika Dar es Salaam na Zanzibar baina ya tarehe 25–30 Oktoba mwaka 2009. Anwani iliyotumiliwa kuutangaza mkutano huo ilikuwa ni "Utumwa wa Waarabu Afrika Mashariki" na sambamba na mkutano huo ni zinduo la "Msafara wa Pembe za Ndovu na Utumwa" ambao utaihusisha miji kadhaa na mwahala munamohusika na utumwa na ubakaji wa Waafrika weusi milioni tano!
Upande mmoja mkutano huo umejihalalisha kwa kushirikiana na Mradi wa Biashara ya Utumwa (Slave Trade Project) wa shirika la Umoja wa Mataifa (UN) UNESCO. Mradi huo una kitengo cha utumwa katika nchi za Kiarabu na za Kiislamu. Kwa upande mwengine, madhumuni khasa ya mkutano huo ni kukuza biashara ya utalii kwa kuihusisha na urathi au turathi ya utumwa. Mashirika ya utalii na usafiri yameangaza na yamegunduwa kuwa kuna mijipesa inasubiri kuokotwa kwenye njia ya misafara ya dhiki na dhuluma. Walichokisahau ambacho hakimo kwenye hisabu yao ni umuhimu wa kuweka misingi ya maadili (ethics) kwenye kulifanyiya biashara suala kama hili ambalo limeamuwa kwenye anwani ya mkutano kuwabebesha Waarabu na watalii mizigo ya hadithi za utumwa ambazo hazina uthibitisho wala mashiko ya kitaaluma.
Mkutano uliwalenga Waarabu dhidi ya Waafrika milioni tano na si kuhusu
18 Mlango wa Pili
utumwa wa Afrika Mashariki au wa Bahari ya Hindi ambao utawahusisha baadhi ya Waarabu, baadhi ya makabila ya Kiafrika, Wazungu na Wahindi. Walitokeya wapi hao Waafrika milioni tano na walimalizikiya wapi na walinunuliwa na kupelekwa na nani na ndani ya vyombo vya nani si suala ambalo limo katika matangazo ya mkutano huo. Wako wanaoamini kuwa mkutano kama huo ni wa kupuuzwa kwa sababu wenye kuuandaa si watu wazito sana duniani. Wanachokoseya ni kuwa mambo ya biashara za kipropaganda hayahitaji wataalamu au utaalamu mkubwa. Mikutano kama hii ndiyo yenye kuivumbika sumu ya chuki dhidi ya kikundi fulani cha watu ambayo mwisho wake hugeuka kuwa ni biashara mbovu kwa alotaka kufanya pesa na zaidi juu ya waliolengwa kufitinishwa, kuuliwa, na kufanyiwa faida juu ya migongo ya mauti yao.13
Mrengo wa Umoja wa Kiafrika-Pan-Africanism
Kwa Zanzibar, siasa ya Pan-Africanism au Pan-Arabism ni mfano wa globu za taa ambazo hazina budi kuzimika kwa sababu ni taa za siasa zenye kuumurika upande mmoja wa jamii na kuuwacha upande wa pili ndani ya giza. Zanzibar ni jamii ya mchanganyiko kwa hiyo mirengo ya kisiasa yenye kuiwacha nje nusu ya jamii na matokeo yake ni kuraruka kwa jamii ambayo ilitakiwa kwa pamoja ilikamate guo la kuwapamba na kuwasitiri.
Siasa ya Pan-Arabism na Uislamu inakuja kuikusanya nusu ya pili ya jamii ya Zanzibar ambayo iliongozwa na chama cha "Hizbu" (Zanzibar Nationalist Party, ZNP) ambalo ni neno la Kiarabu lenye maana ya "chama" kwa Kiswahili. Mchango wa Chama Cha Wafanyakazi cha Tanganyika, Tanganyika Federation of Labour (TFL), ni sehemu muhimu ya historia ya Mapinduzi ya Zanzibar na ndiyo chombo kikuu kilichoendesha Mapinduzi kutoka Tanganyika kwa kushirikiyana na TANU na wafuasi wa Chama cha Wafanyakazi cha Afro-Shirazi (Zanzibar and Pemba Federation of Labour (ZPFL)).
Pan-Africanism kama alivyoichambuwa Dkt. Saleh Al-Miskry katika tasnifu yake ya shahada ya udaktari wa falsafa Pan-Africanism and Nyerere in Tanzania ni harakati yenye kuungwa mkono na kikundi cha watu na si na nguvu za umma. Sababu kubwa anayoitowa Al-Miskry ni ule ukaribu uliopo baina ya thakafa, dini, na mila baina ya viongozi wa Pan-Africanism na thakafa, dini, na mila za Ulaya. Anaendelea Al-Miskry, "…pan-Africanists na mabeberu kutoka Ulaya walifanya kazi kwa pamoja wakati wa ukombozi dhidi ya ukoloni."14
Hoja ya kibaguzi iliyotumika ni kuwa Waarabu kutoka kokote kule ni wageni Zanzibar na Mwambao wa Afrika Mashariki. Na si Waarabu peke yao, bali hata Washirazi pia. Ubaguzi huu unaonekana waziwazi katika barua ya Jumuiya ya Waafrika /African Association ya 1949 waliyomuwandikia Balozi wa Kiingereza Zanzibar na kwa Waziri wa Makoloni wa Uingereza isemayo:
Mirengo ya Kizalendo na Mapinduzi 19
Tunasikitika sana kuona kwamba Serikali imemteuwa Mshirazi, Mwasia kwa ajili ya kumtumiliya, badala ya Waafrika wa Zanzibar. Inaeleweka wazi kwamba Mshirazi ni Mwasia katika rekodi za Serikali ya Zanzibar. Tunaelewa kwamba tunanyimwa haki zetu za uraia na hii imewabakiza Waafrika katika hali ya kukata tamaa. Kwa jina la Demokrasi, Ukristo, na usawa wa Binadamu, tunapinga vikali hatua ya Serikali na tunaomba ufikirie na kutizama upya mwenendo huu wa ubaguzi, ukandamizaji, kunyimwa haki na kunyanyaswa katika nchi yetu.15
Hii ni ajabu kubwa sana kuwa Wakristo, wageni kutoka bara ndiyo wenye kudai haki kwa fujo kwa kumpinga mwenyeji Mshirazi na Muislamu mwenye mizizi Zanzibar kwa kutumia garasa la "Uafrika"!
Tatizo kubwa la Zanzibar ni mavuno ya mti wa udanganyifu na wa mrengo maalum wa kisiasa wenye kuongozwa na kikundi kidogo chenye kuiamini itikadi maalumu ya uzalendo wa Kiafrika (Pan-Africanism) ambayo inasisitiza kuwa Waarabu/Washirazi/Waswahili/Waislamu chini ya Jangwa la Sahara ni wageni na kuwa Zanzibar ni mlango mkongwe uliyouingiza ubeberu Afrika Mashariki na Kati na Ukristo ndiyo muokozi wake.
Kwa nchi kama Zanzibar ambayo ina mchanganyiko mkubwa wa watu wa kila asili, fikra ya umoja wa watu weusi peke yao ni fitina iliyovaa guo la udugu wa kibaguzi dhidi ya Waafrika wa makabila mengine. Fikra ya mrengo huu iko kinyume na ilimu ya asili ya binaadamu ambayo inatuonyesha wazi kuwa binaadamu wote wametoka Afrika kwenda majuu katika nyakati tafauti. Dalili ni kuna watu ambao wamelelewa na fitina maalum na ambao wamewatiya chuki za kidini na za kikabila wenziwao bila ya hata kuona kama iko haja ya kuupima ushahidi wa ukweli au uongo unaotapakazwa au kutafuta juhudi za kuuondowa kwa faida ya makabila na dini nyenginezo.
Kwa mujibu wa falsafa hiyo ya mrengo huo wenye kuweza kutafakhari kuwa "Afrika Kwetu" au "Tupendane Waafrika" ni wale Waafrika wenye asili ya kibara tu peke yao na wakati huohuo kuuficha ukweli kuwa hayati Mwalimu Nyerere asingeliweza kuwa kiongozi wa Tanganyika African Association (TAA), na baadaye wa Tanganyika African National Union (TANU) bila ya kwanza kuungwa mkono na wazee mashuhuri wa Dar es Salaam, wakiwemo wenye asili na makabila tafauti, yakiwemo ndani yake makabila ya Kibantu wenye kuifuata dini ya Kiislamu.
Hayati Mwalimu Nyerere alikuwa ni kiongozi wa Kiafrika mwenye sifa kubwa duniani na kupendwa sana Tanganyika. Mwalimu alijaaliwa kufanya kazi moja kubwa katika maisha yake, nayo ni kuupiganiya na kuupata uhuru wa Tanganyika kutoka kwa Muingereza. Na katika hilo aliwasahau majasiri wa Kiislam ambao ndio chimbuko la harakati za kupiganiya uhuru Tanganyika na waliyoianzisha TANU hata kabla ya yeye kukaribishwa Dar es Salaam na wazee wanaharakati wa uhuru wa Tanganyika. Waislamu ndio waliokuwa wakiumizwa zaidi na ukoloni kuliko kundi au kikundi chengine chochote kile cha kidini Tanganyika.
20 Mlango wa Pili
Waislamu wa Tanganyika walijipinduwa na wakapinduliwa kwa mapinduzi baridi ya mwaka 1954 baada ya kwa makusudi kumuachiya kwa makusudi, Mwalimu Nyerere achaguliwe kuwa kiongozi wa TANU.16
Miaka kumi baada ya hapo, 1964, ikawa zamu ya kupinduliwa Zanzibar kwa mapinduzi ya kumwaga damu. Ndipo ilipoandikwa makala mwezi wa Juni 1964 katika jarida maarufu la The Economist yenye kichwa cha maneno "Mashaka ya Nyerere" kuwa Mwalimu Nyerere "ameweza kuifanya nusu ya kazi ya chatu. Ameimeza Zanzibar sawa, lakini hakuziuwa nguvu zake za kujiteteya kwanza. Mnyama ambaye yungali hai anaendeleya kukila chakula chake, na mateke yake yanaendeleya kumuumiza [chatu] kwa maumivu makubwa, na pengine hata kuyahatarisha maisha yake, ndani huko kunako mwili wa kisiasa wa Tanganyika."17
Katika hotuba yake muhimu kuliko zote aliyoitowa kwenye hoteli ya Kilimanjaro siku ya Jumaane, tarehe 15 Machi 1995, Mwalimu alianza kwa kuuzungumzia ufa mkubwa uliyoipasuwa nyumba ya Tanzania ni ufa mkubwa wa Muungano baina ya Tanganyika na Zanzibar. Mwalimu alitabiri kuwa ama mtikisiko utakwisha na nyumba ya Tanzania itakuwa imara, au utaendeleya na nyumba itabomoka hata ikiwa imara. Alisema lengo liwe mtikisiko usiendelee. Katika kuhamasika na kipaji cha kuzungumza alichojaaliwa Mwalimu Nyerere, kuna Mchungaji ameandika kunako blogi moja: "Hakika alikuwa nabii, zile nyufa alizoona ziliendelea na sasa naona zimekuwa mianya mikubwa kwenye kuta. Kama hatutaangalia, nyumba yetu itabomoka na kuanguka…"
Mwalimu kweli alikuwa "nabii" kwa maana aliweza kuzitabiri nyufa na mianya mikubwa inayoukabili Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Ufa mkubwa kati ya nyufa zote alizozizungumzia Mwalimu ni ufa wa muungano ambao aliongeza kwa kusema kuwa uko katika "hatari ya kuvunjika [na] wala haijesha."
Mwalimu pia alisema "ningependa mjadala wa sasa" uwe kuhusu kueleweka nyufa ziliopo na "tupate uongozi unaoelewa hivyo." Ombi la Mwalimu halikujibiwa ipasavyo na wenye kutaka kuinusuru nyumba ya Tanzania kubomoka ingawa ndani na nje ya nchi tayari wapo watu na mataifa yenye kuanza kukubali kuwa pengine hilo ni jambo ambalo haliwezi kuepukika. Bahati mbaya Mwalimu alitaka mjadala uendelee bila ya kutoa sababu za chanzo au mzizi wa mtikisiko. Hilo asingeliweza kulifanya kwa sababu lilikuwa ni gumu sana kwake, maana kama angelizieleza sababu halisi za mtikisiko basi zingelimuondolea sifa ya kuwa kiongozi pekee katika bara la Afrika ambaye aliweza kuziunganisha kwa hiari nchi mbili huru za Kiafrika.
Tukirudi nyuma kwenye mizizi ya mitikisiko, na kwa mujibu wa ripoti ya mazungumzo ya Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola, Sir N. Pritchard yaliyofanyika Dar es Salaam tarehe 27 Februari 1963, Mwalimu Nyerere alisema:
 
niquist tupatie speech ya Bush inayozungumzia mambo ya "crusade!"
 
Ukisoma kitabu cha KWAHERI UKOLONI KWAHERI UHURU cha mwandishi Harith Ghassany unakaribia kulia ukijua kwamba kumbe Mapinduzi ya Zanzibar si kama tunavyoyajuwa.Kwa upande mwengine kumbe uongo ni kitu kibaya sana kinacholeta maangamizi katika jamii.
Mwandishi anastahiki sifa kubwa ya kuwa mtafiti aliyebobea.Amehojiana na watu muhimu walioshiriki kuipindua serikali ya Zanzibar ambao wengi wala si wenye kusikika.

Ukisoma hiki kitabu ushahidi uko wazi kuwa mapinduzi yale yalikuwa ya chuki za kikabila na kidini na hayakufanywa na wazanzibari wenyewe.Kumbe Nyerere ndiye aliyesuka na kugharimia mapinduzi yale akikitumia chama cha TANU.
Viongozi wa mapinduzi wao wenyewe hawakujua kipi hasa kilikuwa kikiwaongoza kufanya mapinduzi,ni kumuondoa mwarabu mwenye rangi nyeupe na kumuweka mwafrika wa rangi nyeusi au ni kuwaweka watu wa bara waiongoze Zanzibar.Kauli zao na matendo ni vyenye kujichanganya.

Waliokuwa wakitawala Zanzibar walikuwa ni waislamu lakini hawakutekeleza uislamu,hili ni moja ya kosa lao kubwa.Ubwanyenye na ujinga wa kiutawala ulitoa fursa kwa maadui zao kuwapindua kirahisi.Hata hivyo nguvu ya adui aliyekuwa ndani yao na nje wasingekuwa na uwezo wa kuhimili tena.
Katika mkanganyiko huu walioathirika zaidi bila kosa ni wazanzibari waliotafsiriwa na viongozi wa mapinduzi kwamba wana asili ya kiarabu,wengi wao wakiwa wala hawako kwenye utawala.

Nyerere alipata kusema kuwa udini na ubaguzi ni kama ukoma lakini kwa hakika alitumia ukabila na ubaguzi kujenga udini.
Nyerere kwa Afrika anaweza kuitwa baba wa Mapinduzi.Yeye aliweza kuongoza Mapinduzi ya Zanzibar,akawapinduwa waislamu ndani ya TANU na hupati taabu kuona kwamba yeye alishiriki kumuua Karume kupitia kamanda wake Ali Mahfudh.Nyerere alikuwa na damu ya kimapinduzi tu lakini si kwamba mapinduzi aliyoyafanya yalikuwa yana umuhimu.
Kwa wakristo Nyerere anaweza kuonekana ni shujaa lakini kwa waislamu ni mtu mbaya mno.

Mkuu wewe umesoma kitabu hicho kilichopigwa marufuku zanzibar kama vengine vingi. Sie wengine tumekaa na wazee waliokuwapo wakati wa mapinduzi, walioshiriki katika mapinduzi wakikuhadithia yaliyotokea mwanzo mpaka mapinduzi na baada ya mapinduzi utachafukwa na roho. Anyway tuyaache haya maana tumeshayazika for the sake of unity in zanzibar. Zanzibar inahitaji kuyazika haya mambo ili wapate kuendelea na kwa hilo mie nawaunga mkono.
 
Wewe ndiye usiyejua kwamba Marekani wana interest na mafuta tu na ndio maana wanatoa misaada sana kwa baadhi ya nchi za kiarabu ili kuleta influence. Hayo ya udini huwa yanatumiwa ili kupata support ndio maana hata wewe unataja kuwa "damu za waislamu" bila kujali kama kuna watu wengine wasio waislamu wanaouawa!

sasa ndugu yangu afghanistan kuna mafuta gani? tatizo umeshakuwa brain washed ili uamini wanavyo taka wao lakini ukweli utabakia mpaka siku ya mwisho kwani kwa akili iliyo salimika haiwezi kuamini propaganda kama hizi kwani tunajua fika afghanistan ililkuwa ni nchi ya kiislamu na more than 90% ni waislam kwa hiyo ukipiga kombora au risasi ni wazi kuwa chance ya kuuwa muislamu ni zaidi ya asilimia 90. Ndio maana hata Rais wa venezuela hugo chavez alisema sept 11 iliratibiwa na wamerekani wenyewe ili waweze kunyonya haki za wanyonge. angalia hii link Dailymotion - Hugo Chavez Says 9/11 was an Inside Job - a News & Politics video
 
Ukisoma kitabu cha KWAHERI UKOLONI KWAHERI UHURU cha mwandishi Harith Ghassany unakaribia kulia ukijua kwamba kumbe Mapinduzi ya Zanzibar si kama tunavyoyajuwa.Kwa upande mwengine kumbe uongo ni kitu kibaya sana kinacholeta maangamizi katika jamii.
Mwandishi anastahiki sifa kubwa ya kuwa mtafiti aliyebobea.Amehojiana na watu muhimu walioshiriki kuipindua serikali ya Zanzibar ambao wengi wala si wenye kusikika.

Ukisoma hiki kitabu ushahidi uko wazi kuwa mapinduzi yale yalikuwa ya chuki za kikabila na kidini na hayakufanywa na wazanzibari wenyewe.Kumbe Nyerere ndiye aliyesuka na kugharimia mapinduzi yale akikitumia chama cha TANU.
Viongozi wa mapinduzi wao wenyewe hawakujua kipi hasa kilikuwa kikiwaongoza kufanya mapinduzi,ni kumuondoa mwarabu mwenye rangi nyeupe na kumuweka mwafrika wa rangi nyeusi au ni kuwaweka watu wa bara waiongoze Zanzibar.Kauli zao na matendo ni vyenye kujichanganya.

Waliokuwa wakitawala Zanzibar walikuwa ni waislamu lakini hawakutekeleza uislamu,hili ni moja ya kosa lao kubwa.Ubwanyenye na ujinga wa kiutawala ulitoa fursa kwa maadui zao kuwapindua kirahisi.Hata hivyo nguvu ya adui aliyekuwa ndani yao na nje wasingekuwa na uwezo wa kuhimili tena.
Katika mkanganyiko huu walioathirika zaidi bila kosa ni wazanzibari waliotafsiriwa na viongozi wa mapinduzi kwamba wana asili ya kiarabu,wengi wao wakiwa wala hawako kwenye utawala.

Nyerere alipata kusema kuwa udini na ubaguzi ni kama ukoma lakini kwa hakika alitumia ukabila na ubaguzi kujenga udini.
Nyerere kwa Afrika anaweza kuitwa baba wa Mapinduzi.Yeye aliweza kuongoza Mapinduzi ya Zanzibar,akawapinduwa waislamu ndani ya TANU na hupati taabu kuona kwamba yeye alishiriki kumuua Karume kupitia kamanda wake Ali Mahfudh.Nyerere alikuwa na damu ya kimapinduzi tu lakini si kwamba mapinduzi aliyoyafanya yalikuwa yana umuhimu.
Kwa wakristo Nyerere anaweza kuonekana ni shujaa lakini kwa waislamu ni mtu mbaya mno.

Kitabu hicho kimemuongela mpiganaji John Okelo? Cjui kwa nn jamaa hakumbukwi, ni hila au nn jaman? Kwa sabab nackia wakati Okelo anawaondoa warabu Abed karume alikuwa Dar
 
Back
Top Bottom