Mapokezi Ya FC Platinum: Hatimaye 'Wananchi' Waonyesha Uzalendo...!!!

Mapokezi Ya FC Platinum: Hatimaye 'Wananchi' Waonyesha Uzalendo...!!!

kinje ketile

JF-Expert Member
Joined
Dec 12, 2015
Posts
5,089
Reaction score
9,664
Nimekuwa shuhuda siku ya leo majira ya alasiri wakati timu ya Platinum kutoka Zimbabwe ikipokelewa uwanja wa ndege JNIA.Ukweli zile mbwembwe na amsha amsha kutoka kwa wenzetu 'Wananchi' kwenye mapokezi hasa za timu za nje zinapokuja kupambana na 'mnyama' sikuziona.Jambo hili haliwezi kupita hivi hivi bila kupongezwa na limeonyesha dalili za wazi kabisa kuwa wananchi sasa wangependa wazimbabwe WAFE pale kwa Mkapa.
Zipo sababu za wazi kabisa kwa wananchi kuonyesha uzalendo. Mojawapo iwapo FC Platinum akitolewa stage hii Simba itaingia hatua ya Makundi na pia iwapo Namungo atapenya automatically Tanzania itarejesha zile nafasi 4 michuano ya CAF ijayo. Maana yake nini? Wananchi hata wasipochukua Ubingwa wa VPL jambo ambalo lina uwezekano mkubwa kutokea bado watajihakikishia nafasi ya kushiriki michuano ya Kimataifa. Kwa hili,Kongole kwao 'Wananchi'.
 
Dah...nikikumbuka ile amsha amsha siku wale wanigeria Plateau wanapokewa pale JNIA....Hakika waswahili hawakukosea waliposema 'Hasidi Hana Sababu' ..... !
 
Kila mtu apambane kivyake,mbona shida zenu mnatuletea sisi? We ulienda airport kufanya nini.....pambaneni na hali yenu
Ni Taarifa tu mkuu, kwani we mifaida ya mnyama kushinda iyo mechi huoni ? Yaani Yanga wanaingia Kimataifa kiubwete kabisa...!
 
Iwapo ikitokea Simba na Namungo wakifanikiwa ku 'penetrate' na kuingia Stage ya Makundi italeta heshima kubwa kwa Soka letu la Tz..Ligi yetu itapaa itaheshimika. Macho na masikio ya dunia yataigeukia Tanzania..ndio! dunia itaiangaza Tanzania kisoka. Maana yake uwekezaji wa akina GSM na Mo utakuwa umeleta tija.....!
 
Mtu atauliza GSM anaingiaje wakati ni Namungo na Simba ndizo washiriki..? Ukweli ni kwamba timu hizi zinatokea kwenye ligi ambayo ushindani unaletwa na wote yaani Yanga imo, Azam na uwekezaji wao wapo, timu za majeshi pia zina mchango,wawekezaji wengine wapo kama Mwadui, Biashara, Kagera Sugar, Mtibwa n.k.Hivyo issue hapa ni mafanikio ya ligi yetu(VPL) kwamba inaweza kuzalisha ma 'Giants' ambayo wameingia hatua ya makundi. Hivyo tuwaombee Simba na Namungo wafuzu....!
 
Acha hasira km vp jitie dole unuse nyan weeee

Sent from my SM-N910F using JamiiForums mobile app
Kwahiyo Prisons walivyo watia kidole mlinusa?
FB_IMG_1609620068941.jpg
 
Toka kule.. Ety nikae niisupportMikia.. Nyooooooh ukajinyee kabisa.. Young ni wananchi na kombe nilakwetu this year
 
Toka kule.. Ety nikae niisupportMikia.. Nyooooooh ukajinyee kabisa.. Young ni wananchi na kombe nilakwetu this year
Jamaa kajikaza haoni hata noma, mtamaliza ligi bila ya kufungwa ila kombe watabeba simba. Sijui km ishawahi kutokea. Itakuwa historia ya ulimwengu pia
 
Back
Top Bottom