Na hicho mimi ndio nakiamini, hawa watu wameamua kuwatumia washabiki bila wao kujua ili watengeneze pesa. Subiri hizi show zao ziishe kama utawasikia tena.
Kama Harakati ni zile alizofanya Sugu kapiga potepote kuanzia kwenye media, majukwaani, nyimbo na mitandao ya kijamii na sapoti kubwa kutoka kwa wasanii wenzake bado hakufanikiwa kiivyo ije iwe hii ya Jd ambayo anaifanya kwenye blogs? watu ambao wapo nje na mitandao hawajui chochote kinachoendelea kuhusu yeye na Clouds.
Tukubali tukatae issue ya Jd na Clouds ni matatizo yao binafsi, ila kaamua kaamua kuyazungumzia matatizo yao kupitia njia nyingine ili apate sapoti.