Hii video sio mbaya kihivyo kama tunavyoaminishana lakini tukitoa zile tofauti zetu za u-Diamond na u-Kiba, bado kuna kitu cha msingi ambacho kinaweza kumfanya mtu aione ni mbaya ingawaje kimsingi sio mbaya. Kwanza, music video is an
art and
science! Good music video ni lazima iwe na hizo packages kuu mbili za msingi! Video as science, hii ya Kiba imefanikiwa kwa kiasi kikubwa. As a science, tunaangalia sana technical aspects.
As an art, kwenye hii video kuna kitu kimekosekana. Mtoa maada na wengine wanazungumzia suala la video kutoendana na maudhui ya wimbo... niseme tu kwamba, kwenye music video story line isn't the big issue anymore! Kwenye video za kileo, hakuna cha suala la video kuendana na maudhui ya wimbo... that's an old shit of stuff! Cha msingi, as stated earlier, video is an art and science... that's it... music video sio movie kwahiyo si lazima iendane na maudhui ya wimbo!!!
Kukosekana kwa artistic work kwenye video ya Kiba kunaweza kumfanya hata asiye na tatizo na Kiba akaona hii video sio nzuri provided anaifahamu nyimbo ya Mwana Dar es salaam! Wimbo wa Mwana Dar es salaam umetoka zamani sana... huu wimbo watu wameusikia zaidi ya mara kumi na wapo waliosikia kwa karibu mara 50!! Wimbo uliozoeleka namna hii, unapotoa video ni lazima hiyo video iwe na artistic work otherwise, itaonekana imepwaya... itaonekana imepwaya coz' wengi wao hawatakuwa more interested na wimbo wenyewe kwavile wameshausikia sana lakini watakachotaka kuona ni video yenyewe! Je, hujawahi ku-mute TV lakini ukawa bado unaangalia video iliyopo hewani? Katika mazingira kama hayo, unakuwa umevutika na video yenyewe na sio wimbo... more often than not, kunakuwa na some artistic works or scenes kwa video husika ambazo zinakufanya uburudike hata kama husikii sauti!
Mdakuzi, kwenye moja ya post zake amehoji mbona hata video ya Number One Remix haina story line zaidi ya dancing ambayo, nami naongeza yangu kwamba hata dancing yenyewe sio artistic dancing bali ni ordinary dancing ambayo tunaitarajia kwenye any video...! Mdakuzi yupo right katika hili... video ya Number One Remix haina story line, tena kwa maoni yangu ni mbaya ukilinganisha na hii ya Mwana Dar es salaam! Hata hivyo Mdakuzi amesahau jambo moja la msingi ambalo hapo juu nimeliezea. Jambo alilosahau Mdakuzi ni kwamba, Number One Remix ni nyimbo ambayo ilikuwa haijaingia sana masikioni mwa watu; so, ilipotoka video, ni wachache sana ambao wangeanza kuichambua video yenyewe na badala yake watu wangeishia tu kuridhika kwenye wimbo na ushiriki wa Davido kwenye wimbo husika! Mtu asingekuwa na sababu ya kutafuta artistic elements wakati hata wimbo wenyewe haumjamchusha au hajawahi kuusikia! Kwa Kiba, artistic elements were necessary if not MUST kwavile tayari wimbo wake watu wameshausikia sana hata kuchosha kwahiyo kulitakiwa kuwa na artistic packages kwenye video husika ili hamu ya watu iamshwe upya na hayo mautundu ya kisanaa! Unapoangalia Liberian Girl ya Michael Jackson na jinsi watu walivyojipanga huku kila mmoja akionekana yupo busy na issue zake, hii inaleta ladha inayomfanya mtu aendelee kuangalia! Unapoangalia video ya "As" ya George Michael (ft Mary J. Blige) kisha video inavyoonekana ikiwa na watu kibao huku kila mmoja akifanya shughuli yake wakati was just a computer tricks... wahusika wakiwa ni wawili tu... hii ni some artistic work ambayo hata kama mtu angekuwa ameisikia "As" kiasi cha kumchosha, bado mautundu ya kisanaa yangemfanya avutiwe na video husika. Ukiangalia video ya Ting-A-ling ya Shaba Ranks, ukaona Teacher Mnoko anayewa-mind ma-dent waliodata na Ting-A-Ling na kuanza kuchomoka darasani mmoja baada ya mwingine hadi teacher mwenyewe nae uzalendo ukamshinda aka-join kudata nao; ni one of artistic work am talking about! UKiangalia utundu na vurugu vurugu za The Pharcyde kwenye ngoma yao Drop, inafanya video ivutie zaidi... sawa na usela wa hapa na pale ukiambatana na warembo kwenye video ya Dakika Moja ya Mwana-FA! Ukija kwenye most watched/viewed video in You tube 2014... Dark Horse by Katy Perry; nayo unakuta full of artistic works ambazo hata kama nyimbo ilishazoeleka bado watu wangeipa kudos video kwavile kuna something new.
Mifano hiyo hapo juu kwanza inakazia hoja kwamba suala la story line ( video kuendana na mahudhui) kwenye music video isn't an issue and no body entertain in a modern industry but artistic work ni very important! Kwa video ya Mwana Dar es salaam ingekuwa ni muhimu zaidi kwavile tayari nyimbo ilishazoeleka masikioni! Hili neno artistic ni very general lakini kiuhalisia ni kwamba, video inabidi iwe na kitu ama vitu special vitakavyowafanya watu wavutike hata kama wimbo ulishazoeleka! Hili suala la kitu special ndio maana haishangazi kuona Video ya Anaconda ya Nick Minaj nayo ipo kwenye top ten viewed video in 2014 ingawaje ina kiasi cha miezi mitano tu tangu itoke...
Nitampata Wapi ya Diamond ina view za kutosha sana ukilinganisha na life span yake lakini ile video hata kama ingekuwa mbaya na isiyokuwa na any artistic work or story line (kwa wale wafuasi wa story line) bado video ingefanya vizuri coz', kwanza, ilitoka as a suprise na pili, nyimbo ilikuwa haifahamiki kwahiyo udhaifu wa video ungefunikwa na wimbo wenyewe! Sasa ukija kwa Mwana Dar es salaam, si tu kwamba wimbo wenyewe ulishazoeleka sana huku video ikikosa artistic packages bali pia ujaji wa video yenyewe ulitarajiwa na kila mtu baada ya Kiba kuanza ku-post picha kuonesha kwamba video ipo njiani... angefanya suprise nadhani ingeongeza credit!