Pre GE2025 Mara: Jimbo la uchaguzi Serengeti kugawanywa kuwa majimbo mawili, Serengeti Mashariki na Serengeti magharibi

Pre GE2025 Mara: Jimbo la uchaguzi Serengeti kugawanywa kuwa majimbo mawili, Serengeti Mashariki na Serengeti magharibi

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Uzalendo wa Kitanzania

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2020
Posts
3,585
Reaction score
8,106
Wajumbe wa kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Mara (RCC) wamepitisha Jimbo la Uchaguzi la Serengeti kugawanywa na kupata majimbo mawili ya uchaguzi ambapo majina ya majimbo yanayopendekezwa ni Serengeti Mashariki na Serengeti Magharibi.

Mkuu wa Mkoa wa Mara Evans Mtambi aliongoza kikao hicho kilichofanyika katika Ukumbi wa Uwekezaji ambapo aliwataka wakurugenzi wa Halmashauri kujiandaa kuweka mikakati ya ukusanyaji wa mapato ili kutekeleza miradi ya maendeleo ya wananchi.

Hatua hiyo inakuja wakati tayari Tume huru ya taifa ya uchaguzi(INEC) imetangaza mchakato wa kupokea mapendekezo ya kugawa majimbo zoezi linaloendelea kuanzia Februari 27 na litakamilika Machi 26 mwaka huu.

Kulingana na tangazo la Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya uchaguzi INEC, Jaji Jacobs Mwambegele Tanzania ina jumla ya majimbo ya uchaguzi 264 ambapo Bara kuna jumla ya majimbo 214 na visiwani Zanzibar yakiwa 50

Kusoma Habari hii zaidi tembelea epaper.ippmedia.com

Chanzo: Nipashe
 
Watu wanajitaftia tu ilaji, hakuna manufaa kwa wananchi.

Mgawanyiko wa majimbo uwe unafanywa kwa referendum kwa wanachi wa eneo husika kushiriki na kukubaliana na mgawanyo badala ya wanasiasa kuamua.

Kuongeza Majimbo ya uchaguzi ni kuongeza tu gharama za kuendesha serikali.

Tume ya uchaguzi ikatae hizi stori za kugawa majimbo. Magufuli alikataa na hatujaona tatizo lollote, tume pia ikatae.
 
#Repost @nipashetz
——
Wajumbe wa kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Mara (RCC) wamepitisha Jimbo la Uchaguzi la Serengeti kugawanywa na kupata majimbo mawili ya uchaguzi ambapo majina ya majimbo yanayopendekezwa ni Serengeti Mashariki na Serengeti Magharibi.

Mkuu wa Mkoa wa Mara Evans Mtambi aliongoza kikao hicho kilichofanyika katika Ukumbi wa Uwekezaji ambapo aliwataka wakurugenzi wa Halmashauri kujiandaa kuweka mikakati ya ukusanyaji wa mapato ili kutekeleza miradi ya maendeleo ya wananchi.

Hatua hiyo inakuja wakati tayari Tume huru ya taifa ya uchaguzi(INEC) imetangaza mchakato wa kupokea mapendekezo ya kugawa majimbo zoezi linaloendelea kuanzia Februari 27 na litakamilika Machi 26 mwaka huu.

Kulingana na tangazo la Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya uchaguzi INEC, Jaji Jacobs Mwambegele Tanzania ina jumla ya majimbo ya uchaguzi 264 ambapo Bara kuna jumla ya majimbo 214 na visiwani Zanzibar yakiwa 50

Kusoma Habari hii zaidi tembelea epaper.ippmedia.com

#NipasheMwangaWaJamii #NipasheDigital
1-Majimbo yapunguzwe, 2-majina ya majimbo yaweza halisi siyo kusini au mashariki nk, 3-pawe na ukomo wa ubunge miaka kumi tu. 4-viti maalum "ke" viondolewe bali viwe vya makundi km wakulima , wazee, wastaafu, wafugaji, vijana, walemavu, nk (watatu kila kundi).
 
#Repost @nipashetz
——
Wajumbe wa kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Mara (RCC) wamepitisha Jimbo la Uchaguzi la Serengeti kugawanywa na kupata majimbo mawili ya uchaguzi ambapo majina ya majimbo yanayopendekezwa ni Serengeti Mashariki na Serengeti Magharibi.

Mkuu wa Mkoa wa Mara Evans Mtambi aliongoza kikao hicho kilichofanyika katika Ukumbi wa Uwekezaji ambapo aliwataka wakurugenzi wa Halmashauri kujiandaa kuweka mikakati ya ukusanyaji wa mapato ili kutekeleza miradi ya maendeleo ya wananchi.

Hatua hiyo inakuja wakati tayari Tume huru ya taifa ya uchaguzi(INEC) imetangaza mchakato wa kupokea mapendekezo ya kugawa majimbo zoezi linaloendelea kuanzia Februari 27 na litakamilika Machi 26 mwaka huu.

Kulingana na tangazo la Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya uchaguzi INEC, Jaji Jacobs Mwambegele Tanzania ina jumla ya majimbo ya uchaguzi 264 ambapo Bara kuna jumla ya majimbo 214 na visiwani Zanzibar yakiwa 50

Kusoma Habari hii zaidi tembelea epaper.ippmedia.com

#NipasheMwangaWaJamii #NipasheDigital
Tunahitaji Ibrahim nchi hii
 
Kodi zetu zinafunjwa sana kuwanufaisha watu wachache, ilaaniwe serikali dhalimu ya CCM.
 
1-Majimbo yapunguzwe, 2-majina ya majimbo yaweza halisi siyo kusini au mashariki nk, 3-pawe na ukomo wa ubunge miaka kumi tu. 4-viti maalum "ke" viondolewe bali viwe vya makundi km wakulima , wazee, wastaafu, wafugaji, vijana, walemavu, nk (watatu kila kundi).
Haoo maalumu wanavopenda kutoa vitu maalumu wapewe viti maalumu sijui utakuwaje tu...
 
1-Majimbo yapunguzwe, 2-majina ya majimbo yaweza halisi siyo kusini au mashariki nk, 3-pawe na ukomo wa ubunge miaka kumi tu. 4-viti maalum "ke" viondolewe bali viwe vya makundi km wakulima , wazee, wastaafu, wafugaji, vijana, walemavu, nk (watatu kila kundi).
Ni kama una HOJA..disadvantage group wapo wengi
 
Huu ugawaji wa majimbo hauna tija! Jimbo la Nzega liligawanywa kuamua mnyukano wa Bashe na Kigwangala ila jirani yao kuna jimbo la Bukene ni kubwa balaa.
 
Wangoreme na Waisenye jimbo lao na Wakurya jimbo lao
 
KUHUSU SERENGETI MCHAKATO HUU ULICHELEWA SANA, SERENGETI TUNA TAKRIBANI KATA 30, MAENDELEO HAFIFU, USIMAMIZI WA JIMBO ZERO..NAHS SERENGETI TUNA MBUGA KUBWA HALAFU MAENDELEO ZERO
 
Back
Top Bottom