Uzalendo wa Kitanzania
JF-Expert Member
- Mar 8, 2020
- 3,585
- 8,106
Wajumbe wa kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Mara (RCC) wamepitisha Jimbo la Uchaguzi la Serengeti kugawanywa na kupata majimbo mawili ya uchaguzi ambapo majina ya majimbo yanayopendekezwa ni Serengeti Mashariki na Serengeti Magharibi.
Mkuu wa Mkoa wa Mara Evans Mtambi aliongoza kikao hicho kilichofanyika katika Ukumbi wa Uwekezaji ambapo aliwataka wakurugenzi wa Halmashauri kujiandaa kuweka mikakati ya ukusanyaji wa mapato ili kutekeleza miradi ya maendeleo ya wananchi.
Hatua hiyo inakuja wakati tayari Tume huru ya taifa ya uchaguzi(INEC) imetangaza mchakato wa kupokea mapendekezo ya kugawa majimbo zoezi linaloendelea kuanzia Februari 27 na litakamilika Machi 26 mwaka huu.
Kulingana na tangazo la Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya uchaguzi INEC, Jaji Jacobs Mwambegele Tanzania ina jumla ya majimbo ya uchaguzi 264 ambapo Bara kuna jumla ya majimbo 214 na visiwani Zanzibar yakiwa 50
Kusoma Habari hii zaidi tembelea epaper.ippmedia.com
Chanzo: Nipashe
Mkuu wa Mkoa wa Mara Evans Mtambi aliongoza kikao hicho kilichofanyika katika Ukumbi wa Uwekezaji ambapo aliwataka wakurugenzi wa Halmashauri kujiandaa kuweka mikakati ya ukusanyaji wa mapato ili kutekeleza miradi ya maendeleo ya wananchi.
Hatua hiyo inakuja wakati tayari Tume huru ya taifa ya uchaguzi(INEC) imetangaza mchakato wa kupokea mapendekezo ya kugawa majimbo zoezi linaloendelea kuanzia Februari 27 na litakamilika Machi 26 mwaka huu.
Kulingana na tangazo la Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya uchaguzi INEC, Jaji Jacobs Mwambegele Tanzania ina jumla ya majimbo ya uchaguzi 264 ambapo Bara kuna jumla ya majimbo 214 na visiwani Zanzibar yakiwa 50
Kusoma Habari hii zaidi tembelea epaper.ippmedia.com
Chanzo: Nipashe