Mara ya kwanza kuja mjini (Dar) jiji lilikukaribisha kwa style gani ukikumbuka kwa jinsi ulivyokuwa mshamba unakufa mbavu?

Mara ya kwanza kuja mjini (Dar) jiji lilikukaribisha kwa style gani ukikumbuka kwa jinsi ulivyokuwa mshamba unakufa mbavu?

Precious Diamond

JF-Expert Member
Joined
Jun 9, 2023
Posts
593
Reaction score
1,376
Salaam Wakuu, natumai kaubaridi mwororo kawapapasa vyema huko mliko, twende kwenye mada.

Sehemu yoyote mjini inachukuliwa kama sehemu ya kutolea ushamba, kutokana na kupiga hatua kwenye mambo mengi na muingiliano mkubwa na watu kutoka sehemu mbalimbali ulimwenguni. Naona ndio hata mababu zetu wakaja na ule msemo mjini shule, shamba kilimo!

Mara ya kwanza kuja mjini jiji lilikupokeaje? Nini lifanyika ambacho ukifikiria leo unacheka sana nakusema kweli nilikuwa mshamba wakati wakati ule?!

Mimi mzaramo wa hapa hapa, kipindi kile walikuwa wanaita jiji la Makamba, ila kuna tukio lilitokea jamaa yetu mmoja, kipindi kile nilikuwa mdogo sana kuelewa kwanini baba na wengine walikuwa wanacheka wakati nasikia mtu kaibiwa, ila ndio jinsi jiji lilivyompokea na kumtoa ushamba!

Jamaa alikuwa katoka kijijini akiwa na mbuzi wa kutosha kuja kuuza Dar kwenye mnada, akafika salama na kuuza mbuzi wake vizuri akiwa na kitita chake cha milioni kadhaa. Sasa akawa anakuja home asalimie na kuangalia utaratibu wa kugeuza kurudi nyumbani kwake kesho yake au kesho kutwa yake.

Jamaa akakutana na vijana wa mjini, wawili, wana kichupa chenye vipande vya vitu vinanyong'aa wakimwambia ni dhahabu. Wakasema wanatafuta mteja ili warudi zao machimboni kuendelea na shughuli zao, wakampiga bei ya juu kidogo zaidi ya pesa zile alizonazo, jamaa amesikia sikia kuhusu madini na akawa na uhakika kile kichupa kitampa zaidi ya mara 10 ya pesa aliyopata kwenye kuuza mbuzi, akaingia tamaa.

Akawaambia jamaa mimi nina kiasi hiki hiki tu hakitoshi kununua chote, wakamwambia hamna shida tupe hiyo itafaa, tumezunguka mda mrefu kutafuta mteja, hata hii si mbaya ili turudi zetu machimboni. Jamaa akaona ameula, akachukua pesa zote akawapa.

Basi jamaa akaja nyumbani na bashasha kweli kweli kuwa amenunua almasi na sasa yeye ni tajiri, na amenunua kwa pesa ndogo tu, akaanza mpaka kupiga mahesabu ya jinsi atakavyonunua vitu kujenga nyumba na nk.

Sasa wakati stori zinaendelea mimi nikawa nimeshika hiko kichupa nakibiruarua na kuangalia dhahabu inayosemwa ikoje, mara pah, nikaangusha kichupa kikapasuka, kila kitu kikatawanyika, sio ndio "Almasi" yote ikamwagika, kuangalia ilikuwa vipande vya chupa (transparent) vimejazwa humo!

Jamani mzee alikufa mbavu mpaka machozi🤣🤣🤣, akaambiwa bwana mdogo karibu mjini, umepigwa hapa hakuna kitu, mama na wengine wakaungana kwenye vicheko, pole zikaja baadae sana. Aisee jamaa alinywea, na ndoto zote zikazima, aliyumba na kupata stress kiasi, kila akiniona anakumbuka tu nilivyovunja kichupa chake!

Wewe kwako ilitokea tukio gani ukikumbuka unasema kweli hapa nilikaribishwa mjini, kwakweli nilikuwa mshamba?
 
Nimeingia Dar es salaam kwa mara ya kwanza wiki moja kabla ya krismasi ya mwaka 1970. Nimeshuka pale Dar es salaam station kuu ya gari moshi asubuhi saa mbili kwa usafiri wa treni wakati huo ikiwa EAR ikifanya kazi kwa viwango vya kimataifa.
Kivutio nilichokiona wakati huo ni nyumba za ghorofa na nilishangaa sana watu kuishi kwenye nyumba za ghorofa. Bustani ya mnazi moja wakati huo ilikuwa Safi, nadhifu na mahali safi na salama kupumzika.
Nilifikia jengo moja la makazi kwenye kona ya mtaa wa Lumumba na Amani. Majengo maarufu wakati huo yakiwa jego la ushirika, kituo kikuu cha Polisi Central, Kilimanjaro hotel na jego la vijana WA TYL. ....Muda haugandi na mji umebadilika tena sana tu. 😆
 
Salaam Wakuu, natumai kaubaridi mwororo kawapapasa vyema huko mliko, twende kwenye mada.

Sehemu yoyote mjini inachukuliwa kama sehemu ya kutolea ushamba, kutokana na kupiga hatua kwenye mambo mengi na muingiliano mkubwa na watu kutoka sehemu mbalimbali ulimwenguni. Naona ndio hata mababu zetu wakaja na ule msemo mjini shule, shamba kilimo!

Mara ya kwanza kuja mjini jiji lilikupokeaje? Nini lifanyika ambacho ukifikiria leo unacheka sana nakusema kweli nilikuwa mshamba wakati wakati ule?!

Mimi mzaramo wa hapa hapa, kipindi kile walikuwa wanaita jiji la Makamba, ila kuna tukio lilitokea jamaa yetu mmoja, kipindi kile nilikuwa mdogo sana kuelewa kwanini baba na wengine walikuwa wanacheka wakati nasikia mtu kaibiwa, ila ndio jinsi jiji lilivyompokea na kumtoa ushamba!

Jamaa alikuwa katoka kijijini akiwa na mbuzi wa kutosha kuja kuuza Dar kwenye mnada, akafika salama na kuuza mbuzi wake vizuri akiwa na kitita chake cha milioni kadhaa. Sasa akawa anakuja home asalimie na kuangalia utaratibu wa kugeuza kurudi nyumbani kwake kesho yake au kesho kutwa yake.

Jamaa akakutana na vijana wa mjini, wawili, wana kichupa chenye vipande vya vitu vinanyong'aa wakimwambia ni dhahabu. Wakasema wanatafuta mteja ili warudi zao machimboni kuendelea na shughuli zao, wakampiga bei ya juu kidogo zaidi ya pesa zile alizonazo, jamaa amesikia sikia kuhusu madini na akawa na uhakika kile kichupa kitampa zaidi ya mara 10 ya pesa aliyopata kwenye kuuza mbuzi, akaingia tamaa.

Akawaambia jamaa mimi nina kiasi hiki hiki tu hakitoshi kununua chote, wakamwambia hamna shida tupe hiyo itafaa, tumezunguka mda mrefu kutafuta mteja, hata hii si mbaya ili turudi zetu machimboni. Jamaa akaona ameula, akachukua pesa zote akawapa.

Basi jamaa akaja nyumbani na bashasha kweli kweli kuwa amenunua almasi na sasa yeye ni tajiri, na amenunua kwa pesa ndogo tu, akaanza mpaka kupiga mahesabu ya jinsi atakavyonunua vitu kujenga nyumba na nk.

Sasa wakati stori zinaendelea mimi nikawa nimeshika hiko kichupa nakibiruarua na kuangalia dhahabu inayosemwa ikoje, mara pah, nikaangusha kichupa kikapasuka, kila kitu kikatawanyika, sio ndio "Almasi" yote ikamwagika, kuangalia ilikuwa vipande vya chupa (transparent) vimejazwa humo!

Jamani mzee alikufa mbavu mpaka machozi🤣🤣🤣, akaambiwa bwana mdogo karibu mjini, umepigwa hapa hakuna kitu, mama na wengine wakaungana kwenye vicheko, pole zikaja baadae sana. Aisee jamaa alinywea, na ndoto zote zikazima, aliyumba na kupata stress kiasi, kila akiniona anakumbuka tu nilivyovunja kichupa chake!

Wewe kwako ilitokea tukio gani ukikumbuka unasema kweli hapa nilikaribishwa mjini, kwakweli nilikuwa mshamba?
Mimi wakati naingia Dar enzi hizo Kwa mara ya kwanza kuna siku nikawa nazurula kulijua jiji vizuri nilikuwa mitaa ya uswazi Vingunguti huko vichochoroni nikakutana na tukio la kumtoa mwari yaani mabinti watatu wamekalishwa nje nyonyo ziko nje watu wamejaa wanacheza mchiriku!
Wakati mimi nashangaa tukio la wale warembo wabichi kuachwa nyonyo wazi kwenye umati mkubwa vile kumbe watu walikuwa busy kunishangaa mimi naonekana mshamba nimetoka bara😀
Bahati nzuri mpaka nakuwa mwenyeji sikuwahi kuibiwa pengine sababu ya mwonekano wangu nilikuwaga na mwonekano kama mwizi mwizi au mbabe flani hivi halafu nilikuwa nishapewa mbinu na wenyeji kwamba nikiulizwa nimetoka mkoa gani niseme Tabora maana enzi hizo watu wa Tabora walikuwa wanaogopeka sana kwa ubabe na ugomvi na kila aina ya uhuni na hata wakabaji wengi na wahuni wengi walikuwa watu wa Tabora.
Ndani ya muda mfupi nikaanza kupata kampani matafiki wengi mpaka tukaanza mishe za wizi wa mafuta ya transformers ambao kwa miaka hiyo ilikuwa inalipa sana
Mpaka sasa huwa nkitoka zangu hapa Dom nikienda Dar nna marafiki wengi wahuni wastaafu
 
Ukitaka kujua mama anajua kupika au hajui nenda kale na kwa jirani
Ukitaka kujua Dar ni kijiji kilichochangamka toka nje ya Tz nenda huko Istanbul Guangzhou Moscow Cairo Bangkok
Mkuu sasa uko unataka kutupeleka Duniani na sisi bado hatuna mawazo ya kufika uko.
 
Back
Top Bottom