Mara ya mwisho kupigwa, kupigana au kupiga mtu ilikuwa lini na kwanini?

Mara ya mwisho kupigwa, kupigana au kupiga mtu ilikuwa lini na kwanini?

mzee wa kasumba

JF-Expert Member
Joined
Nov 26, 2018
Posts
1,440
Reaction score
2,952
Kwakuwa watu wengi humu hatujuani imekuwa ni kawaida sana kila mtu kujitutumua na kujimwambafai sana katika hili jukwaa. Utasikia ooo nimempiga mtu mawashi, sijui nimemfanya mtu hivi na hivi ilhali siyo kweli (kwasababu tu hatukujui)

Twende kwenye point. Nini sababu ya kuandika uzi huu?

Ebwana leo katika pitapita zangu za kuzuga mjini hapa na pale (leo sikwenda kazini), nilipofika maeneo flani hivi nikamkuta demu mkaaali kasimama akiwa peke yake. Kutokana na kimbelembele changu bwana nikaona hebu ngoja nimsogelee nijaribu kumuimbisha maneno mawili matatu. Kwa bahati nzuri demu alionesha ushirikiano mzuri tu, huku na huku akatoa namba ya simu.

Ebwana kumbe yule mwanamke anamsubiri bwana (mchepuko) wake ambaye alikuwa ametoka kidogo. Kwa bahati mbaya zaidi, yule bwana alitokea kwa nyuma yangu mimi sikumuona. Nakuja kushitukia jamaa amenizaba bonge la kibao cha kichwa. Khaa! ile kutuliza wenge jamaa akawa ananambia kuwa "we unadhani kila mwanamke ni malaya tu fala we, Qumer makoh"

Sijakaa sawa jama kanibamiza ngumi ya kifua, sijakaa vema akarusha tena konde (gang) la uso ila nikaliona. Duuh! nikasema leo naumbuka aisee. Nikaona siyo kesi hebu ngoja tuzikinge kidogo (twende ringi) huku na huku nikam taimu nikamzawadia teke la mbupu moja maridhawa sana likamfanya mpaka akafika chini kwa uchungu.

Baada ya kuona jamaa yupo chini ikabidi tu nisepe wakati huo demu anapiga simu kwa watu wake wa karibu na watu walikuwa wameshaanza kujaa eneo la tukio.

KUSEMA KWELI:

Jamaa alinipiga (yaani nilipigwa vizuri tu) lile teke kama nilifanya kubahatisha baada ya kuona jamaa anataka kunidhuru sana. Sina sababu ya kusema najua kupigana wakati nafsi yangu inanisuta.

Ndugu yenu nimechezea kipondo kitakatifu, nashukuru tu sijavimba wala sijatoka damu.

NILICHOJIFUNZA LEO:

1. Kuna haja ya kuwa mazoezi ya self-defence japo kidogo, kama ningekuwa boya kabisa jamaa angeniuwa.

2. Jamaa uliyenipiga. Mwanangu nisikufiche, demu wako nitahakikisha ninamla.

Na nyie wanawake kama una bwana wako ukisimamishwa na mwanaume mwingine si uwe muwazi tu. Matatizo ya nini?

Sisi wengine ni wababe kitandani tu jamani, ngumi hatujui tutakuja kuuana bure.

mzee wa kasumba

Tiririka...
 
Kwa Mara ya mwisho kupigana ilikuwa 80' nikiwa shule ya msingi kwanza ndio nimehamia shule hio miaka ile kulikuwa na ubabe wa kijinga .kuingia jamaa akawa ananivimbia wadau wakaweka mchanga piga hapa halafu lips ng'ombe zangu ,basi tulipigana na hakupatika mshindi mpaka naondoka shule ile tuliluwa tukitizamana tu
 
Kwa Mara ya mwisho kupigana ilikuwa 80' nikiwa shule ya msingi kwanza ndio nimehamia shule hio miaka ile kulikuwa na ubabe wa kijinga .kuingia jamaa akawa ananivimbia wadau wakaweka mchanga piga hapa halafu lips ng'ombe zangu ,basi tulipigana na hakupatika mshindi mpaka naondoka shule ile tuliluwa tukitizamana tu
Duuu hatar
 
Kwakuwa watu wengi humu hatujuani imekuwa ni kawaida sana kila mtu kujitutumua na kuji mwambafai sana katika hili jukwaa. Utasikia ooo nimempiga mtu mawashi , sijui nimemfanya mtu hivi na hivi ilhali sio kweli. (kwasababu tu hatukujui)

Twende kwenye pont.

Nini sababu ya kuandika uzi huu?

Ebwana leo katika pita pita zangu za kuzuga mjini hapa na pale (leo sikwenda kazini) nilipofika maeneo flani hivi nikamkuta demu mkaaali kasimama akiwa peke yake. Kutokana na kimbelembele changu bwana nikaona hebu ngoja nimsogelee nijaribu kumuimbisha maneno mawili matatu. Kwabahati nzuri demu alionesha ushirikiano mzuri tu, huku na huku akatoa namba ya simu.

Ebwana kumbe yule mwanamke anamsubiri bwana (mchepuko) wake ambaye alikuwa ametoka kidogo. Kwabahati mbaya zaidi, yule bwana alitokea kwa nyuma yangu mimi sikumuona... Nakuja kushitukia jamaa amenizaba bonge la kibao cha kichwa. Khaa ile kutuliza wenge jamaa akawa ananambia kuwa "We unadhani kila mwanamke ni malaya tu fala we, Qumer makoh"

Sijakaa sawa jama kanibamiza ngumi ya kifua, sijakaa vema akarusha tena konde (gang) la uso ila nikaliona

Duuh nikasema leo naumbuka aisee. Nikaona sio kesi hebu ngoja tuzikinge kidogo (twende ringi) huku na huku nikam taimu nikamzawadia teke la mbupu moja maridhawa sana likamfanya mpaka akafika chini kwa uchungu.

Baada ya kuona jamaa yupo chini ikabidi tu nisepe wakati huo demu anapiga simu kwa watu wake wa karibu na watu walikuwa wameshaanza kujaa eneo la tukio.

KUSEMA KWELI
Jamaa alinipiga (yaani nilipigwa vizuri tu) lile teke kama nilifanya kubahatisha baada ya kuona jamaa anataka kunidhuru sana. Sina sababu ya kusema najua kupigana wakati nafsi yangu inanisuta.

ndugu yenu nimechezea kipondo kitakatifu, nashukuru tu sijavimba wala sijatoka damu.



NILICHOJIFUNZA LEO
1. Kuna haja ya kuwa mazoezi ya self defence japo kidogo, kama ningekuwa boya kabisa jamaa angeniuwa.

2. Jamaa uliyenipiga. Mwanangu nsikufiche demu wako nitahakikisha ninamla

nanyie wanawake kama una bwana wako ukisimamishwa na mwanaume mwingine si uwe muwazi tu. Matatizo ya nini?


SISI WENGINE NI WABABE KITANDANII TU JAMANI, NGUMI HATUJUI TUTAKUJA KUUWANA BUREE


mzee wa kasumba


NI LINI MARA YA MWISHO KUPIGWA, KUPIGANA, KUPIGA MTU na ilikuwa ni kwasababu gani?




TIRIIIIIIRIKA
nikimaliza week moja bila kupigana naumwa kabisa.
 
dah nimewah kupigwa na jamaa. mi napenda saana mpira afu ni mshabiki wa man u.siku moja tulikua tunacheza man u na chelsea.hii mechi kawaida huwa inakelele saana na mimi ndo nilikua na kelele mle ndani na nakumbuka man u tulishindaga 2-1 goli la pili alifunga lingard kutokea sub.mimi nilikaa mbele ya jamaa wa chelsea baada ya kuwafunga nikawa na kelele saana.jamaa akanambia namtinga mbele haoni. nikamwambia weee mpumbavu utanambia nini wewe kwa dharau. daah kumbe jamaa kachukia. alinisogelea nikashtukia kanipiga kichwa kimoja matata saana nikaona maluelue mpaka kudondokea ving'amuzi.ile nainuka nakutana na ngumi ya uso nikadondoka chini tena na ilikua karibu na mlango.nilivyo inuka niliangalia mlango nikatoka nduuki break maskan na kelele zoote ziliisha.asubuh niliamka nimevimba uso nilikua kituko mtaani.
 
Wiki ilopita, tulizipiga na bro wangu. Amekuja kwangu,akakata mpira wa kunyeshea bustani maji. Shemeji yenu akanipigia simu,jamaa alikuwa tungi. Nilikuwa mbali,nilitamani nikodishe bombadia. Jioni nilimwuliza nini shida hadi afikie hatua ile kukoseana adabu,tulizichapa kwa mzee wetu. Kesi ya ukoo inaendelea
 
Back
Top Bottom