MARADHI YA KUHARISHA:
MARADHI ya kuharisha ni maradhi ambayo
mgonjwa hupata haja kubwa mara kwa mara na
haja kubwa huwa laini na wakati mwingine
huambatana na gesi au maumivu.
SABABU ZAKE:
(1) Kula chakula kichafu.
(2) Kula chakula kilichoingia viini vya maradhi.
TIBA:
Kanuni ya kwanza:
Chukua kijiko kimoja cha Maua ya babu naji
(chamomile) ukoroge ndani ya kikombe cha chai na
Kanuni ya pili:
Chukua anisuni (aniseed) kijiko kimoja kidogo
uweke ndani ya kikombe kimoja cha chai cha maji
ya moto yaliyochemka kisha ukoroge. Wacha dawa
ikae ndani ya maji dakika tano kisha uchuje halafu
uongeze asali kijiko kimoja. unywa kikombe kimoja
kutwa mara mbili.
Zaidi ya hayo, tukuweke wazi tu kuwa, dawa hii
pia huvipa nguvu jamii ya viungo vya kulia
chakula.
Kanuni ya tatu:
Chukua majani ya nanaa na utayarishe dawa kama
mfano wa hapo juu kuhusu anisuni.
Kanuni ya nne:
Chukua zaatar na uandae dawa kama mfano wa
hapo juu kuhusu majani ya nanaa na anisuni.
maji ya moto. Yakishapoa unywe bila ya kuongeza
sukari.Fanya hivyo kutwa mara tatu. Ndani ya
babunaji mna virutubisho vyenye uwezo wa
kusitisha kuharisha.
Kanuni ya tano
Changanya kijiko kimoja cha mafuta ya habat soda
ndani ya glasi moja ya maziwa ya mtindi unywe
glasi moja kutwa mara mbili.
KICHEFUCHEFU NA KUTAPIKA:
Hali ya kujisikia kuwa unataka kutapika lakini
hutapiki inaitwa kichefuchefu (Nausea). Hali hii ni
kawaida sana hasa wakati unaposafiri kwa chombo
kama meli au ndege, hali ya ujauzito,kupata harufu
mbaya, kuona au kuhisi kinyaa baada ya kuona
kitu au chakula Fulani kibaya chenye ladha na
harufu mbaya, wengine hupata kichefuchefu
akimuona mtu mwengine akitapika. Hali ya
kichefuchefu humsababishia mtu kuweza kutapika
wakati mwingine.
TIBA:
Chukua kijiko kimoja kidogo cha unga wa pilipili
manga ukoroge ndani ya glasi moja ya maji halafu
ukamulie ndani yake ndimu nusu. Kunywa glasi
moja kutwa mara tatu.
GESI TUMBONI (COLIC):
Ikiwa mtu atakula kwa wingi vyakula vinavyoleta
gesi halafu vyakula hivyo visisagike vizuri
tumboni, hukusanya gesi tumboni na kufanya
mingurumo humo na kumsababishia maumivu,
humkosesha mtu utulivu na kumfanya kutoka
jasho na machovu bila ya kufanya kazi.
Mtu hujisikia mara kwa mara aende haja kubwa na
akienda hapati choo. Pia humsababishia mtu
kuumwa kwa mgongo au kiuno.
Ikiwa gesi hii itakosa kutoka kwa njia ya haja
kubwa, basi yaweza kupanda juu na kufanya
presha sehemu au karibu ya moyo na kusababisha
maumivu ya moyo.
TIBA:
Chukua Asali safi mbichi iwe ya Asali ya nyuki robo lita , unga wa arki susi vijiko
vitatu vikubwa na unga wa habat soda vijiko viwili
vikubwa. Koroga zote pamoja kwa kijiko. Chukua
vijiko viwili vya mchanganyiko huu ukoroge ndani
ya kikombe cha maji ya moto halafu yakishapoa
unywe kikombe kimoja kutwa mara mbili asubuhi
na jioni.
Ugonjwa wa BAWASIRI (MGORO): hemorrhoids, piles
Haya ni maradhi ambayo humsibu mgonjwa
sehemu ya haja kubwa ambayo humsababisha
kupata maumivu.
DALILI ZAKE:
(1) Kupata choo kigumu.
(2) Kutokwa damu sehemu ya haja kubwa
baada ya kujisaidia.
(3) Muwasho au maumivu na joto kali sehemu
ya bawasiri.
(4) Kupata maumivu wakati unapokaa.
(5) Vidonda au kutokwa nje na kijinyama
sehemu ya kutokea haja kubwa.
(6) Upungufu wa nguvu za kiume.
TIBA:
Jambo la kwanza kabla ya tiba mgonjwa aweze
kutibiwa maradhi ya kutopata choo vizuri ikiwa
anayo kwa sababu huzidisha maradhi haya. Pia
epuka kula Nyama hasa ya ngombe, Pilipili na vitu
vikali. Halkadhalika usinywe maziwa kwa wingi.
Kanuni ya kwanza:
Kunywa juisi ya tikiti maji asubuhi kabla ya
chakula na usiku kabla ya kulala.Dawa hii hutibu
na kuondoa maumivu ya bawasiri.
Kanuni ya pili:
Chukua asali nusu lita , unga wa kamun aswad
vijiko vitatu vikubwa,unga wa Habat soda vijiko
vitatu vikubwa na unga wa kamun abyadh vijiko
viwili vikubwa. Vitu vyote hivi vichanganye
pamoja kwa kuvikoroga kwa kijiko. Chukua vijiko
viwili vikubwa vya mchanganyiko huu kisha
ukoroge ndani ya kikombe cha maji ya moto.
Yakishapoa uchuje halafu unywe kikombe kimoja
kutwa mara mbili asubuhi na jioni. Ikiwa ni
bawasiri ya kutoka nje au yenye vidonda, paka
mafuta ya nyonyo au mafuta ya lozi. na pia uende Hospitali kufanya oparesheni kuiondowa kabisa hiyo iliyotoka nje Bawasiri.
VIDONDA VYA TUMBO (ULCERS):
Haya ni maradhi ambayo hufanya vidonda upande
wa ndani ya ukuta wa tumbo. Kuna Duodenal
ulcer na Gastric ulcer.
DALILI:
(1) Kupata maumivu makali chini ya kifua kwa
upande wa ndani.
(2) Kuchoka bila sababu.
(3) Kuumwa kwa mgongo au kiuno.
(4) Kupungua kwa nguvu za kiume.
(5) Kuwa na kichefuchefu baadhi ya wakati.
(6) Kuwa na kiungulia .
(7) Tumbo kujaa gesi.
(8) Tumbo kuwaka moto.
(9) Kukosa choo na wakati mwingine kupata
choo kigumu kama cha mbuzi.
(10) Kukosa hamu ya kula.
(11) Kutapika damu au wakati mwingine
kutapika nyongo.
(12) Maumivu makali baada ya kula vitu vikali
au chakula cha moto.
TIBA:
Kanuni ya kwanza:
Chukua Asali safi mbichi ya nyuki robo lita uchanganye na unga wa arki
susi vijiko vinne vikubwa kisha ukoroge kwa
kijiko. Chukua vijiko viwili vikubwa vya
mchanganyiko huu ukoroge ndani ya kikombe cha
maji ya moto. Yakishapoa unywe kikombe kimoja
kutwa mara tatu.
Kanuni ya pili:
Chukua viazi vya mviringo (vya chipsi) kama
vitatu halafu uvikoshe na kuvimenya. Baada ya
kuvimenya upate juisi yake kwa kuvisaga kwenye
blenda. Kunywa vijiko vitatu vikubwa vya chakula
kutwa mara mbili.
Kanuni ya tatu:
Chukua lozi gramu 30 halafu usage iwe unga.
Changanya lozi hii yote ndani ya kikombe kidogo
cha maziwa ya moto kisha uongeze asali vijiko
viwili vikubwa. Kunywa kikombe kimoja robo saa
kabla ya kula chakula cha asubuhi. Fanya hivyo
kwa muda wa mwezi na utapata shifaa