Marafiki hawadumu wanakuja na kuondoka, tuliowahi kuwa mabesti nao leo tunaishia kuchunguliana status hata "hi" hakuna

Marafiki hawadumu wanakuja na kuondoka, tuliowahi kuwa mabesti nao leo tunaishia kuchunguliana status hata "hi" hakuna

round kick

JF-Expert Member
Joined
Feb 3, 2025
Posts
345
Reaction score
1,145
Rafiki wa mtaani, shuleni, chuo, n.k. mlikuwa washikaji sanaaaa kujuliana hali kila siku, muda mwingi mpo wote, kushare siri, n.k. lakini leo mmebaki kuchunguliana view stutus,

Halafu hata mkikutana ni salam za dakika 2 tu, baada ya hapo kila mtu anajidai yupo bize, mnabadilishana za kuchunguliana status,

Nje ya marafiki tunaoishia kuangaliana status nina visa hivi

Kuna siku flani nilikuwa napoteza muda naendesha gari mtaani nilikuwa nimerudi kusalimia mkoani nilikokulia, nikamuona rafiki yangu tuliwahi kuwa mabesti sana primary, vile nilivyomona na yeye aliniona ila akazuga kama hajaniona (niligungua badae) , nikaona niende kupaki gari sehemu ya mbele kidofo maana mazingira hayakuruhusu, nilivyopaki nimeshuka namuona mtu kaongeza mwendo wa kutembea kaingia njia nyingine, nikawasha gari fasta niende mtaa wa barabara atayotokea, mara hii macho yaligongana hakuweza kunizuia, tulisalimiana kidogo ila akaniambia ana haraka, namba aliyonipa haipatikani, sijui sababu lakini labda pengine ni gepu la maendeleo niliambiwa hali yake si nzuri

Niliwahi kuwa na rafiki alikuwa anapenda kunitembelea sana kupiga story, yeye alishatoboa tangu akiwa 22 tayari alikuwa na gari yake, sijui hata kilichotokea mara paap mawasiliano yakapungua, off course mpaka leo tukiwa kwenye 30s bado tunachekiana ila ni zile kupeana heri ya mwaka mpya, story imeisha,

Niliwahi kuwa na rafiki tuliekuwa mbali kwa mwaka moja tu, lakini tunatazamiana status na kupeana hi mara kadhaa japo mara chache, alikuwa ameenda mafunzo idara ya ulinzi akabahatika kupata kazi, aliposti video anavishwa cheo kwenye bega, nilimpa hongera ila hakujibu (Blue tick), mara ya pili niliwahi kumpa heri ya mwaka mpya ila hakujibu, damn ! baada ya mwaka na mimi nilibahatika kwenye shughuli zangu, mimi napenda sana magari nilinunua nikajipost status nikiwa safarini ndipo aliponijulia hali "za siku kaka naona mambo yamejipa" nilibaki na maswali mengi

Nimefikia muafaka kukubaliana na ukweli mchungu, hakuna marafiki wa kudumu, marafiki huja na kuondoka kutokana na mazingira mapya, tabia mpya, nyakati za maisha, n.k. hawa wengine tunaishia kuchunguliana status tu.

Too bad kuna wengine wanapoteza marafiki wote maana kujenga urafiki mpya ni kitu kizito kwa wengine
 
rafiki zangu wa mtaani, shuleni, chuo, n.k. tulikuwa washikaji sanaaaa kujuliana hali kila siku, muda mwingi tupo wote, kushare siri, n.k. lakini leo tumebaki kuwa tuna view stutus,

Halafu hata mkikutana ni salam za dakika 2 tu, namba tunazopeana ni za kuchunguliana status
Good bye Dr. Elihuruma Herman Joseph
 
rafiki wa mtaani, shuleni, chuo, n.k. mlikuwa washikaji sanaaaa kujuliana hali kila siku, muda mwingi mpo wote, kushare siri, n.k. lakini leo mmebaki kuchunguliana view stutus,

Halafu hata mkikutana ni salam za dakika 2 tu, baada ya hapo kila mtu anajidai yupo bize, mnabadilishana za kuchunguliana status,

Ninatoa kisa cha ukweli, Kuna siku flani nilikuwa napoteza muda naendesha gari mtaani, nikamuona rafiki yangu tuliwahi kuwa mabesti sana primary, vile nilivyomona na yeye aliniona ila akakaza shingo mbele baada ya kuniona, nikaona niende kupaki gari sehemu flani namuona mtu kaongeza mwendo wa kutembea ni kama hataki tuonane, nikawasha gari fasta niende mtaa wa barabara atayotokea, mara hii macho yaligongana hakuweza kunizuia, tulisalimiana kidogo akaniambia ana haraka, namba aliyonipa haipatikani,
Aisee JF ni zaidi ya maarifa!Mimi kuna Jamaa alikuwa Best wangu, wakati flani nilibahatika kupata kazi kabla yake akawa anakuja likizo nilipokuwa nafanyia kazi Eeh bwanaee!kapata kazi mambo kwake mazuri hata simu zangu hapokei Huu sio Ubinadamu ni unyama kwa kweli.
 
Me nilikuwaga na mwana fln tangu tukiwa watoto. Baada ya kuhitimu aliwahi kupata kazi kabla yangu urafki uliyumba Sanaa. Hata hivyo nilijua shida ikowapi nlikaza baadae nlpata kazi hata ivyo ubest ulitoweka kabisa. Mwezi jana alipunguzwa kazin kwa makosa ya kinidhamu huwa ananichek mara kwa mara hata ivyo nilimpunguza kwenye cycle ya mabest zangu amebaki kama ndugu tu.
 
rafiki wa mtaani, shuleni, chuo, n.k. mlikuwa washikaji sanaaaa kujuliana hali kila siku, muda mwingi mpo wote, kushare siri, n.k. lakini leo mmebaki kuchunguliana view stutus,

Halafu hata mkikutana ni salam za dakika 2 tu, baada ya hapo kila mtu anajidai yupo bize, mnabadilishana za kuchunguliana status,

Ninatoa kisa cha ukweli, Kuna siku flani nilikuwa napoteza muda naendesha gari mtaani nilikuwa nimerudi kusalimia mkoani nilikokulia, nikamuona rafiki yangu tuliwahi kuwa mabesti sana primary, vile nilivyomona na yeye aliniona ila akazuga kama hajaniona (niligungua badae) , nikaona niende kupaki gari sehemu ya mbele kidofo maana mazingira hayakuruhusu, nilivyopaki nimeshuka namuona mtu kaongeza mwendo wa kutembea kaingia njia nyingine, nikawasha gari fasta niende mtaa wa barabara atayotokea, mara hii macho yaligongana hakuweza kunizuia, tulisalimiana kidogo ila akaniambia ana haraka, namba aliyonipa haipatikani,
Hehehe!!!
 
rafiki wa mtaani, shuleni, chuo, n.k. mlikuwa washikaji sanaaaa kujuliana hali kila siku, muda mwingi mpo wote, kushare siri, n.k. lakini leo mmebaki kuchunguliana view stutus,

Halafu hata mkikutana ni salam za dakika 2 tu, baada ya hapo kila mtu anajidai yupo bize, mnabadilishana za kuchunguliana status,

Ninatoa kisa cha ukweli, Kuna siku flani nilikuwa napoteza muda naendesha gari mtaani nilikuwa nimerudi kusalimia mkoani nilikokulia, nikamuona rafiki yangu tuliwahi kuwa mabesti sana primary, vile nilivyomona na yeye aliniona ila akazuga kama hajaniona (niligungua badae) , nikaona niende kupaki gari sehemu ya mbele kidofo maana mazingira hayakuruhusu, nilivyopaki nimeshuka namuona mtu kaongeza mwendo wa kutembea kaingia njia nyingine, nikawasha gari fasta niende mtaa wa barabara atayotokea, mara hii macho yaligongana hakuweza kunizuia, tulisalimiana kidogo ila akaniambia ana haraka, namba aliyonipa haipatikani,
Marafiki zako ni familia Yako
 
Me nilikuwaga na mwana fln tangu tukiwa watoto. Baada ya kuhitimu aliwahi kupata kazi kabla yangu urafki uliyumba Sanaa. Hata hivyo nilijua shida ikowapi nlikaza baadae nlpata kazi hata ivyo ubest ulitoweka kabisa. Mwezi jana alipunguzwa kazin kwa makosa ya kinidhamu huwa ananichek mara kwa mara hata ivyo nilimpunguza kwenye cycle ya mabest zangu amebaki kama ndugu tu.
Ukimuhurumia sana mpeleke shambani akale kwa kubujikwa na machozi kama Lukas Mwashambwa!
 
Back
Top Bottom