Marafiki hawadumu wanakuja na kuondoka, tuliowahi kuwa mabesti nao leo tunaishia kuchunguliana status hata "hi" hakuna

Marafiki hawadumu wanakuja na kuondoka, tuliowahi kuwa mabesti nao leo tunaishia kuchunguliana status hata "hi" hakuna

Rafiki wa mtaani, shuleni, chuo, n.k. mlikuwa washikaji sanaaaa kujuliana hali kila siku, muda mwingi mpo wote, kushare siri, n.k. lakini leo mmebaki kuchunguliana view stutus,

Halafu hata mkikutana ni salam za dakika 2 tu, baada ya hapo kila mtu anajidai yupo bize, mnabadilishana za kuchunguliana status,

Nje ya marafiki tunaoishia kuangaliana status nina visa hivi

Kuna siku flani nilikuwa napoteza muda naendesha gari mtaani nilikuwa nimerudi kusalimia mkoani nilikokulia, nikamuona rafiki yangu tuliwahi kuwa mabesti sana primary, vile nilivyomona na yeye aliniona ila akazuga kama hajaniona (niligungua badae) , nikaona niende kupaki gari sehemu ya mbele kidofo maana mazingira hayakuruhusu, nilivyopaki nimeshuka namuona mtu kaongeza mwendo wa kutembea kaingia njia nyingine, nikawasha gari fasta niende mtaa wa barabara atayotokea, mara hii macho yaligongana hakuweza kunizuia, tulisalimiana kidogo ila akaniambia ana haraka, namba aliyonipa haipatikani, sijui sababu lakini labda pengine ni gepu la maendeleo niliambiwa hali yake si nzuri

Niliwahi kuwa na rafiki alikuwa anapenda kunitembelea sana kupiga story, yeye alishatoboa tangu akiwa 22 tayari alikuwa na gari yake, sijui hata kilichotokea mara paap mawasiliano yakapungua, off course mpaka leo tukiwa kwenye 30s bado tunachekiana ila ni zile kupeana heri ya mwaka mpya, story imeisha,

Niliwahi kuwa na rafiki tuliekuwa mbali kwa mwaka moja tu, lakini tunatazamiana status na kupeana hi mara kadhaa japo mara chache, alikuwa ameenda mafunzo idara ya ulinzi akabahatika kupata kazi, aliposti video anavishwa cheo kwenye bega, nilimpa hongera ila hakujibu (Blue tick), mara ya pili niliwahi kumpa heri ya mwaka mpya ila hakujibu, damn ! baada ya mwaka na mimi nilibahatika kwenye shughuli zangu, mimi napenda sana magari nilinunua nikajipost status nikiwa safarini ndipo aliponijulia hali "za siku kaka naona mambo yamejipa" nilibaki na maswali mengi

Nimefikia muafaka kukubaliana na ukweli mchungu, hakuna marafiki wa kudumu, marafiki huja na kuondoka kutokana na mazingira mapya, tabia mpya, nyakati za maisha, n.k. hawa wengine tunaishia kuchunguliana status tu.

Too bad kuna wengine wanapoteza marafiki wote maana kujenga urafiki mpya ni kitu kizito kwa wengine
Nyakati zinabadilika jifunze kubadilika nazo😄
 
Nimepoteza marafiki zangu wengi nilipoolewa aisee...wengine naumia maana nikikumbuka moments zetu pindi tupo chuoni daah...sema ndo hivyo no way out...unakuta unamtafuta mtu ww tuu...yani inakua one side communication..unaamua kuacha tuu..
Kuna best angu urafiki umekoma juzi juzi kisa tuu sijamchangia mdogo wake alikua anaoa kiasi cha hela alonichangia kwny harusi yangu jamani tena alikua anakumbushia mimi nilikutolea hii...so mm nimetoa hela ya kadi..as long as harusi iko mbali na nisingeweza kuhudhuria nikamwabia ukiolewaga ww ndo ulalamike akanchunia nahisi kaniblock...
Niliumia basi nimeachana nae...any way maisha nadhani ndivyo yalivyo..
Uzi umenigusa...
 
Kuna tofauti kubwa kati ya rafiki na mtu wako wa karibu.
Lakini pia sio kile ulie soma nae, kuishi nae mtaa mmoja anaweza akawa rafiki.
Mkuu, kuna watu wanazaliwa kwa baba na mama mmoja lakini sio lazima wawe marafiki.
Na mwisho kabla sijasahau......
Mwanaume sio poa sana kujiendekeza kwenye hizo mambo za status mazee....[emoji3525]
Umeongea ukweli halisi.
 
Nimepoteza marafiki zangu wengi nilipoolewa aisee...wengine naumia maana nikikumbuka moments zetu pindi tupo chuoni daah...sema ndo hivyo no way out...unakuta unamtafuta mtu ww tuu...yani inakua one side communication..unaamua kuacha tuu..
Kuna best angu urafiki umekoma juzi juzi kisa tuu sijamchangia mdogo wake alikua anaoa kiasi cha hela alonichangia kwny harusi yangu jamani tena alikua anakumbushia mimi nilikutolea hii...so mm nimetoa hela ya kadi..as long as harusi iko mbali na nisingeweza kuhudhuria nikamwabia ukiolewaga ww ndo ulalamike akanchunia nahisi kaniblock...
Niliumia basi nimeachana nae...any way maisha nadhani ndivyo yalivyo..
Uzi umenigusa...
Poleee Dear!!
 
Marafiki wengi uwa wako kimaslahi zaidi, ndio maana ukiwa na pesa na marafiki wanakua wengi na zikiisha wanakukimbia unabaki mwenyewe. Marafiki wengine unaweza ukawa huna kitu ila wamekuotea kuna siku utakua vizuri kwa hio wanakua na wewe tu, lakini ukweli ni kua URAFIKI NI UNAFIKI. Urafiki wa kweli ni familia yako.
 
Nimepoteza marafiki zangu wengi nilipoolewa aisee...wengine naumia maana nikikumbuka moments zetu pindi tupo chuoni daah...sema ndo hivyo no way out...unakuta unamtafuta mtu ww tuu...yani inakua one side communication..unaamua kuacha tuu..
Kuna best angu urafiki umekoma juzi juzi kisa tuu sijamchangia mdogo wake alikua anaoa kiasi cha hela alonichangia kwny harusi yangu jamani tena alikua anakumbushia mimi nilikutolea hii...so mm nimetoa hela ya kadi..as long as harusi iko mbali na nisingeweza kuhudhuria nikamwabia ukiolewaga ww ndo ulalamike akanchunia nahisi kaniblock...
Niliumia basi nimeachana nae...any way maisha nadhani ndivyo yalivyo..
Uzi umenigusa...
Pole dear mi nipo kwa ajili yako mtani wangu 🤗😊
 
Back
Top Bottom