Marafiki wanafiki wamponza Rich Mavoko. Mwenyewe ajutia na kusaga meno

Watanzania kwa kutungia maisha ya wenzao mistari ni hatari aisee
 
Weekend iliyopita tu tuĺikuwa nae Tanga na kapiga show fresh tu.

Mafanikio hayapo tu WCB
 
Haaaahaaaa chigeeee[emoji119][emoji119]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mavoko oyeeeeee
Handsome man
Bora alipo sasa kuliko alipokuwa kabla.. yupo huruuuuuu
[emoji16] [emoji16] [emoji16] [emoji16] [emoji16] Mimi sijui kuimba tu ila ni handsome kuliko mavoko, vipi nikutolee mahari baby

Super hero daddy
 
Mambo machache ya kishabiki kwenye post yako
1. Alikua na ugumu wa maisha kabla ya kujiunga WCB, kauli kama hii inatakiwa kuja na uthibitisho wa kitu gani alifanya akiwa WCB kuonesha kweli maisha yalimwendea vizuri ambacho hakuweza kukifanya huko nyuma. Kama kumbukumbu zangu ziko vizuri ni kwamba usanii ulimlipa kitambo hadi akaamua kuacha kazi yake ya ualimu na kujiajiri rasmi kwenye muziki.
2. Unadai Diamond aliyaona mataabiko ya Rich na kumchukua WCB, lakini ninavyofahamu mimi Rich kahamia WCB akiwa na nyimbo zinazotamba na alikua na heshima ya kutosha, labda kama kulikua na mataabiko mengine nyuma ya pazia ambayo sisi tunaowaona kwenye TV wamependeza hatuyajui.
3. Unadai akiwa ndani ya WCB mafanikio yakapanda, hapa narudia nililosema kwenye point ya kwanza kwamba utuletee uthibitisho, maana kwa maoni yangu Rich alishuka kimuziki alipoingia WCB, wimbo pekee uliotamba ni Sheri aliyofanya na Fid Q.
4. Umesema kitu alichokua anakitegemea ni clouds na Ruge (hili linaweza kuwa kweli), lakini point hii inakosa mashiko unaposema clouds imeanza kuyumba baada ya kifo cha Ruge, ni kipimo gani unachotumia kupima kuyumba kwa taasisi wiki mbili baada ya kifo cha kiongozi aliekua hospitali kwa zaidi ya miezi sita? Clouds inaweza kuyumba kutokana na kutokuwepo Ruge, lakini sio leo, ni hadi pale itakapofikia hatua ya kuhitaji mawazo mapya.
5. Hapati show, na akipata malipo ni kiduchu! Huko WCB alipata show ngapi za maana unazozitambua? Na mikataba yake ya siku hizi umeiona au umehisi tu?
6. Amerudi nyuma kimuziki! Hili ni kweli kabisa, lakini alianza kurudi nyuma tangu alipojiunga WCB.

Ni kweli kabisa tamaa zilimponza, tamaa za kutaka kung’aa kama wasanii wa WCB, kumbe wenzake hawakua na nia njema ya kumg’arisha


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
WCB nao wajiandae tu kubebeshwa lawama na Wasanii kama wao walivyomlamu Marehemu.

Wao waendelee kusajili tu Wasanii na wadhani wao ni Malaika kwamba watamridhisha kila mmoja.
 
Watu wana Changanya Kutoboa Kimziki na kuwa na hela..

mavoko alikuwa kesha toboa ki mziki kabla ya WCB lakin mtonyo ulikuwa wa mawazo... Kaingia WCB akapata chanel nying ya kupiga pesa.... Mafala wakajaza maneno..akajitoa.. Na chanel ndio zikapaaa..


Alipo kuwa WCB kutoka na mtonyo alio kuwa anaupata.. Kuna Life style alio kuwa akiish , sasa mtonyo ndio hvyo wa mawazo..


Na ndio kinacho mpa stress

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu unaposema wimbo pekee wa Mavoko uliotamba akiwa na Wcb ni Sheri unamaanisha nini au na wewe umetumia vigezo gani? Vipi kuhusu hizi ngoma nyingine inamaana zilibuma?

1.Rudi ft. Patoranking
2. Ibaki stori
3.Kokoro ft. Diamond


Sent using Jamii Forums mobile app
 
[emoji16] [emoji16] [emoji16] [emoji16] [emoji16] Mimi sijui kuimba tu ila ni handsome kuliko mavoko, vipi nikutolee mahari baby

Super hero daddy

Duh
Ngoja nimuambie kwanza mjomba angu wa humu Mshana Jr apokeee hizo milioni 100 unazotaka kuzitoa.
 
Duh
Ngoja nimuambie kwanza mjomba angu wa humu Mshana Jr apokeee hizo milioni 100 unazotaka kuzitoa.
Milioni 100 duh nanunua kiwanda au namtolea mahari mke mtarajiwa,

Happiness is a lifestyle
 
Milioni 100 duh nanunua kiwanda au namtolea mahari mke mtarajiwa,

Happiness is a lifestyle

Unawekeza ili uishi kwa furaha baadae.. hata ukijenga kiwanda mke mtarajiwa atakisimamia na kitazaa matunda mengi chini yake.
 
Tumekusikia mchepuko wa diamond

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…