Marais Wa Africa na Ushirikina. Chanzo cha kutoendelea nchi nyingi za Afrika

Marais Wa Africa na Ushirikina. Chanzo cha kutoendelea nchi nyingi za Afrika

Pamoja na hayo wengi wamekuwa wakiangukia pua vibaya tumeona Gambia nk,nguvu za giza huwa si za kudumu,ni sawa na kucheza mpira wa puto kwenye mimba, ni imani tu zisizo na uhalisia zaid ya kukuongezea kujiamini bandia, zingekuwa na nguvu zingewasaidia waafrika wasitawaliwe au kuchukuliwa utumwani, maana zamani kulikuwa na magwiji kuliko sasa au ingewasaidia majambazi wasikamatwe au kuuwawa, sababu hakuna jambazi asie mshirikina.

Sent from my TECNO-L8Plus using JamiiForums mobile app
 
Maelezo yako no ya kweli.lakini hio in utamaduni wetu.wazungu nao wana mambo yao km.France kuna kabila la waroma ni wachawi sana. Ujerumani wapo jimbo la Bavaria na parts ya east Germany. Italy wapo kibao sehemu za Vernice na na Sicily. Halafu kuna hawa skull&bones. Kuna vyama vingi tuu vya kichawi. Rais wa Ufaransà kaoa mamake iko sawa hio ? huoni kuna siri ya sifuri hapo ? .nikusaidie tuu ukubwa unamambo sana.

Sent from my TECNO-Y2 using JamiiForums mobile app
 
#2 ni kama imemlenga hb

Sent from my SM-G532F using JamiiForums mobile app
 
Viongozi wa kizungu wanawazidi hawa wa kwetu mara 110, amini msiamini, nimeshuhudia kwa macho yangu!
Wawo kiboko na wakaniteka akili kabisa kabisa, nimewakubali, sio huu wa kiafrika bana! Viongozi wa kizungu uchawi wao wa kwanza, miundo mbinu matata kabisa, pili na kuendelea, maji, umeme, afya bora, ustawi wa jamii, maendeleo ya kufa mtu, wamewamaliza kabisa wananchi wao, hawasikii wala hawaoni, hata mie nilipoenda soma kule, hilo limbwata lilinipata, nikawehuka, mpaka niliporudi na kukutana na ule uchafu JK Nyerere fahamu zote zikanirudia! Aacha kabisa na wazungu, wale kiboko aise, wana mandege, matreni kama basi, treni yaenda kasi kama ndege! Kuna mpaka treni inapita chini ya ardhi, nyie juu wala hamsikii! Shenzi kabisa wale, ukienda hata benki sio lazima foleni, mashine kutumbukiza hela, kutoa hela, kutumbukiza cheki! Hospitali napo, huna haja ya kuona receptionist, wewe wagonga tu kwenye kama kakompyuta ukutani jina na tarehe ya kuzaliwa wakaa, muda si muda jina lako latokea kwenye mkanda uko juu kama airport uende chumba gani kwa daktari! Na dawa zozote ukitaka zipo, hamwezi kuamini wala huna haja ya kutoa rushwa upate! Acha hivyo, waweza kaa nyumbani na ka laptop ukaagiza ngosha kuanzia mazagazaga yote mpaka nyama! Teksi na daladala zina barabara zake, daladala hazina konda, ni yule yule dereva, teksi napo hakuna kubishana na dereva, unaangalia mita tu walipa waenda zako, Bar hakuna kuletewa bia, waenda kaunta, ukimaliza tena, hakuna cha bill wala barmaid wa kukupandishia bill au bei za ajabu za vinywaji! Upuuzi kabisa, washirikina sana wale! Shule watoto bure mpaka chuo, huko wanapewa mikopo watakayolipa wakipata kazi, kura sio lazima eti foleni kama sisi, waweza piga home tu, waletewa kura yako wapiga unapost, shenzi kabisa wale jama kama Gambushi! Ukichelewa peleka mtoto shule pale reception wakutana tena na kama kakompyuta kako kamesimama pale kana kila sababu wajaza sababu zako unasepa mtoto anaingia darasani! Wale mafirauni eti hata nyanya za kupitisha umeme kama za kwetu juu ya ardhi hawana! Wamezichimbia chini! Hata mabomba ya maji huoni achana na ya gesi kila nyumba! Ile mizeruzeru ina Broadband karibu kila nyumba! Kama si kuwaroga wananchi ni nini?! Jamaa mvua inanyesha aise! Kama kule kwetu Shinyanga! Ila kwao yaweza piga hata masaa 12! Lakini ikikatika washangaa maji barabarani hamna! Ndorobo wale si wameweka ile mitaro yao ya kichawi ya kunyonya maji yote! Hakuna cha kukwepa mahandaki kama kwetu wala nini wana barabara nyeusi za lami kama zetu kila sehemu! Washenzi wale wanga sana, eti hata usiku wanafanya kazi, hawalali, viwandani wana shift 6-2, 2-10, 10-6! Kama sio kuwanga usiku ni nini ngosha?! Binadamu gani asiyelala kama kwetu?! Nakuapia hata fundi kabambe wa Sumbawanga hatawaweza wale! Yaani yapo mengi mpaka nimesahau ngosha, ntakuhadithia siku nyingine, sina hamu nawo, nyambafu kabisa wale...
Na sirudi tena ng'o, uchawi gani ule?! Nina bahati kweli ngosha, kidogo niwe MSUKULE WAO!
 
There is no place his excellence Mr former president had been mentioned by his name, its better you stop speculations.
Acha hizo, habari imeletwa kwa mtililiko wa matukio ambayo yanajieleza
 
Viongozi wa kizungu wanawazidi hawa wa kwetu mara 110, amini msiamini, nimeshuhudia kwa macho yangu!
Wawo kiboko na wakaniteka akili kabisa kabisa, nimewakubali, sio huu wa kiafrika bana! Viongozi wa kizungu uchawi wao wa kwanza, miundo mbinu matata kabisa, pili na kuendelea, maji, umeme, afya bora, ustawi wa jamii, maendeleo ya kufa mtu, wamewamaliza kabisa wananchi wao, hawasikii wala hawaoni, hata mie nilipoenda soma kule, hilo limbwata lilinipata, nikawehuka, mpaka niliporudi na kukutana na ule uchafu JK Nyerere fahamu zote zikanirudia! Aacha kabisa na wazungu, wale kiboko aise, wana mandege, matreni kama basi, treni yaenda kasi kama ndege! Kuna mpaka treni inapita chini ya ardhi, nyie juu wala hamsikii! Shenzi kabisa wale, ukienda hata benki sio lazima foleni, mashine kutumbukiza hela, kutoa hela, kutumbukiza cheki! Hospitali napo, huna haja ya kuona receptionist, wewe wagonga tu kwenye kama kakompyuta ukutani jina na tarehe ya kuzaliwa wakaa, muda si muda jina lako latokea kwenye mkanda uko juu kama airport uende chumba gani kwa daktari! Na dawa zozote ukitaka zipo, hamwezi kuamini wala huna haja ya kutoa rushwa upate! Acha hivyo, waweza kaa nyumbani na ka laptop ukaagiza ngosha kuanzia mazagazaga yote mpaka nyama! Teksi na daladala zina barabara zake, daladala hazina konda, ni yule yule dereva, teksi napo hakuna kubishana na dereva, unaangalia mita tu walipa waenda zako, Bar hakuna kuletewa bia, waenda kaunta, ukimaliza tena, hakuna cha bill wala barmaid wa kukupandishia bill au bei za ajabu za vinywaji! Upuuzi kabisa, washirikina sana wale! Shule watoto bure mpaka chuo, huko wanapewa mikopo watakayolipa wakipata kazi, kura sio lazima eti foleni kama sisi, waweza piga home tu, waletewa kura yako wapiga unapost, shenzi kabisa wale jama kama Gambushi! Ukichelewa peleka mtoto shule pale reception wakutana tena na kama kakompyuta kako kamesimama pale kana kila sababu wajaza sababu zako unasepa mtoto anaingia darasani! Wale mafirauni eti hata nyanya za kupitisha umeme kama za kwetu juu ya ardhi hawana! Wamezichimbia chini! Hata mabomba ya maji huoni achana na ya gesi kila nyumba! Ile mizeruzeru ina Broadband karibu kila nyumba! Kama si kuwaroga wananchi ni nini?! Jamaa mvua inanyesha aise! Kama kule kwetu Shinyanga! Ila kwao yaweza piga hata masaa 12! Lakini ikikatika washangaa maji barabarani hamna! Ndorobo wale si wameweka ile mitaro yao ya kichawi ya kunyonya maji yote! Hakuna cha kukwepa mahandaki kama kwetu wala nini wana barabara nyeusi za lami kama zetu kila sehemu! Washenzi wale wanga sana, eti hata usiku wanafanya kazi, hawalali, viwandani wana shift 6-2, 2-10, 10-6! Kama sio kuwanga usiku ni nini ngosha?! Binadamu gani asiyelala kama kwetu?! Nakuapia hata fundi kabambe wa Sumbawanga hatawaweza wale! Yaani yapo mengi mpaka nimesahau ngosha, ntakuhadithia siku nyingine, sina hamu nawo, nyambafu kabisa wale...
Na sirudi tena ng'o, uchawi gani ule?! Nina bahati kweli ngosha, kidogo niwe MSUKULE WAO!
Pole sana
 
Hahahahahaha, mbavu zauma! Hahahahah🙂😉
Wajuwa kuna uchawi mwingine uko very "friendly" aise..Why not...
Kweliii uchawi Wao naona ni rafiki kwangu kuliko huu wetu hapa danganyika
 
Bahati mbaya kabisa ni kwamba haya masuala ya uchawi hatuwezi kuweka ushahidi kwenye forum kama hizi au kwenye maandishi au hata kurekodi video maana ile ni teknolijia nyngine kabisa ambayo inahitaji vifaa tofauti na hivi tunavyotumia kwenye maisha yetu....

Kwasababu hiyo ndiyo maana mtoa mada umekuwa ukisema "inasemekana" au alisema fulani na hakuna zaidi ya hayo....

Kwa namna nijuavyo mimi ni kwamba huku Afrika tuna vumbi tu la uchawi na uchawi wenyewe wanao watu weupe.Ninaweza kusema mengi sana kuhusu watu weupe kuwa wachawi na itabaki kuwa ni maneno tu kama alivyoandika mtoa mada lakini kwa nijuavyo mimi hakuna wachawi kama weupe na hii ni kwa weupe wote.....

Kuna ushuhuda wa bwana mmoja Mnigeria anayeitwa Emanueli Yeni,huyu jamaa alikuwa ni Mnigeria,sisi huku tunaiaminia sana Nigeria kwa uchawi lakini anakuambia wao walikuwa wanatoa uchawi India na walikuwa wakienda kwa dakika chache tu kutoka Nigeria hadi India na kurudi na walikuwa wakifumba tu macho kwa dakika kadhaa na baadaye wanaibukia kule.....

Unaweza kuona tu kwamba uchawi wanaotumia hao jamaa wanautoa India,kuna matukio mengi tu zaidi ya hilo lakini yote yanaonesha kuwa "advanced witchcraft" iko kwa weupe huko....

Hii dhana ya kufikiri Waafrika ndiyo wachawi zaidi na uchawi ndiyo unaosababisha maendeleo kutokuwepo ni dhana mbaya kabisa na inatokana na uwongo mkubwa tuliolishwa tangu kale ili tujione kuwa hatuna maana yoyote hapa duniani,"White supremacy"....

Mara nyingi mtu akisimulia mambo haya huonekana mpuuzi na mjinga zaidi lakini ni kinyume kabisa.Waliotengeneza dhana ya kuwa ni upuuzi kuamini uwepo wa uchawi na matukio yake walikuwa na lengo na kuwafanya wengine waudharau ili wao wautumie ipaswavyo na kwa manufaa zaidi na zaidi....

Hakuna wachawi kama watu weupe sisi huku na uchawi wetu wote tunajaribu tu.....
 
Umemsahau Mzee Jommo Kenyatta alikuwa analala baharin kila mara kwa mujibu ya mfanyakaz wake wa Ikulu alikuwa anasimulia kwenye gazeti la Mwananchi
 
Katika nchi moja ya Afrika,kuna mfalme mmoja inaaminika amepewa mashart na mganga wake kuwa asihudhurie misibani haswa misiba mikubwa ya Taifa kwakuwa misiba hyo hutokea kama kafara kwaajili ya kumtengenezea yy mambo yake
 
Back
Top Bottom