Marais wote wenye uchungu na nchi zao huwa wabahili kwenye matumizi mabovu, mfano Trump na late Magufuli, Rais Samia jifunze ubahili

MKATA KIU

JF-Expert Member
Joined
Nov 22, 2010
Posts
3,410
Reaction score
8,184
Habari wadau

Nazani wote tunaona Trump anachofanya.

Trump mwenyewe ni tajiri kweli kweli kuanzia yeye mwenyewe, ukoo wao na mpaka familia yao wote ni matajiri kweli kweli.

Pia Trump anaongoza Taifa tajiri kweli kweli. USA ni taifa tajiri sana.

Pamoja na utajiri wote huo bado Trump ni mbahili kwenye kuruhusu matumizi yasiowafaidisha raia wake. Ndio maana ameanza na kuifuta USAID maana ilikuwa inakula hela za wamarekani.

Nikirudi kwa rais wetu aliyepita late Magufuli na yeye alikuwa mbahili kweli kweli kwenye upuuzi. Ila alikusanya kodi zaidi na kuwekeza kwenye mambo muhimu.. leo hii tunapanda treni ya umeme na kuenjoy bwawa la umeme na Flyovers

Hili ni funzo kubwa kwamba ubahili ni muhimu sana kwenye kuleta maendeleo.

Mtu kama Elon Musk ni tajiri kweli kweli na tena ni tajiri namba moja duniani.. ila na yeye ni mbahili kweli kweli. Ndie anaeiongoza Department of goverment efficiency ya USA ambayo inafuta hizo USAID

Hili ni funzo kwa mama samia

Akitaka kuifanya Tanzania iendelee lazima awe mbahili. Aache ku approve matumizi ya kijinga kama kununua V8.
 
Kufanya hayo yote unatakiwa kuwa mzalendo kweli kweli. Sioni mzalendo ndani ya CCM ukitoa kizazi cha Nyerere na Mwinyi.
 
Kwa Magufuli fedha zilikutwa kwenye mifuko na maroba!
Huo uzarendo wake umetumia parameters zipi?
 
Hivi unamjua vizuri Elon Musk au unamtazama tu kwenye vyombo vya habari?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…