Marekani imedhamiria kuitoa Huawei sokoni, imeituhumu kuwa ni tawi la jeshi la China

Marekani imedhamiria kuitoa Huawei sokoni, imeituhumu kuwa ni tawi la jeshi la China

The Evil Genius

JF-Expert Member
Joined
Mar 21, 2014
Posts
6,017
Reaction score
19,506
Huawei ilikua inakuja vizuri sana kwa miaka 3 iliyopita. Ghafla bin vuu mwaka jana ikawekwa kwenye black list ya serikali ya Marekani ikaanza kupambana na vikwazo.

Sasa Huawei imeanza kupoteza hata ile miradi na mikataba iliyokua imepata ya kufunga mitambo ya 5G. Uingereza iliipa Huawei ila sasa imebadilisha msimamo, inategemewa hivyo hivyo kwa Hispania, na nchi kadhaa kubwa Ulaya kujiondoa kwenye mikataba na Huawei.

Uingereza inasema ni kwa sababu ya vikwazo vipya vinavyotegemewa kutangazwa September, Huawei haitakua na uwezo wowote wa hata kuzalisha vifaa vinavyohitajika sio kwa 5G wala kwa simu zake zote kwa sababu haitakua na uwezo wa kutengeneza chip yake ya Krin.

Sababu ni moja kubwa, teknolojia ya kisasa zaidi inayotumika kuzalisha vifaa vya 5G au chip za simu 90% ina mkono wa Marekani. Kwa sasa Huawei hupata baadhi ya teknolojia kwa kibali maalumu cha serikali ya Marekani. Inategemewa kuanzia September hali inaweza kua mbaya zaidi kwa Huawei.

Marekani imebadilisha tuhuma kwa Huawei kua ni tawi la jeshi la China hivyo itakabiliwa na vikwazo vyote vinavyohusu jeshi la China.

Why Huawei's days in the UK could be numbered
 
Naona Makampuni ya Simu yameanza itupilia mbali.
Singapore wamewapa Nokia na Erricson
Nchi kibao zimeanza kuvunja mikataba na Huawei.

Australia walishaipiga pini muda, New Zealand wamevunja mkataba, Uk inaelekea huko wiki ijayo.

Kwa Asia labda sijui kama kuna nchi itaipa Huawei maana Uarabuni hawawezi kumchefua boss wako Washington, South Korea ana 5G yake na yeye ndie wa kwanza kabisa kuzindua 5G, Japan, Taiwan, Indonesia na India huko haiwezekani.

Ulaya Marekani anawapa mbinyo wavunje mkataba na Huawei ili wasaini mikataba.

Kwa sasa Marekani ametargeti makampuni ya nje au yasiyo ya kimarekani ila yanayotumia teknolojia ya Marekani kushirikiana na Huawei. Ukigundulika unakabiliwa na vikwazo unafilisika. Sidhani kama kuna kampuni inayataka hayo.
 
Nchi kibao zimeanza kuvunja mikataba na Huawei.

Australia walishaipiga pini muda, New Zealand wamevunja mkataba, Uk inaelekea huko wiki ijayo.

Kwa Asia labda sijui kama kuna nchi itaipa Huawei maana Uarabuni hawawezi kumchefua boss wako Washington, South Korea ana 5G yake na yeye ndie wa kwanza kabisa kuzindua 5G, Japan, Taiwan, Indonesia na India huko haiwezekani.

Ulaya Marekani anawapa mbinyo wavunje mkataba na Huawei ili wasaini mikataba.

Kwa sasa Marekani ametargeti makampuni ya nje au yasiyo ya kimarekani ila yanayotumia teknolojia ya Marekani kushirikiana na Huawei. Ukigundulika unakabiliwa na vikwazo unafilisika. Sidhani kama kuna kampuni inayataka hayo.
Nikiona haya mambo ya ubabe wa USA,harafu kuna wajinga wanovaa za kijani,wanafikiri unaweza kuivimbia USA na wenzake wa magharibi,kama China anakimbizwa mchakamchaka,sembuse sie,ambao licha ya kuwa na maji ya kutosha,hatujaweza hata kuzalisha ngano ya kututosha,
 
USA wamechelewa, China haiwezi kudondoka wamejipanga vizuri hii ni vita ya kiuchumi, porojo tu na propaganda kwa sasa. Msimamo wa USA na sera zake zitaonekana baada ya uchaguzi wa November. Nchi za magharibi wameonyesha udhoofu hasa kutokana na haka kaugonjwa kadogo ka Corona ambako kameleta reset button. Huko tuendako ni giza totoro hakuna wa kumtunishia msuli mwenzake kwenye hayo mataifa makubwa.
 
China teknolojia ndogo,maneno tu na ujanja mwingi
Huku uwezo wa kununua vya marekani huna unatumia vya kichina halafu unaponda ama kweli bora ukose mali upate akili!! Wewe huna tu unalolijua china walichokifanya kila mmoja apate kitu kutokana na pesa yake sio kama teknolojia yao haina uwezo kama ulivyokaririshwa wewe na wamagharibi
 
Back
Top Bottom