Marekani: Moto Mkali Wateketeza Ekari 3,000 na Kuwafurusha Maelfu ya Watu Los Angeles

Marekani: Moto Mkali Wateketeza Ekari 3,000 na Kuwafurusha Maelfu ya Watu Los Angeles

Dalton elijah

JF-Expert Member
Joined
Jul 19, 2022
Posts
373
Reaction score
829
Moto mkali umezuka katika eneo la juu la Pacific Palisades huko Los Angeles, na kusababisha uhamishaji wa hofu.

Moto huo, unaosababishwa na upepo mkali wa Santa Ana , tayari umeteketeza karibu ekari 3,000 (hekta 1,200) na kuharibu nyumba nyingi.

Takriban wakaazi 30,000 wameamriwa kuhama huku wengi wakitelekeza magari yao na kukimbia kwa miguu.

Eneo hilo, ambalo lina nyumba za watu mashuhuri, limeathiriwa vibaya na moto huo unaoenea kwa kasi.

Gavana wa California, Gavin Newsom, ametangaza hali ya dharura na kuwataka wakazi kufuata maagizo ya uhamishaji ili kuhakikisha usalama wao. Tayari kikosi cha Zimamoto cha Los Angeles kiko kwenye eneo hilo kupambana na moto huo na kuokoa maisha na mali.

IMG_3141.jpeg
 
Najua mtaniponda nyie WAPINGA MUNGU
ila MALIPO NI DUNIANI AKHERA huesabiwa
ukiua kwa UPANGA si lazima na wewe uuliwe kwa UPANGA mkali

MWENYENZIMUNGU atakulipa kwa namna yoyote mpaka MOYO wako utasema hakika haya sasa ndio malipo ya ubaya wangu

pia soma hapa
[URLunfurl="true"]Janga la Moto Marekani: Unaweza Kudhani Vita Vimetokea Katika Eneo Hili[/URL]
Kariakoo .upaanga ulitutembelea pia msumbij kimbunnga fred pia upanga uliwatembelea hv vitu ni vya kisayansi si vya kimwamposa na shkhe kishk
 
Najua mtaniponda nyie WAPINGA MUNGU
ila MALIPO NI DUNIANI AKHERA huesabiwa
ukiua kwa UPANGA si lazima na wewe uuliwe kwa UPANGA mkali

MWENYENZIMUNGU atakulipa kwa namna yoyote mpaka MOYO wako utasema hakika haya sasa ndio malipo ya ubaya wangu

pia soma hapa
[URLunfurl="true"]Janga la Moto Marekani: Unaweza Kudhani Vita Vimetokea Katika Eneo Hili[/URL]
Kwahiyo unamanisha Mungu anawadhibu wa Merekani au? Sijui walokle mna upungufu wa akili? mbona hayo majanga Africa kuliko walokole wengi ni mengi hata kuliko Ulaya.
 
Zaidi ya wakazi 30,000 wa Los Angeles, wakiwemo mastaa wa Hollywood, wamelazimika kuhama makazi yao kufuatia moto mkubwa uliozuka katika eneo la matajiri la Pacific Palisades na moto mwingine kuibuka Altadena Jumanne usiku.

Gavana wa California, Gavin Newsom, ametangaza hali ya dharura na kufika eneo la tukio kukutana na wazima moto wanaopambana na moto huo ulioteketeza zaidi ya ekari 2,900. Newsom alionya kuwa upepo wenye kasi ya hadi maili 100 kwa saa unatarajiwa kuongeza kasi ya moto huo.

Miongoni mwa walioathirika ni mastaa kama Spencer Pratt na Heidi Montag waliopoteza nyumba yao ya kifahari. Wakati huo huo, wakazi wengine walilazimika kutembea kwa miguu baada ya magari kuziba barabara, hali iliyowafanya wazima moto kutumia vifaa vizito kuondoa magari yaliyotelekezwa.

Moto mwingine uliozuka Altadena umeharibu zaidi ya ekari 400 na kusababisha uhamishaji wa wakazi. Hali ya upepo mkali imeelezwa kuwa tishio kubwa, huku idara ya hali ya hewa ikionya kuwa ni mojawapo ya hali mbaya zaidi za moto kuwahi kushuhudiwa.

Rais Joe Biden ametoa msaada wa haraka kupitia FEMA kusaidia juhudi za kuzima moto, huku akihimiza wakazi kuzingatia tahadhari na amri za kuhamishwa. Moto huu unaendelea kusababisha uharibifu mkubwa wa mali, ikiwa ni pamoja na majumba ya kifahari, huku mamlaka zikiendelea kupambana kuudhibiti.
1736370421933.jpg
1736370402099.jpg
1736370412086.jpg
 

Attachments

  • 1736370416466.jpg
    1736370416466.jpg
    198.7 KB · Views: 6
Hatari sana ni kama wako vitani vile ,vita na nature
Miaka na miaka wameshindwa kupata suluhisho la wild fire !!!ndio maana hii dunia bado sana kufikia real tech ambayo itamsaidia kabisa mwanadam kupambana na vitu halisi eg magonjwa,njaa,umaskini na majanga ya asili kama hayo
 
Kwahiyo na nyumba zinaungua? Hizo nyumba zimejengwa kwa miti au mbao
 
Najua mtaniponda nyie WAPINGA MUNGU
ila MALIPO NI DUNIANI AKHERA huesabiwa
ukiua kwa UPANGA si lazima na wewe uuliwe kwa UPANGA mkali

MWENYENZIMUNGU atakulipa kwa namna yoyote mpaka MOYO wako utasema hakika haya sasa ndio malipo ya ubaya wangu

pia soma hapa
[URLunfurl="true"]Janga la Moto Marekani: Unaweza Kudhani Vita Vimetokea Katika Eneo Hili[/URL]


eheee huo ndio utaratibu wake mola
na wala huukut ukibadilika. nimeona namna majumba yankifahar yalivoungua kweli ukiammua kupata mazingatio utaona mungu akiamua ana majesh ya kila aina. hapo moto na upepo ndio jeshblake hajaamrisha nzige wala ndege. mana kuna society zilikua na kiburi kama hivi zama za zaman wakatumiwq mapigo tisa kutoka kwa mungu .ehapo los angeles sikuwaza kamq patachomwa mchana kweupeee unaweza kujitia pambani maskion ooh vimbunga vya asili sijui palisades ila jicho la tatu hii ni gharika tu.
 
Zikiungua uwa upati kitu japo zikipitiwa na kimbunga utapata kifusu!!
 
Hatari sana ni kama wako vitani vile ,vita na nature
Miaka na miaka wameshindwa kupata suluhisho la wild fire !!!ndio maana hii dunia bado sana kufikia real tech ambayo itamsaidia kabisa mwanadam kupambana na vitu halisi eg magonjwa,njaa,umaskini na majanga ya asili kama hayo
Hao ndio wapinzani wakubwa wa climate change..
 
  • Thanks
Reactions: DPN
Kwahiyo unamanisha Mungu anawadhibu wa Merekani au? Sijui walokle mna upungufu wa akili? mbona hayo majanga Africa kuliko walokole wengi ni mengi hata kuliko Ulaya.
Naona umekuja kwa kushambulia iman za watu bila kutaka kujua huyo ni nani?

Hayo ni matokeo ya kutuchonganisha na kuanzisha vikundi vya kigaidi sasa allah anawaadhibu.
 
Back
Top Bottom