#COVID19 Marekani: Rais Biden ataka kutolewa Dola 100 kwa kila atakayepata chanjo ya COVID-19

#COVID19 Marekani: Rais Biden ataka kutolewa Dola 100 kwa kila atakayepata chanjo ya COVID-19

Wajinga ni watu wa aina gani ambao umewakusudia wewe? Kwa sababu nikiangalia kwa wanaopinga na wanao kukubali chanjo kunapatikana makundi yote ya watu yani huwezi kusema kwamba kundi fulani lina msimamo fulani kuhusu chanjo kwa sababu ni aina fulani ya watu tofauti na upande mwengine.
Kwa maoni yako ni kwa nini wanaopinga chanjo siyo wajinga na wapumbavu?
 
Jamaa katangaza hongo ya dola 100 za marekani ili raia wa Marekani wakubali kuchanjwa. Kwa taarifa tu ni kwamba zaidi ya asilimia 50 ya wamarekani wamekataa kabisa chanjo ya aina yoyote. Kuna watu wasiojielewa wanadhani upinzani wa chanjo upo Tanzania tu, la hasha! Sasa kuona hivyo Rais Biden ameamua kutangaza dau la hongo ya dola 100 kwa kila atakayeshawishika kuchanjwa! Kama Marekani inawashawishi raia wake kwa hongo ili wachanjwe, kwa nini tusiamini piaa kuwa Marekani inawashawishi kwa hongo viongozi wa nchi nyingine ili wakubali kupokea chanjo na kuwashawishi raia wao kuchanjwa!! Tofauti tu ni kuwa kwa marekani anayechanjwa ndiye anayepewa dola 100. Huku kwa wenzangu na mimi kwa nini tusiamini kuwa viongozi watapewa dola 100 kwa kila mtu atakayechanjwa? Zikiingia chanjo milioni moja, kwa nini tusiamini watahongwa kwa dola milioni mia moja ($100,000,000)? Kama huko kwao wanahonga kitu gani kitawazuia huku wasihonge? Mungu amewafunua peupe! Fungua link hapa chini usome uhayawani huo!
point moja kubwa sanaa
 
100×30😳
Hapo nikichanjwa mwezi mzima kila siku chanjo moja jumla napata shilingi ngapi?
 
Kwa maoni yako ni kwa nini wanaopinga chanjo siyo wajinga na wapumbavu?
Kwanini sasa niwaone kuwa wajinga ni kwa sababu tu wanapinga chanjo? wajinga wanaweza kupatikana pande zote kunaweza kuwepo wajinga wanaopinga chanjo na wajinga wanaokubali chanjo, sasa kwa mazingira hayo naanzaje kuwaita wanaopinga chanjo kuwa wote ni wajinga wakati kuna ambao waelevu wana sababu za msingi za kupinga.
 
Mengi yameshaelezwa na wataalamu kuhusu ubaya wa hizi chanjo, na zaidi hatuwezi kufanya majaribio ya chanjo kwa watu wote.

Hatuwezi kufanya majaribio gani wakati hizi chanjo zilishajaribiwa na efficacy yake inajulikana?
imagee12.jpg
 
Hatuwezi kufanya majaribio gani wakati hizi chanjo zilishajaribiwa na efficacy yake inajulikana?View attachment 1877088
Zimejaribiwa kwa muda gani? hatujui miaka kadhaa mbeleni huko watu wanaweza kupata athari gani (ukiacha hizi ambazo zimeshaonekana) halafu wewe unasema zimejaribiwa, Kwa huu muda mchache tu tumeona mara chanjo fulani zimesitishwa mara watu wanataka chanjo fulani nyengine hawaitaki.
 
Zimejaribiwa kwa muda gani?
Katika majaribio ya dawa kinachomatter ni muda au ni matokeo?Kama majaribio yamefanyika kwa muda mfupi na matokeo yakawa positive, huo muda mrefu unaoutaka wewe ni wa kazi gani?
hatujui miaka kadhaa mbeleni huko watu wanaweza kupata athari gani (ukiacha hizi ambazo zimeshaonekana) halafu wewe unasema zimejaribiwa, Kwa huu muda mchache tu tumeona mara chanjo fulani zimesitishwa
Chanjo ambazo zimeathiri watu ni chanjo chache sana kama vile Astrazeneca na Jonson & johnson lakini kuna chanjo kibao kama vile Sputnik,moderna,BioNtech,sinopharm,sinovac,adenovirus na kadhalika ambazo wala hazijaleta shida.Hatuwezi kutumia chanjo mbili ambazo zimeleta shida na tena shida hizo zimeshatatuliwa tayari kumake conclusion kuwa chanjo zote ni mbaya.Huu utakuwa ni ujinga.
mara watu wanataka chanjo fulani nyengine hawaitaki.
Wananchi wanaotumia chanjo siyo wataalam wa madawa,hawawezi kutumika kufanya maamuzi kuwa chanjo fulani ni bora na chanjo nyingine siyo bora.Wananchi wanaotumia chanjo wao wana changamoto zao kwenye chanjo hizi kama vile viwango duni vya elimu,tamaduni mbaya kwenye madawa na kadhalika kwa hiyo hawana utaalam wa madawa na wala hawawezi kutumika katika kuamua kuwa chanjo hazifai.
 
Katika majaribio ya dawa kinachomatter ni muda au ni matokeo?Kama majaribio yamefanyika kwa muda mfupi na matokeo yakawa positive, huo muda mrefu unaoutaka wewe ni wa kazi gani?

Chanjo ambazo zimeathiri watu ni chanjo chache sana kama vile Astrazeneca na Jonson & johnson lakini kuna chanjo kibao kama vile Sputnik,moderna,BioNtech,sinopharm,sinovac,adenovirus na kadhalika ambazo wala hazijaleta shida.Hatuwezi kutumia chanjo mbili ambazo zimeleta shida na tena shida hizo zimeshatatuliwa tayari kumake conclusion kuwa chanjo zote ni mbaya.Huu utakuwa ni ujinga.

Wananchi wanaotumia chanjo siyo wataalam wa madawa,hawawezi kutumika kufanya maamuzi kuwa chanjo fulani ni bora na chanjo nyingine siyo bora.Wananchi wanaotumia chanjo wao wana changamoto zao kwenye chanjo hizi kama vile viwango duni vya elimu,tamaduni mbaya kwenye madawa na kadhalika kwa hiyo hawana utaalam wa madawa na wala hawawezi kutumika katika kuamua kuwa chanjo hazifai.
Hivi mpaka hapo haujaona nafasi ya muda katika hayo majaribio ya chanjo? Ndio maana nikakwambia kuwa kwa huu muda mchache tu wa kutumia hizo chanjo tumeweza kuona hizo chanjo zilizoleta shida ikafikia hadi baadhi ya nchi kusitisha matumizi ya baadhi ya chanjo na hapo ni madhara ya haraka kuyaona kwa huu muda mfupi toka zianze kutumika hizo chanjo hatujui kwa muda mrefu kuna athari gani.

Mimi hoja si kuwa chanjo zote mbaya bali hoja ni Kwamba hatuwezi kufanyia majaribio ya chanjo kwa watu wote, haya majaribio ndio yamefanya tujue haya madhara ya hizo chanjo unazoita chache katika huu muda mfupi. Na kuna changamoto ya kutopata taarifa za kutosha za malalamiko ya madhara kwa hizi chanjo, hata mwanzoni walikuwa wanakataa issue ya Astrazeneca kugandisha damu.
 
Hivi mpaka hapo haujaona nafasi ya muda katika hayo majaribio ya chanjo? Ndio maana nikakwambia kuwa kwa huu muda mchache tu wa kutumia hizo chanjo tumeweza kuona hizo chanjo zilizoleta shida ikafikia hadi baadhi ya nchi kusitisha matumizi ya baadhi ya chanjo na hapo ni madhara ya haraka kuyaona kwa huu muda mfupi toka zianze kutumika hizo chanjo hatujui kwa muda mrefu kuna athari gani.

Mimi hoja si kuwa chanjo zote mbaya bali hoja ni Kwamba hatuwezi kufanyia majaribio ya chanjo kwa watu wote, haya majaribio ndio yamefanya tujue haya madhara ya hizo chanjo unazoita chache katika huu muda mfupi. Na kuna changamoto ya kutopata taarifa za kutosha za malalamiko ya madhara kwa hizi chanjo, hata mwanzoni walikuwa wanakataa issue ya Astrazeneca kugandisha damu.
Chanjo za moderna,Sputnik,BioNtech,sinopharm,sinovac na Adenovirus zimeleta shida gani na wapi?

Unaelewa kuwa chanjo ya Sinopharm imetokomeza Corona huko china kwa kiwango kikubwa sana bila ya kusababisha shida yoyote ile?
 
Chanjo za moderna,Sputnik,BioNtech,sinopharm,sinovac na Adenovirus zimeleta shida gani na wapi?

Unaelewa kuwa chanjo ya Sinopharm imetokomeza Corona huko china kwa kiwango kikubwa sana bila ya kusababisha shida yoyote ile?
Nakwambia hivi hili zoezi la majaribio ya chanjo katika huu muda mfupi tu ndio umefanya wewe hapo uone hizo chanjo ulizotaja hazijaleta shida na kuweza kujua shida za hizo chanjo zengine kama Astrazeneca, kama tusingeingia kwenye haya majaribio ya chanjo kwa watu wote pengine hata wewe usingejua shida za baadhi ya hizo chanjo ungeona zote sawa hazina shida.

Ndio maana nasisitiza kwamba chanjo bado zipo kwenye majaribio, mfano hizo Astrazeneca haikuwa rahisi kukubaliwa kwamba zina shida kwahiyo hizo unazoona hazina shida kumbuka tu kwamba mwanzoni kabisa hatukuwa tunajua kama chanjo fulani ina shida fulani.
 
Nakwambia hivi hili zoezi la majaribio ya chanjo katika huu muda mfupi tu ndio umefanya wewe hapo uone hizo chanjo ulizotaja hazijaleta shida na kuweza kujua shida za hizo chanjo zengine kama Astrazeneca, kama tusingeingia kwenye haya majaribio ya chanjo kwa watu wote pengine hata wewe usingejua shida za baadhi ya hizo chanjo ungeona zote sawa hazina shida.

Ndio maana nasisitiza kwamba chanjo bado zipo kwenye majaribio, mfano hizo Astrazeneca haikuwa rahisi kukubaliwa kwamba zina shida kwahiyo hizo unazoona hazina shida kumbuka tu kwamba mwanzoni kabisa hatukuwa tunajua kama chanjo fulani ina shida fulani.
Sinopharm inatumika karibia kila sehemu duniani including Afrika na haijaleta shida yoyote.
 
Sinopharm inatumika karibia kila sehemu duniani including Afrika na haijaleta shida yoyote.
Bado ni mapema sana kujiridhisha hivyo majaribio bado yanaendelea, hata Astrazeneca zimeshachanjwa kwa mamilioni ya watu na ndio ilikuwa inatumika kama kigezo cha kukataa madhara ya Astrazeneca.
 
Bado ni mapema sana kujiridhisha hivyo majaribio bado yanaendelea, hata Astrazeneca zimeshachanjwa kwa mamilioni ya watu na ndio ilikuwa inatumika kama kigezo cha kukataa madhara ya Astrazeneca.
Kwani Sinopharm haijachanjwa kwa mamilion ya watu?
 
Kwani Sinopharm haijachanjwa kwa mamilion ya watu?
Kwanza kitendo tu cha kutaja hizo baadhi ya chanjo na kusema ndio hazijaripotiwa kuleta madhara na kukubali hizo zengine kuwa zina shida, hilo linatosha kwangu kukazia point yangu ambayo inasema chanjo bado zipo kwenye majaribio. Hizo unazosema hazina shida ishu ni kwamba hatujasikia sana malalamiko kama hizo zengine mfano Astrazeneca ila si kwamba hakuna malalamiko kabisa.
 
Kwanza kitendo tu cha kutaja hizo baadhi ya chanjo na kusema ndio hazijaripotiwa kuleta madhara na kukubali hizo zengine kuwa zina shida, hilo linatosha kwangu kukazia point yangu ambayo inasema chanjo bado zipo kwenye majaribio. Hizo unazosema hazina shida ishu ni kwamba hatujasikia sana malalamiko kama hizo zengine mfano Astrazeneca ila si kwamba hakuna malalamiko kabisa.
Hakuna malalamiko ambayo ni significant.Kama yapo weka hapa.
 
Back
Top Bottom