SaintErick
Member
- Aug 7, 2013
- 90
- 53
Miaka michache iliyopita ilikuwa huwezi kuzungumzia vita kati ya Uchina na Marekani lakini hivi sasa tayari hilo halipo na kinachozungumzwa ni vita kati ya mataifa mawili makubwa zaidi duniani kiuchumi na kijeshi kwa maana ya Marekani na China.
Mapema mwezi huu (Oktoba) wanajeshi 864 wa Marekani walionekana wakiwa kwenye ndege kubwa za kivita za C-17 wakipelekwa kwa ajili ya mazoezi maalumu ya kupelekwa Asia tayari kwa vita. Hata hivyo, ni wanajeshi 492 tu ndio walifanikiwa kufikia lengo huku wengine washindwa kwa sababu mbalimbali.
Pentagon (Wizara ya Ulinzi ya Marekani) inaita vita hii kama Great Power War inaandaa wanajeshi kwaajili ya Vita na China ambavyo mpka sasa ni ngumu kuepuka. Wanaamini katika Jeshi lao la Marine kwa kua na utayari wa kufika mahali popote wakati wowote watakao hitajika. Jeshi lao majini (US NAVY) wana maisha yao katika bahari ya Atlantic na mpango mkakati wa mapigano huko uko kwenye DNA zao kwamba wamekua wakijifunza kila siku tangu wakati na baada ya vita vya pili vya dunia.
Lakini wanajeshi wa ardhini wanahitaji mafunzo zaidi kwani watakutana na jeshi la China ambalo liko na uelewa mpana zaidi wa Jiografia ya huko. Walipata somo wakati wakipigana na Talibani huko Afghanistan.
Sasa tofauti na Talibani, jeshi la China liko imara zaidi. Wana teknolojia ambayo sio sawa lakini inaikaribia kwa kiasi flani teknolojia ya Marekani ikiwa ni pamoja na vita vya kielektroniki (electronic warfare), Satelite na Drones. Hivyo jeshi la Marekani litakua likionekana kuanzia kwenye kujipanga (formation) hadi kwenye utekelezaji (excution) ya mission yao.
Kwa hio kwa sasa wanajeshi wa Marekani wanafanya mazoezi magumu na makali ili kua na uwezo wa kuishinda China katika vita hio ambayo kwa Marekani ni kama haizuiliki haijalishi nani atakuwa Rais baada ya uchaguzi wa November 5, 2024.
Xi Jin Ping anafukuza mwizi kimya kimya. Mshauri wake muhimu katika msawala mbalimbali kwa sasa amepewa mission ya Taiwan na jeshi la China limearifiwa kufanya mazoezi ili kuichukua Taiwan kwa nguvu mwaka 2027.
Hata hivyo kiasi cha makomandoo kutoka kikosi hatari zaidi cha SEAL NAVY kiko Taipei -Taiwan kwa ajili ya kulinda maeneo muhimu ya kimkakati kijeshi ikiwemo viwanja vya ndege na vituo vya mawasiliano.
Kwa hio ni wazi kwamba ikiwa China itaivamia Taiwan basi Marekani ni lazima kuingia vitani na China kwa sababu wakiacha basi China atapata nguvu kubwa Asia na mataifa mengi yatapiga goti kumtii na kuomba ushirika kwa hivyo ni lazima Marekani aipige China kuonyesha ubabe wake.
Source: New York Times
Mapema mwezi huu (Oktoba) wanajeshi 864 wa Marekani walionekana wakiwa kwenye ndege kubwa za kivita za C-17 wakipelekwa kwa ajili ya mazoezi maalumu ya kupelekwa Asia tayari kwa vita. Hata hivyo, ni wanajeshi 492 tu ndio walifanikiwa kufikia lengo huku wengine washindwa kwa sababu mbalimbali.
Pentagon (Wizara ya Ulinzi ya Marekani) inaita vita hii kama Great Power War inaandaa wanajeshi kwaajili ya Vita na China ambavyo mpka sasa ni ngumu kuepuka. Wanaamini katika Jeshi lao la Marine kwa kua na utayari wa kufika mahali popote wakati wowote watakao hitajika. Jeshi lao majini (US NAVY) wana maisha yao katika bahari ya Atlantic na mpango mkakati wa mapigano huko uko kwenye DNA zao kwamba wamekua wakijifunza kila siku tangu wakati na baada ya vita vya pili vya dunia.
Lakini wanajeshi wa ardhini wanahitaji mafunzo zaidi kwani watakutana na jeshi la China ambalo liko na uelewa mpana zaidi wa Jiografia ya huko. Walipata somo wakati wakipigana na Talibani huko Afghanistan.
Sasa tofauti na Talibani, jeshi la China liko imara zaidi. Wana teknolojia ambayo sio sawa lakini inaikaribia kwa kiasi flani teknolojia ya Marekani ikiwa ni pamoja na vita vya kielektroniki (electronic warfare), Satelite na Drones. Hivyo jeshi la Marekani litakua likionekana kuanzia kwenye kujipanga (formation) hadi kwenye utekelezaji (excution) ya mission yao.
Kwa hio kwa sasa wanajeshi wa Marekani wanafanya mazoezi magumu na makali ili kua na uwezo wa kuishinda China katika vita hio ambayo kwa Marekani ni kama haizuiliki haijalishi nani atakuwa Rais baada ya uchaguzi wa November 5, 2024.
Xi Jin Ping anafukuza mwizi kimya kimya. Mshauri wake muhimu katika msawala mbalimbali kwa sasa amepewa mission ya Taiwan na jeshi la China limearifiwa kufanya mazoezi ili kuichukua Taiwan kwa nguvu mwaka 2027.
Hata hivyo kiasi cha makomandoo kutoka kikosi hatari zaidi cha SEAL NAVY kiko Taipei -Taiwan kwa ajili ya kulinda maeneo muhimu ya kimkakati kijeshi ikiwemo viwanja vya ndege na vituo vya mawasiliano.
Kwa hio ni wazi kwamba ikiwa China itaivamia Taiwan basi Marekani ni lazima kuingia vitani na China kwa sababu wakiacha basi China atapata nguvu kubwa Asia na mataifa mengi yatapiga goti kumtii na kuomba ushirika kwa hivyo ni lazima Marekani aipige China kuonyesha ubabe wake.
Source: New York Times