Marekani yaanza kujibabadua kutoka ubashiri wa michezo (Betting).Athari zake zinaharibu uchumi na kutesa watu

Marekani yaanza kujibabadua kutoka ubashiri wa michezo (Betting).Athari zake zinaharibu uchumi na kutesa watu

Webabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2010
Posts
8,870
Reaction score
14,258
Kwa ushamba wa nchi za kiafrika hawatendi mpaka kitu kiwe kimeanzia kwa wazungu na hawaachi kutenga mpaka wazungu waseme kina madhara.

Michezo ya kamari katika michezo imekuwepo kwa miaka mingi nchini Marekani na hata kutungiwa sheria na majimbo mbali mbali ili ifanyike bila matatizo.Hata hivyo kwa vile jambo hilo ni haramu hizo sheria hazijaweza kuzuia athari za ubaya wake.

Ili kufanyika kwa wepesi baadhi ya majimbo ya Marekani yametenga fungu maalum la kusuluhisha matatizo yatokanayo na ubashiri wa michezo. Hata hivyo majimbo hayo yamejikuta yakiishiwa na pesa na huku matatizo yakiongezeka.

Watu binafsi wamepata uraibu wa kubeti mpaka wanashindwa kufanya kazi za maana.Wengi wao wanaishi kwa wasi wasi na majonzi baada ya kujikuta wameshinda kidogo katika ubashiri na baada wakawa wakishindwa mfululuzo mpaka wakapoteza kila kitu na kushindwa kuanzisha mradi wowote wa kujipatia angalau chakula chao.

Unaweza ukajisomea zaidi hapo chini.

How the US became hooked on sports betting – and the cost it’s having on lives

1714803545355.png
 
Huku Tanzania tuna wawekezaji kutoka China wameweka mashine za kamari kila mtaa na serikali ya CCM inawaunga mkono.
 
Huku Tanzania tuna wawekezaji kutoka China wameweka mashine za kamari kila mtaa na serikali ya CCM inawaunga mkono.
Watanzania wengi wanadhani betting na michezo ya kamari kwa ujumla ni jambo lililoanza siku za karibuni kwa sababu tu hatukuwa na hizi betting centers kabla. Wenzetu wameanza siku nyingi sana na ni area inayozipatia serikali mapato mazuri tu. Tatizo la Bongo ni kwamba wameachiwa wachina na watu wengine binafsi kufanya hii shughuli, na zipo kila sehemu, kitu ambacho kina madhara mengi na ku-control inakuwa vigumu sana. Ningeishauri serikali ndiyo ifanye hii shughuli kupitia shirika la bahati nasibu la Taifa, kama kuna umuhimu basi watu binafsi wachache sana waruhusiwe ku operate baadhi ya michezo. Hili litafanya faida (ambayo ni kubwa) kutumika kwa manufaa ya wananchi eg, elimu na afya na pia ku control watu kubeti hovyo.
 
Kwanza naomba kujua maana ya
1. Kujibabadua
3. Uzoefu wako katika betting na athari yake.

Weka picha au video inayoonyesha kujibabadua ili kutusaidia kuelewa msamiati "Kujibabadua"
 
Watanzania wengi wanadhani betting na michezo ya kamari kwa ujumla ni jambo lililoanza siku za karibuni kwa sababu tu hatukuwa na hizi betting centers kabla. Wenzetu wameanza siku nyingi sana na ni area inayozipatia serikali mapato mazuri tu. Tatizo la Bongo ni kwamba wameachiwa wachina na watu wengine binafsi kufanya hii shughuli, na zipo kila sehemu, kitu ambacho kina madhara mengi na ku-control inakuwa vigumu sana. Ningeishauri serikali ndiyo ifanye hii shughuli kupitia shirika la bahati nasibu la Taifa, kama kuna umuhimu basi watu binafsi wachache sana waruhusiwe ku operate baadhi ya michezo. Hili litafanya faida (ambayo ni kubwa) kutumika kwa manufaa ya wananchi eg, elimu na afya na pia ku control watu kubeti hovyo.
Badala ya kusema mchezo huo ufutwe kabisa watu wafanye kazi unataka uhamishiwe shirika la bahari nasibu.
 
Siyo kurithisha umaskini bali ni kujenga umaskini. Nasikitika sana jinzi watu wanavyopoteza muda na pesa zao kucheza kamari na kuwatajirisha wachache. Kungekuwa na kampuni moja au mawili tu, ila Tanzania kuna utiriri wa kucheza kamari mpaka hali inatisha
Haijawahi kutokea mtu kutajirika na roho yake ikamtua kwa kucheza kamari.
Ukitajirika ujue kuna visasi vingi vinakusubiri.Penye kamari huambatana na mauwaji ya visasi vya siri.
Kwanini usiuze biashara yako ndogo na kupata cha halali na ukaishi kwa amani.
 
Back
Top Bottom