Mindyou
JF-Expert Member
- Sep 2, 2024
- 1,869
- 4,877
Wakuu,
Kama alivyotuahidi jana, siku ya leo Mwanaharakati nguli Afrika Mashariki, Maria Sarungi atazungumza kinaga ubaga kuhusu namna alivyotekwa mpaka kupatikana kwake.
Bado haijaeleweka hadi sasa kama atazungumza kwa kujirekodi video kueleza nini hasa kilitokea, atatengeneza thread ya kuelezea tukio zima au atatoa tamko kupitia space.
Soma pia: Kuelekea 2025 Mwanaharakati Maria Sarungi adaiwa kutekwa na watu wenye silaha Nairobi, wakiwa na Noah nyeusi
Tanzania inasubiri. Kaa karibu na uzi huu kujua kitakachojiri
==========================================
"Jana niliondoka nyumbani kwenda saluni ili kutengeneza nywele zangu. Nilipofika, wakati namaliza, niliona mwanamke aliingia ndani ya saluni haraka haraka alafu akatoka, alikuwa amevaa mask. Sikufuatilia sana baada ya kuona hivyo"
"Mara nyingi mimi huwa nawasiliana na mume wangu nimpe updates za wap nilipo. Kwa hiyo nikamtaarifu kwamba nataka kuondoka. Nikatumia app ya Little ya kuita gari y kunirudisha. Yule dereva alifika lakini hakuweza kuingia ndani"
"Kwa hiyo nikawa naenda getini ili niweze kuingia kwenye gari na wakati dereva anajaribu kuondoa gari ili kulipeleka barabarani, kuna mwanaume mmoja mweusi alitoka kwenye gari yao na wengine wawili wakaanza kumfokea dereva kwamba afungue mlango. Na mimi nikamwambia dereva asifungue mlango wa gari"
"Baada ya hapo waliweza kufungua mlango na wakaanza kunivuta nje nikaanza kupambana nao ili nisitoke nje ya gari lakini waliweza kunibeba na kuniingiza kwenye gari yao. Nilikuwa napiga kelele sana kuomba msaada baada ya muda wakaanza kujaribu kufiha uso wangu ili nisiwaone"
View: https://www.youtube.com/watch?app=desktop&v=81e_duSZSc0
Maria akizungumzia iwapo Serikali ya Tanzania ilihusika katika utekaji wake:
Kama alivyotuahidi jana, siku ya leo Mwanaharakati nguli Afrika Mashariki, Maria Sarungi atazungumza kinaga ubaga kuhusu namna alivyotekwa mpaka kupatikana kwake.
Bado haijaeleweka hadi sasa kama atazungumza kwa kujirekodi video kueleza nini hasa kilitokea, atatengeneza thread ya kuelezea tukio zima au atatoa tamko kupitia space.
Soma pia: Kuelekea 2025 Mwanaharakati Maria Sarungi adaiwa kutekwa na watu wenye silaha Nairobi, wakiwa na Noah nyeusi
Tanzania inasubiri. Kaa karibu na uzi huu kujua kitakachojiri
==========================================
"Jana niliondoka nyumbani kwenda saluni ili kutengeneza nywele zangu. Nilipofika, wakati namaliza, niliona mwanamke aliingia ndani ya saluni haraka haraka alafu akatoka, alikuwa amevaa mask. Sikufuatilia sana baada ya kuona hivyo"
"Mara nyingi mimi huwa nawasiliana na mume wangu nimpe updates za wap nilipo. Kwa hiyo nikamtaarifu kwamba nataka kuondoka. Nikatumia app ya Little ya kuita gari y kunirudisha. Yule dereva alifika lakini hakuweza kuingia ndani"
"Kwa hiyo nikawa naenda getini ili niweze kuingia kwenye gari na wakati dereva anajaribu kuondoa gari ili kulipeleka barabarani, kuna mwanaume mmoja mweusi alitoka kwenye gari yao na wengine wawili wakaanza kumfokea dereva kwamba afungue mlango. Na mimi nikamwambia dereva asifungue mlango wa gari"
"Baada ya hapo waliweza kufungua mlango na wakaanza kunivuta nje nikaanza kupambana nao ili nisitoke nje ya gari lakini waliweza kunibeba na kuniingiza kwenye gari yao. Nilikuwa napiga kelele sana kuomba msaada baada ya muda wakaanza kujaribu kufiha uso wangu ili nisiwaone"
View: https://www.youtube.com/watch?app=desktop&v=81e_duSZSc0
