Elections 2010 Marine Hasan amtangaza Kikwete mshindi wa urais

Elections 2010 Marine Hasan amtangaza Kikwete mshindi wa urais

Ah ndugu yangu wewe! Mimi nina maslahi na CCM tena?

Anyway, ila nina bahati mbaya hakuna siku niyomchagua mtu akashinda. Nilishajaribu kwa Mrema - hola, nikajaribu kwa Lipumba - aa wapi, nikarusha karata yangu kwa Mbowe - hamna kitu! Damn it!
Asprin ndugu yangu, umefeli mara tatu, nakuomba jaribu mara ya nne na nina hakika safari hii utafaulu adhima yako. (sio kwamba natabiri kama yule sheikh wa Magomeni la hasha, upepo unaashiria hivyo)
 
Katika hali kushangaza mtangazaji wa TBC1 Marine Hassan Marine wakati anamalizia kipindi chake cha jambo leo asubuhi ametangaza kuwa Kikwete ndio mshindi wa urais na Dr. Slaa na Prof. Lipumba watakuwa wanashindana nani apate kura nyingi. Hivi hii TBC inamwakilisha nani? ni ya taifa au ya CCM? kweli safari yetu ndefu na NEC watakaa kimya kwa hili pia


Huyu jamaa naona sasa amekuwa pweza
 
Jamani tatizo letu sio Democracy ya kumpigia kura mwakilishi kwa maana hata rais. Tatizo letu ni mfumo uliojitengeza kwa maslahi yake. Historia inaonyesha kwamba matokeo ni kusambaratika kwa taifa kutokana na kusambaratika kwa wenye mfumo unaotawala tusubiri tu.
 
Form ya kumripoti hii hapo chini. Nitaijaza na kuwaachia PCCB waamue kama kuna kipengele cha sheria cha kuweza kumtia hatiani kwa kitendo chake cha kutumia chombo cha umma kama vile Televisheni kuwatangazia Watanzania mshindi wa uchaguzi wa urais kabla hata ya kampeni kuanza. Watu hawa ni hatari sana, kwani wanaweza hata kututangazia kupinduliwa kwa serikali, just kwa advantage ya kuwa mbele ya camera na microphone. Angekuwa na akili angejiuliza maswali kadhaa kabla ya kutamka, lakini masikini ndo upeo wake umeishia hapo. Hajui yeye ni mwajiriwa wa taasisi gani.
 
Sidhani kama kuna cha kubisha hapo.
Marine Hassan = CCM
TBC1 = CCM
Msajili wa vyama vya siasa = CCM
Mkuu wa Majeshi = CCM
Jaji Mkuu = CCM
IGP = CCM
Kamishna wa Magereza = CCM
Mwenyekiti Tume ya Taifa ya Uchaguzi = CCM
........................... = CCM
Ukijumlisha vyote hapo utakuta JMK = CCM = Rais wa JMT 2010-2015.

Halafu eti mnataka nipoteze muda wangu kupiga kura? Siku hiyo nitashinda baa!

Hii ni sahihi ndo maana nimekuwa nikisema kuiondoa CCM madarakani ni kama kupindua serikali

Hiyo list yako juu, ongeza: Usalama wa Taifa ...CCM

Maana walihusika eti kumuchunguza aliyekuwa mwenyekiti wa Umoja wa Vijana na gazeti la Habri Leo la tarehe 21 limemtaja afisa usalama wa Taifa wa Wilaya ya Geita Esther Ndazi kachukuwa fomu CCM. Sijui akishindwa atarudi kazini? Baada ya kuvunja sheria.
 
Mkuu,
Sijasema wewe una maslahi na CCM.
Ila wanasema "mwamba ngoma......." Hata mie leo hii marehemu kaka yangu angelikuwa Ofisi ya Kikwete, ningelikuwa na muda mgumu sana kuamua niwe wapi. Ni mambo ya kawaida katika maisha wala usichukulie hilo swala ni wewe pekee. Narudia tena, kuwa hata mie ningelikuwa njia panda kati ya imani yangu na kaka yangu aliyenilea na kunitunza(Mfano tu hapa).
Hapa haimaanishi kuwa mie nina/wewe una maslahi na CCM.
Kama huna chochote kinachokuunga na Kikwete au CCM huko juu, tafadhali usisite kwenda kujiandikisha na kupiga kura na ikibidi kuilinda kura yako. Ameni.
Ah ndugu yangu wewe! Mimi nina maslahi na CCM tena?

Anyway, ila nina bahati mbaya hakuna siku niyomchagua mtu akashinda. Nilishajaribu kwa Mrema - hola, nikajaribu kwa Lipumba - aa wapi, nikarusha karata yangu kwa Mbowe - hamna kitu! Damn it!
 
...Huyu bwana Marin Hassan jana tu nimetoka kusema kwenye uzi mwingine luwa muda mrefu tu yeye ameisjajionyesha kuwa ni miongoni mwa wale wanaojigonga gonga kwa JK na Chama Chao ili wasisahauliwe kwenye Ufalme wa Miaka Mitano ujao! Pathetic.
 
..marine hassan marine ..wakati anaanza alikuwa mwandishi mzuri sana hasa kwa interviews na makala ....lakini kwa kadiri muda unavyooenda amejawa kiburi cha umaarufu...anaofikiri anao...kiasi cha kusababisha hata akose nidhamu ....mara nyingi ...nimekuwa nikishangaa sana....anapohoji hata viongozi wa serikali huuliza maswali yasioyokuwa na msingi.......au kutumia lugha ya dharau kwa anaowahoji...infact kwa mtu yeyete anayejuwa uandishi anaweza kudhani kuwa labda ana elimu ndogo au kuna mtandao aliojumuishwa ambao unampa kiburi...

Mimi nadhani hawa waandishi wanatakiwa kuiga mifano mizuri kama ya kina Tido muhando ,huyu mahojiano yake huwa yapo focused na huepuka sana kuwaudhi anaowahoji bila sababu.....nadhani waandishi wengine wanataka kuiga mahojiano ya mashambulizi kama ya TIM SEBASTIAN lakini wanasahau kuwa yule anafanya utafiti wa kina kabla ya mahojiano....na kumganya awe makini zaidi...na huuliza maswali yake haraka haraka..lakini si kwa lengo la kudhalilisha...
 
mimi huwa hata simsikilizi, ukimsikiliza marine hasan anapotangaza, gesture etc, utaona kuwa kama hajasoma vile, ana upeo mdogo sana wa elimu na uandishi wa habari, na anajifanya kama ana unique sauti fulani hivi....ULISHAWAHI KUONA WATU FULANI/BINADAMU WANAKUWA NA MIILI MIKUUBWAA, LAKINI AKILI KAMA UBONGO WA SAMAKI..nachelea kusema jamaa ni miongoni mwao...yaani nashindwa hata kueleza..ila hana hadhi ya kuwa pale alipo...ni sawa na Tido, Kibonde na Marine hawa wote utafiikiri famiilia moja...sijui shule walikimbia umande?...wanakera kusikiliza halafu ni aibu kwa taifa watu wa nje wakiwasikiliza..imagine mtu akifikiri watz wako kama kibonde, au kama marine...bora hata Tido kidogo...ila hawa wawili....nawaoneaga huruma tu yaani...
 
Kutamka kwa huyo mtangazaji hakunifanyi mimi nimpigie kura JK. Huko ni kutapatapa kwa mfa maji!!
 
Katika hali kushangaza mtangazaji wa TBC1 Marine Hassan Marine wakati anamalizia kipindi chake cha jambo leo asubuhi ametangaza kuwa Kikwete ndio mshindi wa urais na Dr. Slaa na Prof. Lipumba watakuwa wanashindana nani apate kura nyingi. Hivi hii TBC inamwakilisha nani? ni ya taifa au ya CCM? kweli safari yetu ndefu na NEC watakaa kimya kwa hili pia


Mhh kumbe na wewe uliona eeh sasa ndio mjue kua nchi imeshauzwa na sisi wenyewe tumebinafsishwa kazi kwetu wapiga kura tukipiga tutakua tumejipa haki tusipopiga tumejinyima haki tusimamie wapi sasa?.
 
...Huyu bwana Marin Hassan jana tu nimetoka kusema kwenye uzi mwingine luwa muda mrefu tu yeye ameisjajionyesha kuwa ni miongoni mwa wale wanaojigonga gonga kwa JK na Chama Chao ili wasisahauliwe kwenye Ufalme wa Miaka Mitano ujao! Pathetic.



kwanza wewe hushangai mpemba gani yupo CCM kama si kitu kidogo na huenda akawa ametumwa kupiga debe na ameshakula advenca ya ruzuku yake.
 
OFISI ya Rais (Ikulu), imesema imeshtushwa na kushangazwa na katuni iliyochorwa katika gazeti la Kenya la Sunday Nation la Jumapili iliyopita inayomuonyesha Rais Jakaya Kikwete akilambwa viatu na waandishi wa vyombo vya habari hapa nchini.

Akizungumza na Tanzania Daima kwa simu jana, Mwandishi Msaidizi wa Habari wa Rais, Maura Mwingira alisema Ikulu imeiona picha hiyo na kuichukulia kuwa ni dhihaka mbaya kwa Rais Kikwete na kwa vyombo vya habari hapa nchini.
...

Alisema pamoja na wao (Ikulu) kukaa kimya, ana imani kwamba, vyombo vya habari hapa nchini, vina wajibu wa kutokaa kimya katika hili kwani, katuni hiyo nayo inaonyesha kwamba waandishi wa habari wanamlamba Rais Kikwete viatu, jambo alilolielezea kuwa ni udhalilishaji wa taaluma ya uandishi.
Sasa walichokuwa wanasema wamedhalilishwa kiko wapi; hawaoni kama watu wa aina ya Marin ndio wanaowadhalilisha waandishi wenzao?
 
sasa walichokuwa wanasema wamedhalilishwa kiko wapi; hawaoni kama watu wa aina ya marin ndio wanaowadhalilisha waandishi wenzao?

wapashe hao.tatizo la wbongo hupenda ligi za maneno ili wawatengenezee washindi kesi kwani wengi huishi kwa kesi.
 
kwa aliye uliza historia ya huyu Marine Hassan


ni mzanzibari mwenye asili ya comorro kama sikosei...........na amesoma vyuo vya uandishi wa habari hapo hapo Tanzania.

Sitashangaa MALARIA SUGU=MARINE HASSAN
 
kwa mujibu wa sheria ya uchaguzi ni kosa la jinai kumtangaza mtu mshindi bila idhini ya tume ya uchaguzi...
 
Katika hali kushangaza mtangazaji wa TBC1 Marine Hassan Marine wakati anamalizia kipindi chake cha jambo leo asubuhi ametangaza kuwa Kikwete ndio mshindi wa urais na Dr. Slaa na Prof. Lipumba watakuwa wanashindana nani apate kura nyingi. Hivi hii TBC inamwakilisha nani? ni ya taifa au ya CCM? kweli safari yetu ndefu na NEC watakaa kimya kwa hili pia
Mi naona kuna agenda ya TBC kumpigia debe CCM, leo tena wakati nacheki TBC mtangazaji Danieli Kijo karudia yaleyale ya marine! Walikua wanasoma vichwa vya habari vya magazeti kuna habari ya Dr Slaa kuchukua form sasa yeye baada ya kusoma akawauliza wale washiriki wa kipindi chake wao wanaonaje Slaa kupoteza ubunge maana hatapata urais! Watu wote wakawa na mawazo ka yake yaani bora abaki kwenye ubunge! Ivi hawa watangazaji wanajua maana ya chombo cha umma?
 
Back
Top Bottom