Marley Dollars $$ kijana anayetingisha Bongo kwa Mandinga makali

Marley Dollars $$ kijana anayetingisha Bongo kwa Mandinga makali

Duuh... Katika pitapita zangu ndo nimekutana na huu uzi aisee nimegundua wabongo tumeumbwa na roho za chuki, hila, wivu na roho za kwa nini, yaani kama wewe ni masikini unatamani kila mtu awe masikini...😂😂

Kuna vitu vinachekesha sana yaani karibia 90% ya waliochangia wanamponda jamaa mara anauza unga mara amepata hela kwa njia haramu wakati hata wengine hawamfahamu kwa kumuona hata kwa sura.🤔

Nimefahamiana na Marley mwaka 2018 nilikutana naye Arusha katika harakati zangu za utafutaji nilijifunza mengi na alinihamasisha kuzidi kupambana sana, kuna siku tumetoka kupiga mshindo flani baadae tulienda kiwanja flani hivi panaitwa "TRIPPLE A" alikuwa na gari yake jeep rangi ya jeshi ni mtu poa sana na ni mpambanaji haswaaa.

Katika story nilisikia kwa rafiki yake kuwa jamaa aliibukia kwenye madini yaani RUBY, Kipindi machimbo ya msumbiji huko Montepuez(mtipweshi) yalivyopamba moto yeye alizamia huko akitokea Songea tena kwa kudandia usafiri kwa tajiri mmoja hivi mnunuzi wa madini hiyo ni miaka ya 2010 huko,

Marley ni miongoni mwa wachimbaji waliopiga hela kubwa mtipweshi kwa kipindi hicho zaidi ya bilioni 1 ukiachana na wakina ndaki n.k....Naweza sema ni mtu mwenye bahati kubwa na ni wachache wanaoweza kupambana kufika hapo alipo kwa kuanzia chini.

Tupende kujifunza kwa waliofanikiwa na sio kubeza na kuponda mafanikio ya watu, shortcut zipo lakini hata hela za kihalali zinawezekana... MUNGU NI WETU SOTE. 🙏

NB: sitachangia chochote zaidi ya hayo wala kujibu PM ya mtu.
 
Duuh... Katika pitapita zangu ndo nimekutana na huu uzi aisee nimegundua wabongo tumeumbwa na roho za chuki, hila, wivu na roho za kwa nini, yaani kama wewe ni masikini unatamani kila mtu awe masikini...

Kuna vitu vinachekesha sana yaani karibia 90% ya waliochangia wanamponda jamaa mara anauza unga mara amepata hela kwa njia haramu wakati hata wengine hawamfahamu kwa kumuona hata kwa sura.

Nimefahamiana na Marley mwaka 2018 nilikutana naye Arusha katika harakati zangu za utafutaji na baadae tulienda kiwanja flani hivi panaitwa THE PICNIC alikuwa na gari yake jeep rangi ya jeshi ni mtu poa sana na ni mpambanaji haswaaa.

Katika story nilisikia kwa rafiki yake kuwa jamaa aliibukia kwenye madini yaani RUBY, Kipindi machimbo ya msumbiji huko Montepuez(mtipweshi) yalivyopamba moto yeye alizamia huko akitokea Songea tena kwa kudandia usafiri kwa tajiri mmoja hivi mnunuzi madini hiyo ni miaka ya 2010 huko,

Marley ni miongoni mwa wachimbaji waliopiga hela kubwa mtipweshi kwa kipindi hicho zaidi ya bilioni 1 ukiachana na wakina ndaki n.k....Naweza sema ni mtu mwenye bahati kubwa na ni wachache wanaoweza kupambana kufika hapo alipo kwa kuanzia chini.

Tupende kujifunza kwa waliofanikiwa na sio kubeza na kuponda mafanikio ya watu, shortcut zipo lakini hata hela za kihalali zinawekana... MUNGU NI WETU SOTE. 🙏

NB: sitachangia chochote zaidi ya hayo wala kujibu PM ya mtu.
Hongera zake sana......Kazi iendelee...Sasa tuna Chief Godlove mtoto mdogo mwenye pesa nyingi ,kiongozi wa chama na serikali,ukimuona yeye umeona hela.
 
Watu mnazidi kumpa kichwa Magu tena kwa mambo asiyostahili hata robo!!

Akimbie kwa lipi?! Dealers still wapo kila mahali; kwanini wao wasikimbie aje kukimbia yeye?!

Majizi yote serikalini bado yanaendelea kutanua... huyo Magu angekuwa kama mnavyotaka kutuaminisha si wangeanza kukimbia majitu ya serikalini yaliyoifisidi serikali miaka nenda rudi!!
 
Alipotelea wapi hadi Chief goodlove kamzidi,
Nabii shillah alikosea masharti gani asikiki tena
 
Alipotelea wapi hadi Chief goodlove kamzidi,
Nabii shillah alikosea masharti gani asikiki tena
Humjui vizuri Marley Dollars wewe.... Huwezi kumlinganisha na hao makinda akina Chief sijui Godlove, jamaa amevimba sana na hela toka miaka ya 2010s na bado anazidi kutamba na hana hizo show off kama huyo mnyakyusa!
 
Humjui vizuri Marley Dollars wewe.... Huwezi kumlinganisha na hao makinda akina Chief sijui Godlove, jamaa amevimba sana na hela toka miaka ya 2010s na bado anazidi kutamba na hana hizo show off kama huyo mnyakyusa!
Ni Draga au mchimbaji
 
Back
Top Bottom