Mkuu hapo kwenye point yako namba mbili nafikiri umesahau kitu kimoja tu, hiyo zamani wakati sifa za mwanamke kuolewa zilikuwa ni bikira na tabia njema zilikuwa ni enzi ambazo wanaume hawatongozi wanawake hovyo ili wapunguze tu upwiru, bali mwanaume alikuwa akimpenda mwanamke anaenda direct kwao kumchumbia na kumtolea mahari kisha anapewa mke wanaanza maisha ya ndoa
Lakini kwa hii dunia ya leo ambayo watu wamefanya ngono kama chakula mahusiano yanajengwa based on one night stand, friends with benefit, kufurahishana, kulana kimasihara, na upumbavu mwingine kama huo, watu wanajifanyia tu sex halafu mwisho wa siku mwanaume akitaka kuoa, aje aseme eti anataka bikira na tabia njema huyo atakuwa mzima kweli kichwani
Na mbaya zaidi ukisema jinsia zote zibadilike wanaume wanakuambia eti wanaotakiwa kubadilika ni wanawake ndio waache kukubali wakitongozwa, ila wao wanaume wanaona ni haki yao kutongoza wanawake hata wasio na malengo nao kwa gia ya kwamba watawaoa kumbe lengo lao ni kupunguza haja zao tu, yani eti wao kuwahadaa wanawake wanajiona wako sawa na wanafaa kuwa waume ila wanawake kuwakubalia wanaonekana wana matatizo na hawafai kuwa wake
Yani mtu urukeruke huku na huko ufanye umalaya uchezee na uharibu wanawake to your heart's content halafu ukitaka kuoa, ndio uje ujifanye unawalalamikia na kuwatukana wanawake kuwa hawajitunzi na hawajiheshimu kana kwamba siyo wewe uliyeshiriki kwenye kuwaharibu na kuwachezea, huku ukidhani kwamba jinsia yako itakubeba kwa kuwa unajua kwamba siku zote wanaodhalilishwa kuhusu suala la ngono ni wanawake kwa sana
Mimi ninachoweza kusema ni kwamba hao wanaume walioamua kushusha standards siyo kwamba ni wapumbavu ila wameamua kuacha kuwa delusional na kukubaliana na hali halisi, kwamba huwezi kuzini na wanawake halafu ukitaka kuoa uanze kutafuta mabikira katika hao hao wanawake ambao ulikuwa unazini nao sasa hao mabikira watoke wapi, huwezi kuyachafua mazingira halafu utegemee yakupe hewa safi lazima uchague moja ni either uyatunze mazingira ili yakupe hewa safi au uyachafue kisha uikubali hewa chafu yatakayokupa
Yani wanaume mnatakiwa muelewe kwamba kujitunza is not about nani anaonekana malaya na anadharaulika na jamii kati ya hizi jinsia mbili bali it's all about kupata mwenza bora wa maisha, maana hapa tulipofikia wanawake hawajali tena na wameshaanza kuzipuuzia hizo gender stereotypes na ndio kwanza wanazidisha maovu na huko tunakoelekea ndio kubaya zaidi, so it's up to you wanaume kuamua either mbadilike muache kuchezea na kuharibu wanawake au muendelee halafu mwisho wa siku mje kuoa hao hao maana ndio ambao wapo wala msidhani mtashushiwa hao mabikira mnaowataka
Ni kwa sababu imeshaonekana kwamba wenye shida na hizo bikira na tabia njema kutoka kwa wanawake ni ninyi na siyo wao wenyewe so ninyi kama ninyi mnafanya jitihada gani ili mfike nao wakiwa na hizo sifa hadi kwenye umri wa ndoa, kama bado mtaendelea kushindana nao kwamba wao ndio wajitunze kwa visingizio vya kipumbavu eti maumbile sijui nini basi msitegemee lolote na wala msiwalaumu pale ambapo mnataka kuoa bali mkubali tu kushusha vigezo vyenu na kuvuna mlichokipanda, tangu jamii imeanza kuwatukana wanawake matusi na kuwaita majina yote mabaya kama wanawake wangekuwa wanajali basi wangeshaanza kubadilika lakini matokeo yake ndio kwanza wanazidisha tabia za hovyo so my point is wanaume mkiona mnaumizwa na mnachukizwa na umalaya na ukahaba wa wanawake basi chagueni moja either anzeni ninyi kubadilika au la hamuwezi basi kubalianeni na hali halisi
Okay, nina maswali kwako?
1. Nini kitatokea kama wanawake watagomea wanaume kulala nao hadi tu pale watakapojicommit kwa familia zao kwa kuja na wazazi wao kutoa posa na kuoa kihalali, je wanaume wakikutana na huo utaratibu watapata vipi mwanamke wa kufanya nae mahusiano ya kingono nje ya ndoa?
2. So katika haya maelezo yako yote umefanya assumption kuwa mwanamke hana akili wala ufahamu wa kutambua umuhimu wa bikra yake mwenyewe katika kuanza maisha na mwanaume, why aiweke rehani akijua thamani yake, so wanawake hajui thamani ya bikra?
3. Kama una assume wanawake hawajui thamani ya Bikra then nikuulize je ni sahihi pia kwa mwanaume kutojua wajibu wa kujali na kumtunza mke wake atakae muoa? Kama umeweza kumpa mwanamke pass ya kutothamini kitu kinachompa thamani muhimu kama mke wa mtu then automatically unaopia uhalali wa kuassume ni sahihi kwa wanaume wote kupewa pass au kukaushiwa kama wanafeli majukumu yao kwa makusudi, si ndio?
4. Umezungumzia swala la wanaume kutongoza mabinti kama ndio sababu ya mabinti wa kisasa kutokuwa na bikra na kutozitunza, nikuulize mama zetu na bibi zetu unadhani walikuwa hawatongozwi miaka hiyo, haukusikia story zao wakihadithia namna waliwakwepa babu zetu kwa sharti kuwa wakapose kwanza makwao ndipo mengine yataendelea haujawahi sikia hizo story, je swali langu kwako, unahisi ni wanaume wameshusha standards zao kama wanaume au ni wanawake wameacha kusimamia misimamo itakayolinda utu wao kwa wanaume na kuwaandaa kuheshimiwa katika ndoa kama wanawake wanaolinda miili yao?
5. Unajua kwamba kwa wastani miaka hii binti wa kisasa kati ya umri wa miaka 16 hadi 25 huwa ndoa kwake ni kosa, yaani ukimwambia nataka nikuoe na ukiwa tayari kwa kufanya hilo jambo basi atakukataa kwasababu mbali mbali kama kujiona bado mtoto kwa ndoa, shinikizo la wazazi kuwa asome kwanza mahusiano ni baadae, ulimbukeni wa uhuru wa kujiachia umri wa usichana ili watumike kwanza sababu soko la ngono linawaita sana, wanaume wa rika lao wanakuwa bado hawana pesa na mali hivyo kuolewa nao ni kujifunga na maisha ya usichana na kupitwa na fursa nyingi za kujipatia mali.
Je, swali langu, ni nani huwa anamkataa mwenzake katika umri wa miaka 16 hadi 25 kati ya binti ambaye ndio anachanua au kijana ambae bado ndio anajitafuta anauwezo wa kumudu vitu vidogo sana ila maisha ya kuishi pamoja na mke anaweza kujikongoja ,tuongee ukweli, Mwanamke katika umri huo masharti yake ili umuoe uishi nae kama mke na tamaa yake ya kuolewa huwa inakuwa sawa sawa na akifika kuanzia miaka 28 hadi 30+ huko? [emoji848][emoji848][emoji848]