Marriage is an outdated concept

Marriage is an outdated concept

Ukiwa na watoto na mke wako mfanyakazi au mfanyabiashara na wewe pia mfanyakazi au wote wafanyabiashara utaelewa dhana ya mke mama wa nyumbani anashiriki vipi kutafuta mali za familia.

Watoto wanaumwa au mzazi unahitajika shuleni kwa mtoto huku wote shughuli zenu zinawahitaji muwepo ofisini utaelewa hii dhana.

Wote mnahitajika kusafiri au mmoja kazini mwingine safari ya kikazi no changamoto. Huwezi kumuachia majukumu yote mfanyakazi wa ndani hasa hayo niliyotolea mifano.

Ukiwa na mke mama wa nyumbani unarudi unakuta vitu vyote vipo sawa, watoto Wana maadili na tabia njema, wanavaa nguo safi, wanakula vizuri japo kwa pesa yako unakuwa na mawazo kama yako.
Sababu hujapata changamoto nilizo toleq mifano kwa vile mkeo alikuwepo badala yako kusimamia hayo yote.
Hao watoto ni kwa faida ya nani kwanza tuanzie hapo
 
Kutokana na tafiti zilizofsnywa na taasisi moja nchini Kenya imebainisha kuwa ukilinganisha amani na utangamanonkayi ya ndoa za:-
1. Mume mfanya(kazi/biashara) VS mke mfanya(kazi/biashara).
2. Mume mfanya(kazi/biashara) VS mke mama wa nyumbani.

Ndoa namba 2 zina more stable families living joyfully and happily ukilinganisha ndoa namba 1.

Namba 1 pesa ipo lkn wala haifanyi kazi ya kulea vema watoto mliowatafuta. Watoto muda maisha yao % kubwa wako na house girls tu. Na mwisho pesa hiyo hiyo itasimama kama shetani wa kuisamabaratisha hiyo ndoa.
Tunarudi kule kule lazima mke akae nyumbani ili mambo yaende sababu hata yeye ukitengana nae ukamuacha na watoto, still akitoka atataka mwanamke mwenzake (house girl) abakie nyumbani kutazama watoto, why kwann asiweke mwanaume atazame watoto, sababu anajua ukweli kuwa mwanaume hakaagi nyumbani kutazama watoto.
 
1. Mipango gani ambayo unahitaji kufanya before ndoa na haitaweza fanyika ukiwa ndani ya ndoa?

2. Kwann ndoa iwe mpango wa 3 why usifanye isiwepo kabisa si haina umuhimu au?

3. So unahisi mwanaume anapokuja kukutongoza akuoe ni kwa faida yake pekee yake yaani kwa maneno mengine unasema ndoa ni 100% kwaajiri ya mwanaume wewe unakwenda kumfaidisha tu na bila wewe kama mwanamke basi mwanaume hana maisha ya nje ya ndoa kama wewe hapo unavyojinasibu kuwa una mipango yako nje ya ndoa unahisi mwanaume hana?

4. Mipango gani ambayo mwanaume amekamilisha ndipo aoe hebu nipe ufafanuzi eneo hilo labda mimi kuna vitu kama mwanaume sivifahamu au sijavikamilisha.

5. Ni stress gani ambazo anakuwa nazo mwanamke ambazo zinaweza kuwa kikwazo katika kutumikia ndoa yake kwa umakini?

6. Kitu kinakuwaje cha muhimu halafu kisiwe cha ulazima?

7. So una muda gani wa kufanya mipango yako na wakati ukifanya hiyo mipango unakuwa single bila kuwa na mahusiano yaani hakuna kuingiliwa kimwili na mtu?

8. Je hiyo mipango yako inafaida gani kwa huyo unayekwenda kuolewa nae na kuishi nae pamoja na kama ina faida nae why ufanye pekee yako?

Naomba unijibie hayo maswali kwanza.
1. Siwezi kusoma nikiwa ndani ya ndoa

2.Ndoa ni muhimu lakini sio lazima
Ukitaka kuamini sio lazima 'Twende makaburini ukanioneshe kaburi la mwanamke aliyekua hajaolewa'

3. Ndoa ni faida ya wote, kabla ya kuingia kuna maandalizi kwa mwanaume na mwanamke
Ndio maana unaweza kumuuliza mwanaume utaoa lini anakujibu 'nikijipanga' (Mimi sijajipanga bado!!!!)

4.Mwanaume unatakiwa uoe ukiwa unaweza kujimudu wewe mwenyewe kiuchumi na akili.
Ndoa ni ya wanaume na sio wavulana.

5.Sijui stress za wanawake wengine,
Najua stress zangu ambazo ni masomo.

6.Kitu cha lazima ni kile ukikosa utaumwa au kufa mfano; Uhai, Chakula, afya njema
Cha muhimu ni kile kinachoongeza faida lakini ukikosa hupati madhara mfano; kumiliki gari, kua na ndoa.

7. Kuingiliwa ni jambo la muhimu ila sio lazima, Nikiamua hakuna wa kunizuia.

8. Mipango yangu ina faida kwangu kwa 100% mafanikio yangu yatamnufaisha yeye baadae.... Ndoa inahitaji kupewa muda
Muda wangu hautoshi kumpikia, kumfulia, kuzaa na mtoto wa mtu kwasasa.
 
Sheria ya ndoa imemtasfiri mwanamke wa kizazi cha nyuma kidogo ambae alikua na maadili mema, mtiifu na ana dhamira ya dhati kuidumisha ndoa yake. Kwa sasa wanawake wamejanjaluka na washaona sheria ya ndoa na mahusiano kiujumla ina mianya ambayo inaweza kuwapa pesa/utajiri kirahisi.

Hata wanawake wanaotetea ndoa point zao huwa wanazielekeza zaidi kwenye kuonyesha madhaifu ya wanaume ili ionekane jinsia zote mbili zina shida lakini hapo kwenye upendeleo wanaopewa na sheria mfano kugawana mali ambazo hawanashiriki kuzitafuta huwa hawapagusi.

Kwa mwanaume mwenye ndoto kubwa za kufika mbali kiuchumi basi ndoa ni mtego mkali sana ambao uko mbeleni unaweza kwenda kuiangusha himaya yako uliyoitolea jasho kuijenga kwa miongo mingi

Kwa mwanamke ambae hana mchango wa moja kwa moja kwenye shughuli za kiuchumi za mwanaume sioni kama ana uhalali wa kupata mgao wa mali baada ya ndoa kuvunjika, hivi mke ambae ni std 7 au o-level failure atatoa mchango gani kuhusu masuala ya tax clearance au business law kwenye biashara zangu?

Kama suala ni kuitunza nyumba na kunipikia chakula je yeye alikua haishi hapo? Alikua hali hapo? Kama mimi natakiwa kufidia muda na jitihada zake kunitunzia nyumba na kunipikiq chakula kupitia kugawana mali mbona mwanamke hawajibiki kunirudishia fidia ya gharama nilizoingia kumpa hifadhi na chakula na matunzo mengine(mavazi, matibabu n.k)?

Kuna watu watakuja hapa kusema vijana tunaona malaya, tunachagua mke instagramu n.k, lakini kumbuka watu wanabadilika hata ukimchukua mke ambae hajasoma uko kijijini sio guatantee ya kusema atabaki ivyo ivyo siku zote.

Hofu ya mustakabali wa maisha ndio umfanya mwanamke aone ndoa ni security kwake. Mwanamke huyu akishapata uhakika wa mustakabli wa maisha yake bila kumtegemea mwanaume basi uona mwanaume ni kikwazo kwake katika kujitawala na hapa ndipo hekaheka zinaanza. Ni wakati wa sheria kumuangalia mwanamke pia kama predator.
Tafuta ajira kwanza
 
Okay, nina maswali kwako?

1. Nini kitatokea kama wanawake watagomea wanaume kulala nao hadi tu pale watakapojicommit kwa familia zao kwa kuja na wazazi wao kutoa posa na kuoa kihalali, je wanaume wakikutana na huo utaratibu watapata vipi mwanamke wa kufanya nae mahusiano ya kingono nje ya ndoa?

2. So katika haya maelezo yako yote umefanya assumption kuwa mwanamke hana akili wala ufahamu wa kutambua umuhimu wa bikra yake mwenyewe katika kuanza maisha na mwanaume, why aiweke rehani akijua thamani yake, so wanawake hajui thamani ya bikra?

3. Kama una assume wanawake hawajui thamani ya Bikra then nikuulize je ni sahihi pia kwa mwanaume kutojua wajibu wa kujali na kumtunza mke wake atakae muoa? Kama umeweza kumpa mwanamke pass ya kutothamini kitu kinachompa thamani muhimu kama mke wa mtu then automatically unaopia uhalali wa kuassume ni sahihi kwa wanaume wote kupewa pass au kukaushiwa kama wanafeli majukumu yao kwa makusudi, si ndio?

4. Umezungumzia swala la wanaume kutongoza mabinti kama ndio sababu ya mabinti wa kisasa kutokuwa na bikra na kutozitunza, nikuulize mama zetu na bibi zetu unadhani walikuwa hawatongozwi miaka hiyo, haukusikia story zao wakihadithia namna waliwakwepa babu zetu kwa sharti kuwa wakapose kwanza makwao ndipo mengine yataendelea haujawahi sikia hizo story, je swali langu kwako, unahisi ni wanaume wameshusha standards zao kama wanaume au ni wanawake wameacha kusimamia misimamo itakayolinda utu wao kwa wanaume na kuwaandaa kuheshimiwa katika ndoa kama wanawake wanaolinda miili yao?

5. Unajua kwamba kwa wastani miaka hii binti wa kisasa kati ya umri wa miaka 16 hadi 25 huwa ndoa kwake ni kosa, yaani ukimwambia nataka nikuoe na ukiwa tayari kwa kufanya hilo jambo basi atakukataa kwasababu mbali mbali kama kujiona bado mtoto kwa ndoa, shinikizo la wazazi kuwa asome kwanza mahusiano ni baadae, ulimbukeni wa uhuru wa kujiachia umri wa usichana ili watumike kwanza sababu soko la ngono linawaita sana, wanaume wa rika lao wanakuwa bado hawana pesa na mali hivyo kuolewa nao ni kujifunga na maisha ya usichana na kupitwa na fursa nyingi za kujipatia mali.

Je, swali langu, ni nani huwa anamkataa mwenzake katika umri wa miaka 16 hadi 25 kati ya binti ambaye ndio anachanua au kijana ambae bado ndio anajitafuta anauwezo wa kumudu vitu vidogo sana ila maisha ya kuishi pamoja na mke anaweza kujikongoja ,tuongee ukweli, Mwanamke katika umri huo masharti yake ili umuoe uishi nae kama mke na tamaa yake ya kuolewa huwa inakuwa sawa sawa na akifika kuanzia miaka 28 hadi 30+ huko? [emoji848][emoji848][emoji848]
1. Na hicho ndicho nilichokuwa nakisema kwamba wanaume hamjui mnachotaka, sasa mnapotaka wanawake wajitunze mlikuwa mnafikiri mtapata wapi wanawake wa kufanya nao ngono kabla ya ndoa, hiyo inamaanisha kwamba na ninyi mtatakiwa mjitunze ili mkutane kwenye ndoa mkiwa wote mmejitunza na kama mnaona ngumu hamuwezi basi msiwalaumu wanawake

2. Hapo nafikiri hujanielewa sijasema kwamba wanawake kukubali hovyo ndio hawana makosa bali nilichosema ni wote mna makosa, ila ninawashangaa wanaume kujitoa na kujiona mko innocent hamna makosa kwa kisingizio kwamba jinsia yenu inawabeba kwahiyo kwenu ni sahihi tu kuendelea kuwahadaa wanawake, ila wanawake ndio wajinga kukubali eti kisa wao ndio wanaodharaulika kwenye jamii what kind of cockamamie logic is this

3. Wakati mwingine wanawake huwa ni victims tu wa uongo wenu kwa sababu wenyewe huwa mnakiri kwamba, mara nyingi mnawaingia wanawake kwa gia ya kuwaoa sababu mnajua ni kitu ambacho wengi wanakitamani, na kweli mwanamke anakubali anajua anaenda kuolewa kumbe wewe lengo lako lilikuwa kula na kusepa tu sasa hapo kwanini umlaumu mwanamke mind you wanawake siyo malaika mkuu

4. Enzi za bibi zetu angalau babu zetu walipokuwa wakiwatongoza bibi zetu kisha wakaambiwa wakapose kwanza walikuwa wanakubali kama wamependa kweli lakini je hawa wanaume wa leo wanakubali, wewe mwenyewe shahidi sema tu ukweli leo hii mwanaume yeyote ukimuambia aende kujitambulisha tu achilia mbali kuposa kisha ndio ale mzigo anakuambia hawezi kuuziwa mbuzi kwenye gunia, yani dunia ya leo mwanamke kubania mzigo siyo tena ticket ya kuolewa kama zamani kwahiyo wanawake nao wanakata tamaa wanaamua kutoa tu na hapo sasa ndipo wanapokutana na mafisi waliojificha kwenye kivuli cha waoaji wazee wa kula na kusepa

5. Mkuu ni kweli kwamba siku hizi wanawake wengi wa umri huo wanatakaa kuolewa kwa sababu za kimasomo na kujiona hawako tayari kwa ajili ya ndoa, lakini kama mtu anajiona hayuko tayari kwa ajili ya ndoa kwanini umlazimishe huoni kama anakuwa amekusaidia kuliko kukudanganya kuwa anafaa kuwa mke halafu mkifika ndoani akionesha tabia zake halisi uanze kulalamika tena kwamba amefungua makucha yake, lakini pia jambo lingine nimegundua wanawake wa umri huo wanaokataa kuolewa na vijana wa rika lao sababu siyo kutokuwa na pesa au mali tu bali vijana wa umri huo pia wameshaonekana kuwa bado hawajatulia bado damu inachemka hawawezi kutulia na mwanamke mmoja wengi wanaoa lakini michepuko kama yote sasa sidhani kama kuna mwanamke atakuwa tayari kwa hilo labda awe desperate na mwenye low self esteem
 
U
Sheria ya ndoa imemtasfiri mwanamke wa kizazi cha nyuma kidogo ambae alikua na maadili mema, mtiifu na ana dhamira ya dhati kuidumisha ndoa yake. Kwa sasa wanawake wamejanjaluka na washaona sheria ya ndoa na mahusiano kiujumla ina mianya ambayo inaweza kuwapa pesa/utajiri kirahisi.

Hata wanawake wanaotetea ndoa point zao huwa wanazielekeza zaidi kwenye kuonyesha madhaifu ya wanaume ili ionekane jinsia zote mbili zina shida lakini hapo kwenye upendeleo wanaopewa na sheria mfano kugawana mali ambazo hawanashiriki kuzitafuta huwa hawapagusi.

Kwa mwanaume mwenye ndoto kubwa za kufika mbali kiuchumi basi ndoa ni mtego mkali sana ambao uko mbeleni unaweza kwenda kuiangusha himaya yako uliyoitolea jasho kuijenga kwa miongo mingi

Kwa mwanamke ambae hana mchango wa moja kwa moja kwenye shughuli za kiuchumi za mwanaume sioni kama ana uhalali wa kupata mgao wa mali baada ya ndoa kuvunjika, hivi mke ambae ni std 7 au o-level failure atatoa mchango gani kuhusu masuala ya tax clearance au business law kwenye biashara zangu?

Kama suala ni kuitunza nyumba na kunipikia chakula je yeye alikua haishi hapo? Alikua hali hapo? Kama mimi natakiwa kufidia muda na jitihada zake kunitunzia nyumba na kunipikiq chakula kupitia kugawana mali mbona mwanamke hawajibiki kunirudishia fidia ya gharama nilizoingia kumpa hifadhi na chakula na matunzo mengine(mavazi, matibabu n.k)?

Kuna watu watakuja hapa kusema vijana tunaona malaya, tunachagua mke instagramu n.k, lakini kumbuka watu wanabadilika hata ukimchukua mke ambae hajasoma uko kijijini sio guatantee ya kusema atabaki ivyo ivyo siku zote.

Hofu ya mustakabali wa maisha ndio umfanya mwanamke aone ndoa ni security kwake. Mwanamke huyu akishapata uhakika wa mustakabli wa maisha yake bila kumtegemea mwanaume basi uona mwanaume ni kikwazo kwake katika kujitawala na hapa ndipo hekaheka zinaanza. Ni wakati wa sheria kumuangalia mw
Umeandika vizuri sana na ukweli mtupu .

Ndoa kwa sasa wanawake wote hata wa vijijini wanaingia kama ajira ili baadae kupitia udhaifu wa sheris na ujinga wa wanaume wavune mali ambazo hawakuzitolea jasho hata kama ni muajiriwa. Wanaume wengi wamekubali upumbavu wa kuruhusu mke asichangie gharama za uendeshaji fanilia wakati ana kipato, lakini baadae anadai tena mgawanyo wa mali ambayo kwanza hakuichuma lakini pia hata chakula tu alikuwa hachangii. Hoja inayotumiwa kuwa alikuwa anampikia chakula ni mufilisi sababu mume naye alikuwa ananunua hicho chakula lakini pia licha ya mume kununua chakula ni ukweli kuwa chakula hicho kinapikwa na housegirl kwa sababu mke anashinda kazini na kusafiri kikazi.

Starting point kwa mume anayejitambua ni kumbana na kumlazimisha mke kama anafanya kazi/biashara achangie gharama za chakula kwa uwiano wa kipato chake au pasu kwa pasu kama kipato chake ni sawa au kikubwa kuliko cha mume. Gharama za maendeleo kama ujenzi au gari kila mtu afanye kivyake bila kuchangishana ila mnaweza kutumia pamoja mfano nyumba mnaweza ishi ingawa ni mali ya mmoja wenu.

Kama hukumbana tangu mwanzo wa ndoa na ukakubali kuishi kwa kunyonywa basi kwa mke ni ushindi wa kwanza na huko mbeleni lazima atang'ang'ania mali zako tena waume wengine wanadhulumiwa mali zote sio tena 50 kwa 50..
 
@Jadda njoo usome hapa, mtu anataka kuoa anajibiwa "bado nipo nipo kwanza". Sasa kwann nisimtafutie ela ya simu mpya, saloon na kitimoto ili anipe hata nafasi ya kumkula tu kisha nitemane nae.
Si unaona sasa na hapo ndipo tatizo lilipo hapo ambapo wanaume hamtaki kukubali kwamba mna makosa kwahiyo wewe suala la kutaka kula na kusepa kisa kakataa kuolewa na wewe unajiona uko sawa, huwa nashindwa kuelewa kwanini wanaume you never take no for an answer when it comes to approaching women sijui kwanini huwa mnahisi mna haki ya kukubaliwa tu na mwanamke yeyote yule mnayetongoza na mkikataliwa basi inakuwa ni uadui na visasi where do you get this sense of entitlement from, kama mtu amekataa kuolewa na wewe kuna ulazima gani wa kuzini naye si umuache uendelee kutafuta yule ambaye atakuwa tayari kuolewa na wewe kisha umuoe na kama mnaona hilo ni gumu hamuwezi sasa hizi lawama na matusi kwa wanawake vinatoka wapi wakati ninyi ndio mnafanya kila namna ili muwashawishi wanawake wasiowapenda kwa kutumia udhaifu wao to fall into your trap..pathetic!!
 
Si unaona sasa na hapo ndipo tatizo lilipo hapo ambapo wanaume hamtaki kukubali kwamba mna makosa kwahiyo wewe suala la kutaka kula na kusepa kisa kakataa kuolewa na wewe unajiona uko sawa, huwa nashindwa kuelewa kwanini wanaume you never take no for an answer when it comes to approaching women sijui kwanini huwa mnahisi mna haki ya kukubaliwa tu na mwanamke yeyote yule mnayetongoza na mkikataliwa basi inakuwa ni uadui na visasi where do you get this sense of entitlement from, kama mtu amekataa kuolewa na wewe kuna ulazima gani wa kuzini naye si umuache uendelee kutafuta yule ambaye atakuwa tayari kuolewa na wewe kisha umuoe na kama mnaona hilo ni gumu hamuwezi sasa hizi lawama na matusi kwa wanawake vinatoka wapi wakati ninyi ndio mnafanya kila namna ili muwashawishi wanawake wasiowapenda kwa kutumia udhaifu wao to fall into your trap..pathetic!!
Bora mtu usiolewe kuliko kukubali kuolewa na yeyote muhimu anapumua.
Kwenda kuishi ndoa ya mateso kwanini???

Wanaopapatikia kuolewa na yeyote umri ukienda wengi wao ni wale waliofail maisha!

Wanatafuta msaada ni wapi wataenda kuolewa ili wale chakula cha Bure!
 
Tunarudi kule kule lazima mke akae nyumbani ili mambo yaende sababu hata yeye ukitengana nae ukamuacha na watoto, still akitoka atataka mwanamke mwenzake (house girl) abakie nyumbani kutazama watoto, why kwann asiweke mwanaume atazame watoto, sababu anajua ukweli kuwa mwanaume hakaagi nyumbani kutazama watoto.
Swadakta mkuu
 
Wanawake wa kiafrika wameiga life style ya wanawake wa kizungu bila kujua wenzao wana advantage ya kiuchumi kuwa na mazingira na maisha mazuri so hata maswala ya kifedha sio issue sana kwao.

Ila hawa Waafrika wanaleta viburi huku uchumi wenyewe huu unatandika balaa hata mkiwa wawili, sasa wao wakiwa bado wabichi dharau kibao, balaa ni wakishafika 30+ hapo ndipo wanaelewa kwann afrika ndoa ni muhimu kwa mwanamke kuliko elimu.

Ila ngoja watajifunza kwa vitendo kama kuwafundisha kwa maneno tumeshawaambia sana hadi tumechoka.
Uko vizuri katika vita ya kisaikolojia! 😂😂

Masikini binti ambaye hajajengwa vizuri kisaikolojia akisoma hapa anatetereka anaenda kuolewa na “chochote” kinachokuja mbele yake 🤣

Kwa ndoa gani? Hizi tunazoziona mtaani au? Wana JF Yawezekana mna kamtaa chenu mnaishi ambapo mimi sijawahi kufika.

Wewe ungekuwa na binti wa miaka 20 sasa ungemshauri nini? Be practical please.
 
Bora mtu usiolewe kuliko kukubali kuolewa na yeyote muhimu anapumua.
Kwenda kuishi ndoa ya mateso kwanini???

Wanaopapatikia kuolewa na yeyote umri ukienda wengi wao ni wale waliofail maisha!

Wanatafuta msaada ni wapi wataenda kuolewa ili wale chakula cha Bure!
Yani ukisema hivi wanaume wanakuambia eti oo ngoja ukifika umri fulani bila ndoa au ukiwa single mother utatafuta mwanaume yeyote tu mradi anapumua, sijui wao wanaume wanawachukuliaje ila binafsi wanawake wa aina hiyo huwa nawachukulia kama walio desperate na wenye low self esteem tu mwanamke anayejitambua hawezi kukubali kuolewa na mwanaume yeyote ili mradi tu anapumua no matter the circumstances, wanaume nao wanatakiwa kujua kwamba siyo sifa wala raha mwanamke kufikia hatua hiyo bali inaonesha jinsi gani kwenye dunia ya leo wanawake wanawachukulia wanaume kwamba ni kimbilio pale tu wanapokuwa na matatizo na wameshachoka na si vinginevyo
 
Si unaona sasa na hapo ndipo tatizo lilipo hapo ambapo wanaume hamtaki kukubali kwamba mna makosa kwahiyo wewe suala la kutaka kula na kusepa kisa kakataa kuolewa na wewe unajiona uko sawa, huwa nashindwa kuelewa kwanini wanaume you never take no for an answer when it comes to approaching women sijui kwanini huwa mnahisi mna haki ya kukubaliwa tu na mwanamke yeyote yule mnayetongoza na mkikataliwa basi inakuwa ni uadui na visasi where do you get this sense of entitlement from, kama mtu amekataa kuolewa na wewe kuna ulazima gani wa kuzini naye si umuache uendelee kutafuta yule ambaye atakuwa tayari kuolewa na wewe kisha umuoe na kama mnaona hilo ni gumu hamuwezi sasa hizi lawama na matusi kwa wanawake vinatoka wapi wakati ninyi ndio mnafanya kila namna ili muwashawishi wanawake wasiowapenda kwa kutumia udhaifu wao to fall into your trap..pathetic!!
Hili andiko lipo makini sana. Truth be told, wanaume hautupendi kukataliwa for sure. Tujifunze kukubaliana na hali if someone is not interested let them go. Matatizo ya ndoa mengi hanzia pale relationship inapokua mbich ukiona your partner is tolerating you, au it's like una invest nguvu nying kuliko yeye jua tayar ukuta una nyufa it's a matter of time ndoa itavunjika. Na hii concept ya ndoa is an outdated thing sio valid, tatizo sio ndoa tatizo ni wanandoa!
 
Back
Top Bottom