Masahihisho: Kinachosherehekewa ni Uhuru wa Tanganyika siyo Tanzania Bara. Hatutavumilia upotoshaji

Zaire, the Congo, Congo Kinshasa,DRC......Swaziland, Eswatin..... Malawi ,Nyasaland.... Nk. Wanaposherehekea siku ya uhuru wao sijui wanasemaje! Confused.
Hawa walibadili majina hawakubadili Utaifa wala mipaka ya Nchi yao
 
Tanganyika siyo Tanzania, Acha Uongo
Heshima kitu cha bure, kuita wazee wako waongo sio heshima!. Uhuru ni wa Tanganyika, hivyo kumbukumbu ni ya uhuru wa Tanganyika lakini sherehe za uhuru ni sherehe za uhuru wa Tanzania bara! Kwasababu Tanganyika haipo tena, kilichopo ni Tanzania bara.
P
 
Hivi sherehe za uhuru wa Tanganyika na za Muungano ziko sawa??
 
Tanganyika siyo Tanzania, Acha Uongo
Nawatakia mapumziko mema ya kumbukumbu ya siku uhuru na jamhuri ya nchi iliyokuwa Tanganyika sasa Tanzania。Tarehe 9 Desemba 1961 Tanganyika ilipata uhuru toka kwa mkoloni Mwingereza,9 Desemba 1962 ikawa jamhuri。 Tarehe 26 April 1964 ikaungana na Zanzibar na kubadili jina na kuwa Tanzania,hivyo leo tunapoadhimisha siku hii,ile Tanganyika iliyopata uhuru wake siku hii sasa haipo tena,iliyopo ni Tanzania hivyo kumbukumbu ndio ya Tanganyika lakini maadhimisho ni ya Tanzania。

Heri ya Uhuru na Jamhuri。

P。
 
Ni lini Tanganyika ilibadilishwa jina kutoka Tanganyika hadi kuwa Tanzania bara? Huo ni uongo wa ccm. Hakuna nchi inayoitwa Tanzania bara hata kwenye katiba ya nchi haipo.
 
Hatutakubali kupigwa fix hata kama anayetudanganya anatembelea mkongojo, Heshima ya namna hiyo hata Mungu ametukataza
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…