Masaki, Dar: Adam Malima atishiwa kwa Bunduki, Risasi zarindima kama Njugu

Masaki, Dar: Adam Malima atishiwa kwa Bunduki, Risasi zarindima kama Njugu

Ila hili jambo ni rahisi, sana tutii sheria bila shuruti na tujiheshimu na tuheshimu polisi nchi yetu itakuwa salama nasi tutaona mambo Safi.

Ila Kama, sisi ndiyo chanzo cha dharau na kutetea waharifu tegemea jamii kuwa na migogoro mingi.
Kwa Sababh Polisi wamekuwa kama tawi la chama kimoja cha Siasa
 
Kwa maelezo haya, polisi hajafanya kosa kabisa kufyatua risasi hewani.

Kwa sababu, naona maelezo hapo yanasema wananchi walikuwa Karibu kujichukulia sheria mikononi.

Hivyo, polisi kuokoa maisha ya aliyedhaniwa ni jambazi ili asitolewe roho.

Au mi nimeelewa tofauti!?

Wananchi walikuwa wanafuatilia Majalibizano ya Malima na Askari hao Wananchi wawe Vichaa waanze kumshambulia Adamu?

Halafu kumbuka huku ni Masaki sio Tandale kwa Mkunduge?( kidding) [emoji12][emoji12]
 
Haihitaji akili ya kukaa darasani kujua ujinga wa Malima na hao waliokuwa pembeni wanachagiza maneno ya dharau kwa askari..body language ya malima dhahiri inaonyesha dharau..kwa mwenye akili na anayefahamu jukumu alilo nalo polisi na mazingira wanamofanyia kazi huwezi fanya vile malima alikuwa anaonyesha kwa polisi, tuwaheshimu askari wetu..hayo maneno maneno ya kujifanya kujua sheria ilihali sheria hawazijui bora kukaa kimya!

Humiliki hata Spoke ya Baiskeli Ndio sababu hujui adha na karaha za kusumbuliwa kwny Parking
 
I hate politician wanawapa watu ugumu wa kufanya kazi , kakosea hataki kurekebishwa eti kwa sababu alikuwa waziri , ingekuwa mm ningepiga likumbo lile wajifunze . Kwa hivi vitu wanavyofanya hata wananchi wataiga matokeo yake ni madhara makubwa . Kiongizi inapaswa awe mfano ili wananchi waige kutoka kwake . Nchi imejaa vichaa tupu
 
Bila ya kujali adha ya parking na kero nyingine ingegharimu kiasi gani kwa mtu kama malima kuomba radhi na kuyaweka sawa, mbona tunapaki vibaya mara nyingi huku tukitambua kuwa tunavunja sheria na taratibu za jiji lakin kauli njema zimekuwa zikituokoa nnahic kuna dalili za ulofa ndani ya akili za malima
 
Watu Wengi humu JF, wanawalaumu polisi ila ukiwa pale Benki unaambiwa egesha au ondoa gari eneo hili au lile mbona huwa hamji humu kusema polisi wabaya!?

Mbona tukiwa tunachukua hela kiasi kikubwa tunawalilia polisi watufanyie escort ili pesa zetu ziwe salama!?

Majambazi, wakikuvamia mbona kilio cha kwanza huwa ni kutoa taarifa polisi na kuomba msaada wao!?

Hebu jiulize, kama gari lilokuwa limeegeshwa kisha aliyeegesha akatenda uhalifu!?
Sasa hivi, ingekuwa tofauti kabisa humu JF , kuwa polisi inawaachia watu wanapaki ovyo na kusababisisha waharifu kutekeleza azima zao.

Angalia, lugha iliyotumiwa na hao waliopaki gari , kweli mtu mwenye sitaha na kujiheshimu na kuheshimu watu wengine anaweza kujibu vile!? Mbaya zaidi eti amekuwa hadi naibu waziri!?

Jiulize, ni mara ngapi watu wanapaki mahala siyo sahihi ila wanatumia lugha ya staha ao hao watendaji wanawaacha na kuondoa magari kwa ustarabu!?

Vyeo, nafasi fedha isiwe chanzo baadhi kuwadharau na kuona kazi za wengine hazifai.

Kutii, sheria na amri ndiyo suruhisho tu kwa mambo kama haya ili yasijitokeze.
 
Humiliki hata Spoke ya Baiskeli Ndio sababu hujui adha na karaha za kusumbuliwa kwny Parking
Ndio ujinga ninaousema..gari yako ina thamani zaidi ya maisha yako ambayo askari wetu wanakesha doria wewe ukiwa un.aj.amba ucku . hata shukurani huna minga wewe.baada ya kuposti ujinga hapa.
 
Uyo polisi mwenye koti kubwa sijamuelewa..alikuwa anajitetea, anatishia au alitaka watu wamsifie? Jambo lenyewe la kijinga mnapoteza silaha na muda bure
 
Nina mkanda wenye bendera ...nimeapa ...
Hata plate no za magari na pikipiki zina bendera.

Kikubwa ninachokiona ni kwamba askari wetu huwa hawapendi kusikiliza. Wanachopenda wao ni amri tu basi. Mimi sikuona cha kumfanya afyatue risasi hewani.
Alichokua anajaribu kufanya ni kumtishia yule jamaa ili asiongee.

Naipenda nchi yangu nawapenda askari. Ila wajifunze namna ya kuwa na busara. Sio kila raia ni mharifu. Ndio maana wanapewa mafunzo ya kumjua mharifu kwa kumtazama tu.

Alafu wapunguze ubabe na wafuate sheria
 
Ndio ujinga ninaousema..gari yako ina thamani zaidi ya maisha yako ambayo askari wetu wanakesha doria wewe ukiwa un.aj.amba ucku . hata shukurani huna minga wewe.baada ya kuposti ujinga hapa.

Mie ni Mkazi wa Jaribu Mpakani huku Mkuranga, unaweza kurudia kuandika comment yako?
 
Nadhani yule askari alifanya alivyofanya kwa kutokuwa na mafundisho sahihi au anatafuta kupandishwa cheo.
Busara ni vyema sasa ikatumika kuanzia sasa kuhakiki kila askari anayepewa bunduki kama ana akili timamu.

Haya matukio askari dhidi ya wabunge yamekuwa too much sasa.
 
Back
Top Bottom