Masanja Mkandamizaji aonesha mjengo wa Kanisa lake la Feel Free Church kwa mara ya kwanza

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Msanii, mtangazaji, na mtumishi wa Mungu, Emmanuel "Masanja Mkandamizaji" Mgaya, leo Disemba 25, ameonesha kwa mara ya kwanza maendeleo ya ujenzi wa kanisa lake jipya, Feel Free Church.

Kanisa la Feel Free Church linajengwa maeneo ya Uwanja wa Barafu, Mburahati, jijini Dar es Salaam, linatarajiwa kuwa kitovu cha ibada na huduma za kiroho kwa jamii.
Your browser is not able to display this video.
 
Mungu hakaagi kwenye mijengo inayoweza kulipuka na kubaki majivu..

Bishop angelijua hili wala asingehangaika kupiga hela za watu kwa kisingizio cha kumjengea Mungu..

Hapo kashusha mjengo wa makahaba na wauza unga tu na ndio watoa michango (sadaka) wake.
 
Usalama wa Taifa Tanzania umelala ,wanatakiwa wafanye investigation wangegundua utapeli mwingi sana

Matokeo yake wapo bize na Upinzani

Mfano Kiboko ya wachawi,bila kujichanganya yeye mwenyewe angeendelea kuibia watu Hadi sasa

Sasa Sampuli ya kina Kiboko ya wachawi ni wengi sana ,mwamposa,masanja,Bushiri,mwingira,kuhani Musa, n.k
 
Mtu akishasoma mistari miwili mitatu ya mtume Paulo ,anatafuta mabanzi na vitambaa vyekundu ,vyeupe, spika ya JBL ,mic mbili ,na suti ya mtumba ,anajiita mtume na nabii anafungua kanisa

Serikali ipo inakula nao
 
Usanii umehamia kwenye dini.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…