Masanja Mkandamizaji: Msinifananishe na Mchungaji wenu

Masanja Mkandamizaji: Msinifananishe na Mchungaji wenu

BigTall

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2022
Posts
525
Reaction score
1,257


Masanja Mkandamizaji ameulizwa anahisi kwa nini watu wengi hawamuelewi kwa namna yake ya mahubiri amesema kuwa sababu kubwa ni kuwa kuna watu wengi wanatamani awe kama Mtumishi wao yaani afanane nao mpaka mavazi.

Amesema “Msinifananishe na mtumishi wenu bali mwambieni mtumishi wenu afanane na mimi kwa sabanu yeye ni mtumishi wa kisasa zaidi.”

Ameeleza hayo Jijini Dar es Salaam wakati anaongea na waandishi kuhusu kampeni za kudumisha Uzalendo kwa Watanzania ili kuyasifia na kuyatangaza mambo mazuri ya taifa la Tanzania.

Mbali na hilo kampeni hii inahusu kuhamasisha zoezi la Sensa ya watu na makazi ambayo itafanyika tarehe 23-8-2022.

Chanzo: Bongo5
 
Tukumbuke biblia imeandika kuhusu manabii wa uwongo, wachungaji au watumishi wa Mungu wana demeanor au tabia, mienendo, mavazi, kutembea, kuongea, life style na kila kitu ambacho kinawatofautisha na wengine kwa kiasi kikubwa, aache janja janja kuingiza watu chaka.
 
Mbinguni mbali tutaona mwisho wake hapahapa
 


Masanja Mkandamizaji ameulizwa anahisi kwa nini watu wengi hawamuelewi kwa namna yake ya mahubiri amesema kuwa sababu kubwa ni kuwa kuna watu wengi wanatamani awe kama Mtumishi wao yaani afanane nao mpaka mavazi.

Amesema “Msinifananishe na mtumishi wenu bali mwambieni mtumishi wenu afanane na mimi kwa sabanu yeye ni mtumishi wa kisasa zaidi.”

Ameeleza hayo Jijini Dar es Salaam wakati anaongea na waandishi kuhusu kampeni za kudumisha Uzalendo kwa Watanzania ili kuyasifia na kuyatangaza mambo mazuri ya taifa la Tanzania.

Mbali na hilo kampeni hii inahusu kuhamasisha zoezi la Sensa ya watu na makazi ambayo itafanyika tarehe 23-8-2022.

Chanzo: Bongo5
Huyo ni mjini tu kama wahuni wengine hakuna injili ya kizamani na ya kisasa Neno la Mungu halijawahi kubadilika.
 
Anajiita " Askofu" ? Ametunukiwa na nani, taratibu za kupatikana kwa askafu anajua,? Au ukienda bible school hapo Arusha basi unajiita askofu?
 
Anajiita " Askofu" ? Ametunukiwa na nani, taratibu za kupatikana kwa askafu anajua,? Au ukienda bible school hapo Arusha basi unajiita askofu?
Maana ya Neno Askofu kibiblia ni mwangalizi wala siyo ukubwa kama madhehebu mengi yanavyotafsiri uaskofu.
 
Back
Top Bottom