Masauni aagiza GBT kudhibiti ushiriki wa watoto michezo ya kubahatisha

Masauni aagiza GBT kudhibiti ushiriki wa watoto michezo ya kubahatisha

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mhandisi Hamad Yussuf Masauni, ameiagiza Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania (GBT) kuhakikisha inadhibiti ushiriki wa Watoto chini ya miaka 18 katika michezo ya kubahatisha na kuandaa mkakati na mapendekezo kwa Serikali ya namna ya udhibiti huo kutokana na athari zake katika jamii.

Mhandisi Masauni ametoa agizo hilo jijini Dar es Salaam alipotembelea na kufanya mazungumzo na Menejimenti ya Bodi hiyo pamoja na wafanyakazi, katika mwendelezo wa ziara yake ya kutembelea taasisi zilizo chini ya Wizara ya Fedha na Mipango, jijini Dar es Salaam.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania (GBT), Bw. James Mbalwe, alisema kuwa kwa kipindi cha miaka mitano iliyopita kuanzia 2016/17 hadi 2020/21 jumla ya kodi zilizokusanywa na Bodi hiyo ikiwa ni mapato ghafi yanayotokana na michezo ya kubahatisha yalifikia shilingi bilioni 428.97, bila kuhusisha kodi nyingine ikiwemo Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT).

Alisema kuwa dhima ya Bodi hiyo ni kukuza, kusimamia, kufuatilia na kudhibiti tasnia ya michezo ya kubahatisha nchini ili kuhakikisha uadilifu, kuongeza faida za muda mrefu za kijamii na kiuchumi na ulinzi wa umma kwa kutekeleza Sheria yenye viwango vya kimataifa na mazoea bora.

Alisema kuwa Michezo ya kubahatisha nchini imeajiri zaidi ya watu 20,000 na kwa mwaka wa fedha wa 2020/2021, michezo hiyo imewezesha kuwepo kwa mzunguko wa fedha katika sekta ya michezo ya kubahatisha unaofikia zaidi ya shilingi trilioni 3.2 na hivyo kuchangia ukuaji wa uchumi wa nchi.


ITV
 
Back
Top Bottom