Mashabiki tuwasapoti wachezaji wetu pamoja na viongozi na benchi la ufundi pamoja na matokeo ya leo

Hakuna shabiki wa Yanga aliyeangalia mpira leo akasononeka. Kwenye mpira kuna matokeo halafu kuna performance. Yanga hawakubebwa na matokeo ila performance imekuwa juu mno. Unatazama mpira una enjoy mpira unaochezeka.
Hapa napokaa hata shabiki mmoja wa Simba alikuwa anakiri tunacheza vizuri, ila nikamwambia tatizo la soka ni kuwa, mpira ni magoli na ndio kilichotokea, lakini alikiri Yanga inacheza vizuri kuliko Simba wakati mechi inaendelea kabla hata penati hazijaanza.
 
Musonda anahitaji training ya kulenga goli, Leo mpira ulijaa akafumua shuti Kali , Huyu atatusaidia pakubwa sana
Kikosi Kiko poa Sana na kocha nizuri zaidi ya Nabi. Tunahitaji straika mwenye uwezo..... Timu iko vizuri Sana.
 
Unalazimusha wewe kuonekana kama kuna masononeko ila sisi mashabiki wa Yanga leo tume enjoy burudani.. Kutotumia nafasi kwa leo ni sehemu ya makosa yaliyotugharimu kufika penati, lakini benchi la ufundi linalo nafasi ya kulirekebisha. Game tatu tumecheza kubwa na leo ndio mechi ya kwanza kutoa sare. Hivyo kocha atajua ni wapi pa kuweka sawa

Makocha huwa wanapoanza kuinoa timu kwanza huanza kwa kutengeneza ukuta kwa maana wasiweze kuruhusu magoli, pili ni namna ya kutengeneza mashambulizi kisha mwisho ni mifumo mizuri ya kupata magoli.
Kocha yupo hatua ya mwisho hivyo huku kwenye kiungo, beki na utengenezaji mashumbulizi kamaliza kabakiza tu kwenye namna ya kufanya nafasi zinakuwa converted kuwa magoli. Muda bado anao
 
Musonda anahitaji training ya kulenga goli, Leo mpira ulijaa akafumua shuti Kali , Huyu atatusaidia pakubwa sana
Yeah but sio wakutegemea... Mechi ya Leo Kama kungekuwq na straika wa maana Wala tusingefika kwenye penati.
 
Mkude kamficha vipi Ngoma, umeangalia mpira upi? Kwanza Mkude kagusa mpira mara ngapi?
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] poleee kunywa maji mengii na u relaaaaaxxxxxx
 
Wakati kocha wako anajitafuta kutekebisha finishing atakuta tayari Simba imepata muunganiko.

Atapigwa tena halafu awe na kazi nyingine ya kwenda kufanyia kazi madhaifu ya siku hiyo ili ajirekebishe.

Ndo itavyokuwa kama umeshindwa kushinda mechi ya leo ambayo kila kitu kilikuwa upande wenu.
 
Uzuri unakiri tuliwazidi.
 
Acheni kujipa moyo kwa porojo zenu za ovyo. Yanga hamna timu, mwaka huu ni wabovu.
Haka kama yanga ni mbovu ila Simba ni zaidi , Kwa Lile pira la uturuki walilopiga Simba , aisee hakuna kitu
 
Uzuri unakiri tuliwazidi.
Mlituzidi ila mlitumia vipi advantage hiyo kuhakikisha mnachukua ngao?

Hapo ndio naposema mpira unamuheshimu fundi.

Mpira unajua tu kuwa leo fundi hajaamka vizuri hivyo siwezi nikapeleka ushindi kwenye timu mbovu.
 
Mayele1 ni sawa na Mamsonamzizee 70....dk90 uwanja umeinama lkn yanarukaruka tu mbele mpaka moloko akawa anafanya majukum ya no.9; yote sawa Timu inawatu sanaaa...ukiwaambia akina chamaa,Ngomaa,shabalala iludiwe wanakupiga mawe game ilikua motoo Sanaa kwao uchawi umewabebaa mafalaa.
 
Msonda duu naye hajatulia anajitahidi sana kupiga puu ambazo ni off target japo kocha anampenda sana ila anashindwa ku deriver
 
Umeandika kila ambacho unatamani kiwe kwa upande wako ila ulichoandika hukuwaza kiuwanamichezo. Kwanini hukuwaza kuwa yeye ataweza kutatua kabla ya nyie kupata muunganiki? Halafu ishu ipo very complicated maana mpaka sasa hamjui mna matatizo yanayotokana na nini. Wengine wanalaumu kocha wengine mfumo wengine wachezaji. Labda wewe unaona shida kwenu ni kipi?
 
Sio rahisi tukutane mara ya pili tukiwa bado tunacheza kwa aina hii ya mpira.

Kuna kipindi kirefu sana hapa katikati kabla hatujaonana. Na hivyo ishu yetu ya kupata muunganiko sio complicated kama ambavyo wewe unasema.

Mfumo mbovu ndio unaoenda kumuathiri mchezaji aonekane amecheza under performance.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…