George Betram
JF-Expert Member
- Oct 10, 2015
- 4,672
- 6,272
- Thread starter
- #21
Hakika..!Acha tuendelee kuenjoy soka la Ulaya tu
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hakika..!Acha tuendelee kuenjoy soka la Ulaya tu
Kama kutumia u freemason ni rahisi kiasi hicho. Basi ndugu zetu wa Kigoma wangeshatumia Kemia ya Kiafrika kuunda ndege za kwenda mabara mengine na zenye kubeba watu wengi zaidi.Mmmmh...
Hili gumu sana chief..!
Ila wapo watakao husisha popularity ya wanamuziki wengi wa Merikani na nguvu za "freemasons"
mimi ni mtoto wa miaka ya tisini hivyo sijui sana, ila katika pita zangu humu jamiiforums nilipata kusoma mwanajamii mmoja akisimulia jinsi walivyokuwa wakisoma gazetini habari za kina beatles na timu za ulayaHeshima kwenu wakongwe..!
Leo tujadiri kidogo kuhusu hii mada.
Kumekuwa na utaratibu wa mashabiki wa timu kubwa zilizopo Ulaya hasa Uingereza kuhoji uhalali wa mashabiki wa Man City waliopo Afrika na Tanganyika kwa ujumla.
Sasa naomba niulize,hawa mashabiki wa hizi timu kubwa za Ulaya,hapa nazizungumzia timu kama Man Utd,Liverpool,Barcelona,Chelsea,Arsenal na Real Madrid ambao wapo Tanganyika wamepatikanaje..?
Asante sana Broh kwa kuniweka sawa...
Nimeanza kufuatilia mpira wa miguu mwaka 2009 (hiyo ni kutokana umri wangu),kuna mambo mengine nalazimika nisome kwanza kwenye mtandao ndio nije huku, hata hivyo nimefurahi sana kuona baadhi ya maeneo umekubaliana na mimi..!
Duuuuh...mimi ni mtoto wa miaka ya tisini hivyo sijui sana, ila katika pita zangu humu jamiiforums nilipata kusoma mwanajamii mmoja akisimulia jinsi walivyokuwa wakisoma gazetini habari za kina beatles na timu za ulaya
kwa nionavyo asili ya mashabiki wa kiafrika wa mambo ya ulaya ulianza na magazeti
yani tangu enzi za ukoloni, magazeti na magazines ya ulaya, ya london, times ama marekani kama vile newsweek huko yaliletwa huku kusomwa na wazungu ama waafrika wasomi.
wazungu walitaka magazeti ya kwao ili wasome yanayoendelea kwao ulaya
matokeo yake waafrika wakawa nao ni wasomaji ya hayo magazeti,
humo magazetini kukawa na habari za mastaa na wanasiasa na wanamichezo wa ulaya wa enzi hizo
yamkini magazeti yalisifu na kupamba sana performance za wanamichezo wa ulaya
halafu kukawa na sinema ambapo moja ya vitu vilivyoangaliwa ilikuwa ni marudio ya recorded matches zilizochezwa huko ulaya, nayo waafrika wakajumuika kuangalia hapo ndio mashabiki walipoanza kupatikana na utamaduni huo ukaendelea kizazi hadi kizazi hadi leo hii ni mazoea yetu kupenda vya kizungu
kwahiyo chanzo cha mashabiki wa timu na miziki na bendi hata bendi za ulaya ni uwepo wa magazeti na magazines za ulaya hapa afrika miaka hiyo ya zamani, jumlisha na sinema, ambazo zilijaa content za wazungu tu
mimi ni mtoto wa miaka ya tisini hivyo sijui sana, ila katika pita zangu humu jamiiforums nilipata kusoma mwanajamii mmoja akisimulia jinsi walivyokuwa wakisoma gazetini habari za kina beatles na timu za ulaya
kwa nionavyo asili ya mashabiki wa kiafrika wa mambo ya ulaya ulianza na magazeti
yani tangu enzi za ukoloni, magazeti na magazines ya ulaya, ya london, times ama marekani kama vile newsweek huko yaliletwa huku kusomwa na wazungu ama waafrika wasomi.
wazungu walitaka magazeti ya kwao ili wasome yanayoendelea kwao ulaya
matokeo yake waafrika wakawa nao ni wasomaji ya hayo magazeti,
humo magazetini kukawa na habari za mastaa na wanasiasa na wanamichezo wa ulaya wa enzi hizo
yamkini magazeti yalisifu na kupamba sana performance za wanamichezo wa ulaya
halafu kukawa na sinema ambapo moja ya vitu vilivyoangaliwa ilikuwa ni marudio ya recorded matches zilizochezwa huko ulaya, nayo waafrika wakajumuika kuangalia hapo ndio mashabiki walipoanza kupatikana na utamaduni huo ukaendelea kizazi hadi kizazi hadi leo hii ni mazoea yetu kupenda vya kizungu
kwahiyo chanzo cha mashabiki wa timu na miziki na bendi hata bendi za ulaya ni uwepo wa magazeti na magazines za ulaya hapa afrika miaka hiyo ya zamani, jumlisha na sinema, ambazo zilijaa content za wazungu tu
Daaah...Ushabiki wa timu unaweza kuja na njia nyingi lakini mtazamo wangu ni kwamba ushindi wa mara kwa mara unachukua asilimia zaidi ya 70.
Issue zingine zinaweza kuwa:-
All in all, kila mtu ana sababu ya kwa nini timu hii na si ile.
- Kufata mchezaji unayemkubali, mfano ni jinsi ambavyo Ronaldo na Messi watu wanawafatilia.
- Ushabiki kwa influence ya mtu, mfano unapokuwa na mzazi au mshikaji akawa anakusimulia ubora wa timu yake unapoanza ushabiki unajikuta umefata.
- Kuwa tofauti na wengi, yaani kuchagua timu ambayo siyo ile inayopendwa na wengi au na mtu wako wa karibu ili tu kuleta upinzani.
- First time impression: kwamba mara ya kwanza kuangalia unajikuta unaiangalia hiyo na inashinda.
- Timu za maeneo unakoishi, mfano kuna wabongo waliosoma nje, na wanajikuta hizo timu zilikuwa mtaani (% ndogo).
- N.k
Kwa nini hao watu wa Ulaya wasiwe kama watu Tanzania, kwa kuishabikia Simba/Yanga kwanza hata kama wanakutana na timu ya nyumbani(kwa mashabiki eg Lipuli) kwao?Good topic halafu why mashabiki wa soka Tanzania wengi wao wapo Simba na Yanga tu?why Simba inapokwenda pale Iringa kucheza na Lipuli bado watajiona kama wako nyumbani,wao mashabiki wa Iringa hawaishabikii timu yao(maana bila Lipuli kuwepo wasingeona hizi timu zikija kwao)why hatuwi kama mashabiki wa UK ambao wanashabikia timu zao za nyumbani no matter what?
Mimi nilianza kumshabikia Beckham yeye kama yeye kabla ya kuanza kuipenda Man United, nilikuwa napenda sana kumuangalia akicheza, nikajikuta taratibu nakuwa shabiki wa timu
That Night at instabull huenda ndo ilifanya niipende Liverpool, enzi hizo 2005 nikiwa darasa La 4 , ile fainali nilienda kuangalia na baba( yeye ni man utd) nikatokea kumkubali Steven Gerrard kwa hiyo mpaka nakuakua nikawa naipenda liver, nakumbuka fainali ya 2007 enzi hizo niko darasa la sita niliwekeana sh 50 na rafiki yangu yeye alikua Ac Milan wa kutupwa sababu ya Ricardo kaka, daah nakumbuka sh 50 yangu ililiwa, soka nilianza kulijua kitambo sana sababu baba ,kaka walikua watu wa mpiraGeorge Betram naomba nirekebishe kidogo kwa Liverpool.
Liverpool ilipata washabiki wengi miaka ya 70 - 90, kipindi hiki ndicho kipindi ambacho Liverpool ilikuwa na mafanikio makubwa domestically na Europe kwa ujumla, chini ya Bill Shankly, Bob Paisley, Joe Fagan na Kenny Daglish.
Baada ya hapo, Liverpool imeendelea kusafiria huo upepo wa mafanikio mpaka leo hii, impact ya Benitez ilikuwa ndogo sana kuongeza washabiki ukilinganisha na misingi aliyoiweka Bill Shankly.
Nakubaliana na wewe kwa Man United, wamewahi kuwepo kwenye mafanikio chini ya mkongwe Matt Busby, lakini Ferguson ndiye aliyewapa mafanikio kwa kipindi cha 1990s - 2013. Same to Liverpool now, Man United anatembelea upepo wa Fergie leo.
Nini point yangu kuweka hiyo miaka:-
Kutengeneza loyal fans si kitu cha muda mfupi, na wale ambao wanashuhudia mafanikio kwa kipindi cha muda mrefu wanakuja kukaa na hiyo timu kwa kipindi cha muda mrefu kwa sababu inakuwa kama ndoa iliyokaa muda mrefu, hivyo unakuwa unaona hata nikiachana naye naenda wapi.
Arsenal, Chelsea zina washabiki, lakini misingi iliyojengwa kwa washabiki wa Liverpool na Man United ni imara kupita ya Arsenal na Chelsea.
Ndiyo maana ukiangalia asilimia kubwa ya washabiki wa Man City ni wanaotoka Arsenal na Chelsea, au wale wanaonza ushabiki kipindi hiki.
Na kama ghafla City akapoteza utawala wake utaona mashabiki wanarudi walikotoka au kuhamia kwa timu itakayoibuka.
Mpaka sasa Man City bado hajashinda kiasi cha kutengeneza strong bond kati yake na washabiki wake.
Ni kweli washabiki wote ni glory hunters, lakini kwenye hunting inafika sehemu unatengeneza loyalty, na hiyo lazima iwe ya muda mrefu hasa.
Kuanzia mwaka 2000 hiviItakuwa ni kipindi kile anafuga nywele, miaka ya 1997-2001.
Kuanzia mwaka 2000 hivi
Mimi ni under mtu mzimaAhahaaaaah...
Unataka kusema kitu gani Kiongozi..?
Hii Newcastle si imejichokea sasa hivi tu..!
Newcastle imesumbua sana Uingereza...
Na ilikuwa na mashabiki kibao tu hapa Tanganyika...
Miaka ya 1996 mpaka 2000 Newcastle ilikua timu ya hatari...
Labda utaje timu nyingine Chief,lakini sio Newcastle ya Alan Shearer..!
Mashabiki wa Newcastle wapo sana tu,ila wengi ni watu wazima...
Katika miaka fulani ilikuwa kidogo kuna unafuu enzi za kina Pamba, Majimaji, Reli Moro, CDA, RTC Kigoma, Tukuyu, Milambo na zingine ilianza kuleta upinzani na team hizi mbili kubwa lakini tumeruudi zero tena. Ili tuendelee kikweli lazima tushabikie kwa nguvu team zetu tunakotoka. Napenda sana EPL watu wanapenda team zao hata za wilaya tu tena kwa nguvu. Juzi nilikuwa naangalia Charlton sijui wako Div 2 uko South London na ilikuwa Premier wakati fulani lakini watu wamejaa na wanashangilia team yao. Tukibadilika kwa hili basi na mpira utakuwa ila inakera kuona simba au Yanga wanaenda mikoani halafu watu wanaandamana kuzishangilia haiko sawa kabisa. sijui kama linawezekana lakini naomba siku nione haya na hizi team kubwa ndio zitapata adabu.Good topic halafu why mashabiki wa soka Tanzania wengi wao wapo Simba na Yanga tu?why Simba inapokwenda pale Iringa kucheza na Lipuli bado watajiona kama wako nyumbani,wao mashabiki wa Iringa hawaishabikii timu yao(maana bila Lipuli kuwepo wasingeona hizi timu zikija kwao)why hatuwi kama mashabiki wa UK ambao wanashabikia timu zao za nyumbani no matter what?
Full stop mkuu... umemalizaUshabiki wa timu unaweza kuja na njia nyingi lakini mtazamo wangu ni kwamba ushindi wa mara kwa mara unachukua asilimia zaidi ya 70.
Issue zingine zinaweza kuwa:-
All in all, kila mtu ana sababu ya kwa nini timu hii na si ile.
- Kufata mchezaji unayemkubali, mfano ni jinsi ambavyo Ronaldo na Messi watu wanawafatilia.
- Ushabiki kwa influence ya mtu, mfano unapokuwa na mzazi au mshikaji akawa anakusimulia ubora wa timu yake unapoanza ushabiki unajikuta umefata.
- Kuwa tofauti na wengi, yaani kuchagua timu ambayo siyo ile inayopendwa na wengi au na mtu wako wa karibu ili tu kuleta upinzani.
- First time impression: kwamba mara ya kwanza kuangalia unajikuta unaiangalia hiyo na inashinda.
- Timu za maeneo unakoishi, mfano kuna wabongo waliosoma nje, na wanajikuta hizo timu zilikuwa mtaani (% ndogo).
- N.k
That Night at instabull huenda ndo ilifanya niipende Liverpool, enzi hizo 2005 nikiwa darasa La 4 , ile fainali nilienda kuangalia na baba( yeye ni man utd) nikatokea kumkubali Steven Gerrard kwa hiyo mpaka nakuakua nikawa naipenda liver, nakumbuka fainali ya 2007 enzi hizo niko darasa la sita niliwekeana sh 50 na rafiki yangu yeye alikua Ac Milan wa kutupwa sababu ya Ricardo kaka, daah nakumbuka sh 50 yangu ililiwa, soka nilianza kulijua kitambo sana sababu baba ,kaka walikua watu wa mpira
Chief...washabiki wa ukweli ni wa arsenal na man u, hao wa timu nyingine ni bendera fuata upepo
Kwani wa Kagera amewezaje kushangilia simba na sio kageraHeshima kwenu wakongwe..!
Leo tujadiri kidogo kuhusu hii mada.
Kumekuwa na utaratibu wa mashabiki wa timu kubwa zilizopo Ulaya hasa Uingereza kuhoji uhalali wa mashabiki wa Man City waliopo Afrika na Tanganyika kwa ujumla.
Sasa naomba niulize,hawa mashabiki wa hizi timu kubwa za Ulaya,hapa nazizungumzia timu kama Man Utd,Liverpool,Barcelona,Chelsea,Arsenal na Real Madrid ambao wapo Tanganyika wamepatikanaje..?