Mashariki ya kati yasema hawataiokoa Ulaya pindi wakijizuia kununua gesi ya Urusi

Mashariki ya kati yasema hawataiokoa Ulaya pindi wakijizuia kununua gesi ya Urusi

Webabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2010
Posts
8,870
Reaction score
14,258
Mtaalamu wa uzalishaji na biashara za mafuta na gesi wa Abudhabi bw Said Albakr amebainisha kuwa iwapo nchi za Ulaya zitaendelea kujizuia kununua gesi ya Urusi basi wasitarajie kupata mbadala kutoka nchi za mashariki ya kati na kokote kwengine duniani katika kipindi cha miaka ya karibuni ijayo.

Katika uchambuzi wake huo mtaalamu huyo amebainisha sababu kadhaa zitakazopelekea hali hiyo.Alisema ni kweli nchi za mashariki ya kati ni wazalishaji wa zaidi ya nusu ya nishati itumikayo duniani ikiwemo gesi lakini kwa sasa nchi hazina uwezo wa kufidia pengo litakalotokana na kukatika kwa gesi ya Urusi katika nchi za Ulaya.

Sababu kubwa kati ya hizo aliitaja ni kukosekana kwa miundombinu ya kuzalisha na kusafirisha kiwango kitakachohitajika kwa mataifa hayo.Nchi hizo ili ziweze kufidia gesi ya kutoka Urusi kwa kipindi kifupi kijacho itabidi wakatishe mikataba ya kuyauzia mataifa ya Mashariki ya mbali ikiwemo China jambo alilosema litazigharimu nchi za mashariki ya kati kwa kukatisha mikataba na kuhatarisha biashara zao hapo baadae.

Ukiondoa Saudi Arabia ambayo imekataa tu lakini Zipo nchi 4 zingeweza kufidia gesi hiyo lakini tatu kati ya hizo kutokana na vikwazo vya muda mrefu walivyowekewa na nchi hizo za Ulaya kwa kushirikiana na Marekani hazina uwezo wa kuzalisha gesi hiyo.Nchi hizo tatu ni Venezuela,Iraq na Libya.Kwa upande wa Iran ina gesi nyingi iliyokwisha kujazwa kwenye meli zilizoelea baharini,lakini ni lazima mataifa hayo yaiondoshee vikwazo vya kiuchumi ili iweze kuwauzia.

Kikwazo kingine alichokitaja mtaalamu huyo ni kuwepo kwa makundi yanayopingana katika nchi hizo ambayo yamechipuka kutokana na mizozo iliyopandikizwa na mataifa hayo ya Ulaya na Marekani.Alitolea mfano wa nchi ya Libya kwamba visima vya mafuta na gesi havina usalama wa kutegemewa kuzalisha na kusafirisha chochote kutokana na kila eneo kudhibitiwa na makundi yanayopingana.


1652168602563.png
 
IMG_6883.jpg


Hao waarabu watulie wahindi washapiga bao huko India inanunua mafuta na makaa ya mawe kutoka Urusi na kuyauza tena Ulaya kwa bei ya juu. Ulaya siimegoma kununua kutoka Urusi so India anaenda kutumika tu hapo na ukute mwenye kampuni yakutoa mafuta India to Europe ni Mmarekani haha.
 
View attachment 2218852

Hao waarabu watulie wahindi washapiga bao huko India inanunua mafuta na makaa ya mawe kutoka Urusi na kuyauza tena Ulaya kwa bei ya juu. Ulaya siimegoma kununua kutoka Urusi so India anaenda kutumika tu hapo na ukute mwenye kampuni yakutoa mafuta India to Europe ni Mmarekani haha.
Daah, kufa kufaana, wahindi wameishaona fursa acha wapige hela

Nilisikia hata Ujerumani naye anafanya hivo kwa Poland
 
Mrusi hawezekani hata wafanyie vp huko Ulaya wao wenyewe wanapingana huko G7 pia hivyo hivyo amebaki kupiga kelele Muingereza tu sababu kala hasara na hukuna alicho kipata USA karibu atakwepa sababu silaha zake nyingi zimetekwa na kubomolewa na hakuna alicho kipata.

Mrusi anaendeleza moto wake kama kawaida pale Odessa
 
Kwa wanaoamini unabii wa Ufunuo wa Yohana wanaona kabisa unabii huo unatimia katika nyakati ngumu wanazopitia NATO ambao wamefananishwa na Babeli, mkuu wa makahaba mwenye maneno ya makufuru juu yake.

Ukisoma Ufunuo wa Yohana ile sura 18 nzima na kwa mfano mstari wa 19 wa sura hiyo unakutana na maneno haya 19"Wakatupa mavumbi juu ya vichwa vyao, wakalia, wakitokwa na machozi na kuomboleza, wakisema, Ole, ole, mji ule ulio mkuu! Ambao ndani yake wote wenye merikebu baharini walipata mali kwa utajiri wake; kwa kuwa katika saa moja umekuwa ukiwa"

Juzi tumemsikia Rais Urusi akisema ikitumika nuclear basi ndani ya nusu saa tu nchi zote za NATO zitakuwa zimeangamia na katika mstari huo wa 19 wa sura hiyo ya 18 unasema katika lisaa limoja BABELI itakuwa ukiwa na ukisoma kwa makini sura nzima ya 18 utaona BABELI itakuwa ukiwa kutokana na kuangamizwa.

NATO wakubali tu angamizo la BABELI lipo na atakayefanya hivyo ni taifa lenye nguvu kutoka kaskazini mwa dunia na Ramani ya dunia inaonesha ni Urusi pekee nchi iliyo kaskazini mwa dunia yenye uwezo wa kuiangamiza NATO.
 
View attachment 2218852

Hao waarabu watulie wahindi washapiga bao huko India inanunua mafuta na makaa ya mawe kutoka Urusi na kuyauza tena Ulaya kwa bei ya juu. Ulaya siimegoma kununua kutoka Urusi so India anaenda kutumika tu hapo na ukute mwenye kampuni yakutoa mafuta India to Europe ni Mmarekani haha.
Sasa uko si kuluka tope na kukanyaga Mavi
 
Kwa wanaoamini unabii wa Ufunuo wa Yohana wanaona kabisa unabii huo unatimia katika nyakati ngumu wanazopitia NATO ambao wamefananishwa na Babeli, mkuu wa makahaba mwenye maneno ya makufuru juu yake.

Ukisoma Ufunuo wa Yohana ile sura 18 nzima na kwa mfano mstari wa 19 wa sura hiyo unakutana na maneno haya 19"Wakatupa mavumbi juu ya vichwa vyao, wakalia, wakitokwa na machozi na kuomboleza, wakisema, Ole, ole, mji ule ulio mkuu! Ambao ndani yake wote wenye merikebu baharini walipata mali kwa utajiri wake; kwa kuwa katika saa moja umekuwa ukiwa"

Juzi tumemsikia Rais Urusi akisema ikitumika nuclear basi ndani ya nusu saa tu nchi zote za NATO zitakuwa zimeangamia na katika mstari huo wa 19 wa sura hiyo ya 18 unasema katika lisaa limoja BABELI itakuwa ukiwa na ukisoma kwa makini sura nzima ya 18 utaona BABELI itakuwa ukiwa kutokana na kuangamizwa.

NATO wakubali tu angamizo la BABELI lipo na atakayefanya hivyo ni taifa lenye nguvu kutoka kaskazini mwa dunia na Ramani ya dunia inaonesha ni Urusi pekee nchi iliyo kaskazini mwa dunia yenye uwezo wa kuiangamiza NATO.
Acha kupotosha maneno ya Mungu. Kama hujui unauliza. Hayo mambo hayatimi wakati huu na Wala Russia Hana uhusiano na hicho kilichoandikwa hapo. Hayo mambo yatatimia kipindi Cha dhiki kuu. Na biblia inaposema babeli mama wa makahaba inazungumzia taifa la Iraq. Kimsingi Iraq ndipo chanzo Cha dhambi zote ulimwenguni. Ukahaba unaozungumzwa hapo ni wanadamu kijichanganya na mambo ya shetani, yaani wamekuwa na miungu wengi.
 
Acha kupotosha maneno ya Mungu. Kama hujui unauliza. Hayo mambo hayatimi wakati huu na Wala Russia Hana uhusiano na hicho kilichoandikwa hapo. Hayo mambo yatatimia kipindi Cha dhiki kuu. Na biblia inaposema babeli mama wa makahaba inazungumzia taifa la Iraq. Kimsingi Iraq ndipo chanzo Cha dhambi zote ulimwenguni. Ukahaba unaozungumzwa hapo ni wanadamu kijichanganya na mambo ya shetani, yaani wamekuwa na miungu wengi.
Source please naomba ushahidi wa haya uyasemayo kuhusu Iraq
 
Acha kupotosha maneno ya Mungu. Kama hujui unauliza. Hayo mambo hayatimi wakati huu na Wala Russia Hana uhusiano na hicho kilichoandikwa hapo. Hayo mambo yatatimia kipindi Cha dhiki kuu. Na biblia inaposema babeli mama wa makahaba inazungumzia taifa la Iraq. Kimsingi Iraq ndipo chanzo Cha dhambi zote ulimwenguni. Ukahaba unaozungumzwa hapo ni wanadamu kijichanganya na mambo ya shetani, yaani wamekuwa na miungu wengi.
wacha wee! kwahiyo wewe ndio unasema ukweli
 
Soma hoja yangu Ina logic hata kama hujui mambo ya bible. Kinachoendelea sasahivi hakina uhusiano wowote na haya mambo ktk kitabu Cha ufunuo wa yohana.
hapo hakuna logic yoyote ilioiandika wewe mwenyewewe unaleta tafasiri kwa utashi wako kama uyo jamaa uliokua unampinga
 
Back
Top Bottom