Masharti nafuu tunayopewa na China

Masharti nafuu tunayopewa na China

Masharti yake ni kama vile Wachina wanavyodaiwa kuchukua Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kenneth Kaunda jijini Lusaka kutokana na nchi hiyo kushindwa kulipa madeni. Pia China imechukua Shirika la Umeme Zambia (ZESCO) na Shirika la Habari Zambia (ZNBC).
 
Mkuu

Hakuna nafuu yeyote...lazima waje kubakwa on the day light

Waulize Kenya na Sri Lanka,wananyang'anywa bandari zao na tako wanatoa

Hua nawashangaa sana CCM kushangilia oppressors,wote ni oppressors tu,eti CHina this,China that..etc
Kenya ameingia mkenge, hakujua janja ya China. Hata mradi wa kujenga Bagamoyo port kama tungeukubali bila marekebisho ndio ungekuwa mbaya sana kama utumwa mamboleo. Na sisi tukiendekeza misifa ya kujenga miradi mikubwa bila uchambuzi yakinifu na baadae kukwama kifedha na kuja kutegemea China, kuna uwezekano wa kushindwa kulipa.

China ya sasa siyo China ya Mao na rafiki yake Nyerere. Kumbuka siku hizo China ilikuwa imetengwa na dunia, ikatumia urafiki wake na Tanzania ya Nyerere kujitangaza kwa kutupa misaada mikubwa ya Mawasiliano, Uchukuzi, Kijeshi, viwanda, Afya, Utamaduni, Elimu, Kilimo n.k

China ya sasa ipo kileleni kiuchumi kwa kutumia njia hizo hizo za mabeberu tena kwa ujanja zaidi. Labda Raisi Magufuli ana jibu kama alivyogundua udhahifu kwenye mradi wa Ujenzi wa bandari ya Bagamoyo uliokuwa ukisifiwa na kupigiwa upatu na Spika Ndugai.
 
Mfumo wa BOOT unatumika sehemu nyingi duniani ambapo mwekezaji anajenga na kumiliki kwa muda mpaka atakaporudisha gharama zake. Cha msingi ni kuangalia Maslahi ya kila upande yaani kila mmoja ashinde.

Kwa upande wetu ni kuwa labda hatuna watu mahiri wa kufanya majadiliano na mikataba. Wawekezaji mara nyingi wanataka kupata faida kubwa.
Kenya ameingia mkenge,hakujua janja ya China.
Hata mradi wa kujenga Bagamoyo port kama tungeukubali bila marekebisho ndio ungekuwa mbaya sana kama utumwa mamboleo.
Nasisi tukiendekeza misifa ya kujenga miradi mikubwa bila uchambuzi yakinifu na baadae kukwama kifedha na kuja kutegemea China ,kuna uwezekano wa kushindwa kulipa.
China ya sasa siyo China ya Mao na rafiki yake Nyerere.
Kumbuka siku hizo China ilikuwa imetengwa na dunia,ikatumia urafiki wake na Tanzania ya Nyerere kujitangaza kwa kutupa misaada mikubwa ya Mawasiliano,Uchukuzi, Kijeshi,viwanda,Afya,Utamaduni,Elimu,Kilimo n.k
China ya sasa ipo kileleni kiuchumi kwa kutumia njia hizo hizo za mabeberu tena kwa ujanja zaidi.
Labda Raisi Magufuli ana jibu kama alivyogunduwa udhahifu kwenye mradi wa Ujenzi wa bandari ya Bagamoyo, uliokuwa ukisifiwa na kupigiwa upatu na Spika Ndugai.
 
Tumeambiwa ana masharti nafuu kuliko marekani je unayajua masharti nafuu ya china
Masharti nafuu ni kutokuhoji demokrasia na Utawala bora. Masharti magumu ni kuhoji mambo ya demokrasia na Utawala bora.
 
Bado wanasisitiza nchi hii ni tajiri, inawezekana mikopo ya wachina ikalipwa bila shida yoyote.
 
Wakuu habari:

Mara kwa Mara viongozi wetu wamekuwa wakituambia tumepata mkopo kutoka China wenye masharti nafuu.

Swali langu ambalo natamani kila mtanzania ajiongeze na aweze kufikiria nje ya box je mkopo wa masharti nafuu ukoje je masharti nafuu ni yapi?

Mara nyingi tumesikia kauli kuwa hatutaki mikopo ya mataifa ya kibepari yenye masharti magumu je ugumu wa masharti yao unakuja vp?

Je urahis upi huo tunaoupata kutoka China?

Je marekani ikitaka kukupa mkopo huwa inazingatia vigezo gani kukupa mkopo?


Nawasilisha

falcon mombasa
Usharti nafuu wa Kichina ninaoujua na ambao nimejaribu Kuufuatilia ni Kukujengea haraka nchi yako, ila Wao Kuchukua Rasilimali zako Miaka 100.
 
Some how..... Bandari ya bagamoyo ingekamilika ingepunguza mizigo kurasini.... hasa inayorejeshwa Ulaya... shida ni vipengele vya mikataba... Chinese ain't good people. Niliwahi danganywa na kampuni moja ya kuvuna resins kweny mipaina,, we kufika camp balaa aisee sio watu Hawa...
 
Mfumo wa BOOT unatumika sehemu nyingi duniani ambapo mwekezaji anajenga na kumiliki kwa muda mpaka atakaporudisha gharama zake. Cha msingi ni kuangalia Maslahi ya kila upande yaani kila mmoja ashinde.

Kwa upande wetu ni kuwa labda hatuna watu mahiri wa kufanya majadiliano na mikataba. Wawekezaji mara nyingi wanataka kupata faida kubwa.
Nasikia Wachina wanamazingaombwe unashtukia unaweka signature bila kutaka,baadae unagundua wametutapeli,ndio malimwengu.
 
Kutamka kwamba hatutaki pesa za mabeberu zile ni siasa tu, huu ndiyo ukweli sasa kwamba tunashida na tunapokea...





Cc: mahondaw
 
Mkuu 'Falcon'

Baadhi ya masharti nafuu wanayoyapenda watawala wetu ni baadhi ya haya:

1. Wasiambiwe kwamba wanawanyima haki watu wao.

2. Wakiua kiasi kadhaa ya watu wao, wasihojiwe na yeyote kwa kisingizio cha kuingiliwa mambo yao ya ndani

3. Mkubwa akiamua kuharibu mazingira kwa kuweka mradi wake anaoupenda, asibughudhiwe na mtu, kwa vile uamzi wake ndio wa mwisho

4. Mambo ya riba na masharti mengine ya muda wa kulipa, wao hayo huwa sio masharti wanayoona kuwa na ugumu kama hayo matatu ya mwanzo

Lakini, ili nisionekane kuwa nina upendeleo wa upande mmoja:
Hata hao watoa mikopo nao kweli huwa wanayo matatizo yao. IMF au WB wanakupa mkopo wenye riba ya 0.5%, kwa muda wa miaka 30 kurudisha mkopo, lakini wanakurundikia masharti ambayo wakati mwingine huwa magumu kuyakubali, kama alivyoshindwa kuyakubali Mwalimu Nyerere wakati wake.

China wao wanakwambia hawataingilia mambo yako; kama unataka kuwachinja watu wako kwa kitoweo, hilo ni shauri lako, mradi pesa yao na faida irudi.
 
China ni bure kabisa, mbona wameshindwa kuwasadia marafiki zao kama Zimbabwe au Venezuela? Wao wanaangalia faida tu mambo ya urafiki ni kwenye majukwaa tu ya kisiasa.
 
IPO siku bandari PM hataweza kuitembelea kwa kuzuka.....itakuwa chini machina china
 
China ni marafiki zetu wa enzi na enzi na kwa sasa wanajitanua zaidi duniani na wanaoushawishi mkubwa kuliko USA. Hawanaga kazi mbovu
Hakuna mtu mbaya kama mchina linapokuja suala la mahusiano ya kiuchumi.

Wazungu waneikopesha Afrika miaka na miaka. Nchi nyingi za Afrika (Tanzania mojawapo) zikashindwa kulipa. Lakini haijawahi kutokea mataifa hayo ya wazungu kuchukua bandari au viwanja vya ndege kama wanavyofanya Wachina ukichelewa/kushindwa kulipa deni.

Mataifa ya wazungu yamekwishazifutia nchi nyingi za Afrika madeni lakini China haijawahi kuisamehe deni nchi yoyote Duniani.

Watawala wa Afrika wanawachukia wazungu kwa sababu sharti kubwa la kupata mkopo au msaada ni kuheshimu haki za binadamu na misingi ya demokrasia. Watawala wa Afrika, wengi wao ni madikteta wanaotaka kuwagandamiza raia wao, na wanaotaka kuendelea kutawala hata bila ya kuchaguliwa. Wanampenda mchina kwa sababu na yeye utawala wake ni wa kidikteta, na jamii ya Wachina kwa kiasi kikubwa ni primitive na inayokumbatia utawala primitive sawa na tawala nyingi za Afrika.

Wachina wamejaa Zimbabwe, kwa sababu dikteta Mugabe baada ya kupewa kisogo na mataifa ya Ulaya, aliona aheri amkumbatie dikteta mwenzake, mchina, akitarajia atamsaidia, lakini akaishia kwenye aibu kubwa ya kiuchumi. Hakuna nchi duniani iliyoachana na Dunia, ikamkumbatia mchina, halafu ikapata maendeleo.

Wachina walimdanganya Magufuli kuwa wataigeuza Tanzania kuwa nchi ya viwanda, wakawa wanajenga tu uwigo wa mabati, halafu wanamwita Magufuli akaweje jiwe la msingi. Maeneo mengi mbao zilizoshikilia hayo mabati zinazidi kuoza na mabatai kulala chini. Ikamlazimu Magufuli aache kabisa kuongelea tena Tanzania ya viwanda. Hana hamu nao.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa ufupi hakuna masharti nafuu ktk mikopo usidanganywe ndugu! Vijana wa lumumba watasema ipo lkn wakiambiwa wafafanue wanakimbia kwani hawajui lolote!
 
China ni marafiki zetu wa enzi na enzi na kwa sasa wanajitanua zaidi duniani na wanaoushawishi mkubwa kuliko USA. Hawanaga kazi mbovu
Mkuu usijitutumue Sana kwa mambo yaliyokuzidi uwezo kufikiri.siyo kila jambo unaweka ushabiki wa kijinga.China ya leo haina urafiki na yeyote zaidi ya kujitanua kiuchumi.
 
Issue ni simple Mzungu akikupa msaada au mkopo anataka aingilie mambo yako ya kisiasa na utawala wakati mchina hana muda wa kujua mambo ya siasa zako za ndani na utawala
 
Nina uhakika hata ukiwahoji hao Viongozi hawana jibu lolote kusema ni China ina unafuu gani.
 
Back
Top Bottom