Tetesi: Masharti ya mikopo yameikumba Tanzania, kupata mkopo sharti Makamu wa Rais atokee upinzani

Trable

JF-Expert Member
Joined
Jan 3, 2023
Posts
1,781
Reaction score
3,288
Asanteni wazungu juu yahili, naombea liwe ni kweli.

Tulikuwa watoto mpaka tunataka kuzeeka, hatujawahi kuona nafuu ya maisha chini ya serikali inayoongozwa na ccm miaka zaidi ya 60.

Maji tu yamewashinda, umeme ndio usiseme, suala la afya ni jambo la anasa kwetu, ukiuumwa na huna pesa, hata kama ulikuwa ni wa kupona, ndio basi tena, hata ukipona, bili yake mtaichanga ukoo mzima na mtadaiwa bado".

Shule zetu sasa, mtoto anaingia shule hajui kusoma na kuandika, anasoma miaka saba anarudi hajui kusoma na kuandika, hii ndio CCM.

Kwa aina ya mkopo huu; walau watanzania twaweza anza kuuona mwezi na mambo yakaenda sawa!
 
Ha

Hamna awezaye kuuzuia wakati wa Mungu. Wakati wa Mungu ndio wakati sahihi
 
Hii ni mpya isiyowezekana
 
Ngumu kumeza.
Kwa deni la taifa lilipofikia, serikali ijiandae kuchezeshwa kwata na mabeberu. Sasa hivi tunafurahia mikopo ila itafika wakati serikali itachezeshwa kwata hadi tuwachukie mabeberu.
 
Trust me hakuna kitakachobadilika.
Huyo makamu raisi ataungana na mwenzake waelewane wale mema ya nchi.
Watz wakifika kwenye kula hawapigi kelele kabisa.
 
Inamaana hayo masharti yanataka tuvunje katiba
 
Trust me hakuna kitakachobadilika.
Huyo makamu raisi ataungana na mwenzake waelewane wale mema ya nchi.
Watz wakifika kwenye kula hawapigi kelele kabisa.
Umeona mbali mkuu! Ikitokea ikawa hivyo,makamu wa Rais atakuwa kapewa ulaji wa waziwazi.
 
Hiyo SUK haikubaliki bara,

Tunataka KATIBA mpya itokanayo na Rasimu alosimamia Judge WARIOBA.

Aamen
 
Makamo akitoka upinzani chapu beberu anaua raisi ili makamu awe raisi na kuvuruga mifumo ya nchi.
 
CCM msianze leta janja janja kutafuta pakutokea.... 2025 Samia anarudi Oman.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…