Mashine ya kunyanyua vitu vizito (crane) bandarini Dar Es Salaam yatumbukia baharini

Mashine ya kunyanyua vitu vizito (crane) bandarini Dar Es Salaam yatumbukia baharini

Acha majungu kwa Rais,
Mtake msitake Samia ndio Rais kwasasa!, Mumpende au musimpende,yeye ndio amir jeshi mkuu kwasasa, Mwendazake kashajiua hatorudi Tena,,
Maana kutokuchukua tahadhali kwa jambo la hatari hadi likachukua uhai wako,, Ni sawa tu na umejiua mwenyewe"
Mbona sasa umeweza kuandika sentensi kadhaa za mawazo yako bila ya kutukana?

Achana na tabia ya kutukana maana haithibitishi ujanja ulionao wala msimamo thabiti kwa Rais,

Rais mwenyewe ana incourage mawazo huru sasa Wewe unakuaje Mfuasi wake halafu hukubali msimamo wake?

Waachie hiyo tabia watu wa Instagram na Facebook

Humu tunapingana kwa lugha ya kistaarabu na tukishindwana tunabaki na msinamo wake kila mtu
 
hujuma tena. naona mambo yameanza kufanyika kiholela holela au ni kwamba taarifa za mambo kama haya zilikuwa zinafichwa?
 
Kuna kilaza alisahau madesa ya equilibrium ya form one.
 
Hawa wamechoka na kazi wanalipwa mishahara ya bure wapishe watu wenye uwezo
 
View attachment 1797848
Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) inaujulisha Umma kuwa, Jumapili tarehe 23 Mei 2021, Majira ya saa 8 Mchana katika Bandari ya Dar es Salaam, mashine ya kunyanyua vitu vizito (crane) iliyokuwa ikishushwa kutoka kwenye meli ya LCT AJE 1 ilipata ajali ya kutumbukia baharini.

Mashine hiyo yenye uzito wa takribani tani 70 iliwasili kwa meli katika Bandari ya Dar es Salaam ikitokea visiwa vya Songosongo na ilikuwa ikishushwa katika eneo la Gati la Malindi. Zoezi la kuiopoa mashine hiyo linaendelea.
View attachment 1797847
Credit: Le Mutuz TV
Tunataka mhusik mkuu ajiuzulu, asisubiri kuondolewa.
 
Hiyo kazi angepewa white isingetumbukia, mswahili anakufanyia kazi shingo upande na dharau juu.. ..in short hana uchungu na mali ya mtu, isipokua wachache wanaojitambua. Nimefanya kazi na waswahili, anakuharibia gari yako, wewe tajiri unahangaika kutafuta spea yeye hana time na wewe, n still anakuteta pembeni. Nyambafu kabisa.. ..


🇦🇷🇦🇷🇦🇷🔥🔥
Ngozi nyeusi tuna matatizo sana chief
 
Mama anazidi 'kukaribishwa' mjini

Tumetoka kwny Luku, tukapitie kwny mfumo wa malipo siku mbili tatu, tukapumzika kwny uvamizi na Ujambazi sasa hivi tupo bandarini 'tunalowanisha' vitendea kazi!

Karibu Nyumbani kumenoga!
Na kumenoga haswaaah lol

Sent from my Infinix X652C using JamiiForums mobile app
 
Tumbukizeni zote Dili tuwape tenda kampuni binafsi
 
Hujuma ya wazi kabisa. Mama Samia ana kazi sana bila kupangusa kabisa wale wa Mwendazake ataonekana hatoshi kwenye hicho cheo
vitu vingine ni ajali tu za kawaida nadhani, Wala Haina haja kutimua watu kazi mkuu
 
Back
Top Bottom