Mashirika na Taasisi za Umma zinazostahili kufutwa na zile zinazostahili kuunganishwa

Mashirika na Taasisi za Umma zinazostahili kufutwa na zile zinazostahili kuunganishwa

Hili geshi kama halitakuwa- restructured basi lihamishiwe ccm makao makuu.
Hata hivyo inasemekana kwamba Jeshi ni Moja tuu nalo ni JWTZ, hao wengine ni taasisi tuu! Sema Tunasafari ndefu bado...
 
NUKUU.
iv: Mageuzi katika utendaji na uendeshaji wa mashirika ya Umma ni zoezi endelevu. Serikali itaendelea kuimarisha mifumo ya kupima na kutathmini utendaji wa Mamlaka na Taasisi za Umma kwa lengo la kuongeza tija katika Maendeleo ya nchi...

Kwa muktadha huo hapo juu, nawiwa na shauku ya kushauri yafuatayo;

# EWURA iunganishwe TPDC.

# Tanzania Fertilizer Co. Iunganishwe na Tanzania Seed Agency.

# Bodi za Mazao zote zingekuwa kwenye wakala/ bodi moja.

# VETA unga na SIDO.

# Mzinga Cooperation iwe Suma Jkt Construction co.

# Futa RUWASA imarisha Mamlaka za Maji za Maeneo husika.

# TEMESA na TBA zirudi kama zilivyokuwa mwanzo au Masuala ya umeme kwenye majumba ikarudishwa TBA, Masuala ya mategenezo ya magari ya serikali yakapelekwa Government Transport Agency na majukumu ya vivuko na uwekaji wa taa za barabarani yakahamishiwa TANROADS hivyo kuifuta kabisa TEMESA.

# Mamlaka za Mabonde ya Maji/ Mito ziwe chini ya RUWASA kama itaendelea kuwepo.

# NHC iungwe na TBA.

# COASCO ivunjwe na kazi zake pamoja na watumishi wake waende kwa CAG...Vyama vya Ushirika vikaguliwe kama zilivyo taasisi zingine.

# Mamlaka ya Usimamizi wa Nafaka na Mazao Mengine iunganishwe na Wakala wa Taifa wa Uhifadhi wa Chakula.

# Tanzania Airport Authority unga na Tanzania Civil Aviation Authority.
[emoji122][emoji122][emoji122]
 
Kuivunja TAKUKURU au kuiunganjsha kazi zake either na TISS au Polisi ni ngumu na haiwezekani kabisa never na kuwa chombo hiki kikivunjwa jua misaada toka abroad itasitishwa chombo hiki hata kama kina madhaifu yake lakini mama hawezi kukivunja anajua nini kilimfanya akiwa ktk mashirika ya kimataifa ana kiporo chake PCCB even late Magu they are not so integrity
 
Bodi zote zaMazao zinapaswa kuwa bodi moja, na kila zao kuwa kitengo au idara ndani ya mwamvuli unaoitwa bodi ya mazao, hii itapunguza gharama ya kila zao kuwa na bodi.
 
Mashirika ambayo kwangu naona bora yaunganishwe..
  • TARURA Na TANROADS
  • LATRA na TASAC (bora zote zirudi kuwa SUMATRA)
  • REA na TANESCO
  • TCU na NACTE
  • Tungekuwa Na wizara moja yenye Jina la Wizara ya Usalama Wa Raia,Ulinzi wa mali,Rasilimali,Utu na Haki ya Raia.. (JESHI LIKABAKI MOJA TU)
    • Halafu tukawa na idara kama zamani au kama wenzetu nchi za nje.. Kwenye hii wizara kama POLISI,UHAMIAJI,TAKUKURU,ASKARI WA TANAPA,MGAMBO,Na kukaanzishwa Idara ya uchunguzi ambayo ingekuwa tofauti na POLISI,USALAMA WA TAIFA TISS,MAGEREZA,FIELD FORCE,USALAMA BARABARANI , MAPAMBANO MADAWA YA KULEVYA etc zikawa ni idara zinazojitegemea
  • COASCO na CAG (Hawa naona waunge nguvu liwe shirika moja hatuwezi kuwa na Mamlaka mbili za ukaguzi katika nchi moja)
  • Shirika la POSTA , TCRA na TTCL hizi zilipaswa kuwa kitu kimoja huku vikiongoza sector binafsi
  • SIONI KAMA KUNA HAJA YA WIZARA YA TAMISEMI wakati kazi zake nyingi zipo kwenye Wizara nyingine..kwa mfano kusimamia Afya kazi ya Wizara ya afya, Kusimamia Elimu kazi ya wizara ya Elimu, Kusimamia utumishi wa Sekretarieti za mikoa na mitaa Lipo Chini ya Wizara ya Utumishi na Utawala Bora
  • TMDA ingepelekwa ikawa kitengo Ndani ya MSD cha ukaguzi
  • Sioni sababu kuwepo na Mkuu wa wilaya kma kuna Mkurugenzi wa wilaya hii ndo hupelekea migongano ya kimajukumu Aidha ifutwe Mkuu wa wilaya au iondolewe post moja kati ya hizo
[emoji122][emoji122][emoji122]
 
SUMATRA iligawanywa na kuwa LATRA na nyingine ile ya usafiri wa majini (sikumbuki jina). Mimi ninaona imependeza ikiwa hivyo.

Ila TANESCO ilitakiwa igawanywe ziwe tatu: kazalisha umeme, ugavi wa umeme na kukusanya madeni na malipo ingependeza sana kuliko sasa ambapo TANESCO ni kama imezidiwa
[emoji848][emoji19]
 
Mnyumbuliko WA mashirika unatokana hasa na dira na dhima zao katika nchi na katika kuleta mgawanyo WA majukumu ie specialization. Hii unasaidia nchi kufocus kwenye maeneo inayotaka kwa kuhakikisha rasilimali zinafika huko.

Kuunganisha taasisi kuzimgatie ;
1.ikiwa kweli taasis zinaovelap kwa kiwango kubwa yaan dhima zao zinafanana
2.mahitaji ya nyakati ikiwa shirika halihitajiki tena.ie mission fullfilled.
3.Ikiwa shirika halina tija kabisa
[emoji122][emoji122]
 
Bodi zote zaMazao zinapaswa kuwa bodi moja, na kila zao kuwa kitengo au idara ndani ya mwamvuli unaoitwa bodi ya mazao, hii itapunguza gharama ya kila zao kuwa na bodi.
[emoji122][emoji122]
 
Hapana mkuu Mi naona NIMR ndo ingeunganishwa na TPRI siku hizi Imeunganishwa na Maswala ya kilimo Inaitwa TPHPA..
Ila combination ya NIMR na TPRI ingekuwa moto sana
Aaah, kweli TPHPA! Yeah, hata NIMR huku panawafaa maana wote wanashughulika na vimelea vya magonjwa!
 
Huku Shinyanga kuna dude linaitwa KASHUWASA linapaswa kuunganishwa na SHUWASA maana linatuongezea gharama bure tu!
 
Back
Top Bottom