Masikitiko - Timu ya Taifa yawa timu ya Mkoa wa Dar es salaam

Masikitiko - Timu ya Taifa yawa timu ya Mkoa wa Dar es salaam

Beki mbovu sijapata kuona...Kapombe toka augue hayuko vizuri..combination ya Nyoni na Banda mbovu ....mechi ijayo wacheze Mbonde na Dante walicheza wote Mtibwa..wachezaji waongeze juhudi kama hawataki watoke kwenye timu
 
Kwahiyo hadi timu ya taifa mnataka ijae wa call me J na chattle si ndiyo??haya tutawapisha msijali
 
Mbona kuna waliotoka ulaya Spain na Belgium, morogoro pia wametoa na mtibwa yao.
 
Sitaki kuamini kwamba wachezaji wazuri nchi hii wamo kwenye timu zile 3 tu za mkoa wa DSM , hii itakuwa ni kashfa kubwa sana na ni kutowatendea haki wachezaji wengine waliojazana kila pembe ya nchi .

Sijaridhishwa na uteuzi wa timu yetu ya Taifa , ni wa kibaguzi na umejaa ubabaishaji mtupu.

Nakulilia Maximo .
Dah.... Siyo vizuri mwanaume kulalamikalalamika bana [emoji12]
 
Ilichukua ubingwa
Hukumbuki mwaka fulani iliundwa timu ya taifa B nadhani ilikuwa inaitwa KAKAKUONA ikafika nusu fainali kama sio fainali challenge.....mwenye kumbukumbu anirekebishe tafadhali
 
Tumia akili basi kidogo, wachezaji wazuri wote Tanzania wanachukuliwa na timu hizi tatu, yaani ukiwika tu kidogo kwenye team ya kolomije fc unajikuta upo yanga, simba na Azam. Pili hizi timu zina wachezaji ambao wanauzoefu angalau na international matches, ningeliona bandiko lako la maana kama ungesema badala ya kumweka hajibu wa simba angemweka Alberto baskite wa Call me J fc, ila kama na wewe haujawajua wachezaji wazuri nje ya simba, yanga na azam. Basi hawajafikiu uzuri unaouongelea
Mmmh huu mwaka, hadi kuna stadium inaitwa Bashite stadium!!
 
Watanzania ni watu wa kulalama tu na ndo maana wanaonekana ni watu wasio na furaha kila pahala. Ulalamishi ndo kuferi kwao na ni sehemu ya maisha yao, liwe jema watalalama, liwe baya watalalama
Tena wanalalamika hata kama hawana utaalam na jambo husika
 
IMG_3196.JPG
H
Mmmh huu mwaka, hadi kuna stadium inaitwa Bashite stadium!!
 
Sitaki kuamini kwamba wachezaji wazuri nchi hii wamo kwenye timu zile 3 tu za mkoa wa DSM , hii itakuwa ni kashfa kubwa sana na ni kutowatendea haki wachezaji wengine waliojazana kila pembe ya nchi .

Sijaridhishwa na uteuzi wa timu yetu ya Taifa , ni wa kibaguzi na umejaa ubabaishaji mtupu.

Nakulilia Maximo .
Inawezekana hawana nauli kuwatumia wale wa mikoani,,,#@si bure beki zipi !!!!? Prison beki zake zipo njema sana
 
Ahh ht england ipo kuna mwaka ilkuw liverpool, chelsea na man u..!! Me nadhn co mby maana ht asipokuja samata inamaana foward aje wa mbeya cty? Hahahaaa
 
Ishu ni timu ishinde hata wakitoka timu moja kwani sio watanzania ?kila kitu ni siasa za kipuuzi puuzi tuu...
 
Ndio maana hili timu silipendi.Jana wamewafunga wale makirikiri wanajiona wanajua
 
Hukumbuki mwaka fulani iliundwa timu ya taifa B nadhani ilikuwa inaitwa KAKAKUONA ikafika nusu fainali kama sio fainali challenge.....mwenye kumbukumbu anirekebishe tafadhali
Mkuu ilifika fainali ya chalenge na ilifungwa na uganda goli moja kwa bila...ilikua timu nzuri sana haijawahi kutokea..ilichaguliwa kila mkoa walitoka wachezaji
 
Tumia akili basi kidogo, wachezaji wazuri wote Tanzania wanachukuliwa na timu hizi tatu, yaani ukiwika tu kidogo kwenye team ya kolomije fc unajikuta upo yanga, simba na Azam. Pili hizi timu zina wachezaji ambao wanauzoefu angalau na international matches, ningeliona bandiko lako la maana kama ungesema badala ya kumweka hajibu wa simba angemweka Alberto baskite wa Call me J fc, ila kama na wewe haujawajua wachezaji wazuri nje ya simba, yanga na azam. Basi hawajafikiu uzuri unaouongelea
Mbona msimu ukiiasha hao simba na yanga wanaenda mikoani kuchukua wachezaji? Kama mikoani hakuna wachezaji wazuri.angalia hata uingereza wachezaji aliwika tu zile big four team wanawachukua .mbona kocha wa england achukui tu timu za big four? yeye huchukua mpaka timu ndogo ndogo
 
Back
Top Bottom