Masimango na kejeli kwa wanaoonekana wamechelewa kuoa/ kuolewa na kupata watoto uzeeni au umri ukiwa umekwenda

Masimango na kejeli kwa wanaoonekana wamechelewa kuoa/ kuolewa na kupata watoto uzeeni au umri ukiwa umekwenda

Habari za muda huu marafiki,

Siku za hivi karibuni kumekuwa na hali ya kushangaza kustaajabisha kwenye jamii yetu na hasa huku mitandaoni.

Kumekuwa na wimbi la watu kuwasimanga, kuwakejeli na hata kuwacheka ndugu zetu, jamaa zetu na marafiki zetu wanaoonekana kwa vigezo, mitazamo na viwango vilivyowekwa kwenye jamii kuwa wamechelewa kuoa au kuolewa hivyo kuonekana wamepata watoto wa uzeeni.

Ni jambo linaloonekana kama la kawaida lakini kwa upande mwingine linasononesha na kuvunja mioyo ya watu walioamua kujenga familia.

Ni kauli za kitoto zinazoonyesha kuwa bado hawajakomaa kiakili kwenye ulimwengu huu uliojaa harakati na purukushani za kila aina.

Ningependa kuchukua nafasi hii kuwakumbusha hao wenye kuwakejeli wengine kwenye hili ya kuwa.

1) Maisha ni fumbo zito Sana ambalo mara nyingi ni wachache Sana wenye kufumbua. Mara nyingi mipango yako inaweza ikapishana na mipango ya Mungu.

2) Uhai na kifo ni vyake Mungu mwenyewe kwani hakuna ajuaye kuwa amebakisha muda gani wa kuishi hapa duniani. Wapo vijana wengi wametangulia mbele za haki wakiacha watoto wao na familia zao zikiteseka na kuwaacha wazee wakiendelea kulea watoto wao wa uzeeni mpaka wakijitegemea na kufurahia matunda yao. Hivyo kusema kuwa mwanaao akifika miaka kadhaa wewe utakuwa umeshachoka au umeshakufa ni maneno ya kufuru au ya mtu asiye na Imani kwa mola wake mlezi.

3) Kwenye maisha kila mtu Mungu amemuwekea wakati wake wa kufanya jambo lake kwa rehema zake. Wapo watu waliowahi kuoa lakini Mungu akawanyima watoto mpaka wanazeeka na wengine wanawapata uzeeni kabisa. Wapo watu wamejikuta wapo jela wakitumikia vifungo virefu na mpaka wanatoka umri umekwenda na wanaamua kujenga familia. Wapo watu walikuwa wanaugua kwa muda mrefu na hatimaye wakapona na kuanzisha familia. Hivyo basi kama wewe umewahi ni sahihi kwako lakini haiwezi kuwa makosa kwa anayeonekana amechelewa.

4) Changamoto za kifamilia na vifo.
Kuna mwingine anawahi kuoa lakini Kati Kati ya safari anawapoteza mke na watoto wote kwa pamoja Kwa ajali au maladhi ya kawaida na anaamua kuoa na kuanzisha familia upyaaa.

Kwa kifupi mambo na changamoto za kidunia ni nyingi zinazopelekea watu kuonekana wamechelewa kupata watoto au kuoa na kuolewa. Tujifunze kuwa wastaarabu kwenye maisha ya watu kwani hatujui matamshi yetu yanawaathiri vipi wenzetu.

Niko tayari kusahihishwa.

Nawasilisha.
kila Jambo na wakati wake, tena ulopangwa na kuthibitishwa na Mungu .

Mungu hakawii kuitimiza ahadi yake kwa waja wake. Ikiwa amekupangia kupata mtoto ukiwa u18 utapata tu, na vilevile ikiwa amekupangia upate mtoto ukiwa above 60 uta pata tu...

Yote haya ni kwa Neema na Baraka za Mungu tu.
 
Achana nao kenge hao....yaan inashangaza sana “wewe umepata tuliza komwe bas,ya nini kuangaika na sauté nacho” Hizi mambo za kushupalia maisha za watu mtakuja kukutana na mnachokitaka
Kuna watu ni makatili Sana....sio makatili kwa kutumia upanga bali kwa kutumia ndimi zao......wanaongea maneno yanayoishi kwenye vifua vya wenzao kwa uchungu mkubwa Sana.....
 
kila Jambo na wakati wake, tena ulopangwa na kuthibitishwa na Mungu .

Mungu hakawii kuitimiza ahadi yake kwa waja wake. Ikiwa amekupangia kupata mtoto ukiwa u18 utapata tu, na vilevile ikiwa amekupangia upate mtoto ukiwa above 60 uta pata tu...

Yote haya ni kwa Neema na Baraka za Mungu tu.
Hakika ndugu yangu.......

Watu tunajisahau sana......maisha na uzima vinatupa viburi vya ajabu Sana.....mpaka kuwanenea wengine mabaya.......

Mungu atufanyie wepesi na awajaze mioyo ya subira wote ambao hawakujaaliwa kupata neema hiyo.....
 
Unawazungumziaje wanaokosa familia kutokana na sababu hizi
1. Uzembe, dating for fun
2. Peer pressure, kufata mkumbo wa wasiooa bila kujiuliza kesho itakuwaje
3. Tamaa, kutaka mwenza asie wa levo yako na kuangalia vigezo feki kama shepu au maokoto
4. Kujiona mtoto kumbe umri umeenda
5. Kutokujitambua na kutowajibika
6. Utapeli wa mapenzi
7. Kununua ngono
Kwani Lazima kuoa...
 
Kwani Lazima kuoa...
Ulazima au sio lazima inategemea na utashi wa mtu mwenyewe......na ndio maana ni vizuri kuheshimu maamuzi ya watu kwani hatujui kuna msukumo gani nyuma ya maamuzi hayo.......aliyeamua kuoa au kuolewa inapaswa ayaheshimu maamuzi ya aliyeamua kutokuoa au kuolewa....na sio kusimangana.....
 
Unawazungumziaje wanaokosa familia kutokana na sababu hizi
1. Uzembe, dating for fun
2. Peer pressure, kufata mkumbo wa wasiooa bila kujiuliza kesho itakuwaje
3. Tamaa, kutaka mwenza asie wa levo yako na kuangalia vigezo feki kama shepu au maokoto
4. Kujiona mtoto kumbe umri umeenda
5. Kutokujitambua na kutowajibika
6. Utapeli wa mapenzi
7. Kununua ngono
Hiyo haiusu mtu ni maisha yake na garama ya anacho atalipia mwenyewe kwann umseme au umkejel
 
Sema sisi Waafrika tuna mambo ya kifala sana.
Mtu ukichelewa kuoa utashangaa watu wanaanza kukushupalia ooh kwanini huoi, unasubiri nini, uzee unakuja nk

Haya, unaamua kuoa.

Mwaka mmoja bila mtoto watu wanaanza ooh mbona hamzai, mna matatizo gani, sijui nini...

Haya, mnapata mtoto

Mwaka mmoja wanaanza ooh, mbona katoto kamoja, ongezeni bana, mnasubiri nini...

Haya, mnapata wapili

Bado tu hawawaachi utasikia ooh mbona watoto wote wa kike, pambaneni mpate na wakiume..!!
 
Sema sisi Waafrika tuna mambo ya kifala sana.
Mtu ukichelewa kuoa utashangaa watu wanaanza kukushupalia ooh kwanini huoi, unasubiri nini, uzee unakuja nk

Haya, unaamua kuoa.

Mwaka mmoja bila mtoto watu wanaanza ooh mbona hamzai, mna matatizo gani, sijui nini...

Haya, mnapata mtoto

Mwaka mmoja wanaanza ooh, mbona katoto kamoja, ongezeni bana, mnasubiri nini...

Haya, mnapata wapili

Bado tu hawawaachi utasikia ooh mbona watoto wote wa kike, pambaneni mpate na wakiume..!!
Yaani ni balaa......
 
kila Jambo na wakati wake, tena ulopangwa na kuthibitishwa na Mungu .

Mungu hakawii kuitimiza ahadi yake kwa waja wake. Ikiwa amekupangia kupata mtoto ukiwa u18 utapata tu, na vilevile ikiwa amekupangia upate mtoto ukiwa above 60 uta pata tu...

Yote haya ni kwa Neema na Baraka za Mungu tu.
Kwa hiyo Mungu ndio hupanga watu kutopata watoto, Na watu wengine kupata watoto?

Huyo Mungu ana upendeleo sana.



Sent from my Infinix X657B using JamiiForums mobile app
 
Habari za muda huu marafiki,

Siku za hivi karibuni kumekuwa na hali ya kushangaza kustaajabisha kwenye jamii yetu na hasa huku mitandaoni.

Kumekuwa na wimbi la watu kuwasimanga, kuwakejeli na hata kuwacheka ndugu zetu, jamaa zetu na marafiki zetu wanaoonekana kwa vigezo, mitazamo na viwango vilivyowekwa kwenye jamii kuwa wamechelewa kuoa au kuolewa hivyo kuonekana wamepata watoto wa uzeeni.

Ni jambo linaloonekana kama la kawaida lakini kwa upande mwingine linasononesha na kuvunja mioyo ya watu walioamua kujenga familia.

Ni kauli za kitoto zinazoonyesha kuwa bado hawajakomaa kiakili kwenye ulimwengu huu uliojaa harakati na purukushani za kila aina.

Ningependa kuchukua nafasi hii kuwakumbusha hao wenye kuwakejeli wengine kwenye hili ya kuwa.

1) Maisha ni fumbo zito Sana ambalo mara nyingi ni wachache Sana wenye kufumbua. Mara nyingi mipango yako inaweza ikapishana na mipango ya Mungu.

2) Uhai na kifo ni vyake Mungu mwenyewe kwani hakuna ajuaye kuwa amebakisha muda gani wa kuishi hapa duniani. Wapo vijana wengi wametangulia mbele za haki wakiacha watoto wao na familia zao zikiteseka na kuwaacha wazee wakiendelea kulea watoto wao wa uzeeni mpaka wakijitegemea na kufurahia matunda yao. Hivyo kusema kuwa mwanaao akifika miaka kadhaa wewe utakuwa umeshachoka au umeshakufa ni maneno ya kufuru au ya mtu asiye na Imani kwa mola wake mlezi.

3) Kwenye maisha kila mtu Mungu amemuwekea wakati wake wa kufanya jambo lake kwa rehema zake. Wapo watu waliowahi kuoa lakini Mungu akawanyima watoto mpaka wanazeeka na wengine wanawapata uzeeni kabisa. Wapo watu wamejikuta wapo jela wakitumikia vifungo virefu na mpaka wanatoka umri umekwenda na wanaamua kujenga familia. Wapo watu walikuwa wanaugua kwa muda mrefu na hatimaye wakapona na kuanzisha familia. Hivyo basi kama wewe umewahi ni sahihi kwako lakini haiwezi kuwa makosa kwa anayeonekana amechelewa.

4) Changamoto za kifamilia na vifo.
Kuna mwingine anawahi kuoa lakini Kati Kati ya safari anawapoteza mke na watoto wote kwa pamoja Kwa ajali au maladhi ya kawaida na anaamua kuoa na kuanzisha familia upyaaa.

Kwa kifupi mambo na changamoto za kidunia ni nyingi zinazopelekea watu kuonekana wamechelewa kupata watoto au kuoa na kuolewa. Tujifunze kuwa wastaarabu kwenye maisha ya watu kwani hatujui matamshi yetu yanawaathiri vipi wenzetu.

Niko tayari kusahihishwa.

Nawasilisha.
Religious people especially Christians are worst,hawa viazi wana masimango na judgemental sana kwa ambao bado kuoelwa

Wengine ni newly weds,hawa watu wana masimango sana....majinga kabisa haya
 
Back
Top Bottom