Masjid Rawadha na Soko Mjinga Kisutu

Masjid Rawadha na Soko Mjinga Kisutu

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
MASJID RAWDHA NA SOKO MJINGA KISUTU
Masjid Rawdha ni huo msikiti kushoto ambao zamani ulikuwa ukijulikana kama Masjid Badawy na hili ndilo jina nililolikuta mimi wakati napata akili.

Kulia ni soko maarufu likijulikana kama Soko Mjinga.

Majengo yote hayo yamebadilika kwa kuvunjwa yale ya zamani na kujengwa mapya.

Hii barabara haikuwa hivi.

Nina picha nilipiga Mnazi Mmoja na nyuma yangu inaonekana barabara hii wakati huo ni barabara ya vumbi.

Nyuma ya barabara hii katika hiyo picha ya mwaka wa 1966 ni barabara ya kupita na kupishana gari moja utaona vibanda vya Soko Mjinga. Barabara hii sasa inajulikana kana Bi. Titi Street.

Leo mchana nimepita hapo nikitokea Mtaa wa Mkunguni na ilipowaka taa nyekundu nimetoa simu yangu na kwa haraka nikapiga picha hii.

Nyuma yangu kwenye makutano ya Lumumba Avenue na Mtaa wa Mkunguni kulikuwa na mti unaitwa Sycamore.

Barabara hii ya Lumumba nayo halikadhalika ilikuwa nai barabara moja na kwenye kona upande wa pili katika miaka ya 1960 ilikuwa barza ya vijana maarufu kwa jina la ''Jobless.''

Turudi kwenye Masjid Rawdha.

Muonekano wa majengo haya mawili kwa pamoja ulinishtua kwani nilikuwa bado sijaliona Soko la Kisutu toka lifunguliwe.

Haraka fikra zangu zikarudi nyuma miaka mingi wakati Mufti Sheikh Hassan bin Ameir akidarsisha hapo hata uhuru bado.

Hii ilikuwa miaka ambayo Shariff Hussein Badawy alikuwa hapo akisomesha vijana usomaji wa Qur'an kwa njia ya tajwid.

Akili yangu ilituama mwaka wa 1963 Mfungo Sita kama huu tulionao hivi sasa Maulid yanasomwa hapo jirani ya msikiti Viwanja Vya Mnazi Mmoja.

Maulid yale yalileta matatizo makubwa yaliyoishia Shariff Hussein kufukuzwa Tanganyika na kurudishwa kwao Kenya.

Mwalimu wangu Mzee Kissinger kwa jicho lake akiwa kasimama Soko Mjinga aliwaona maofisa wawili wa uhamiaji Wazungu wakiingia msikitini na viatu kutoa notisi ya kufukuzwa nchini Shariff Hussein na ndugu yake Mwinyibaba.

Miaka ile wote wawili vijana wadogo.

Chini ya kila paa hukosi historia.

Hiyo picha ya pili ni mimi nimesimama Viwanja Vya Mnazi Mmoja na nyuma yangu ni barabara iliyokuja kupewa jina la Bi. Titi Mohamed na ukivuka hiyo barabara ndiyo Soko Mjinga.

Hii ilikuwa 1966.

Hebu angalia picha hizi mbili kwa utulivu.

Picha ya tatu ni ya miaka hiyo Shariff Hussein Badawy akiwa na Sheikh Ismail Mohamed mmoja wa wanafunzi wake.

Screenshot_20211031-064827_Facebook.jpg
 
Sharif Husein Badawy amefariki mwaka jana nyumbani kwake Mambrui Kenya baada ya kuuguzwa Dar es Salaam kwa muda mrefu ugonjwa wa kisukari(nakumbuka niliwahi kusoma taazia yake uliyoiandika humu).

Yeye na nduguye Seyyid Ahmad bin Ahmad Badawy (Mwenyebaba)ambaye bado yupo hai(Allah Ampe umri zaid) wameleta athar kubwa kutokana na maisha yao na juhudi zao za kueneza mafundisho sahihi ya Uislamu.

Video za mawaidha ya Mwenyebaba zipo kwa makumi youtube, na mwezi huu amekua akihudhuria maulid mengi kuanzia Mambrui, Malindi, Mombasa, Takaungu, Watamu, Eldoret, Nairobi, Tanga, Dar es Salaam nk na kutoa nasaha zenye ilm kubwa.

Seyyid Hussein Badawy(Allah amrahmu) yeye aliasisi madrasa kubwa pale Lushoto (Irshaad) ambayo sasa hivi inawanafunzi zaidi ya mia moja kutoka sehemu mbalimbali za Afrika Mashariki. Kwa miaka yote wanapokua pale hawalipi chochote na wakipewa huduma zote kama kama chakula, malazi na hayo masomo yao.

Watoto wake wakikuhadithia namna baba yao alivyofukuzwa nchini miaka ya sitini kama ulivyoeleza kwenye uzi, hakika utapata kujua sura nyingine na pengine halisi ya baadhi ya watawala wetu ambao hadharani huonekana ni rahimu, wapenda haki na wanaofuata sheria!
 
Sharif Husein Badawy amefariki mwaka jana nyumbani kwake Mambrui Kenya baada ya kuuguzwa Dar es Salaam kwa muda mrefu ugonjwa wa kisukari(nakumbuka niliwahi kusoma taazia yake uliyoiandika humu).

Yeye na nduguye Seyyid Ahmad bin Ahmad Badawy (Mwenyebaba)ambaye bado yupo hai(Allah Ampe umri zaid) wameleta athar kubwa kutokana na maisha yao na juhudi zao za kueneza mafundisho sahihi ya Uislamu.

Video za mawaidha ya Mwenyebaba zipo kwa makumi youtube, na mwezi huu amekua akihudhuria maulid mengi kuanzia Mambrui, Malindi, Mombasa, Takaungu, Watamu, Eldoret, Nairobi, Tanga, Dar es Salaam nk na kutoa nasaha zenye ilm kubwa.

Seyyid Hussein Badawy(Allah amrahmu) yeye aliasisi madrasa kubwa pale Lushoto (Irshaad) ambayo sasa hivi inawanafunzi zaidi ya mia moja kutoka sehemu mbalimbali za Afrika Mashariki. Kwa miaka yote wanapokua pale hawalipi chochote na wakipewa huduma zote kama kama chakula, malazi na hayo masomo yao.

Watoto wake wakikuhadithia namna baba yao alivyofukuzwa nchini miaka ya sitini kama ulivyoeleza kwenye uzi, hakika utapata kujua sura nyingine na pengine halisi ya baadhi ya watawala wetu ambao hadharani huonekana ni rahimu, wapenda haki na wanaofuata sheria!
Sesten,
Ahsante sana.
 
Kama mwaka 66 ulikuwa hivyo sasahivi ukoje!? Shikamoo babu!

Sent from my SM-G532F using JamiiForums mobile app
Trainee,
1966 nilikuwa na miaka 14 na siku hii nilikuja Mnazi Mmoja kuangalia mazoezi ya Everton sikuja kucheza.

Nakumbuka wakati huu matokeo ya kuanza sekondari yalikuwa yametoka.

Hii ilikuwa kabla hatujaingia katika mzozo tukaunda Saigon.

Sasa nina miaka 69 ni mzee kwa hakika lakini siwezi kuwa babu yako kwa kuwa wajukuu zangu ni wadogo sana umri wa chekechea.

Mimi ni umri wa baba yako yaani wewe ni sawa na wanangu katika umri wa kumaliza chuo kikuu.
 
Wewe tatizo lako ni umri wake au contente na mada alio andika? lakini akili za vijana wa siku hizi CCM intaendelea kututawala
Mul...
Mbona unamjibu hivyo?
Hajafanya kosa kauliza tu nikoje hivi sasa.

Au kuna ujumbe ambao mimi sikuuelewa?

Nimeweka video hiyo fupi 1:37 ili muone haiba yangu yaani muonekano wangu.

Hapa mtaani nina wachumba kila nyumba kwa hiyo nikiwa barazani kwangu nahakikisha sikosi loose coins maana lazima wasimame kuniamkia babu yao.
 

Attachments

  • VID-20211027-WA0047.mp4
    15 MB
Mul...
Mbona unamjibu hivyo?
Hajafanya kosa kauliza tu nikoje hivi sasa.

Au kuna ujumbe ambao mimi sikuuelewa?

Nimeweka video hiyo fupi 1:37 ili muone haiba yangu yaani muonekano wangu.

Hapa mtaani nina wachumba kila nyumba kwa hiyo nikiwa barazani kwangu nahakikisha sikosi loose coins maana lazima wasimame kuniamkia babu yao.
I adore you indeed!!!! Proud of what you ure.
 
Sharif Husein Badawy amefariki mwaka jana nyumbani kwake Mambrui Kenya baada ya kuuguzwa Dar es Salaam kwa muda mrefu ugonjwa wa kisukari(nakumbuka niliwahi kusoma taazia yake uliyoiandika humu).

Yeye na nduguye Seyyid Ahmad bin Ahmad Badawy (Mwenyebaba)ambaye bado yupo hai(Allah Ampe umri zaid) wameleta athar kubwa kutokana na maisha yao na juhudi zao za kueneza mafundisho sahihi ya Uislamu.

Video za mawaidha ya Mwenyebaba zipo kwa makumi youtube, na mwezi huu amekua akihudhuria maulid mengi kuanzia Mambrui, Malindi, Mombasa, Takaungu, Watamu, Eldoret, Nairobi, Tanga, Dar es Salaam nk na kutoa nasaha zenye ilm kubwa.

Seyyid Hussein Badawy(Allah amrahmu) yeye aliasisi madrasa kubwa pale Lushoto (Irshaad) ambayo sasa hivi inawanafunzi zaidi ya mia moja kutoka sehemu mbalimbali za Afrika Mashariki. Kwa miaka yote wanapokua pale hawalipi chochote na wakipewa huduma zote kama kama chakula, malazi na hayo masomo yao.

Watoto wake wakikuhadithia namna baba yao alivyofukuzwa nchini miaka ya sitini kama ulivyoeleza kwenye uzi, hakika utapata kujua sura nyingine na pengine halisi ya baadhi ya watawala wetu ambao hadharani huonekana ni rahimu, wapenda haki na wanaofuata sheria!
Sesten...
 
Sesten...
Sheikh Mohamed

Nimefaidika sana na maelezo haya.

Nimejipatia nakala yangu ya "Life and Times of Abdulwahid Sykes". Nitaanza kusoma leo hii. Nadhani kuna mengi ndani ya kitabu hiki
 
Trainee,
Vipi ndugu yangu kwa nini unasema basi tu?
Kuna tatizo?
Ndugu huyo aliponishambulia nikataka kuleta ujana wa kujibizana ghafla ndipo nikakumbuka kuwa niliwahi kuleta uzi humu wa kuomba radhi watu niliowaudhi nikitaka nisamehewe.

Masharti ya (utaratibu wa kufanya) toba (kwa sisi waislamu) yapo hivi;
1.Kuacha dhambi
2.Kujutia kwa dhambi uliyoifanya
3.Kunuia kutokurudia tena dhambi
4.Kurudisha haki iliyonyang'anywa (iwapo dhambi iliambatana na kuzuia au kupora haki ya mtu mwingine)

Sent from my SM-G532F using JamiiForums mobile app
 
Ndugu huyo aliponishambulia nikataka kuleta ujana wa kujibizana ghafla ndipo nikakumbuka kuwa niliwahi kuleta uzi humu wa kuomba radhi watu niliowaudhi nikitaka nisamehewe.

Masharti ya (utaratibu wa kufanya) toba (kwa sisi waislamu) yapo hivi;
1.Kuacha dhambi
2.Kujutia kwa dhambi uliyoifanya
3.Kunuia kutokurudia tena dhambi
4.Kurudisha haki iliyonyang'anywa (iwapo dhambi iliambatana na kuzuia au kupora haki ya mtu mwingine)

Sent from my SM-G532F using JamiiForums mobile app
Trainee,
Ahsante sana.
 
MASJID RAWDHA NA SOKO MJINGA KISUTU
Masjid Rawdha ni huo msikiti kushoto ambao zamani ulikuwa ukijulikana kama Masjid Badawy na hili ndilo jina nililolikuta mimi wakati napata akili.

Kulia ni soko maarufu likijulikana kama Soko Mjinga.

Majengo yote hayo yamebadilika kwa kuvunjwa yale ya zamani na kujengwa mapya.

Hii barabara haikuwa hivi.

Nina picha nilipiga Mnazi Mmoja na nyuma yangu inaonekana barabara hii wakati huo ni barabara ya vumbi.

Nyuma ya barabara hii katika hiyo picha ya mwaka wa 1966 ni barabara ya kupita na kupishana gari moja utaona vibanda vya Soko Mjinga. Barabara hii sasa inajulikana kana Bi. Titi Street.

Leo mchana nimepita hapo nikitokea Mtaa wa Mkunguni na ilipowaka taa nyekundu nimetoa simu yangu na kwa haraka nikapiga picha hii.

Nyuma yangu kwenye makutano ya Lumumba Avenue na Mtaa wa Mkunguni kulikuwa na mti unaitwa Sycamore.

Barabara hii ya Lumumba nayo halikadhalika ilikuwa nai barabara moja na kwenye kona upande wa pili katika miaka ya 1960 ilikuwa barza ya vijana maarufu kwa jina la ''Jobless.''

Turudi kwenye Masjid Rawdha.

Muonekano wa majengo haya mawili kwa pamoja ulinishtua kwani nilikuwa bado sijaliona Soko la Kisutu toka lifunguliwe.

Haraka fikra zangu zikarudi nyuma miaka mingi wakati Mufti Sheikh Hassan bin Ameir akidarsisha hapo hata uhuru bado.

Hii ilikuwa miaka ambayo Shariff Hussein Badawy alikuwa hapo akisomesha vijana usomaji wa Qur'an kwa njia ya tajwid.

Akili yangu ilituama mwaka wa 1963 Mfungo Sita kama huu tulionao hivi sasa Maulid yanasomwa hapo jirani ya msikiti Viwanja Vya Mnazi Mmoja.

Maulid yale yalileta matatizo makubwa yaliyoishia Shariff Hussein kufukuzwa Tanganyika na kurudishwa kwao Kenya.

Mwalimu wangu Mzee Kissinger kwa jicho lake akiwa kasimama Soko Mjinga aliwaona maofisa wawili wa uhamiaji Wazungu wakiingia msikitini na viatu kutoa notisi ya kufukuzwa nchini Shariff Hussein na ndugu yake Mwinyibaba.

Miaka ile wote wawili vijana wadogo.

Chini ya kila paa hukosi historia.

Hiyo picha ya pili ni mimi nimesimama Viwanja Vya Mnazi Mmoja na nyuma yangu ni barabara iliyokuja kupewa jina la Bi. Titi Mohamed na ukivuka hiyo barabara ndiyo Soko Mjinga.

Hii ilikuwa 1966.

Hebu angalia picha hizi mbili kwa utulivu.

Picha ya tatu ni ya miaka hiyo Shariff Hussein Badawy akiwa na Sheikh Ismail Mohamed mmoja wa wanafunzi wake.

View attachment 1992825
we mzee hunaga hoja hadi huwa unatia huruma.
 
Back
Top Bottom