Maskini wenye hasira kali Zambia wamuua kwa kumchoma moto Mtanzania

Maskini wenye hasira kali Zambia wamuua kwa kumchoma moto Mtanzania

MamaSamia2025

JF-Expert Member
Joined
Mar 29, 2012
Posts
14,588
Reaction score
32,361
POLISI ZAMBIA wamethibitisha kifo cha Mfanyabiashara maarufu wa Nkeyema, Zambia, Sikaonga Ernest almaarufu Yakaipa na rafiki yake David Mwakyoma Mtanzania aliyechomwa moto na kundi la maskini wenye hasira kali.

Wawili hao wameuawa katika Wilaya ya Mumbwa na kundi la maskini wenye hasira kali wakati wa ghasia baada ya taarifa kuenea kuwa mtu mwingine aliyejulikana kama Mwiya Kashweka ameuawa na kuondolewa sehemu za siri ambapo kina Mwakyoma walidhaniwa ndo walifanya unyama huo.

Majengo mbalimbali ya umma yameharibiwa na wananchi waliofanya ghasia miongoni mwao ofisi ya Mifugo kuteketezwa na kuwa majivu, madirisha ya ofisi za Polisi, Uhamiaji na Usajili wa Taifa yote yamevunjwa.

Magari na lodge ya marehemu Yakaipa yaliharibiwa kwa kuchomwa moto. Hii ilikua tarehe 13/09/2023.

Binafsi nimesikitishwa sana na hizi taarifa na kulaani maskini wote wanaodhani matajiri wote wamepata utajiri wao kwa kutumia nguvu za giza. Wazambi ni wapole ila wana wivu mkubwa kwa kudhani wanaopambana na kufanikiwa hudhulumu haki zao. Ndugu Mwakyoma na mwenzie wameuwawa kwa kudhaniwa kuwa wanahusika na ushirikina uliosababisha kifo cha Mwiya. Na kwa siku za karibuni kumekuwa na kamata kamata ya watanzania waliopo huko.

Ila pia kwa upande mwingine kuna watanzania wenzetu wanaotuchafua sana kwa majirani kwa kuendekeza ushirikina. Mwaka jana kuna watanzania waliokamatwa Zambia kwa kwenda kufanya kazi ya kutoa uchawi kule Zambia kama wanavyofanya Kigoma na Sumbawanga. Ukiwa mtanzania kwa nchi za jirani unachukuliwa kama mbobevu kwenye ushirikina.

FB_IMG_1695584643983.jpg
FB_IMG_1695584648474.jpg
FB_IMG_1695584472217.jpg
FB_IMG_1695584468906.jpg
FB_IMG_1695584465399.jpg
FB_IMG_1695584477617.jpg
FB_IMG_1695584479773.jpg
 

Attachments

  • 0c66b0b7871b427cad1537679db36b45.mp4
    2.5 MB
  • 5639cdf29c3140a697232ef183ded7b7.mp4
    2.5 MB
POLISI ZAMBIA wamethibitisha kifo cha Mfanyabiashara maarufu wa Nkeyema, Zambia, Sikaonga Ernest almaarufu Yakaipa na rafiki yake David Mwakyoma Mtanzania aliyechomwa moto na kundi la maskini wenye hasira kali.

Wawili hao wameuawa katika Wilaya ya Mumbwa na kundi la maskini wenye hasira kali wakati wa ghasia baada ya taarifa kuenea kuwa mtu mwingine aliyejulikana kama Mwiya Kashweka ameuawa na kuondolewa sehemu za siri ambapo kina Mwakyoma walidhaniwa ndo walifanya unyama huo.

Majengo mbalimbali ya umma yameharibiwa na wananchi waliofanya ghasia miongoni mwao ofisi ya Mifugo kuteketezwa na kuwa majivu, madirisha ya ofisi za Polisi, Uhamiaji na Usajili wa Taifa yote yamevunjwa.

Magari na lodge ya marehemu Yakaipa yaliharibiwa kwa kuchomwa moto. Hii ilikua tarehe 13/09/2023.

Binafsi nimesikitishwa sana na hizi taarifa na kulaani maskini wote wanaodhani matajiri wote wamepata utajiri wao kwa kutumia nguvu za giza. Wazambi ni wapole ila wana wivu mkubwa kwa kudhani wanaopambana na kufanikiwa hudhulumu haki zao. Ndugu Mwakyoma na mwenzie wameuwawa kwa kudhaniwa kuwa wanahusika na ushirikina uliosababisha kifo cha Mwiya. Na kwa siku za karibuni kumekuwa na kamata kamata ya watanzania waliopo huko.

Ila pia kwa upande mwingine kuna watanzania wenzetu wanaotuchafua sana kwa majirani kwa kuendekeza ushirikina. Mwaka jana kuna watanzania waliokamatwa Zambia kwa kwenda kufanya kazi ya kutoa uchawi kule Zambia kama wanavyofanya Kigoma na Sumbawanga. Ukiwa mtanzania kwa nchi za jirani unachukuliwa kama mbobevu kwenye ushirikina.
Mbon matajiri Zambia ni wengi kwanini Yeye?
 
Mbon matajiri Zambia ni wengi kwanini Yeye?
Huyo marehemu kama ilivyo kwa matajiri wengine hata hapa TZ alikuwa akituhumiwa kutumia ushirikina kwenye ishu zake. Kuna kesi ziliibuka za watu kupotea na kukutwa wameuwawa huku sehemu za siri zikiwa zimenyofolewa. Watu wakawa wanamyooshea kidole kuwa ni mhusika. Tukio la kifo cha Mwiya ndo ikawa kama 40 yake ingawa bado wananchi hawakuwa na uhakika 100%. Mwakyoma nae alikuwa mfanyabiashara huko Mumbwa na alifahamika zaidi kwa jina la Dollar One (a.k.a). Huenda pia sababu nyingine iliyofanya maskini wawe na hasira ni tabia ya jamaa enzi za uhai wake kugawa pesa kwa kurushia watu.
 
Huyo marehemu kama ilivyo kwa matajiri wengine hata hapa TZ alikuwa akituhumiwa kutumia ushirikina kwenye ishu zake. Kuna kesi ziliibuka za watu kupotea na kukutwa wameuwawa huku sehemu za siri zikiwa zimenyofolewa. Watu wakawa wanamyooshea kidole kuwa ni mhusika. Tukio la kifo cha Mwiya ndo ikawa kama 40 yake ingawa bado wananchi hawakuwa na uhakika 100%. Mwakyoma nae alikuwa mfanyabiashara huko Mumbwa na alifahamika zaidi kwa jina la Dollar One (a.k.a). Huenda pia sababu nyingine iliyofanya maskini wawe na hasira ni tabia ya jamaa enzi za uhai wake kugawa pesa kwa kurushia watu.
Pesa pesa hizi ni noma sana.
 
Back
Top Bottom