Maslahi ya Mbunge wa Tanzania ni kufuru

Yaani isiishie kwa Trump tu, hata Wazungu wengine nao inabidi wafutilie mbali hii misaada maana inaliwa tu na hawa mafisadi.
 
Ndio maana nchi hii uchaguzi mkuu ni pambano la kufa na kupona maana kuna ulaji wankutosha.Unyang'anyi uliohalalishwa na nyang'au wachache kwa maumivu ya wengi
 
Unapataje ubunge? Kumbe Kuna vinono hivyo? Kisha unakaa kupiga dawati tu unapata vyote hivyo.
 
Hapo bado kwenye kamati za kibunge wanahongwa! Ndio maana wagombea wanahonga wajumbe wawapigie kura za kushinda ubunge, siasa Tanzania ni biashara purely
 
Kabisa aisee maana hadi inatia hasira kuona wachache ndiyo wananeemeka wakati wengine wanaishi Kwa maumivu
Yaani isiishie kwa Trump tu, hata Wazungu wengine nao inabidi wafutilie mbali hii misaada maana inaliwa tu na hawa mafisadi.
 
Hv zile mbwembwe za mwanzon za magu alipoingia madarakani na kusema mshahara wake utakuwa mil 9,zilikuwa za kweli?
Kuna watu walikuwa wanaamini kila asemacho. Kwa kusia tu, mshahara wa rais wa Tanzania haupungui 100m.
 
Katiba inasema kuwa mbunge "ujue tu kusoma na kuandika " ndio wanaofaidi kodi za wananchi.
 
Bila shaka ili kupata daktari mzuri ni asomee udaktari miaka 7,
Askari wetu wanahenyeka kwa jasho na damu,
Waalimu ndiyo ambao wanatengeneza wataalamu mbalimbali kwenye taifa letu,
 
Halafu tapeli Kigwangala anasema ubunge ni kujitolea.
 
Mwalimu miaka 35 anastaafu analipwa milion 46, huu ni ukichaa
 
Alafu eti Mtu aliwataka kina Khalima waachie tu kirahisi hizo Neema.
 
Ndio maana wanasiasa wanauwana, wanalogana kwasababu ya MASLHI MANONO.
Kila mtu anataka maisha mazuri.
Siasa pekee ndio inalipa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…