Masomo 21 Kwa Ajili ya karne ya 21: Ukweli Kinyonga, Kuna Ukweli Bandia Unaodumu Milele

Masomo 21 Kwa Ajili ya karne ya 21: Ukweli Kinyonga, Kuna Ukweli Bandia Unaodumu Milele

Kwenye psychology unaweza ukaona vizuri kwa nini hayo aliyoandika mwandishi yanatokea na kukua zaidi na hata kuweza kufikiriwa kuwa ni ukweli.

Ubongo unaweza kukudanganya ukaona unachokihisi, sikia, gusa, nusa, onja au ona ni kweli au ni uongo au haiwezekani. Hii ni tabia ya ubongo.

Mambo unayofanya mara kwa mara au taarifa inayojirudia rudia mara nyingi, ubongo huweza kukudanganya kuwa ni sahihi, vema; ndio ukweli.

Ukweli hatahivyo, ni kuwa hao wanaotengeneza habari au taarifa zisizo za kweli, ukweli fake wanafahamu kwa kina ubongo ulivyo; ni wanasaikolojia wa hali ya juu.

Katika hili, hao wanaotengeneza ukweli fake wanafahamu jamii. Wanajua wazi kuwa watu wengi duniani wameshajiingiza kwenye mambo ambayo haiwezekani akili kufanya kazi kwao inavyotakiwa.
 
Kwenye psychology unaweza ukaona vizuri kwa nini hayo aliyoandika mwandishi yanatokea na kukua zaidi na hata kuweza kufikiriwa kuwa ni ukweli.

Ubongo unaweza kukudanganya ukaona unachokihisi, sikia, gusa, nusa, onja au ona ni kweli au ni uongo au haiwezekani. Hii ni tabia ya ubongo.

Mambo unayofanya mara kwa mara au taarifa inayojirudia rudia mara nyingi, ubongo huweza kukudanganya kuwa ni sahihi, vema; ndio ukweli.

Ukweli hatahivyo, ni kuwa hao wanaotengeneza habari au taarifa zisizo za kweli, ukweli fake wanafahamu kwa kina ubongo ulivyo; ni wanasaikolojia wa hali ya juu.

Katika hili, hao wanaotengeneza ukweli fake wanafahamu jamii. Wanajua wazi kuwa watu wengi duniani wameshajiingiza kwenye mambo ambayo haiwezekani akili kufanya kazi kwao inavyotakiwa.

Kauli yako Ni kweli kwa asilimia kubwa. Lkn kuna kanuni ya mchepuko (exception rule).

Hadhira iliyo na weledi wa kuhakiki habari inaweza kuzitambua na kuzikataa habari feki. Naongelea information analysis evaluation and verification
 
Kauli yako Ni kweli kwa asilimia kubwa. Lkn kuna kanuni ya mchepuko (exception rule).

Hadhira iliyo na weledi wa kuhakiki habari inaweza kuzitambua na kuzikataa habari feki. Naongelea information analysis evaluation and verification
Kuhusu hii kanuni uliosema ni kweli. Lakini kuna suala la tamaa ya mdaraka, si "utawala" na tamaa ya mali si "utajiri". Haya yote yako kwenye ubongo.

Watu wengi duniani wanaodhibiti Serikali hawako kwenye hizo nafasi kupitia utaratibu unaotakiwa, ambao kimsingi ndio ukweli halisi.

Kwa sababu hiyo haishangazi kuona ukweli fake ukitawala na kuongoza maisha ya watu.

Hao kwa sababu wanajua wanadhibiti Serikali, kwa mfano kinyume na utaratibu unaotakiwa hawawezi kukubali kanuni ya mchepuko (exceptional rule).

Kanuni hii itaweza kufanya kazi pale jamii itakapo kuwa na uelewa wa kina wa mambo, elimu na maarifa ya vitu.
 
Mwandishi anadai kuwa Biblia ni hadithi za Kutunga, Japo hajatueleza Chanzo cha Maisha kwa falsafa yake. Hapo Kakosea.

Nimekubali ulipomnukuu Hitler kuwa ili kutengeneza propaganda utahitaji kurudia maneno, Hata Kibiblia hii inakubalika inaunda Imani.
 
Mwandishi anadai kuwa Biblia ni hadithi za Kutunga, Japo hajatueleza Chanzo cha Maisha kwa falsafa yake. Hapo Kakosea.

Nimekubali ulipomnukuu Hitler kuwa ili kutengeneza propaganda utahitaji kurudia maneno, Hata Kibiblia hii inakubalika inaunda Imani.
Muandishi ni atheist na gay. Anaamini kuhusu evolution ila ni jamaa mwenye akili sana na hachoshi kumsoma.
 
Kauli yako Ni kweli kwa asilimia kubwa. Lkn kuna kanuni ya mchepuko (exception rule).

Hadhira iliyo na weledi wa kuhakiki habari inaweza kuzitambua na kuzikataa habari feki. Naongelea information analysis evaluation and verification
Nakubaliana nawewe kwa hili, Mwandishi angefanya uchambuzi yakinifu wa madai yake mfano Uhusiano wa Soda za Coca Cola na Magonjwa. Angechambua pia changamoto za dini (maana amedai ni hadithi)

Akibainisha pasi na Shaka yoyote kuwa madai yake ni ya Kweli, Weledi wake utadhihirishwa Vinginevyo Yeye ndiyo Katunga hoja zisizo na majibu
 
Nakubaliana nawewe kwa hili, Mwandishi angefanya uchambuzi yakinifu wa madai yake mfano Uhusiano wa Soda za Coca Cola na Magonjwa. Angechambua pia changamoto za dini (maana amedai ni hadithi)

Akibainisha pasi na Shaka yoyote kuwa madai yake ni ya Kweli, Weledi wake utadhihirishwa Vinginevyo Yeye ndiyo Katunga hoja zisizo na majibu
kudai kwako "uchambuzi yakinifu" wa uhusiano kati ya soda za Coca Cola na magonjwa, ni ushahidi mwingine wa dunia inaishi na kuamini ukweli wa kutunga na kubuni.

Kuhusu dini, hana cha kuthibitisha (kuwa ni ukweli wa kutunga) kwa kuwa hakuna ushahidi wa kihistoria, sayansi au hata wa kimantiki dhidi ya yasemwayo. Utathibitisha nini apo?
 
kudai kwako "uchambuzi yakinifu" wa uhusiano kati ya soda za Coca Cola na magonjwa, ni ushahidi mwingine wa dunia inaishi na kuamini ukweli wa kutunga na kubuni.

Kuhusu dini, hana cha kuthibitisha (kuwa ni ukweli wa kutunga) kwa kuwa hakuna ushahidi wa kihistoria, sayansi au hata wa kimantiki dhidi ya yasemwayo. Utathibitisha nini apo?
Unapokuja na madai ya 'Aina' yoyote unapaswa kuthibitisha pasi na Shaka yoyote, Uhalali wa madai hayo.Mwandishi ameshindwa kama ambavyo wewe pia umeshindwa.

Katika hali ya kawaida kuna usiku na mchana ambao watu wote wanaamini upo, unapokuja na hoja za kuupinga utatakiwa kuleta ushahidi kuwa 'haupo ' hivyo hadhira itajiridhisha, hivyo Sayansi na mantiki zina ukomo wake kuna vitu huwezi kuvielezea kwa misingi ya sayansi.
 
Muandishi ni atheist na gay.

Mwandishi anaweza kuwa atheist, theist, au deist.

Pia anaweza kuwa gay, straight au ambivalent.

In each case, what difference would it make as far as his arguments in the book are concerned?

Lkn pia, unaandika kauli bilanithibati.

How do you know that XYZ ni atheist au shoga na sio vinginevyo?

Ni kama umeanguka kwenye mtaro uliolilima ngwara Kanida Katoliki mwaka 1968 Papa Paul VI alipotangaza waraka uitwao Humanae Vitae (on human life).

Bila kujibu swali hilo la kiepistemolojia ktk maelezo yako unakuwa unafanya propaganda, na sio uchambuzi.
 
Kuhusu hii kanuni uliosema ni kweli. Lakini kuna suala la tamaa ya mdaraka, si "utawala" na tamaa ya mali si "utajiri". Haya yote yako kwenye ubongo.

Watu wengi duniani wanaodhibiti Serikali hawako kwenye hizo nafasi kupitia utaratibu unaotakiwa, ambao kimsingi ndio ukweli halisi.

Kwa sababu hiyo haishangazi kuona ukweli fake ukitawala na kuongoza maisha ya watu.

Hao kwa sababu wanajua wanadhibiti Serikali, kwa mfano kinyume na utaratibu unaotakiwa hawawezi kukubali kanuni ya mchepuko (exceptional rule).

Kanuni hii itaweza kufanya kazi pale jamii itakapo kuwa na uelewa wa kina wa mambo, elimu na maarifa ya vitu.
Nakubaliana nawe.
Hata viongozi wa dini zetu pendwa za Ukristo na Usilam wanapitia barabara hiyo.
Tanzania ina watu wenye elimu ya kidato cha 4 au zaidi walio chini ya 10%, per UNESCO's data.
Kwa hiyo, watu 90% wanaongozwa na hoja zinazooanzia kwenye hisia badala ya hoja zinazooanzia kwenye mantiki.
Tupanue education attainment level ya nchi angalau kufikia F4 education attainment level ya 51%, na mengine yatafuata.
 
Mwandishi anaweza kuwa atheist, theist, au deist.
Pia anaweza kuwa gay, straight au ambivalent.
In each case, what difference would it make as far as his arguments in the book are concerned?
Mbona umekopy kipande kidogo tu ya niliyoandika? Huo ndiyo upotoshaji wenyewe na si uungwana.
 
Nakubaliana nawe.
Hata viongozi wa dini zetu pendwa za Ukristo na Usilam wanapitia barabara hiyo.
Tanzania ina watu wenye elimu ya kidato cha 4 au zaidi walio chini ya 10%, per UNESCO's data.
Kwa hiyo, watu 90% wanaongozwa na hoja zinazooanzia kwenye hisia badala ya hoja zinazooanzia kwenye mantiki.
Tupanue education attainment level ya nchi angalau kufikia F4 education attainment level ya 51%, na mengine yatafuata.
Bado kwenye hiyo asilimia 10 waliopata elimu ya kidato cha nne na kuendelea kama ulivyosema, zaidi ya robo tatu elimu yao ni service education si analysis.
 
Mwandishi anaweza kuwa atheist, theist, au deist.
Pia anaweza kuwa gay, straight au ambivalent.
In each case, what difference would it make as far as his arguments in the book are concerned?
Hili suala la kuweka umuhimu kwenye alichosema mtu na sio mtu mwenyewe ni dhana nzuri. Wakati mwingine inaleta mkanganyiko. Hata na Yesu aliipigia chapuo. Yafuatwe wanayosema na si walivyoishi na kutenda waandishi! Mtu mwovu unena maovu. Mti tunautambua kwa matunda yake. Mtu awazavyo rohoni mwake ndivyo alivyo. Tunaenenda kwa imani. Tunaishi kulingana na tunavyoamini. Tuaminivyo ndivyo tuishivyo. Imani sio tu katika dini bali ni katika maisha yote ya binadamu.
 
Hili suala la kuweka umuhimu kwenye alichosema mtu na sio mtu mwenyewe ni dhana nzuri. Wakati mwingine inaleta mkanganyiko. Hata na Yesu aliipigia chapuo. Yafuatwe wanayosema na si walivyoishi na kutenda waandishi! Mtu mwovu unena maovu. Mti tunautambua kwa matunda yake. Mtu awazavyo rohoni mwake ndivyo alivyo. Tunaenenda kwa imani. Tunaishi kulingana na tunavyoamini. Tuaminivyo ndivyo tuishivyo. Imani sio tu katika dini bali ni katika maisha yote ya binadamu.
Umeeleza vema mkuu.

Lakini kuna ukweli mmoja nao ni huu: matendo ni muhimu kuliko maneno.

Ukiwa mtu makini unagundua kuwa masimulizi ya biblia yalikusanywa kwa nyakati mbalimbali na watu mbalimbali.

Biblia kwangu binafsi ni zaidi ya maandishi. Naweza kwa hakika kusema, biblia ndio msingi na kilele cha sayansi.

Katika biblia utakuta nini kinatakiwa na nini hakitakiwi kufuata au kuishi. Hivi viliwi utavikuta kwenye biblia.

Watu walio wengi wanaona katika biblia kuwa chote kilichomo, kilichoandikwa katika vitabu vya biblia ndicho kinachotakiwa kufuatwa. Hili ni kosa.

Kwa wengine kwa sababu kwamba biblia ni Neno la Mungu, takatifu; kwao kila kilichoandikwa ndani ya biblia ni sahihi. Mwelekeo huu ndio unapelekea mawazo kwamba masimulizi ya biblia yametungwa.

Biblia yote ni mafundisho ya imani na maadili; inahusu kweli za kiakili hivyo ni pia kweli za mwili.

Biblia si masimulizi ya hovyohovyo.

Biblia ni masimulizi yalio ya akili ya kina yahusuyo maisha ya mtu ya sasa na ya badae na utaratibu wa kuishi unaotakiwa. Inaeleza mwanzo wa vitu, maarifa na elimu ya vitu. Lakini pia ina vitabu vihusuyo tafiti na uzoefu binafsi wa kibinadamu kuhusu maisha.
 
Hili suala la kuweka umuhimu kwenye alichosema mtu na sio mtu mwenyewe ni dhana nzuri. Wakati mwingine inaleta mkanganyiko. Hata na Yesu aliipigia chapuo. Yafuatwe wanayosema na si walivyoishi na kutenda waandishi! Mtu mwovu unena maovu. Mti tunautambua kwa matunda yake. Mtu awazavyo rohoni mwake ndivyo alivyo. Tunaenenda kwa imani. Tunaishi kulingana na tunavyoamini. Tuaminivyo ndivyo tuishivyo. Imani sio tu katika dini bali ni katika maisha yote ya binadamu.

Sijaelewa hoja yako.
Katika falsafa ya maadili tunasema matendo yanabatiza majina.

Ukiiba na wizi ukafamika kwa watu baki unaitwa mwizi.

Ukizini na uzinzi ukafahamika kwa watu baki unaitwa mzinzi.

UKidanganya na uwongo ukafahamika kwa watu baki unaitwa mwongo.

Hivyo, hitimisho kwamba "Mti tunautambua kwa matunda yake," ni sahihi katika mipaka hiyo.

Mpaka hapo "mkanganyiko" uko wapi?

Pia, katika falsafa ya maadili kuna kambi ya deontoligists.
Hawa wanasema kuwa "Mtu awazavyo rohoni mwake ndivyo alivyo." kama ulivyodai.

Kuna kambi ya teleologists.
Hawa wanasema kuwa "Mtu awazavyo rohoni mwake [sivyo] alivyo."

Kwao, kilichomuhimu ni matokeo ya ulicbofikiria kufanya, ukafanya, na watu wakajua kwamba umefanya.
Watu wasipojua hakuna shida.

Hata kama umeua bado wewe sio muuaji.

Mfano:

Chukulia kuwa, umeketi katika chumba cha giza na wanawake watatu;
Halafu unajenga dhamira ya kuzini na mwanamke mmojawapo asiyemkeo;
Unapapasa na kumpata mmoja, anakulegezea, na mnakamilishana.

Deontologist kama Yesu anakuita mzinzi.

Teleologist kama Maaskofu wa Kianglikana wanasema wewe sio mzinzi.

Baada ya haya, sasa hebu hitimisha hoja yako ili twende pamoja.
 
Mbona umekopy kipande kidogo tu ya niliyoandika? Huo ndiyo upotoshaji wenyewe na si uungwana.

Najaribu kuhakikisha kuwa kanuni za makabiliano ya kimantiki zinazingatiwa.
Mosi, tunatofautisha mleta hoja na hoja.

Pili, tunatofautisha mleta hoja na rafiki wa mleta hoja.
Tatu, tunakwepa kosa la kimantiki liitwalo genetic fallacy.

Nilipoona bandiko lako, nikafikiri kwamba umekiuka kanuni hizi.

Tatizo zaidi ulitoa tamko bila ithiobati.

Na kama unavyojua, tamko lisilo na vazi la ushahidi hupigwa pingamizi lisilovaa nguo ya ushahidi pia.

Na ikitokea hivyo, makabiliano ya kinatiki huwa yamekufa.

Kwa hiyo, ni muhimu kukubaliana juu ya rules of engagement kabla ya engagement yenyewe.
 
Najaribu kuhakikisha kuwa kanuni za makabiliano ya kimantiki zinazingatiwa.
Mosi, tunatofautisha mleta hoja na hoja.
Pili, tunatofautisha mleta hoja na rafiki wa mleta hoja.
Tatu, tunakwepa kosa la kimantiki liitwalo genetic fallacy.
Nilipoona bandiko lako, nikafikiri kwamba umekiuka kanuni hizi.
Tatizo zaidi ulitoa tamko bila ithiobati.
Na kama unavyojua, tamko lisilo na vazi la ushahidi hupigwa pingamizi lisilovaa nguo ya ushahidi pia.
Na ikitokea hivyo, makabiliano ya kinatiki huwa yamekufa.
Kwa hiyo, ni muhimu kukubaliana juu ya rules of engagement kabla ya engagement yenyewe.

Nimekuelewa kiasi. Lakini pale yule bwana niliyemjibu alitaka kujua Bwana Noah anaamini nini/ana falsafa gani kuhusu chanzo cha maisha. Ndiyo nikaona nimuambie kuhusu jinsi muandishi alivyo, kwamba ni aetheist, ni shoga(yaani hakubaliani na viwango vya maadili vinavyokubaliwa na watu wengi) na pia anaamini kwenye evolution.

Mimi sijali kama Noah ni shoga na ndiyo maana nimesoma vitabu vyake, Homo sapiens na Homo Deus na humo ndimo kuna ushahidi kwamba yeye ni Atheist na Anaamini evolution.
 
Nimekuelewa kiasi. Lakini pale yule bwana niliyemjibu alitaka kujua Bwana Noah anaamini nini/ana falsafa gani kuhusu chanzo cha maisha. Ndiyo nikaona nimuambie kuhusu jinsi muandishi alivyo, kwamba ni aetheist na ni shoga (yaani hakubaliani na viwango vya maadili vinavyokubaliwa na watu wengi) anayeamini katika nadharia ya evolution. Mimi sijali kama Noah ni shoga na hapana maana nimesoma vitabu vyake, Homo sapiens na Homo Deus na humo ndimo kuna ushahidi kwamba yeye ni Atheist anayeamini katika nadharia ya evolution.

Bado nina mawazo tofauti na yako kuhusu rai kwamba mwandishi Noah ni atheist.

Vitabu hivyo vyote nimevisoma.

Hata softcopy zake ninazo ktk digital library yangu.

Tathmini yangu ni hii: mwandishi Noah sio atheist wala theist.

Badala yake, naona kwamba mwandishi Noah ni deist.

Tofauti zake:

An atheist says: Most probably God is not there.


A theist says: Most probably God is there, and continually intervenes in the world via miracles.

And a deist says: Most probably God is there, but he does not continually intervene in world affairs via miracles, as he did when he created the world via the creation ex-nihilo miracle.

Inadvertently or otherwise, all empirical scientists fall within the category of deism.

They call into question the so called divine providence by theistic theologians.


They call into question the possibility of divine miracles except the creation ex-nihilo miracle.

And this is nakedly understandable. If you believe in continual miracles, given a puzzle before you, you would not have a reason to propose a hypothesis and proceed to emperically test it, as God's intervention would be a predetermined answer to your puzzle.


Kwa hakika, nilielewa tofauti kati ya theism na deism baada ya kusoma kitabu kiitwacho THE UNIVERSE NEXT DOOR kilichoandikwa na James Sire.

Nakala tepe ya kitabu hiki nimeiweka hapa chini, kwa wasomaji wanaopenda kupekua vitabu.

Ni mtazamo wangu kwamba, kama Hayati Magufuli angejitenga na kambi ya wanateolojia walioko katika kambi ya tehizimo ("theism") na kuambatana na wanateolojia walio katika kambi ya deizimo ("deism"), huenda angeepuka mauti haya, japo kwa miaka mingine kadhaa.

Kwa ufupi:


Theistic miraculous prayers + pathogens such as corona virus = superstition + death!

Kila mwanasayansi mamboleo anaujua ukweli huu.

Hata hayati Magufuli alipaswa kufahamu ukweli huu.

Lakini, Maaskofu na makuhani wake wakam-brainwash hadi ukomo!

Akafwariki kwa sababu ya kibiriti cha kifuani kufyatuliwa na korona.

Nimesikitishwa sana na kifo chake kwa sababu hii zaidi kuliko sababu nyingine yoyote.

Ni jambo ambalo linapaswa kukosolewa na wanazuoni.

Lakini pia, tumepata ushahidi usiokanushuka kwamba kuna wakati imani za kidini ni tishio kwa usalama wa nchi, kwa kiwango kisichokubalika.

Yafaa sasa hatua za haraka zichukuliwe na wahusika, na hasa wale wenye dhamana ya kuandaa na kusimamia utekelezaji wa Mkakati wa Usalama wa Kitaifa, yaani National Secutity Strategy.

Mikakati mingi ya aina hii ninayoifahamu inataja wazi wazi kwamba udini mkali na ushirikina ni aina mojawapo ya vitisho dhidi ya Usalama wa Taifa, na inaweka mikakati ya kupambana navyo.

My main thesis is: Theistic religious practices, as opposed to deistic religious practices, constitute a clear and present threat to national security.

Nikipata muda nitaandika kutetea rai hii.
 

Attachments

Back
Top Bottom