Habari ya wikend wakuu......
Kuna hawa watu niliowataja hapo juu wote ni wachoraji wa katuni wazuri
Masoudy kipanya huyu huchora katuni kwenye gazeti la mwananchi ukiachilia mbali kama CEO wa Maisha plus katuni zake huwa zinafurasha sana........
Lakini huyu mwingine Nathan Mpangala huyu mara nyingi katuni zake huwa wakati taarifa ya habari ya ITV inaishia,nae katuni zake huwa ni nzuri........
Sasa yupi kati ya hawa ubunifu wake katika uchoraji huwa unakuvutia sana hasa ukizingatia wakati mwingine huwa na maudhui yanaendani mfano, michezo,siasa,uchumi n.k
Karibuni tujadili huku tukiukaribisha mwaka mpya......